Kifo cha hawara (Mkono Wa Jini)

Kifo cha hawara (Mkono Wa Jini)

KIFO CHA HAWARA (mkono wa jini)
SEHEMU YA SITINI NA TISA
MTUNZI: Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA SITINI NA NANE: vyema kama tutaondoka kimya kimya tukiwapiga chenga ya mwili, lakini swali likaja tutawatoroka vipi, lakini wakati nafikiria hilo nikakumbuka kuwa mzee Mangeu anaishi ndani ya shamba hili, hapo nikamshika mkono Jesssenia, “twende kwa mangeu” nilimueleza Jessenia kwa sauti ya kunong’ona, ambae mwanzo aliinuka na kutaka kunifuata lakini aliposikia nilichosema akasimama kwa kukataa kuelekea nilikomueleza, “hapana kwahuyo mzee hunipeleki, huyo ndiyo chanzo cha hayo yote” alisema Jessenia kwa sauti ya kunong’ona…….….…. ENDELEA..
nikamuonyeshea ishara ya kukaa kimya, maana tayari watu saba walikuwa wamesha karibia pale tulipokuwepo, maana walikuwa wanakuja usawa wetu, nikampa ishara ya kubonyea kisha tukaanza kutembea taratibu kuelekea upande wa kibanda cha babu mangeu, na baada ya kutembea kama mita kumi hivi, tukachuchumaa chini, maana tayari walishakaribia usawa ule, na kama tungeendelea kutembea wangetuona au kusikia vishindo, japo vilikuwa hafifu.
Naam nikweli mawazo yetu yalikuwa sahihi, maana wakati tukiwa chini tuliweza kuwaona watu wakikatiza usawa ule kuelekea mbele zaidi, japo kulikuwa na kijigiza kidogo, lakini tuliweza kuona vizuri tu maana mita kumi sio mbali sana, huku mimi nikijitahidi kuwatazama watu wale ambao sasa walikuwa wameondoa vitambaa usoni mwao, “tuongeze mwendo kabla hawaja fika mbali” alisema mmoja wao huku wanaendelea kutembea kwa haraka kukatiza eneo lile katika mtindo wa mstari mmoja, nikamuona Jessenia akinitazama kwa mshangao, huku anaonyesha kidole kule walikokuwa wale jamaa, kuna kitu alitaka kuongea nikamziba mdomo haraka sana, “tena huku wamejileta machinjio, yaani hakikisheni wote tunawamalizia huku huku” safari hii ilikuwa ni sauti ya Ussi, na hapo Jessenia akageuza uso wake kwa haraka kutazama upande ule, lakini ndio kwanza walikuwa wanamalizikia, “Eric njoo huku” tulishtuliwa na sauti ya Mangeu toka nyuma yetu, na hapo Jessenia akageuka kutazama ilikotokea sauti ile na kumuona Mangeu ambae alikuwa karibu yetu kabisa, akamtazama kwa macho ya mshangao, huku na mimi nikimtazama Jessenia kuona atavyo pokea jambo lile.
Kama mtu ambae alikuwa ameshikwa na mshangao mkubwa kupita kiasi, akanitazama mimi kama vile ananiuliza ina maana unafahamiana na huyu mzee, hapo na mimi nikampa ishara ya kutulia na hakuwa mbishi, nikamshika mkono kisha tukainuka na hapo pasipo kuongea lolote tukaanza kutembea kuelekea upande wa juu, tukitoka nje ya shamba la Mangeu na kuingia kwenye vichaka hafifu pembezoni mwa kuta ndefu za uzio za majumba yale ya kifahari, ikiwa ni upande wa nyuma, “ni hatari sana kwenu endapo mutaendelea kubakia hapa” alisema mzee Mangeu kwa sauti tulivu, huku akiongoza njia mimi nikiwa sambamba na Jessenia ambae bado alikuwa katika mshangao mkubwa sana, asielewa kinachoendelea kati yangu na Mangeu, “gari lako lipo wapi, au kuna ulazima wa kuwatafutia gari jingine?” aliuliza Mangeu, na hapo ndipo nilipokumbuka kutoa simu yangu na kumpigia Mwasenga, ambae hakuchelewa kupokea, na bahati nzuri kwetu, Mwasenga alikuwa pale Mess na kamanda aliekuwa ana muendesha alikuwa na wenzie wanaendelea kunywa bia, na alikuwa ni mmoja kati ya wageni waliofikia pale pale Messi.
