mc gregor
JF-Expert Member
- Mar 17, 2017
- 1,121
- 2,194
Ukiona unawaza sana kusave hela ndo uwe tajiri ujue bado sana kutajirika hakuna tajiri duniani popote ambae hatumii pesa acheni kudanganyana mtaendelea kujinyima na kuishi kimaskini na bado hela msizione wangapi wanajinyima huku mitaani wanaishi kwa taabu na bado masikini??
Siri ya utajiri haipo kwenye kusave dogo bali ipo kwenye kuwekeza, ongeza vyanzo vyako vya mapato kila siku matajiri wanachowazidi masikini kama nyie wao wanawaza kuingiza pesa nyingi kuliko wanazotumia wakati masikini kama mtoa mada anawaza kukibania hiko kidogo alichonacho kimtoshe
Hakuna tajiri yoyote dogo anayeishi kwa kujibana au kimaskini unavyosema wewe labda utajiri wa ndumba
Siri ya utajiri haipo kwenye kusave dogo bali ipo kwenye kuwekeza, ongeza vyanzo vyako vya mapato kila siku matajiri wanachowazidi masikini kama nyie wao wanawaza kuingiza pesa nyingi kuliko wanazotumia wakati masikini kama mtoa mada anawaza kukibania hiko kidogo alichonacho kimtoshe
Hakuna tajiri yoyote dogo anayeishi kwa kujibana au kimaskini unavyosema wewe labda utajiri wa ndumba
utawezaje kuwekeza kama usipo kuwa na akiba, Akiba ni nini, ni kuweka sehemu ya ulichokipata kwa ajili ya kesho. Kwa sababu Bela haijawahi kutosha ndio pale tunapoita kujinyima, kuna vitu ambavyo sio vya msingi, ukijaribu kupunguza matumizi katika vitu hizo ndio itakapopatikana akiba ya ajili ya kesho yako kufanya mambo mbali mbali ikiwemo uwo uwekezaji unao uzungumzia.