Kigamboni New City Master Plan

akili fupi za kusema nchi imeuzwa huwa sipendi hata kusikiliza. hata mlimani city mlipiga sana kelele kuwa tumeuza sehemu ya udsm, lakini sasaivi mmejaa pale kusukuma tolori zimejaa vitu mnavyonunua....watu kama ninyi ni wa kuwapuuzia tu, msema mlieee hadi mchoke, lakini kitu ambacho selikali inaona kuwa kinafaa, bora kifanyike tu.

kitu kingine, kuna watu wana alergy na wamarekani au westerners....wakisikia mradi unataka kufadhiliwa na watu wa magaribi, WANASEMA NCHI INAUZWA...kwasababu ya uranium, watu wanasema nchi inauzwa kwasababu watu wa magharibi wanaitaka...mlitaka waje waarabu?HAO WAARABU wakija na sisi tutasema nchi imeuzwa....na huwa inauzwa kama livyofanya MWINYI kwenye LOLIONDO, kule ndo kuuzwa..lakini kwa kigamboni, ni kitu kizuri na kitafanyika hata mkipiga kelele. hii nchi ya kwetu sote, na si kwasababu baadhi yenu hamuwapendi wa magaribi ndo sote tuko hivyo, na si kwamba kwasababu baadhi yenu mnawapenda waarabu na kupenda miradi yote tz ingekuwa chini ya waarabu kwamba sote tuko hivyo...mimi kwa upande wangu, mradi uwe wa magaribi au kiarabu naupokea tu..pamoja na kwamba kama ningesema nichague, ningesema waarabu waende zao huko na huwa siwaamini..hauwapendi wamagaribi na mimi sipendi kushirikiana na waarabu...na sote tunaishi kwenye nchi moja, sasa cha maana ni kuacha tu wote waje, waarabu, wachine, wahindi wazungu wote waje...na tuache kupiga makelele kuwa nchi imeuzwa.....mlitaka hiyo uranium anunue nani?waarabu iran?..hii inakera kusikiliza kwakweli...

Serikali gani/ipi itatekeleza mradi huu? Nyumba za waalimu zimewashinda, mradi wa mabasi hata harufu tu mpaka sasa hakuna! Daraja la kigamboni limeanza kuzungumziwa tangu lini? Mara flyovers Dar, Sembuse na kitu kikubwa namna hiyo? Hivi hamelewi nini kuhusu usanii wa CCM, kaahidi viwanja vya ndege na meli kubwa za kifahari kanda ya ziwa wakati akina mama wanaenda kujifungua kwa mikokoteni!!
Hakuna kitu kilichouzwa hapo, wala hakuna kitu kama Kigamboni New City! They are simply papers and bunch of models kuwadanganya wapiga kura!
 
The Blue Diamond of Tanzania- Kigamboni New City Plan 2011- 2030
Maeneo ya Vijibweni, Kibada, Mjimwema na Somangila ya Kigamboni kugeuzwa mji wa kisasa kabisa na hivyo wakaazi wa sasa Kigamboni kuupisha mji huo wa kisasa na kusukumizwa maeneo mengine.

Hii itatokana na ujenzi wa bandari mpya (New Port area), Exclusive schools for foreigners, Apartments and detached houses, central park n.k n.k Tizama clip hii ambayo mwisho kuna picha ya Mh. Rais J.M Kikwete imetiwa ndani ya hii clip, hivyo kutia uzito kuwa mradi huu ni wa serikali ya Tanzania.
 
Last edited by a moderator:
Mwananchi wa kigamboni zaidi ya kufukuzwa kwa kupewa vipesa kidogo unadhani atanufaika wapi na mradi wenyewe? kwa mbali utakuta wanufaikaji ni viongozi walio na share katika mradi wenyewe.
 
