Kigoma yaanza kufunguka

Kigoma yaanza kufunguka

Kumbe nawe ni mhenga. Ulikuwa ukisubiri basi la kurudi kwa wiki nzima. Halafu Barabara ya Kasulu Kibondo ilikuwa ni tabu sana. Mvua ikinyesha, utelezi na wakati wa kiangazi poda (vumbi). Kama sasa ni lami lazima Quinine , pamoja na ubishi wake, akubali kuna maendeleo (bila kusahau kuwa Magu kiboko ya njia) therefore maendeleo ni infrastructure. Mtu akitoka ulaya haangalii kama kuna mikutano au Lissu kapigwa shaba au Kabendera yupo ndani au Mbowe ananyimwa kibali cha kuhutubia; anaangalia infrastructure then anaconclude kuwa hii nchi aidha imeendelea au la.
Watu mna maneno!
 
Binafsi maendeleo ya miundombinu nayaona manispaa ya kigoma tu, huko kwingine (wilayani) bado sana.
 
Hivi Maruzuku Khamisi, aliacha warithi wa kuendesha biashara yake ya usafiri?
Maruzuku Khamis alikuwa kati ya matajiri kanda ya ziwa, akishindana na mwarabu mmoja aliyeitwa Shariff Mohamed na kaka zake.
 
Fika na ujiji na kibirizi ujionee mradi mkubwa wa bandari, fika ujiji na uvinza ujionee miradi mikubwa ya maji, pia upo mradi mkubwa wa barabara kutoka kabingo mpaka manyovu unaenda Burundi kilometres zaidi ya 200 mradi utaanza muda wowote sababu pesa tayari zipo, gridi ya taifa inakuja mkandarasi yupo njiani, SGR nayo inakuja, serikali imepanua kilimo cha michikichi huko Kigoma kwa maelfu ya mahekari.

Msipomshukuru JPM mtakua wehu. Hata kama ni kodi zenu lakini sio peke yenu wenye uhitaji wa Miundombinu yote hii kwa wakati mmoja.
Naam tutakuwa na mapepo kabisa
 
Muongo wewe hiyo barabara ya kasulu - Kibondo- kakonko ni vumbi tupu na sidhani kama itawekwa lami.. Maana ile lami ya kuanzia nyakanaz kuja kibondo imeanza kupigwa lami kuanzia mwaka 2012 ila mpaka sasa haijafika hata kakonko ... Sasa sijui unazungumzia kigoma IPI..


Kigoma iliyoendelea ni Kigoma Municipality tu kasulu na kibondo bado wako kwenye medieval era .. Naongea kwasababu nimeishi maeneo yote ya Kigoma ... Halafu hiyo kasulu na kibondo ndio kuna mawaziri kama Ndalichako, waziri mpango , naibu waziri wa habari .. Kigoma mjini haijawahi kutoa waziri lakini ina maendeleo kushinda huko kibondo na kasulu .. Wameanza kutoa mawaziri miaka na miaka ... Kibondo na kasulu wamejaa wajinga sana sijui kama wataendelea wale ...



Unapoitaja Kigoma uwe specific kabisa kuwa kuna Kigoma mjini na hizo takataka zingine
Utakuwa unatoka ujiji bilashaka
 
sasa Kuna maana gani ya kukomaa na kitu ambacho hakiishi? Huoni kama ni kupoteza fedha zaidi? Kwa Kama ni pesa za ndani ndio ziendelee kutolewa tu kwa Kazi isiyoonesha mwisho wake? Nadhani wangeweka fungu la kutosha na kumakiza project moja kwa ukamilifu kisha wanaanza nyingine kuliko kujificha kwenye hoja ya NI FEDHA ZA ndani. Kwa hiyo zenyewe hazfai kukamilisha? Na kwa nini kila miaka hizi tender ni kwa Nyazroad ? Huku ni failure wakubwa?
Fedha inayotolewa ni kidogo sana,serikali hainaga utaratibu wa kutoa pesa yote kwa pamoja kwa miradi mikubwa badala yake huwa inatolewa kila mwaka hadi project inaisha labda iwe mkopo ndio pesa inaweza kuwa yote ipo
Hayo ya tender waulize Tanroads na wizara
 
Pongezi hapana, hayo yote tuliyastahili lakini maksudi viongozi wakatufanyia mtima nyongo
Japo mama alikuwa na wajibu wake wa kukupikia na kuhakikisha kuwa umekula lakini tulifundishwa kusema asante kwa chakula. Kupongeza na kushukuru ni tabia njema na haidhuru hata kama ulistahili kufanyiwa... Je, ni mara ngapi umejisikia vizuri ulivyopongezwa kwa jambo ambalo lilikuwa ni waljibu wako kulitenda, kwa mfano kufaulu masomo darasani..
 
Kilichoandikwa ni Ukweli serikali kuanzia ya Kikwete ilianza kuonyesha kigoma ni sehemu ya Tanzania.Nililala Siku mbili kigoma na nikagundua kigoma kuna chakula kingi na bei chini kushinda Mbeya nilipopazoea bidhaa nusu bei Kigoma ni Robo bei. Tatizo ukienda kigoma kuna beria ni nyingi sana
 
Tanzania yote ina haki ya kuwa na maendeleo.

Nilimuelewa JPM alipoweka mkazo wa kuhamia Dodoma. Anatenganisha serikali na wafanyabiashara.

Pia anaiweka serikali mahali inapoweza kufikiwa na kila mtanzania.
 
Kilichoandikwa ni Ukweli serikali kuanzia ya Kikwete ilianza kuonyesha kigoma ni sehemu ya Tanzania.Nililala Siku mbili kigoma na nikagundua kigoma kuna chakula kingi na bei chini kushinda Mbeya nilipopazoea bidhaa nusu bei Kigoma ni Robo bei. Tatizo ukienda kigoma kuna beria ni nyingi sana
Kila sehemu unakutana na askari wa uhamiaji, unaulizwa kitambulisho mpaka kero
 
Barabara ya Simbo Ilagala mpaka Kalema Rukwa ni ya muhimu sana kwa uchumi wa watu wa kusini lakini haizungumziwi popote na wabunge wote wawili wa eneo hili nikama hawapo.
 
Kanyonza Vs kibonge. Barabara ya nyakanazi ina zaidi ya miaka kumi haiishagi na mkandarasi Nyanzaroad yuko site anakumbatiwa tu.
2014 gari ikifika nyakanazi from KGM gari zima vumbi tupu..
Watu wanadhambi kweli hadi Leo haijaisha!
 
Barabara ya Simbo Ilagala mpaka Kalema Rukwa ni ya muhimu sana kwa uchumi wa watu wa kusini lakini haizungumziwi popote na wabunge wote wawili wa eneo hili nikama hawapo.
Siku hizi Kalema ni Katavi sio Rukwa tena kama zamani
 
Visasi vyaweza kuwepo iwapo kuna watu wanaona kazi unayofanya ni ya hovyo!!inatia hasira.ndo maana Mungu aliamua kumfukuza Shetani na malaika zake kwa kosa LA kuanza kuona kazi na sheria za Mungu ni za hovyo! Watu wa hovyo ni mbora wasiwepo
"---watu wa hovyo". Ni akina nani hawa!
Nani ana mamlaka ya kuhukumu na kuwaweka pembeni hawa 'watu wa hovyo'; mwenye madaraka (vyombo vya dola, au wananchi wenye uwezo wa kuamua nani awe kiongozi wao?
 
Back
Top Bottom