Da Vinci XV
JF-Expert Member
- Dec 7, 2019
- 3,838
- 6,387
Wasalaam,
Kumekuwa na Hadithi nyingi sana Kumuhusu diktekta maarufu , mwamba wa Ujerumani Adolph Hitler, katika hatma yake Wengine wakidai alichomoka kwenda kwa wafadhili wake wa Argentina kustirika Aibu ya kushindwa Vita, wengine Wakadai alijitumbukiza kwenye Tindikali Eti baadala ya Mabaki ya nguo zake kukutwa pembeni ya Tindikali nadharia hiyo hata mimi miaka ile nakua ilikaa kwenye Ubongo wangu, wengine wakasema Diktekta huyo alikufa kwa kushambuliwa na Mbu yule mdudu wa Malaria ,habari zipo nyingi nyingi.
Katika utafiti wa wanasayansi wa Ufaransa walichambua vipande vya meno ya Adolf Hitler ili kudhibitisha kuwa alikufa mwaka 1945, baada ya kujipatia sumu (cyanide) na kujipiga risasi kichwani. Utafiti huo, uliochapishwa katika Jarida la ulaya la Internal Medicine, Mei 2018, hii ilimaliza kabisa nadharia nyingi juu ya kifo cha Adolf Hitler kupitia uchambuzi wa kisayansi wa meno na fuvu la dikteta Huyo.
"Utafiti wetu unathibitisha kwamba Hitler alikufa mwaka 1945,"
mwandishi mkuu wa utafiti huo Philippe Charlier aliiambia AFP.
"Ni Meno halisi ya Hitler na hakuna shaka"
PHILLIPE CHARLIER
Ingawa imejulikana hivyo kwamba Hitler alikufa katika jumba lake la Utawala pale Berlin, lakini uvumi wa kutoroka na kukimbia ni mwingi sana.
Utafiti wao unathibitisha kwamba hakufanikiwa kukimbia
"hakukimbilia Argentina kwa manowari, wala hakwenda katika kituo kilichofichwa "
Alisema Charlier
Inaelezwa Mwishoni mwa Aprili 1945, wakati vikosi vya Soviet vilipovamia Berlin, .
Hitler alifanya mipango ya kujiua hii ni baada ya kuagiza vidonge vya Sumu kabla hajaacha wosia wa mwisho.
Siku mbili kabla , Mussolini alikuwa amepigwa risasi na kikosi cha warusha risasi na kisha kunyongwa hadharani ,katika uwanja huko Milan Italia.
Hatima kama hiyo ilionesha hiltler hakutaka imtokee akachukua maamuzi kama hayo. Akajiua.
Aprili 30, miili ya Hitler na mkewe Eva Braun, ilipatikana ndani ya jumba hilo, huku ikiwa na shimo la risasi
Aprili 2018, Chapisho la Kiingereza la kumbukumbu za mkalimani wa Urusi ilidokeza jinsi alivyokabidhiwa meno kadhaa mnamo 1945, na akapewa jukumu la kulinda rekodi zote kuanzia meno, na habari za dikteta za na vyote vinavyomuhusu vilibaki mikononi mwa Urusi
Baada ya mazungumzo ya miezi kadhaa, Secret service ,Ya Urusi ,FSB na serikali ya Urusi ziliwapa watafiti ruhusa ya kuchunguza kipande cha fuvu na vipande vya meno yake. Kipande cha fuvu kilikuwa na shimo upande wake wa kushoto, sawa na jeraha la risasi,
Ingawa wanasayansi hawakuruhusiwa kuchukua sampuli kutoka kwenye fuvu hilo, walibaini katika utafiti huo, muonekano wa sura ya fuvu hilo ilionekana kufanana kabisa na picha za fuvu la kichwa la Hitler lililochukuliwa mwaka mmoja kabla ya kifo chake.
Picha za meno zilizochapishwa katika utafiti huo zinaonyesha taya iliyotengenezwa na meno chuma. na inaelezwa Wakati wa kifo chake waliandika katika ripoti kuwa Hitler alikuwa na meno manne tu yaliyosalia.katika kinywa chake.
Uchambuzi huo ulithibitisha madai yaliyotajwa hapo, lakini hawakuweza kuthibitisha kabisa kama hitler alichukua sumu (cyanide) kabla ya kujipiga risasi. Lakini mabaki ya rangi ya Ubluu kwenye meno yake fake(metal), watafiti waliandika, inawezekana chemical Reaction ilifanyika katika meno yake bandia na sumu hiyo wakati wa kifo
Swali mabaki mengine yalizikwa AU???
"Bila kuchukua sampuli kwa uchambuzi, ni ngumu kusema kwa uhakika"
"Hatukujua ikiwa alikuwa ametumia Sumu ya (cyanide) kujiua au ikiwa ni risasi kichwa, ila kuna uwezekano wa vyote kufanyika "
Charlier alisema.
Kwa vyovyote vile, utafiti unaweza kusaidia hatimaye kuweka kando stori za kukimbia kwa hitler Argentina kupumzika Vurumai la Vita, na habari zingine zingine juu ya kifo chake.
