Kijiji cha Kwikerege Chaamua Kujenga Zahanati Yake - Musoma Vijijini

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,897
941

KIJIJI CHA KWIKEREGE CHAAMUA KUJENGA ZAHANATI YAKE

Kijiji cha Kwikerege ni moja ya vijiji vitatu (3) vya Kata ya Musanja.

Kijiji hiki hakina zahanati, kwa hiyo wakazi wake wanapohitaji Huduma za Afya wanalazimika kutembea umbali usiopungua kilomita tano (5) kwenda kwenye Zahanati ya Kijiji jirani cha Rusoli.

Wananchi wameamua kujenga Zahanati ya kijiji chao.

Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo aliongozana na Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Musoma Vijijini (chini ya Mwenyekiti, Ndugu Denis Ekwabi) kwenda kupiga HARAMBEE ya ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Kwikerege.

Hali ya utoaji wa Huduma za Afya Jimboni mwetu iko hivi, tuna:

Hospitali ya Halmashauri
*Ina hadhi ya Hospitali ya Wilaya

Vituo vya Afya sita (6)
*Baadhi, vipya, vinasubiri kupewa wafanyakazi na vifaa tiba

Zahanati 44
*24 za Serikali
*4 za Binafsi
*16 zinajengwa

Tafadhali sikiliza CLIP/VIDEO kutoka Kijijini Kwikerege, Kata ya Rusoli - imeambatanishwa hapa

Usisahau kutembelea TOVUTI ya Jimbo letu ambayo ni:
www.musomavijijini.or.tz

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

Tarehe:
Jumapili, 1.10.2023

 
Back
Top Bottom