CCM wakikosa uchaguzi huu, sehemu ya Tanzania ya kigamboni haitauzwa kwa gaidi....
 
wee na akili zako zote uanfikiri huu mradi uatamalizika?
si kama ule wa mabasi yaendayo kasi tu, mpaka leo ni kitendawili......
mpaka kitukuu chako kinakufa hapo hakuna kigamboni city
 
wee na akili zako zote uanfikiri huu mradi uatamalizika?
si kama ule wa mabasi yaendayo kasi tu, mpaka leo ni kitendawili......
mpaka kitukuu chako kinakufa hapo hakuna kigamboni city

Dodoma kwenyewe hawajahamia miaka mingapi leo...? They should get the hell on up outta here...I'm not buying it...
 
Dodoma kwenyewe hawajahamia miaka mingapi leo...? They should get the hell on up outta here...I'm not buying it...

Dodoma ni mradi wa serikali lakini huu ni mradi wa matajiri ambao mpaka hatujatajiwa ni kina nani.....sidhani kama Govt inahusika zaidi ya kuwauzia hawo mabepari.....lakini tukiangali on bright side ni project nzuri kwa kuleta ajira lakini ikija kumalizika nadhani itakuwa ni NO go area kwa sisi WaTandika.
 
Dodoma ni mradi wa serikali lakini huu ni mradi wa matajiri ambao mpaka hatujatajiwa ni kina nani.....sidhani kama Govt inahusika zaidi ya kuwauzia hawo mabepari.....lakini tukiangali on bright side ni project nzuri kwa kuleta ajira lakini ikija kumalizika nadhani itakuwa ni NO go area kwa sisi WaTandika.

I'm still not buying it...but I'll believe it when I see it.
 
Dodoma ni mradi wa serikali lakini huu ni mradi wa matajiri ambao mpaka hatujatajiwa ni kina nani.....sidhani kama Govt inahusika zaidi ya kuwauzia hawo mabepari.....lakini tukiangali on bright side ni project nzuri kwa kuleta ajira lakini ikija kumalizika nadhani itakuwa ni NO go area kwa sisi WaTandika.

Uko sahihi kabisa kwamba eneo hilo mara baada ya kukamilika ujenzi litakuwa ni kwa ajili ya foreigners na wazawa walio nazo, ndio maana kuna mahali wanasema watajenga shule exclusive kwa ajili ya foreigners, impliedly hata apartments na nyumba nazo zitakuwa kwa ajili ya foreigners tu na bado serikali inakubali. Hivi dunia hii kuna serikali inaweza kujenga kitu kwa ajili ya foreigners tu? Mbona wanataka kuturudisha zama za Ubaguzi?

Kama huo siyo mradi, kwanini waziri wa ardhi anaushughulikia? Mimi nilidhani kwamba kama ni mradi wa wawekezaji, ni juu yao kuongea na wananchi moja kwa moja kwa kununua vibanda/nyumba/viwanja/mashamba yao at market price then wao watajua waende kununua wapi viwanja vingine.

Kitendo cha serikali kutaka kuwahamisha na kujifanya kwamba watatoa compensation kuna harufu fulani ambayo nina mashaka kwenye hiyo project kuna mikono ya watu walio serikalini ndio maana wanatishia kuhamisha watu ili eneo hilo wawape wawekezaji kwa ajili ya project hiyo na huko ndiko watapewa 10% yao kama kawaida. Ndiyo maana Kikwete anakwepa kujibu hilo swali na kuwasukumia watu wa Halmashauri ya Jiji wakati hayo mambo yanashughulikiwa na Wizara ya Ardhi.
 
h

uwiiiii - kiamba changu heka 2 pale kibada na chenyewe hope kishaingizwa humo -- ssasa ijui ka ntaja lipwa hata laki moja - hii sirikari haiaminiki. Nikienda mahakamani yale yale - sasa nikimbilie wapi kupata haki zangu wandugu?

mpeni sifa yesu- acha kushabikia picha za video na master plan. Tuna sheria zetu za ardhi, tatizo ni kutekelezwa kwa sheria hizi ili waliopo walipwe fidia kwa mujibu wa sjeria husika. Kama hamjui nini maana ya hii miradi kajifunzeni kibamba waliohamishwa wamekuwa maskini hadi leo, imebidi wahamie katika maeneo duni yasiyopimwa kutokana na kushindwa kumudu bei za viwanja viwanja vilivyopimwa kutokana na kulipwa fidia hafifu.

