Kigoma yaanza kufunguka

Kigoma yaanza kufunguka

Ujenzi wa barabara hizi (Kahama-Kibondo-Kasulu) na Tabora-Uvinza zinafanywa kisiasa mnoo in my opinion. Yaani zinakwenda kwa mwendo wa kinyonga. Bila shaka mwakani zitatumika kwenye kampeni. Ombeni Mungu japo ziishe before 2025.
Yaani wanazingua ni shida licha ya kuwa na mawaziri senior lakini ni bure kabisa imagine barabara ya mpanda Tabora ina wakandarasi 3 na itakamilika kabla ya hizo zilizoanza awamu iliyopita,mwaka huu mpanda wanapata umeme wa grid huko haieleweki.Katavi kuna waziri mmja tu wa ujenzi wao wana mawaziri 3 lakini hakuna wanachosaidia
 
Kanyonza Vs kibonge. Barabara ya nyakanazi ina zaidi ya miaka kumi haiishagi na mkandarasi Nyanzaroad yuko site anakumbatiwa tu.
Mkuu ukiona hivyo jua ni ujenzi wa pesa za ndani yaani za madafu hapo tatizo sio mkandarasi bali mtoa pesa hata huku Swax barabara ya swax kasanga toka 2009 mchina yuko site haiishagi wakati ni 115 km tu labda mwaka huu itaisha wako hatua za mwisho napo ni kwa msukumo binafsi wa waziri wa ujenzi kufanya lobbying maana ni mtu wa Katavi vinginevyo.
Hiyo road uliyoisema haiishi leo au kesho maana hata bajeti yake ni kiduchu sana
 
Asante sana kwa habari..adventure na saratoga za juzi hizo..kulikuwa na ..superstar..kanyonza..kibodeco..maruzuku..kiganza ..mgalaganza..hey few to mention
Zamani kulikuwa na basi mara moja kutoka Mwanza hadi kigoma wakati nikienda kinonko shule ya msingi pale kakonko 1980, tumshukuru anayepigwa vita na akina Quinine na BAK . Nasisitiza maendeleo ni infrastructure tu, vingine vikolombwezo
 
Kwa hiyo Tanzania inapiga hatua kwenda mbele au sio?

Nilisoma kwa makini andiko lako, nikitegemea kuona 'lawama' na 'pongezi' vikiegemea ulipo ushabiki, lakini sikuona; ndio maana andiko lako likawa la kupendeza kulisoma.

Umeandika kuhusu Kigoma, lakini wapo wengine wanaoweza kuandika mambo yalivyobadilika sehemu nyingine ndani ya Tanzania hii, si katika miundombinu tu, lakini pia katika mambo mengine ya msingi zaidi kama elimu, na kilimo.

Natumaini siku moja utapata fursa ya kutueleza hali ya elimu ya waTanzania hapo Kigoma imebadilika kiasi gani

Wakati tukisherehekea haya uliyoweka hapa, tusisahau mshikamano wetu waTanzania. Ni tunu iliyotutambulisha duniani kote. Ujenzi wa haya m'mavitu' yote yasiwe ndio iwe bei ya kuipoteza tunu hiyo. Haya mavitu tunaweza kuyajenga bila ya lazima ya kuwekeana visasi na kuoneana. Kwa hakika ujenzi huo utakuwa wa furaha sana tukiutekeleza bila ya kuvunja haki za mTanzania yeyote. Na kama ilivyo kawaida, uhalifu unapojitokeza, sheria iachwe ifanye kazi yake bila ya kuipindisha.
Visasi vyaweza kuwepo iwapo kuna watu wanaona kazi unayofanya ni ya hovyo!!inatia hasira.ndo maana Mungu aliamua kumfukuza Shetani na malaika zake kwa kosa LA kuanza kuona kazi na sheria za Mungu ni za hovyo! Watu wa hovyo ni mbora wasiwepo
 
Fika na ujiji na kibirizi ujionee mradi mkubwa wa bandari, fika ujiji na uvinza ujionee miradi mikubwa ya maji, pia upo mradi mkubwa wa barabara kutoka kabingo mpaka manyovu unaenda Burundi kilometres zaidi ya 200 mradi utaanza muda wowote sababu pesa tayari zipo, gridi ya taifa inakuja mkandarasi yupo njiani, SGR nayo inakuja, serikali imepanua kilimo cha michikichi huko Kigoma kwa maelfu ya mahekari.

