Mbowe anakanusha uongo. Na hizi ni Photoshop?
ulikuwa kwenye kikao? We uko Nkasi, Namanyere, mwenzio alikuwa kwenye kikao akiongoza kikao na amekuambia hakuwepo.
Najua unafahamu sana kiswahili.Sasa ulitaka akanushe ukweli??
Issue sio nani kambadilisha nani, hiyo sio agenda kuu kwa Sasa. Linalotakiwa kwanza ni CCM itoke madarakani.
Mbowe anakanusha uongo. Na hizi ni Photoshop?
Mpaka sasa Chadema haijabadili chochote kwa Lowassa, yeye ndio anawabadili.
Chadema badala ya kuleta mabadiliko, yenyewe ndio inabadilishwa...
Unabadilisha vipi mfumo wakati chama chako kimeshaanza kubadilishwa na mgeni?
Hapo ndipo utakapojuwa jinsi gani wanasiasa wanachezea akili za wananchi. Wanatufanya mazuzu tunaoweza kulishwa chochote kutoka kwao. Mbowe ametufanya sisi Wananchi ni wajinga sana wa kutokujua nini feki na nini si feki. Kifupi ametudharau.
Mtu mzima ukishajua mtu mwenye akili timamu anakudharau na kukufanya wewe zuzu haupigi naye kelele, muache aamini kuwa uongo wake umeaminiwa unakuja kumuonyesha siku ys siku kuwa wewe si wakudharauliwa kiasi hiki.