Wameshindwa kujenga nyumba kama zile walizokuwa nazi kabla ya kutakiwa kuhama eneo la luguruni kibamba; kifupi wamekuwa maskini kuliko walivyokuwa awali.

Mimisishobokei picha za video wala master plan ni muhumu wananchi kubaki nbgangari na ardhi yao na wafanye mazunguzmo na wawekezaji moja kwa moja na sio kupitia serikali hii ya mafisad
 
ninashukuru kwa post hii muhimu kwa wanamtandao na wananchi kwa ujumla. Je, naomba mwenye kujua anijulushe kama Kimbiji nayo imo ktk huu mradi kwani nina personal interest huko?
 
Kinachoweza kutekelezeka kwenye mradi huo ni hiyo zoning tu.

tunachokiona kwenye clip ni volume design/plan ambayo itakuwa tofauti kabisa na reality kwa sababu kiwanja kinapouzwa kwa uendelezaji hakiuzwi na sharti la muonekano wa jengo lake (facade design), na developer anakuwa na uwezo wa kufanya anachotaka.
Atakachoweza kulazimishwa kufuata ni masharti ya zoning tu ambayo ni kama jengo liwe na kuanzia ghorofa ngapi, liwe umbali wa meter ngapi kutoka kwenye barabara, aina ya jengo (residential, commercial, )


bila ya ujenzi wa daraja, ujenzi wa large scale kama huu tusiutegemee pia kwa sababu gharama zitakuwa kubwa mno kusafirisha vifaa vya ujenzi kupitia barabara moja tu ya sasa ile ya mbagala. (japo kwa hapa serikali inaweza isijali sana)

napata wasi wasi pia kuwa bila ya kuimarika uchumi wa tanzania huu ujenzi utakuwa ndoto tu. Wawekezaji hawawezi kujenga commercial buildings kwa gharama kubwa kisha kukosa makampuni ya kuwakodisha.
 
Kuna episode moja ya show ya zamani ya TV ya kimarekani "Little House on The Prairie" inayoonyesha struggle ya modernization against individual rights of land ownership inayoonyesha vizuri challenge ya situation ya Kigamboni. Katika kutafuta maximum capitalization ya ardhi na maendeleo, wananchi wa kijiji kimoja wanaitwa katika mkutano na kuambiwa kwamba ardhi yao itauzwa kwa wageni, wananchi wanaposema kwamba hawataki kuuza ardhi yao na wanaishi kwa kujikimu vizuri tu, wanaambiwa kwamba watendelea kuishi kwa kujikimu vizuri tu, tofauti ni kwamba badala ya kuwa mabwana wa mashamba yao, watakuwa vibarua/ wafanyakazi wa bwana mpya atakayenunua ardhi yao. Jambo hili linasababisha mtafaruku mkubwa. Hapa kunatokea msuguano mkubwa kati ya kupigania haki ya mtu binafsi kupigania anachoamini ni sawa kwa upande mmoja na maendeleo ya usasa kwa upande mwingine.

Of course Tanzania mambo yetu yanaweza kuwa tofauti sana na hii episode, tunaweza kuwa tunahitaji usasa kuliko tunavyohitaji kutetea "individual rights" - a foreign concept in a country following the compass of "ujamaa and kujitegemea" ( which in itself is a contradictory concept in my opinion anyway, I mean fundamentally Ujamaa is contrary to Kujitegemea, but that is another matter).

For the sake of argument, let's say tunahitaji modernity and what some interpret to be development ( the promised skyscrapers, better housing, world class college campuses etc), kuliko individual rights at least at our stage of economic prosperity, basically development first and democracy later - kwamba the lofty ideals of democracy na individual rights might actually serve to hinder development than advance it, as some take the evidence of the rise of China to promote, bado nitataka ku highlight points hizi chavhe za chini.