Msipomshukuru JPM mtakua wehu. Hata kama ni kodi zenu lakini sio peke yenu wenye uhitaji wa Miundombinu yote hii kwa wakati mmoja.
 
Muongo wewe hiyo barabara ya kasulu - Kibondo- kakonko ni vumbi tupu na sidhani kama itawekwa lami.. Maana ile lami ya kuanzia nyakanaz kuja kibondo imeanza kupigwa lami kuanzia mwaka 2012 ila mpaka sasa haijafika hata kakonko ... Sasa sijui unazungumzia kigoma IPI..


Kigoma iliyoendelea ni Kigoma Municipality tu kasulu na kibondo bado wako kwenye medieval era .. Naongea kwasababu nimeishi maeneo yote ya Kigoma ... Halafu hiyo kasulu na kibondo ndio kuna mawaziri kama Ndalichako, waziri mpango , naibu waziri wa habari .. Kigoma mjini haijawahi kutoa waziri lakini ina maendeleo kushinda huko kibondo na kasulu .. Wameanza kutoa mawaziri miaka na miaka ... Kibondo na kasulu wamejaa wajinga sana sijui kama wataendelea wale ...



Unapoitaja Kigoma uwe specific kabisa kuwa kuna Kigoma mjini na hizo takataka zingine
 
Hivi nani alaumiwe na nani tumpongeze kwa hili la kigoma?
 
Yaani wanazingua ni shida licha ya kuwa na mawaziri senior lakini ni bure kabisa imagine barabara ya mpanda Tabora ina wakandarasi 3 na itakamilika kabla ya hizo zilizoanza awamu iliyopita,mwaka huu mpanda wanapata umeme wa grid huko haieleweki.Katavi kuna waziri mmja tu wa ujenzi wao wana mawaziri 3 lakini hakuna wanachosaidia
Hapo ndipo tunapokosea, ni kweli Magufuli kateua seniors minister wawili toka Kigoma, lakini mawazili ni wa Watanzania yote na hawapaswi kuwa wabinafsi kwa kupeleka miradi nyumbani kwao.
Prof Mbwiliza alishawahi kuwa waziri hakujipendelea na Mporogomyi nae alishawahi kuwa naibu waziri wa fedha wakatie wa serikali ya Mkapa lakini hakujipendelea kwa chochote kwani Manyovu na Muyama kulibaki kama pangoni.
Watu wa Kigoma wana uzalendo wa kupenda Watanzania wenzao bila kujipendelea.
 
Kwa hiyo Tanzania inapiga hatua kwenda mbele au sio?

Nilisoma kwa makini andiko lako, nikitegemea kuona 'lawama' na 'pongezi' vikiegemea ulipo ushabiki, lakini sikuona; ndio maana andiko lako likawa la kupendeza kulisoma.

Umeandika kuhusu Kigoma, lakini wapo wengine wanaoweza kuandika mambo yalivyobadilika sehemu nyingine ndani ya Tanzania hii, si katika miundombinu tu, lakini pia katika mambo mengine ya msingi zaidi kama elimu, na kilimo.

Natumaini siku moja utapata fursa ya kutueleza hali ya elimu ya waTanzania hapo Kigoma imebadilika kiasi gani

Wakati tukisherehekea haya uliyoweka hapa, tusisahau mshikamano wetu waTanzania. Ni tunu iliyotutambulisha duniani kote. Ujenzi wa haya m'mavitu' yote yasiwe ndio iwe bei ya kuipoteza tunu hiyo. Haya mavitu tunaweza kuyajenga bila ya lazima ya kuwekeana visasi na kuoneana. Kwa hakika ujenzi huo utakuwa wa furaha sana tukiutekeleza bila ya kuvunja haki za mTanzania yeyote. Na kama ilivyo kawaida, uhalifu unapojitokeza, sheria iachwe ifanye kazi yake bila ya kuipindisha.
Acha maneno ya kisiasa siasa..
 