Nikiwa naongea kwa sauti ya chini, nikimuomba aje anichukue kwenye eneo lile la karibu na njia ya kuingilia huku Msingini, “yani muda wote nilikuwa natazama simu kuona kama umepiga, inaoekana ulikuwa juu ya kifua eeh” alisema Mwasenga ambae kiukweli alikuwa na dalili zote za kwamba alikuwa amelewa, “tutaongea kaka, naomba ufanye haraka si unajuwa usiku huu” nilimueleza Mwasenga nikimsisitiza na kukata simu, wakati huo tulikuwa tunaendeelea kutembea huku Jessenia ni kama alikuwa hajaelewa elewa hivi, maana alikuwa anatushangaa na kumtazama mzee Mangeu kwa uoga, sijui alikuwa anawaza nini huyu mwanamke, ila kwa haraka haraka unaweza hata wewe msomaji kuhisi alicho kuwa anawaza Jessenia, kwamba wakati amegundua kuwa Ussi ni mmoja kati ya watu waliokuwa wanatufukuza huku akiwa amemuona mtu anae mfahamu kati ya wale saba, pia anakuja kugundua kuwa mimi na Mangeu ni watu tunao fahamiana, na chakushangaza zaidi ni kwamba Mangeu anatoa msaada wa kututorosha pale Msingini.
Dakika kumi baadae tulikuwa tumeshaibukia barabarani, Jessenia akilalamika nyayo zina muuma, “umeona nilichokuwa namaanisha mzee” nilimuuliza mzee Mangeu, huku tukiwa tume simama pembeni sana ya barabara tukitumia maficho ya kichaka flani, “Eric sidhani kama huu ni wakati wa kuongelea hilo, japo nadhani Mashaka yangu yalikuwa sawa ” alisema babu Mangeu, na hapo Jessenia ambae alikuwa bado amenishika mkono akikaa ubavu wangu wa kushoto akijitenga kabisa na Mangeu akakosa uvumulivu, “munaweza kuniambia nini kinaendelea, maana nimemuona Ussi na wakina Mussa wakitufukuza na panga, sasa namuona Mangeu na wewe munafahamiana kuna kitu gani kinaendelea Eric” aliuliza Jessenia huku ananitikisa mkono, akitaka nimueleze kinachoendelea, nilimtazama Mangeu ambae alikuwa anamtazama Jessenia, huku anatabasamu, sasa kama ukibahatika kuliona tabasamu la Mangeu ndio ungetafuta pakutokea, maana sijui nifananishe na nini, ujuwe yale mapanga usoni kwa mzee huyu yalikuwa yame muharibu sana,
Jessenia alimtazama mzee Mangeu kwa Macho ya tahadhari, akimuona anavyo tabasamu, kisha akamsikia akiongea kwa sauti ya upole, “Jessenia hapa tulipo hatuwezi kuongea chochote ukanielewa, maana tuna muda mfupi sana” alisema Mangeu na kisha akanitazama mimi, “Eric naamini Jessenia yupo salama pamoja na wewe, hivyo hakikisha unamaliza hili salama na mimi siwezi tena kuwa hapa karibu, nitaenda kujificha sehemu mpaka kila kitu kiwe sawa” alisema Mangeu kisha akatoa kijimfuko mkononi mwake na kunikabidhi ni kitu mfano wa chupa bapa, nilisha juwa kuna umuhimu wa kumficha Jessenia na anatakiwa kufichwa mpaka usiku wa leo, nitakueleza baadae ilikuwaje cha msingi nenda na Jessenia mpaka Mantariff Lodge, mtakuta nimesha weka oder ya chumba, najuwa huwezi kukosa gari, ukikwama jambo lolote nijulishe, hizo kwenye mfuko ni fedha zitawasaidia, lakini usiku huu musilale maeneo ya hapa karibu, sasa hivi ni saa mbili kasoro munaweza kufika lodge mapema sana” alisema Mzee Mangeu na kumuacha mdomo wazi Jessenia, kwamba mzee Mangeu ndie wakuweka oder Mantariff, inawezekana vipi, wakati huo huo tukaona mwanga wa gari unatokea upande wa macho mane, sambamba na ngurumo ya gari, ambalo niligundua kuwa ni defender la jeshi.
