Ukweli UKAWA mmetuaibisha, naombea kusema tumeaibishwa; kitendo cha kumtaka LOWASA agombee URAIS kupitia UKAWA imetuonyesha walivyo waroho wa madaraka. mlituaminisha kuwa LOWASA no fisadi, mlipiga kelele mpaka akafukuzwa uwaziri mkuu sasa nchi inapata hasara kwa kuwalipa mawaziri wakuu wawili ndani ya miaka 10. LOWASA NA PINDA ni mzigo ulisababishwa na kelele za UKAWA hasa CDM. Kila kona tuliambiwa LOWASA ni fisadi mwizi na nk. leo mnatuambia kuwa ni mtu safi wakati mkijua siyo mtu safi, hivi nyie viongozi wa UKAWA mnafikiri watanzania ni mbumbumbu? tumewaunga mkono na kuwatetea vijiweni, kwenye mitandao leo hii mnakaribisha zimwi lililoshindikana CCM, UKAWA mtaliweza?
Nimgundua kuwa UKAWA siyo wapigania haki au ukombozi wa nchi hii bali ni wajasiliamali wanaotafuta pesa au kutaka madaraka badala ya kupigania wanyonge, kwa ilivyo UKAWA wapo tayari hata kutafuta mifupa ya binadamu ilimradi kwenda ikulu.
Nimeamini Dr Slaa siyo mwadirifu kama nilivyokuwa nikiamini kwa kuwa yeye ni padre, niliamini hakuna Padre anayeweza kuwa MWONGO. leo hii Padre Slaa atasimama jukwaani bila woga kumtetea LOWASA eti siyo mwizi? wakati anajua katika amri kuu za MUNGU kuna moja inayosema " USIMSEMEE UONGO" lkn leo Padre Slaa anasema uongo siyo dhambi. Ukweli tumeumia sana, sasa hatuna jinsi zaidi ya kuwaomba msamaha CCM.