Wanabodi heshima kwenu....heri ya mwaka mpya..,mwaka iliopita katika harakati za kusaka ndururu...nikapata mchongo wa kwenda mkoa wa katavi wilaya ya Tanganyika,tarafa ya Karema Kijiji Cha IKOLA..mwanaume nikajikoki huyoo mpaka katavi mjini mpanda...kufika ikola nikadandia kihaisi ...masaa matano njiani tunakata pori...mida ya saa moja jioni naingia ndani ya ikola..nampijia simu mwenyeji wangu anakuja kunipokea haoo mpaka nyumbani...kwa kuwa ulikuwa Giza tayari mwanaume nikaoga huyoo nikalaza ubavu maana Kila kiungo kulikuwa kinauma kutokana uchovu....saa Tisa usiku naanza kusikia makelele ya watu nafungua dirisha kidogo kucheki nje naona wajuba wanapita na mandoo,tochi,masufuria,,majiko,,wanakielekea sipajui...,huku na huku kukakucha ebwanaeee kumbe nyumba ya jamaa yangu iko mita 35 kutoka ziwa Tanganyika....mwenyeji wangu anaamka ananiambia karibu ikola Kijiji Cha maajabu..kimoyomoyo nikasema safari hii nimeuvagaa..,,ITAENDELEA.