KIGWANGALLA: Serikali isipofanya kweli NAJIUZULU

Saint Ivuga

JF-Expert Member
Aug 21, 2008
54,363
58,386
[h=2] KIGWANGALLA: serikali isipofanya kweli NAJIUZULU[/h] By TZA | October 27, 2011 | HARD NEWS | No comments
mbungwa wa Nzega, Khamis Kigwangalla.

Mbunge wa NZEGA Tabora, Khamis Kigwangalla amesema amedhalilishwa sana kutokana na mkuu wa polisi wilaya ya Nzega, kumuweka ndani na kumnyanyasa, kumnyima nafasi ya kuwapigia simu ndugu zake, kutomruhusu aonane na watu, baada ya fujo kutokea wakati alipokwenda kusuluhisha ugomvi wa wananchi wake na wawekezaji kwenye mgodi wa madini.

Kigwangalla amesema kama tatizo hilo halitatuliwa, au yeye kusikilizwa ATAJIUZULU Ubunge kwa sababu hataki kuendelea kuwa chini ya mfumo ambao unadhulumu na kukandamiza wanyonge.
amesema amehuzunishwa pia kufikishwa mahakamani kwa sababu ktk maisha yake yote, hajawah kuingia kwenye mgogoro na sheria….
VURUGU kubwa zilitokea kati ya wachimbaji wadogowadogo na wawekezaji wadogo kwenye Mgodi wa Dhahabu wa Isungangwanda uliopo Kijiji cha Mwabangu, Kata ya Nata wilayani Nzega, Tabora walipokuwa wakigombea kitalu ambapo Watu kadhaa walijeruhiwa.
Wachimbaji wawili wadogo walijeruhiwa na gari la Mbunge huyo Dk Hamisi Kigwangalla kuvunjwa kioo cha mbele.
chanzo cha mgogoro huo ni wawekezaji kuingilia eneo la wakazi wa kijiji hicho huku akiacha eneo lake ambalo amekuwa akilimiliki kwa muda mrefu, mgogoro ambao umedumu kwa muda mrefu na Serikali ya Wilaya imeshindwa kuutatua.
Kigwangalla alifika kwenye hicho kijiji baada ya kupata taarifa kuwa wawekezaji hao wana mpango wa kufanya vurugu dhidi ya wachimbaji wadogowadogo ambao wamekuwa wakimiliki eneo hilo kwa muda mrefu ambapo mbunge huyo aliwataka wananchi pamoja na wachimbaji kuwa watulivu wakati wa kutafuta suluhu ya tatizo hilo, jitihada ambazo hazikufanikiwa, ambapo pande hizo mbili zilianza kushambuliana.
source.millardayo.com
 
Hakuna picha hapa... anazani nai atasikiliza vijitisho vyake?
Ajiuzulu ale nyasi...
 
Hajajiuzulu bado Bashe yuko wapi amsaidie kumfahamisha jinsi ya kujiuzulu. Magamba bana tabu tupu aende huko anatafuta umaarufu wa kizamani.
 
Kigwangalla amesema kama tatizo hilo halitatuliwa, au yeye kusikilizwa ATAJIUZULU Ubunge kwa sababu hataki kuendelea kuwa chini ya mfumo ambao unadhulumu na kukandamiza wanyonge. Amesema amehuzunishwa pia kufikishwa mahakamani kwa sababu ktk maisha yake yote, hajawah kuingia kwenye mgogoro na sheria….

Hon Kigwangalla;

I am sorry to let you know that you are very lucky! I will xplain this!!

1. What they did to you .. its our daily routine .. that is our daily life .. its living

2. Now you know the real situation .. yes .. not the laboratory tests ..Its what is happening in the real time and space in the filled!

3. This is great opportunity in that .. you can ACT ..basing on Reality and true xprience..

Having saying that: Now should not go anywhere other than staying n your post and work for your people!!
 
Karibu kwenye ulimwengu halisi, hivi hawa wajamaa walivyokua wakiona wabunge wa CDM wanapigwa virungu na kuswekwa ndani walidhani wao hawako bongo,? yalikua hayawahusu? leo anasema hataki kua kwenye mfumo unaodhulumu na kukandamiza wanyonge baada ya kuionja hali halisi, awe tayari maana akijiuzulu ajue kashkashi ndio zitaanza rasmi asije akataka kujiuzulu kiuhai hapo baadae (joking) Mh bila nyinyi sisiem tusingefika hapa tulipo.
 