Kwa maoni yangu,serikali kuu isijiingize katika ku-fund large projects ambazo ufanisi wake ni mgumu kutabiri kwa sasa. Katika kitabu cha "Confessions of an Economic Hitman' (a must read for all "Third World" policy makers and influentials) John Perkins , an ex-CIA front man details how American companies fronting for the CIA, were able through bribery and other means, to peddle large multi billion USD projects, e.g., energy projects (Hydro Electric Dams etc) with promises of unrealistic returns, just to milk these "Third World" governments of their hard earned foreign currencies. In any case, kwa kufuatilia masharti ya the dreadfual "Structural Adjustment Programmes" serikali zetu hazitakiwi kujiingiza katika maswala ya kibiashara, zinachotakiwa kufanya ni kuhakikisha kwammba kuna mazingira yanayomwagilia ufanisi wa maendeleo tu.

Kwa kufuata maadili haya, ningependa kumuunga mkono rais Kikwete (ingawa sipendi utovu wa uongozi wake kwenye mengine) katika hotuba yake ya kampeni Kigamboni juzi aliposema - key word ni aliposema, viongozi wetu wanajua kusema maneno sahihi lakini ukiangalia utendaji utalia- aliposema kwamba ni muhimu kwa wawekezaji hawa kuthamini wakazi wa maeneo wanapowekeza. Ningependa kuona maendeleo yatakayowahusisha wananchi wa Kigamboni, na siyo kuwasukuma wananchi wa Kigamboni na kuwapeleka Mkuranga na Muhoro Rufiji.Unaweza kuangalia hotuba ya rais Kikwete kwenye link hii hapa chini. Endorsement yangu inaishia pale aliposema kwamba mradi huu usitumike kuwahamisha wananchi wa Kigamboni na kutoa fidia hafifu au zisizolipika mara moja, bali uwajumuishe wananchi, na kamwe endorsement hii haihusiki na kauli za ajabu kama pale rais anayeomba kura za wananchi aliposema "Mswahili uongo, hachoki !" how absurd (Kikwete si mswahili ?)

http://www.youtube.com/v/UaviGdsJJNI&rel=0&color1=0xb1b1b1&color2=0xd0d0d0&hl=en_US&feature=player_embedded&fs=1"></param><param

Naamini serikali ina jukumu la kuhamasisha foreign investment. Na mimi pia nilipata nafasi kuangalia hiyo video . Kwa kweli inavutia, mainjinia na wasanifu majengo wanaweza kutupa input zaidi kuhusu feasibility yake. Lakini nilishtushwa na ukweli kwamba hata hiyo kampuni inayotaka kufanya hiii investment haijawa na ujasiri wa kutupa jina lake tuidadisi zaidi. Inawezekana ni mambo ya kibiashara na hawa watu hawataki kujitangaza sana katika stage hii ya mapema. Lakini hii inaleta maswali mengi kuhusu professionalism na transparency ya hawa watu, na kama hawako wazi kiasi cha kutupa jina la kampuni yao, kuna nini wanaweza kuwa wanaficha ? I don't want to sound like a conspircy theorist -most conspiracy theories are based on ignorance- lakini hii lack of transparency inanipa concern. Ni nani anataka kuja kuwekeza Kigamboni? Atakabili vipi matatizo yanayojitokeza katika uwekezaji mkubwa wa kujenga miji mipya kama ya Dubai na Songdo Korea, nchi ambazo zina maendeleo ya kiuchumi zaidi yetu ? Kweli ni sawa kujenga daraja na underwater tunnel ? Hapo Boston MA mpaka leo wanahangaika na "Big Dig" na tunnel linalovuja, sie tutaweza? Kama tutaweza kuna ulazima huu ?

