Nafaka
JF-Expert Member
- Feb 17, 2015
- 12,156
- 31,045
Kama kuna jambo linalolipa ukipatia ni game development. Basi mwaka 2012 kijana mmoja wa Vietnam aliyekuwa na umri wa miaka 25, akiwa kaanzisha kampuni yake ya kutengeneza magame ya simu ambayo mengi hayakuwa yamefanya vizuri maana yeye alikuwa anatengeneza games za 2D wakati dunia ilikuwa inahamia kwenye games za 3D, alitengeneza game kwa ajili ya iOS lijulikanalo kama Flappy bird. Lilikuwa game simple lakini ukianza kulicheza basi unakuwa addited.
Ndani ya game hilo lilijumuisha kugonga gonga screen ya simu ili kufanya ndege aliyekuwa anaruka akwepe vikwazo. Game hilo aliliwweka kwenye Apple Store lakini nalo halikupata watumiaji kwa miezi kadhaa, mara ghafla mwaka 2013 mwezi wa pili, watu walianza download gamehilo kwa kasi. Baada ya muda mchache game hilo ndiyo ikawa app inayoongoza kusownlodiwa.
Game likawa maarufu, na jamaa akawa maarufu watu wakaanza kumfuatilia twitter, vyombo vya habari vya nchi mbalimbali hasa Marekan vikawa vinaomba mahojiano lakini anagoma. Ikafika kipindi ikawa inakadiliwa kuwa anatengeneza dollar 50,000 kwa siku kutokana na matangazo yaliyomo kwenye game. Hii habari ilipotoka ndipo ikawa balaa. Huko kwao vietnam akawa star, hawezi tena kutoka nje, nyumba ya wazazi wake ambao mpaka muda huo hawakujua kuwa mtoto wao ni tajiri na mashuhuri ikavamiwa na mapaprazi. Ndipo wazazi kupata hizo habari.
Basi kijana akaanza kuwa na stress maana hakupenda huo umaarufu, akawa hawezi tena kuishi maisha yake ya kawaida. Wazazi wakaanza kuwa na wasiwasi na kijana wao. Vyombo vingine na watu walio na mtima nyongo wakawa wanasema Nitendo imfungulie mashitaka kwa kuiga mazingira ya game la super mario.
Kijana akaona isiwe tabu, akaandika twitter kuwa amechoshwa na umaarufu na maisha yake yalivyobadilika. Hivyo samahani sana, hilo game analiondoa maana halimpi furaha bali amenza kujuta kulitengeneza. Na kweli kesho yake flappy bird ikawa haipo tena Apple store.
Kijana akawa kimya wengine wakadai kajiua, kila mtu akawa anasema anachodhani. kumbe kijana alikuwa kachill tu.
Kwa sasa amerudi, anaendelea kutengeneza magame lakini hayapati ule umaarufu kama wa flapy bird. Anasema japo maisha yake hayako kama zamani lakini walau ana amani.
Bwan Don Guyen
Ndani ya game hilo lilijumuisha kugonga gonga screen ya simu ili kufanya ndege aliyekuwa anaruka akwepe vikwazo. Game hilo aliliwweka kwenye Apple Store lakini nalo halikupata watumiaji kwa miezi kadhaa, mara ghafla mwaka 2013 mwezi wa pili, watu walianza download gamehilo kwa kasi. Baada ya muda mchache game hilo ndiyo ikawa app inayoongoza kusownlodiwa.
Game likawa maarufu, na jamaa akawa maarufu watu wakaanza kumfuatilia twitter, vyombo vya habari vya nchi mbalimbali hasa Marekan vikawa vinaomba mahojiano lakini anagoma. Ikafika kipindi ikawa inakadiliwa kuwa anatengeneza dollar 50,000 kwa siku kutokana na matangazo yaliyomo kwenye game. Hii habari ilipotoka ndipo ikawa balaa. Huko kwao vietnam akawa star, hawezi tena kutoka nje, nyumba ya wazazi wake ambao mpaka muda huo hawakujua kuwa mtoto wao ni tajiri na mashuhuri ikavamiwa na mapaprazi. Ndipo wazazi kupata hizo habari.
Basi kijana akaanza kuwa na stress maana hakupenda huo umaarufu, akawa hawezi tena kuishi maisha yake ya kawaida. Wazazi wakaanza kuwa na wasiwasi na kijana wao. Vyombo vingine na watu walio na mtima nyongo wakawa wanasema Nitendo imfungulie mashitaka kwa kuiga mazingira ya game la super mario.
Kijana akaona isiwe tabu, akaandika twitter kuwa amechoshwa na umaarufu na maisha yake yalivyobadilika. Hivyo samahani sana, hilo game analiondoa maana halimpi furaha bali amenza kujuta kulitengeneza. Na kweli kesho yake flappy bird ikawa haipo tena Apple store.
Kijana akawa kimya wengine wakadai kajiua, kila mtu akawa anasema anachodhani. kumbe kijana alikuwa kachill tu.
Kwa sasa amerudi, anaendelea kutengeneza magame lakini hayapati ule umaarufu kama wa flapy bird. Anasema japo maisha yake hayako kama zamani lakini walau ana amani.
Bwan Don Guyen