Ahhh bwana mdogo Khamisi Kigwangalla!!! Naona UNATISHIA NYAU!!!!!!! Ujiuzuru WAPI??? UHESHIMIWA MTAMU BANA, Malaria tu Unapanda Pipa INDIA, hebu jaribu kujiuzuru uone kama hata ukivunjika mgongo uone kama utapelekwa hata muhimbili private ward kama sio holini mwaisela tena wagonjwa watatu kitandani??? Weeeee Usijaribu kabisa. Waulize Akina Lema wa CDM, mbona hiyo ndio daily life yao?????
 
Akijiuzulu halafu atakula na kutanua wapi? Opportunisty will awalys ramain an opportunisty!!! ameaona kuna mwelekeo wa nguvu ya "umma" kushinda 2015 ndio maaana anacheza kote kote.... Ni popo huyo!! but at least anakiri kuwa CCM and co ni washenzi lakini bado yupo kule kwa posho n other benefits.... Anajua akisema anaacha Ubunge na gharama na ushenzi ambao MAGAMBA (yeye akishiriki na kujua) wameingia kwa uchaguzi wa Igunga tu, jamaa zake wa magamba hawatakubali maana this time HATA WAKIUA WAPIGA KURA WOTE HAWAWEZI KUSHINDA NZEGA ndio maana anatikisa kiberitu ilinae awe somehow MORE RECOGNISED!!!
 
Ahhh Dr. Ongea kama Dr halisi, tupe KPIs za statement yako ambazo ni tangible, unatoa muda gani kwa Serikali?
 
Just a word of advice to you Mr Mp.....this ain't no time of speaking louder, but to act louder.
My question to you as people's representative and prolific academician with incontestable tertiary academy qualifications, have even tried to jot down and submit your concerns to the authorities? or it's just a another Political Panorama?
 
Just a word of advice to you Mr Mp.....this ain't no time of speaking louder, but to act louder.
My question to you as people's representative and prolific academician with incontestable tertiary academy qualifications, have even tried to jot down and submit your concerns to the authorities? or it's just a another Political Panorama?

Mchumia tumbo huyo
 
Kwanini ujiuzulu na umechaguliwa na wananchi. If anything mwanzo wa vita ndio umeanza, sasa wewe kama kiongozi unataka kuweka silaha chini kukaacha wanajeshi (wananchi) wako vitani? Nani alikuambia kupigania haki ya mnyonge ni kazi rahisi? However, this might be a wake up call for you i.e. wakati wakufikiria kwa undani kama kweli politics is the right thing for you or medical field. Otherwise jiandae tu Mh. the road ahead is more likely to be more challenging.
 
Hakuna picha hapa... anazani nai atasikiliza vijitisho vyake?
Ajiuzulu ale nyasi...

Pamoja na kwamba naamini hawezi kujiuzulu, Hamisi sio mtu wa kushindwa kuishi asipokua mwanasiasa, he is well covered and to be he is better off a business man than a politician

Nasikitika sana, kwasababu nashidnwa kumuamini Hamis, kwani angekua reliable, he is a very good fighter, ni ule unafiki wa kisiasa ndio unaonisumbua kwa huyu mdogo wangu
 
Ama kweli,nyani haoni .........Sasa wewe Kigwangalla unasubiri nini tena wakati serikali imeshafanya kweli kwa kukuweka ndani tena chini ya ulinzi,ila madaraka matamu nyie acha tu,fanya maamuzi magumu,tatizo ni huo ubongo wako kung'ang'ania ubunge wako,nenda ubungo upate ushauri wa kazi ya kufanya.Asante kwa kuunga mkono hoja,wanaoafiki waseme ndio,wasioafiki waseme sio.
 
Karibu chadema ndiko kwenye wapiganaji. CCM wanatetea ufisadi na mafisadi hivyo ukiwatetea wanyonge unakuwa adui wao
 
Hamisi my friend is it possible if we can meet and relieve your headache. This is the really homy boy and this is what the rest of the people not called waheshimiwa experience every day called today. Polle sana.
 
Just a word of advice to you Mr Mp.....this ain't no time of speaking louder, but to act louder.
My question to you as people's representative and prolific academician with incontestable tertiary academy qualifications, have even tried to jot down and submit your concerns to the authorities? or it's just a another Political Panorama?

Huwezi kupigana vita ya kweli kudai haki ukiwa magamba. Karibu huku wapo wapiganaji wa kweli-zito,tundu lisu, lema
 
Back
Top Bottom