Kuna wakati huwa nawaza na kufikiria nyuma kidogo naanza kufurahi. Miaka ishirini iliyopita Kigoma ilikuwa kama si sehemu ya Tanzania.

Umeme ulikuwa makao makuu tu ya mkoa yaani Kigoma Ujiji. Tena ukiwaka mara mbili tu kwa wiki.

Nilikuwa najua ratiba ya umeme kuwaka kuanzia Gungu, Masanga, SIDO, Mwanga sokoni,Kibilizi, Katubuka, Mlole,Majengo na Kilimahewa. Waliokuwa na uhakika wa umeme ni mjini kati na Mji mwema kwakuwa kule waliishi wanene.

Kutoka Kigoma kwenda Kasulu na Kibondo ilikuwa ni Safari ya kutwa nzima na mabasi yetu ya Adventure na Saratoga za wakati ule.

Kutoka Kigoma kwenda Manyovu na Muyama hakukuwa na mabasi bali magari ya mizigo tena ya kuvizia.

Kasulu pamoja na kuwa Mji mkubwa zilitawala kalabai, chemli na vibatali tu,huku Kibondo ikiwa kama mji wa kale wa enzi za ustaarabu wa Kichina yaani China Dynasty.

Hakuna aliyepangiwa kufanya kazi Kigoma aliyekubali kirahisi.

Sasa Kigoma imenza kuwa sehemu nzuri sana kwa kuishi. Barabara ya kuiunganisha na Tabora itakamilika muda si mwingi.

Hata ile ya kuiunganisha na Nyakanazi inaenda vizuri nimepita pale mpakani na mkoa wa Kagera daraja kubwa linajengwa na litaisha muda si mwingi.

Nimeona umeme ukiwaka kuanzia Kakonko, Kibondo yote,Kasulu na vijiji vyake,Heru juu,Kabanga, Muganza, Mwanga,Kasumo,Kalege, Muyama,Biharu,Nyamgali,Buhigwe,Muhaluro,Mnanila na kwingineko.

Mgao haupo tena,
Siku hizi hatusubirii tiketi za kulangua za train maana mabasi tele ya kwenda DSM,Mwanza,Bukoba,Arusha,Tabora,Mpanda na Sumbawanga.

Siku hizi kwenda Kasulu na Kibondo ni muda wowote.

Nimeona maji vijijini yakimwagika mitaani, barabara za vijijini zimeboreshwa sana.
Tunaweza kuwa tunaenda taratibu lakini tunasonga mbele.

Japo bado mkoa wote wa Kigoma tunatumia umeme wa generator lakini unatosheleza mahitaji ya umeme.

Kuishi kwingi ni kuona mengi, kuna vitu vimetokea mazingira yetu sikutarajia kama vingetokea nikiwa bado niko hai.

Mwezi uliopita nimekuta viguzo vya kuonyesha mwisho wa barabara vikiwa nyuma ya choo chetu badala ya kusikitika kwani nyumba yetu yote imeangukia kwenye hofadhi ya barabara lakini nilicheka kwa furaha kwani inawezekana nikaona barabara nzuri sana ya lami ikipita kijijini kwetu

And this happens once in life time.
Mungu nijalie nione mengi zaidi ambayo sikuyategemea kutokea nikiwa bado hai.
Nakumbuka miaka ya mwanzoni mwa 90 kuna jamaa mmoja alikuwa na Landover anaitwa Rombo kwa usafiri wa kutoka kigoma mjini mpaka manyovu huko..kweli hii nchi imetoka mbali.
 