Once the project passes my above concerns (Chiefly the funding, technical issues and especially the "Economic Hitmen" aspect of it, plus the indigeneous advancement angle) wanaweza kuispin hii kama investment attraction pitch. Kwamba once they establish a modern city in Kigamboni, ku attract further foreign investment itakuwa rahisi zaidi. It is much easier to attract foreign investment into an established world class business hub than to do so by mere security, political stability and economic policy. Wanaweza kutuambia kwamba kuna projects nyingine haziwezi kuja Dar kwa sababu Dar haina adequate office space, au ina long traffic jams, au ina frequent power blackouts. All these issues can be addresed adequately within the new project. In essence, kama huu mji mpya unaweza kusimama na ku address concerns zangu nilizozieleza kotehapo juu, kuanzia kuwahusisha wenyeji mpaka umeme, huu mji unaweza kuwa a living testament to the mere "security status, political stability and economic policies" aspects of our attractiveness. Nchi nyingi zina usalama, uthabiti wa kisiasa na sera nzuri za kiuchumi, lakini zenye miji iliyosimama kuonyesha hivyo ni chache.

In my heart of hearts, nataka hii project ifanikiwe, na sisi tuwe na sehemu ya kupigiwa mfano - after the colossus laughingstock failure of the move of our capital city to Dodoma- tunayoweza kujivunia kwamba inaweza kuwekwa katika vitabu vya dunia sawa na the Singapores, Dubais, and Hong Kongs of the world. Kikwete akiweza ku oversee hili naweza hata kumsamehe makosefu yake mengine. Lakini maswali niliyouliza hapo juu bado ni ya muhimu sana.
 
Mh.Raisi J.M Kikwete asema yeye hana details za mradi huo maana upo chini ya halmashauri ya Jiji la Dar-es-Salaam na kuwa madiwani wa CCM ndio wana details zote. Mh. Rais aliyasema hayo wakati wa mkutano wa kampeni jimboni Kigamboni, Dar-es-Salaam wakati akiomba kura za mafiga matatu kwa CCM, tizama clip hii:
 
Last edited by a moderator:
Hii project inahusisha vitu vingi mno. Naona kuna mpaka Wind power plant ya 36 MW. Sio farm kubwa (will cost only about $80million) lakini kigamboni ni mjini na ni eneo lenye makazi ya watu.

nataraji wataalamu wa kitanzania wameshirikishwa kutathmini athari ya wind farm kwa mandhari na wakazi wa maeneo ya karibu
 
Kiranga hivi unamwamini Kikwete kwa asilimia ngapi kwa maneno anayozungumza? Mi najua mwisho lazima wana kigamboni watatoka kavu. Katika policy ipi unayojua katika nchi yetu ambayo mwananchi anatakiwa atumie ardhi yake kama mtaji wa ku share na mwekezaji? Mimi nitakuwa mtu wa kwanza kuikubali policy hiyo. Lakini lazima iwe ni policy iliyotengenezwa for the all country including maeneo ya madini.

Mbali na hivyo najua zitabaki ni nyimbo za kuombea kura kisha 2011 wote wale wataondolewa kwa vipesa kidogo vinavyoitwa fidia. Kwisha kazi. Mzungu + Kikwete & Co watakuwa wanaendelea kula matunda ya uhuru for the rest of their life.
 
Kiranga hivi unamwamini Kikwete kwa asilimia ngapi kwa maneno anayozungumza? Mi najua mwisho lazima wana kigamboni watatoka kavu. Katika policy ipi unayojua katika nchi yetu ambayo mwananchi anatakiwa atumie ardhi yake kama mtaji wa ku share na mwekezaji? Mimi nitakuwa mtu wa kwanza kuikubali policy hiyo. Lakini lazima iwe ni policy iliyotengenezwa for the all country including maeneo ya madini.

Mbali na hivyo najua zitabaki ni nyimbo za kuombea kura kisha 2011 wote wale wataondolewa kwa vipesa kidogo vinavyoitwa fidia. Kwisha kazi. Mzungu + Kikwete & Co watakuwa wanaendelea kula matunda ya uhuru for the rest of their life.