Kumekuwa na Hadithi nyingi sana Kumuhusu diktekta maarufu , mwamba wa Ujerumani Adolph Hitler, katika hatma yake Wengine wakidai alichomoka kwenda kwa wafadhili wake wa Argentina kustirika Aibu ya kushindwa Vita, wengine Wakadai alijitumbukiza kwenye Tindikali Eti baadala ya Mabaki ya nguo zake kukutwa pembeni ya Tindikali nadharia hiyo hata mimi miaka ile nakua ilikaa kwenye Ubongo wangu, wengine wakasema Diktekta huyo alikufa kwa kushambuliwa na Mbu yule mdudu wa Malaria ,habari zipo nyingi nyingi.
Katika utafiti wa wanasayansi wa Ufaransa walichambua vipande vya meno ya Adolf Hitler ili kudhibitisha kuwa alikufa mwaka 1945, baada ya kujipatia sumu (cyanide) na kujipiga risasi kichwani. Utafiti huo, uliochapishwa katika Jarida la ulaya la Internal Medicine, Mei 2018, hii ilimaliza kabisa nadharia nyingi juu ya kifo cha Adolf Hitler kupitia uchambuzi wa kisayansi wa meno na fuvu la dikteta Huyo.
"Utafiti wetu unathibitisha kwamba Hitler alikufa mwaka 1945,"
mwandishi mkuu wa utafiti huo Philippe Charlier aliiambia AFP.
"Ni Meno halisi ya Hitler na hakuna shaka"
PHILLIPE CHARLIER
Ingawa imejulikana hivyo kwamba Hitler alikufa katika jumba lake la Utawala pale Berlin, lakini uvumi wa kutoroka na kukimbia ni mwingi sana.
Utafiti wao unathibitisha kwamba hakufanikiwa kukimbia
"hakukimbilia Argentina kwa manowari, wala hakwenda katika kituo kilichofichwa "
Alisema Charlier
Inaelezwa Mwishoni mwa Aprili 1945, wakati vikosi vya Soviet vilipovamia Berlin, .
Hitler alifanya mipango ya kujiua hii ni baada ya kuagiza vidonge vya Sumu kabla hajaacha wosia wa mwisho.
Siku mbili kabla , Mussolini alikuwa amepigwa risasi na kikosi cha warusha risasi na kisha kunyongwa hadharani ,katika uwanja huko Milan Italia.
Hatima kama hiyo ilionesha hiltler hakutaka imtokee akachukua maamuzi kama hayo. Akajiua.
Aprili 30, miili ya Hitler na mkewe Eva Braun, ilipatikana ndani ya jumba hilo, huku ikiwa na shimo la risasi
Aprili 2018, Chapisho la Kiingereza la kumbukumbu za mkalimani wa Urusi ilidokeza jinsi alivyokabidhiwa meno kadhaa mnamo 1945, na akapewa jukumu la kulinda rekodi zote kuanzia meno, na habari za dikteta za na vyote vinavyomuhusu vilibaki mikononi mwa Urusi
Baada ya mazungumzo ya miezi kadhaa, Secret service ,Ya Urusi ,FSB na serikali ya Urusi ziliwapa watafiti ruhusa ya kuchunguza kipande cha fuvu na vipande vya meno yake. Kipande cha fuvu kilikuwa na shimo upande wake wa kushoto, sawa na jeraha la risasi,
Ingawa wanasayansi hawakuruhusiwa kuchukua sampuli kutoka kwenye fuvu hilo, walibaini katika utafiti huo, muonekano wa sura ya fuvu hilo ilionekana kufanana kabisa na picha za fuvu la kichwa la Hitler lililochukuliwa mwaka mmoja kabla ya kifo chake.
Picha za meno zilizochapishwa katika utafiti huo zinaonyesha taya iliyotengenezwa na meno chuma. na inaelezwa Wakati wa kifo chake waliandika katika ripoti kuwa Hitler alikuwa na meno manne tu yaliyosalia.katika kinywa chake.
Uchambuzi huo ulithibitisha madai yaliyotajwa hapo, lakini hawakuweza kuthibitisha kabisa kama hitler alichukua sumu (cyanide) kabla ya kujipiga risasi. Lakini mabaki ya rangi ya Ubluu kwenye meno yake fake(metal), watafiti waliandika, inawezekana chemical Reaction ilifanyika katika meno yake bandia na sumu hiyo wakati wa kifo
Swali mabaki mengine yalizikwa AU???
"Bila kuchukua sampuli kwa uchambuzi, ni ngumu kusema kwa uhakika"
"Hatukujua ikiwa alikuwa ametumia Sumu ya (cyanide) kujiua au ikiwa ni risasi kichwa, ila kuna uwezekano wa vyote kufanyika "
Charlier alisema.
Kwa vyovyote vile, utafiti unaweza kusaidia hatimaye kuweka kando stori za kukimbia kwa hitler Argentina kupumzika Vurumai la Vita, na habari zingine zingine juu ya kifo chake.