Hapo ndipo tunapokosea, ni kweli Magufuli kateua seniors minister wawili toka Kigoma, lakini mawazili ni wa Watanzania yote na hawapaswi kuwa wabinafsi kwa kupeleka miradi nyumbani kwao.
Prof Mbwiliza alishawahi kuwa waziri hakujipendelea na Mporogomyi nae alishawahi kuwa naibu waziri wa fedha wakatie wa serikali ya Mkapa lakini hakujipendelea kwa chochote kwani Manyovu na Muyama kulibaki kama pangoni.
Watu wa Kigoma wana uzalendo wa kupenda Watanzania wenzao bila kujipendelea.
Hicho unachoongea wewe hakiendani na falsafa ya charity bigins at home,hii ndio inayoiongoza Tzn ever since
So brother mtachelewa sana ikiwa watu wenu hawaanzi na kwao na hakuna atakayewaona wamefanya jambo zaidi ya wa kwao.Wakati mikoa mingine inaweka lami barabara za mikoa Kigoma hakuna trunk road yoyote imekamilika kuunga na mkoa mwingine ukiacha ya Manyovu kwenda Burundi.
Mfano Dodoma,Arusha,Kilimanjaro,Iringa,Mwanza,Dar,Singida karibu barabara zote kuu za kuingia na kutoka ni lami..Mbeya,Morogoro,Njombe,Songea,Rukwa zimesalia barabara moja moja ili kumaliza mtandao wa lami wa barabara kuu
 
Kuna wakati huwa nawaza na kufikiria nyuma kidogo naanza kufurahi. Miaka ishirini iliyopita Kigoma ilikuwa kama si sehemu ya Tanzania.

Umeme ulikuwa makao makuu tu ya mkoa yaani Kigoma Ujiji. Tena ukiwaka mara mbili tu kwa wiki.

Nilikuwa najua ratiba ya umeme kuwaka kuanzia Gungu, Masanga, SIDO, Mwanga sokoni,Kibilizi, Katubuka, Mlole,Majengo na Kilimahewa. Waliokuwa na uhakika wa umeme ni mjini kati na Mji mwema kwakuwa kule waliishi wanene.

Kutoka Kigoma kwenda Kasulu na Kibondo ilikuwa ni Safari ya kutwa nzima na mabasi yetu ya Adventure na Saratoga za wakati ule.

Kutoka Kigoma kwenda Manyovu na Muyama hakukuwa na mabasi bali magari ya mizigo tena ya kuvizia.

Kasulu pamoja na kuwa Mji mkubwa zilitawala kalabai, chemli na vibatali tu,huku Kibondo ikiwa kama mji wa kale wa enzi za ustaarabu wa Kichina yaani China Dynasty.

Hakuna aliyepangiwa kufanya kazi Kigoma aliyekubali kirahisi.

Sasa Kigoma imenza kuwa sehemu nzuri sana kwa kuishi. Barabara ya kuiunganisha na Tabora itakamilika muda si mwingi.

Hata ile ya kuiunganisha na Nyakanazi inaenda vizuri nimepita pale mpakani na mkoa wa Kagera daraja kubwa linajengwa na litaisha muda si mwingi.

Nimeona umeme ukiwaka kuanzia Kakonko, Kibondo yote,Kasulu na vijiji vyake,Heru juu,Kabanga, Muganza, Mwanga,Kasumo,Kalege, Muyama,Biharu,Nyamgali,Buhigwe,Muhaluro,Mnanila na kwingineko.

Mgao haupo tena,
Siku hizi hatusubirii tiketi za kulangua za train maana mabasi tele ya kwenda DSM,Mwanza,Bukoba,Arusha,Tabora,Mpanda na Sumbawanga.

Siku hizi kwenda Kasulu na Kibondo ni muda wowote.

Nimeona maji vijijini yakimwagika mitaani, barabara za vijijini zimeboreshwa sana.
Tunaweza kuwa tunaenda taratibu lakini tunasonga mbele.

Japo bado mkoa wote wa Kigoma tunatumia umeme wa generator lakini unatosheleza mahitaji ya umeme.

Kuishi kwingi ni kuona mengi, kuna vitu vimetokea mazingira yetu sikutarajia kama vingetokea nikiwa bado niko hai.

Mwezi uliopita nimekuta viguzo vya kuonyesha mwisho wa barabara vikiwa nyuma ya choo chetu badala ya kusikitika kwani nyumba yetu yote imeangukia kwenye hofadhi ya barabara lakini nilicheka kwa furaha kwani inawezekana nikaona barabara nzuri sana ya lami ikipita kijijini kwetu

And this happens once in life time.
Mungu nijalie nione mengi zaidi ambayo sikuyategemea kutokea nikiwa bado hai.