Nimesema jinsi gani wanasiasa wetu walivyo wazuri katika kusema lakini vitendo hamna. Kuna mtu alisema kuhusu vita dhidi ya rushwa na kuleta ukweli na uwazi kuliko Mkapa? Angalia alipotupeleka.

Kabla hatujaanza chochote Kikwete kashaanza kunawa mikono na anawatupia kazi watu wa serikali za miji.
 
Wakuu hii nimeona kwa macho yangu,ule Mradi wa Kigamboni new city,pamoja umekuwa ukiendelea chini chini kumezuka mradi mwingine mpyaaa!wa kuuza CD ambazo zinaonyesha jinsi mradi utakavyo kuwa na zinauzwa shs. 5000/- hapo Ferry (ng'ambo ya kigamboni)kwenye duka la samsung.
Cd hizi zilitoka nyuma kidogo wakati mambo yapo hot hot kwa wenyebahati tulizipata,cha ajabu bwana huyo mwenye duka ameipata hiyo CD na anatoa nakara na kuwauzia watu kwa gharama hiyo.
Nina maswali nataka kuuliza hapa.
1.HIVI SISI WATANZANIA TUMEROGWA???..yaani pamoja ya kuwa mustakabari wetu uko hatari na hatujui nini kitaamuliwa na hii serikali yetu,eti tunanunua hizi CD,kwa lipi hasa??

2.WIZARA YA ARDHI,NYINYI SI NDIO MNAPASWA KUJU KUFANYA PRESENTATION YA NINI KITAKUA KWENYE MRADI??....sasa mbona mmewamua kutufanyia hivi mmempa huyo bwana cd ili aje atuuzie???sasa nyie kazi yenu nini?

PILOT PROJECT YA MIRADI HUU UNAOITWA MRADI WA KUENDELEZA MAENEO PEMBEZONI MWA DAR ES SALAAM ILIFANYIKA KIBAMBA WILYA YA KINONDONI, NA SASA NDIO INASAMBAZWA KIGAMBONI, KONGOWE, MBAGALA. PUGU KAJIUNGENI, BUNJU.

ILIRIPOTIWA KUWA SHS BILIONI 3 ZILITENGWA KUWALIPA WANANCHI FIDIA LAKINI TULIONA WENYEWE NINI KILITOKEA WANANCHI WALIGHAMISHWA KWA NGUVU BAADA YA MAFISADI KUKWAPUA FEDHA HIZO, INADAIWA HATA MHE CHILIGATI KUPELEKWA WIZARA YA ARDHI ILIKUWA NI MKAKATI WA KUIPATIA CCM FEDHA ZA UCHAGUZI WA 2001 KUTOKA MRADI HUU MKUBWA.

HIVYO BADALA YA KUSHABIKIA KUNUNUA CD's TEMBELEENI KIBAMBA MJIFUNZE UFISADI ULIVYOFANYIKA. WANANCHI WALILALAMIKA KUWA WALILIPWA FIDIA KIDOGO SANA KIASI CHA KUSHINDWA KUNUA VIWANJA VILIVYIOPIMWA, KUJENGA NYUMBA KAMA WALIZOKUWA NAZO N.K KWA KIFUPI SHERIA ZA ARDHI,HAZIKUZINGATIWA HATA KIDOGO. KAMA KAWAIDA WAKATI WANANCHI WANAFANYIWA UFISADI NA HATIAMAYE KUHAMISHWA KWA KUBOMOLEWA NYUMBA ZAO HAKUNA KIONGOZI YEYOTE SI WA MTAA, DIWANI AU MBUNGE ALIYEJITOKEZA KUWASAIDIA AU KUWATEMBELEA LICHA YA KUWA WALICHAGUA WAGOMBEA WA CCM KWA KISHINDO KIKUBWA SANA 2005 KATIKA NAFASI ZOTE HIZO.

FANYENI MAKOSA YA KAMA YA WENZENU KIBAMBA MTAKIONA CHA MOTO
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom