Saint Ivuga
JF-Expert Member
- Aug 21, 2008
- 54,363
- 58,386
[h=2] KIGWANGALLA: serikali isipofanya kweli NAJIUZULU[/h] By TZA | October 27, 2011 | HARD NEWS | No comments
mbungwa wa Nzega, Khamis Kigwangalla.
Mbunge wa NZEGA Tabora, Khamis Kigwangalla amesema amedhalilishwa sana kutokana na mkuu wa polisi wilaya ya Nzega, kumuweka ndani na kumnyanyasa, kumnyima nafasi ya kuwapigia simu ndugu zake, kutomruhusu aonane na watu, baada ya fujo kutokea wakati alipokwenda kusuluhisha ugomvi wa wananchi wake na wawekezaji kwenye mgodi wa madini.
Kigwangalla amesema kama tatizo hilo halitatuliwa, au yeye kusikilizwa ATAJIUZULU Ubunge kwa sababu hataki kuendelea kuwa chini ya mfumo ambao unadhulumu na kukandamiza wanyonge.
amesema amehuzunishwa pia kufikishwa mahakamani kwa sababu ktk maisha yake yote, hajawah kuingia kwenye mgogoro na sheria .
VURUGU kubwa zilitokea kati ya wachimbaji wadogowadogo na wawekezaji wadogo kwenye Mgodi wa Dhahabu wa Isungangwanda uliopo Kijiji cha Mwabangu, Kata ya Nata wilayani Nzega, Tabora walipokuwa wakigombea kitalu ambapo Watu kadhaa walijeruhiwa.
Wachimbaji wawili wadogo walijeruhiwa na gari la Mbunge huyo Dk Hamisi Kigwangalla kuvunjwa kioo cha mbele.
chanzo cha mgogoro huo ni wawekezaji kuingilia eneo la wakazi wa kijiji hicho huku akiacha eneo lake ambalo amekuwa akilimiliki kwa muda mrefu, mgogoro ambao umedumu kwa muda mrefu na Serikali ya Wilaya imeshindwa kuutatua.
Kigwangalla alifika kwenye hicho kijiji baada ya kupata taarifa kuwa wawekezaji hao wana mpango wa kufanya vurugu dhidi ya wachimbaji wadogowadogo ambao wamekuwa wakimiliki eneo hilo kwa muda mrefu ambapo mbunge huyo aliwataka wananchi pamoja na wachimbaji kuwa watulivu wakati wa kutafuta suluhu ya tatizo hilo, jitihada ambazo hazikufanikiwa, ambapo pande hizo mbili zilianza kushambuliana.
source.millardayo.com
mbungwa wa Nzega, Khamis Kigwangalla.
Mbunge wa NZEGA Tabora, Khamis Kigwangalla amesema amedhalilishwa sana kutokana na mkuu wa polisi wilaya ya Nzega, kumuweka ndani na kumnyanyasa, kumnyima nafasi ya kuwapigia simu ndugu zake, kutomruhusu aonane na watu, baada ya fujo kutokea wakati alipokwenda kusuluhisha ugomvi wa wananchi wake na wawekezaji kwenye mgodi wa madini.
Kigwangalla amesema kama tatizo hilo halitatuliwa, au yeye kusikilizwa ATAJIUZULU Ubunge kwa sababu hataki kuendelea kuwa chini ya mfumo ambao unadhulumu na kukandamiza wanyonge.
amesema amehuzunishwa pia kufikishwa mahakamani kwa sababu ktk maisha yake yote, hajawah kuingia kwenye mgogoro na sheria .
VURUGU kubwa zilitokea kati ya wachimbaji wadogowadogo na wawekezaji wadogo kwenye Mgodi wa Dhahabu wa Isungangwanda uliopo Kijiji cha Mwabangu, Kata ya Nata wilayani Nzega, Tabora walipokuwa wakigombea kitalu ambapo Watu kadhaa walijeruhiwa.
Wachimbaji wawili wadogo walijeruhiwa na gari la Mbunge huyo Dk Hamisi Kigwangalla kuvunjwa kioo cha mbele.
chanzo cha mgogoro huo ni wawekezaji kuingilia eneo la wakazi wa kijiji hicho huku akiacha eneo lake ambalo amekuwa akilimiliki kwa muda mrefu, mgogoro ambao umedumu kwa muda mrefu na Serikali ya Wilaya imeshindwa kuutatua.
Kigwangalla alifika kwenye hicho kijiji baada ya kupata taarifa kuwa wawekezaji hao wana mpango wa kufanya vurugu dhidi ya wachimbaji wadogowadogo ambao wamekuwa wakimiliki eneo hilo kwa muda mrefu ambapo mbunge huyo aliwataka wananchi pamoja na wachimbaji kuwa watulivu wakati wa kutafuta suluhu ya tatizo hilo, jitihada ambazo hazikufanikiwa, ambapo pande hizo mbili zilianza kushambuliana.
source.millardayo.com