Kijana auawa na kuporwa simu

Kijana auawa na kuporwa simu

Halafu wakianza kuuawa utasikia haki za binadamu wanakuja, Huwa sijui wanatetea haki za binadamu wa wapi?? Polisi msako uendelee
 
Kuna muda huwa nawaelewa mapolice, mijitu kama hii ikipigwa risasi ni sawa tu, ingawa kisheria na haki za binadamu si sawa ila inauma mno.... simu unamuua mtu.
 
Halafu wakianza kuuawa utasikia haki za binadamu wanakuja, Huwa sijui wanatetea haki za binadamu wa wapi?? Polisi msako uendelee
sema ukiua huwezi kuwa na uhakika je uliyemuua ndiye ama siye !! na ukiruhusu hivyo Askari anaweza kutumia mwanya huo kuua kwa sababu zake zingine afu akasema jambaz sugu.
 
Mkazi wa Mwananyamala, Manjunju mkoani Dar es Salaam, Billal Hoza (21), amefariki dunia baada ya kuvamiwa na kundi la vijana waliomchoma kisu sehemu mbalimbali za mwilini na kumpora simu.

Vijana hao wapatao watano walimvamia kijana huyo aliyekuwa amekaa nje ya nyumba yao na kumchoma kisu mgongoni, upande wa moyo. Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo lililotokea juzi saa 3:30 usiku, wakati Hiza na rafiki yake wakiwa wamekaa barazani nyumbani kwao, wakichezea simu.

“Wakati wanachezea simu walipita vijana kama wanne, kati yao mmoja akamfuata huyu kijana (Hoza) akampokonya simu, akaendelea kutembea na wenzake, ndipo Hoza akamfuata, akambana na kumtupa chini na mmoja wao akatoa kisu na kumchoma."
Ni kisasi hiki.
 
Unamuua binadamu mwenzako kisa simu mali yake.
Bongo ni hatari mzee na uhatari wake hatuna vifaa vya kuwabaini hao wezi ni bahatisha bahatisha tuu na wezi wengi wanajua kuwa wanaowafanyia umafia hawana siraha yeyote ndio maana tunasikia haya matukio na wenye siraha pana vipengele vya kuwabana hata wakitumia siraha zao..itokee mtu awafyatue panya road watano utasikia kaua kisa simu kumbe mtu alikua anaokoa maisha yake sio simu..
 
Kwa sasa watakuwa wametorokea mikoani kujificha
Iringa ikiwemo! Juzi nilikuwa huko, nikalala maeneo ya barabara 2, asubhi natoka kuwahi stendi nikakatiza nyuma maeneo hilo ghorofa la hapo stendi ya zamani walivyokuwa wamejazana almanusra nitimue mbio. Wako busy wanavuta mimoshi yao tu
 
Taarifa kama hizi huwezi kumuona Abdul Nondo na watetezi wengine WA Haki za binadamu.


Wahuni Dawa Yao ni Risasi tu

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom