Kweli nimetazama anavyoanguka kwenye hii video imeniuma sana na imenisikitisha. Katika hali ya ubinadamu, inasikitisha sana kuona binadamu mwenzio akizimika vile. Halafu alipoanza kusema 'aise' kabla hajaanguka, nadhani alikuwa anajisikia vibaya sana au maumivu lakini akajikaza aendelee na hotuba. Nimeumia pia jinsi sauti ilivyoanza kufifia kama anayetaka kutafuna ulimi, yaani kama ni ndugu yako yuko katika hali hiyo utatishika sana.
Kama kuna wanaofurahia kitendo cha binadamu mwenzao kuteseka vile mbele ya watu, hao ni makatili tu. Hakuna siasa hapa. Siasa ni kupingana kwa hoja na si kutakiana mabaya. Mimi napinga CCM kwa dhati, lakini nimesononeshwa sana na madhila yaliyompata JK pale jukwaani. Kama binadamu mwenye umri sawa na babangu, nimemtazama anavyoanguka kwa masikitiko makubwa, ikanijia picha kama babangu mzazi akianguka vile mbele ya umati, itakuwaje. Nimeumia sana.
Pole sana mheshimiwa, Mungu akujalie afya njema uwe salama, urudi kwenye mpambano. Tunahitaji mpambano baina ya watu walio wazima wa afya ndio maana napenda upone, tupate nafasi ya kukusikia katika kampeni, ujibu hoja zetu ukiwa mzima tufanye uchaguzi tukiwa tumesikia hoja za wagombea wote.
ai jamani nyie ...........angekuwa baba yenu nyie mngefurahi anadishwe kila kona alivyoanguka na alivyobebwa kama maiti?
kuanguka kwa kikwete hakuna na mahusiano na imani.
Ha ha ha hii forum na Kikwete ni kama pete na kidole.
Picha zimekwenda wapi tena?
Hawa madaktari wa JK ni wazembe, inakuwaje mkuu anajulikana kuwa ana kisukari na pressure, na amekuwa na tatizo la kuanguka mara kadhaa kwa nini hawampi ushauri mzuri (kama kutokufunga wakati akiwa na shughuli nzito kama hii na pia kumcheck muda mchache kabla ya kupanda jukwaani). Kipimo cha sukari huwa hakichukui hata dk 5.
Mkuu ukizitaka sema ninazo kwenye makataba yangu! Naona leo wale jamaa zetu wapo wengi sana
ohh I see,
Mzee wangu Masa....... hawa jamaa jinsi wanavyojiaibisha hadi inachekesha.
Yaani Raisi wa nchi anaanguka,
Mijamaa yote inakimbia kumbeba mzobe mzobe bila hata kutumia machela au kitu chochote maalumu. Bila kujali kama kuanguka kwake kumetokana na ukosefu wa hewa au la, minjemba yote inajazana na kumeza oxygen yote.
Badala ya kukaa na kujadili namna ya kufanya vyema next time (trust me, there will be a next time on this guy), yenyewe inakuja hapa kupumua kijuu kama imeishiwa hewa.
Zitunze tu mkuu maana kuna siku zitatumika kwa ufanisi zaidi.
ohh I see,
Mzee wangu Masa....... hawa jamaa jinsi wanavyojiaibisha hadi inachekesha.
Yaani Raisi wa nchi anaanguka,
Mijamaa yote inakimbia kumbeba mzobe mzobe bila hata kutumia machela au kitu chochote maalumu. Bila kujali kama kuanguka kwake kumetokana na ukosefu wa hewa au la, minjemba yote inajazana na kumeza oxygen yote.
Badala ya kukaa na kujadili namna ya kufanya vyema next time (trust me, there will be a next time on this guy), yenyewe inakuja hapa kupumua kijuu kama imeishiwa hewa.
Zitunze tu mkuu maana kuna siku zitatumika kwa ufanisi zaidi.
alisahau kuvaa ile pete yake yenye kirungu!
ha ha ha, pete yenye kirungu ndiyo ipi hiyo tena?
Ha ha ha hii forum na Kikwete ni kama pete na kidole.
Picha zimekwenda wapi tena?
Mkuu hata mimi najiuliza sana tena sana. Kwa nini picha za hii thread ni mobile kiasi hiki. Yaani huwezi kuwa na hakika na picha utakazozikuta kila unapofungua.
Nadhani Mod aweke mambo vizuri tu kuwa hizo picha za KJ alipokuwa anaanguka hazitakiwa hapa JF. Naona yanakaribia kuwa kama mambo ya Swaziland ambapo jamaa alitupwa jela kwa kukutwa na gazeti linaloongelea kisa cha mke wa King Mswazi kufumaniwa. Mhhh. hata siamini.
Ni hirizi iko muundo wa pete!
Ndio JF mpya hiyo mkuu .... mambo yamebadilika sana hapa
Ngoja tusubiri, labda mod atatujibu. But kama ni hivyo basi ....life is never the same as it used to be!!