Hizo unazoongea hapa ni KUFURU tupu, Kigoma inayo maendeleo gani ya kuja kadamnasi kutamba??!!,

Unataka "waleta maendeleo" waone mmeridhika na hicho kidogo mnachojivunia??!!, wewe hujui mnajiroga??
 
Zamani kulikuwa na basi mara moja kutoka Mwanza hadi kigoma wakati nikienda kinonko shule ya msingi pale kakonko 1980, tumshukuru anayepigwa vita na akina Quinine na BAK . Nasisitiza maendeleo ni infrastructure tu, vingine vikolombwezo
Maendeleo sio infrastructure ndugu is more than that.
 
Zamani kulikuwa na basi mara moja kutoka Mwanza hadi kigoma wakati nikienda kinonko shule ya msingi pale kakonko 1980, tumshukuru anayepigwa vita na akina Quinine na BAK . Nasisitiza maendeleo ni infrastructure tu, vingine vikolombwezo
TANGANYIKA BUS
 
TANGANYIKA BUS
Kumbe nawe ni mhenga. Ulikuwa ukisubiri basi la kurudi kwa wiki nzima. Halafu Barabara ya Kasulu Kibondo ilikuwa ni tabu sana. Mvua ikinyesha, utelezi na wakati wa kiangazi poda (vumbi). Kama sasa ni lami lazima Quinine , pamoja na ubishi wake, akubali kuna maendeleo (bila kusahau kuwa Magu kiboko ya njia) therefore maendeleo ni infrastructure. Mtu akitoka ulaya haangalii kama kuna mikutano au Lissu kapigwa shaba au Kabendera yupo ndani au Mbowe ananyimwa kibali cha kuhutubia; anaangalia infrastructure then anaconclude kuwa hii nchi aidha imeendelea au la.
 
Mkuu ukiona hivyo jua ni ujenzi wa pesa za ndani yaani za madafu hapo tatizo sio mkandarasi bali mtoa pesa hata huku Swax barabara ya swax kasanga toka 2009 mchina yuko site haiishagi wakati ni 115 km tu labda mwaka huu itaisha wako hatua za mwisho napo ni kwa msukumo binafsi wa waziri wa ujenzi kufanya lobbying maana ni mtu wa Katavi vinginevyo.
Hiyo road uliyoisema haiishi leo au kesho maana hata bajeti yake ni kiduchu sana
sasa Kuna maana gani ya kukomaa na kitu ambacho hakiishi? Huoni kama ni kupoteza fedha zaidi? Kwa Kama ni pesa za ndani ndio ziendelee kutolewa tu kwa Kazi isiyoonesha mwisho wake? Nadhani wangeweka fungu la kutosha na kumakiza project moja kwa ukamilifu kisha wanaanza nyingine kuliko kujificha kwenye hoja ya NI FEDHA ZA ndani. Kwa hiyo zenyewe hazfai kukamilisha? Na kwa nini kila miaka hizi tender ni kwa Nyazroad ? Huku ni failure wakubwa?
 
Kumbe nawe ni mhenga. Ulikuwa ukisubiri basi la kurudi kwa wiki nzima. Halafu Barabara ya Kasulu Kibondo ilikuwa ni tabu sana. Mvua ikinyesha, utelezi na wakati wa kiangazi poda (vumbi). Kama sasa ni lami lazima Quinine , pamoja na ubishi wake, akubali kuna maendeleo (bila kusahau kuwa Magu kiboko ya njia) therefore maendeleo ni infrastructure. Mtu akitoka ulaya haangalii kama kuna mikutano au Lissu kapigwa shaba au Kabendera yupo ndani au Mbowe ananyimwa kibali cha kuhutubia; anaangalia infrastructure then anaconclude kuwa hii nchi aidha imeendelea au la.
Unachosangaza unasahau hata Malaysia walikuwa kama sisi bado huoni tatizo, nakusikitikia sana, ukikua utajifunza kama tayari ni mtu mzima pole muda umeshakupita hutaelewa tena.
 
Back
Top Bottom