Hii inashangaza sana. Hebu sote tuwe makini na tujiulize maswali haya?
1. Huyu ni Rais wa nne Tanzania Bara, je wale watatu waliopita walianguka mara ngapi?
2. Kwani wao hawakuwa na kazi nzito kama yeye JK kwa sasa?
3. Awamu ya pili alikuwa ni his ex Mzee Mwinyi, na alikuwa ni moslem!! Je alianguka mara ngapi jukwaani au popote au hata kuzimia?
4. Huyu Rais wetu JK ameshaanguka mara nne public, na hatujui private ni mara ngapi?? Je hatujaweza kuona kuwa kuna hutilafu kubwa sana katika mwili wake na afya kwa ujumla?
5.Saumu ya masaa machache haiwezi kabisa kumwangusha mtu mwenye afya yake. Ninafahamu daku huliwa usiku, say kama hata amekula daku saa 2 mbili usiku, bado ana uwezo wa kushinda njaa kwa masaa mengi sana. Mbona wakristu wakifunga ni say kuanzia saa mbili usiku baada ya dinner na hakuna cha daku na bado hata hawasinzii ofisini? Tuwe tunajadili masuala kwa upana!! Afya ya huyu mheshimiwa ni zaidi ya ujuavyo!!
6. Ni kweli Dr. Slaa alianguka bafuni Mwanza na kuvunjika mkono, kumbuka kuwa mahoteli mengi yanatumia tiles za bafuni imara kiasi gani? Tena ukizingatia ni za China mara nyingi? Ile ilikuwa ni accident, hii ya JK si accident, ni madhaifu ya afya yake.
Watanzania wote, ni vema tufumbue macho na kuvaa kiona mbali kuhusu afya ya huyu mtukufu wetu!! Ifahamike kuwa ugonjwa hauombwi na kila mtu angefurahi kama asingeugua, ila basi unapoumwa ni vema ukaweka wazi, hata kama si details but tunajua kabisa huyu ndugu pengine ana low/High BP/Sugar and many other serious illiness!! Kulikoni kujitafutia visingizio lukuki, mara saumu kali, mara alisafiri mno hajapumzika ndiyo maana mwili umeishiwa nguvu, etc, etc. Hivi kweli kama unajua kuwa huna stamina ya kustahimili kazi nyingi ni kwa nini usi-delegate? (Hapa ni kwasafari zaidi).
Pole Rais, pole sana, weka wazi afya yako ilii tukuombee. Ugonjwa ni jambo la kawaida!!Hakuna atakayekunyang'anya hicho kitu eti kwa kuwa umeweka bayana afya yako. Mtasema pengine ugonjwa ni siri ya Dr. na Mgojwa, ni kweli ila magonjwa kama lilivyo general si siri, pengine details zake ndiyo siri. Kwani nini bwana!! Mimi nitasema tu, mbona hata wenye ukimwi wameamua kuvunja ukimya siku hizi na hawaogopi? Sembuse wewe mheshimiwa ambaye tatizo lako ni la kawaida si ukimwi??!!
Dr. wa Rais, tafadhali eleza report ya kiukweli, not propaganda!! Ugonjwa hauna propaganda!! Au ikiwezekana apumzike, bado ataendelea kupata maisha bora kama Rais mtaafu tu na aweze kuishi maisha marefu. Msimchoshe tafadhadhali. Mpeni ushauri wa ukweli.