Unapo taja Mantariff Loder, unazungumzia hotel moja kubwa ya kifahari yenye hadhi kubwa ya kimataifa iliyoko pemba kaskazini kwenye ras ya panga la mtoro, hivyo watalii na watu wenye fedha nyingi pekee ndio huenda mahali hapo kuenjoy na kula maisha, mimi nilisha wahi kufika, lakini ilikuwa ni kuangalia mazingira na kuendelea na safari zangu, “sawa mzee lakini kuwa makini ukae ukijuwa na wewe hawato kuacha salama endapo watakupata” nilimueleza mzee Mangaeu huku natokeza barabarani kusimamisha gari, ambalo lilikuwa limesha karibia, “nalijuwa hilo, na nimesha andaa mipango yote, usisahau kunipigia, hakikisha Jessenia anakuwa salama” alisema Mangeu, huku anaanza kutembea kuifuata njia ya kuelekea msingini ile ambayo hata magari yanapita, huku akimuacha Jessenia anashangaa jinsi babu Mangeu anavyoonyesha kumjali.
Gari lilisimama na sisi tukaingia ndani ya gari, na safari ikaanza kwa mwasenga kugeuza gari kuelekea macho manne, “hooo shemeji naona kama kawaida mnaeda Mess kula bata au?” aliuliza Mwasenga ambae alionekana amesha lewa tayari, “hapana tunahitaji kupumzika kaka, ila nahitaji gari lako” nilimjibu Mwasenga huku Jessenia akiachia tabasamu la kuzuga, maana bado alikuwa na maswali kichwani ambayo hayakuwa yamepata majibu, “gari mbona lipo tu, halafu nimelipiga kiwese cha kutosha jioni hii, si unajuwa kukiwa kuna wageni kama hivi mafuta yana kuwa mengi sana” alisema Mwasenga ambae alikuwa amevalia sale za kazi, zile zenye mabaka baka, yaani combat, huku anamalizia kuliweka gari sawa na kulielekeza upande wa Macho manne na kukanyaga mafuta kuelekea upande huo, itakuwa vuzuri sana, maana nataka niende sehemu moja hivi na shemeji yako nikale kuku kidogo” nilimueleza Mwasenga, wakati huo tumesha tembea kama mita mia moja hivi.
Naam na hapo ndipo kwa msaada wa gari tuliweza kuwaona vijana Saba wanatokea kichani, na kuibukia barabarani, mimi na Jessenia ambao tulikaa seat ya mbele tukatazamana, maana tuliwatambua kuwa ni wakina Ussi, “ndiyo maana sijamuona mess leo kumbe anamishe mishe zake” alisema Mwasenga huku anapunguza mwendo akitaka kusimamisha gari amsalimie Ussi, “twende twende usisimame” nilimnong’oneza Mwasenga nae akakanyaga mafuta huku anapiga honi za kuwasalimia wakina mwasenga, “nilitaka nisahau wivu wa Ussi kwa dada yake” alisema Mwasenga akimalizia kwa kicheko, na sisi tukacheka huku tukigeuza vichwa vyetu kutazama tulikotoka tuka waona wakina Ussi wakiwa wamesimama wanalitazama gari, mpaka tulipo tokomea.
Dakika baadae tayari tulikuwa tumeshafika wawi mess, ambapo tulichukuwa gari jingine, yaani lile Toyota spacio na kuondoka zetu kueleka Ali Khamis Camp, ambako nilipanga nika lchukuwe lap top yangu ambayo ina mambo mengi ya kazini, pamoja na nguo chache kisha tuje macho mane tuchukue nguo za kubadili za Jessenia, kisha tuanza safari ya kaskazini, ambako tungetumia kama lisaa lizima maana kipindi kile barabara zilikuwa hazina lami, lami ilikuwa inaishia wete mjini.
Naam ile tunaikamata barabara ya vitongoji Jessenia akanipachika swali, “Eric sasa unaweza kuniambia kinachoendelea?” aliuliza Jessenia aliekuwa amekaa kwenye seat ya pembeni yangu, “nitakueleza kila kitu Jesse, sikuweza kukueleza mwanzo, maana usinge amini” nilimueleza Jessenia kwa sauti tulivu, ili kumtuliza na yeye mwenyewe, wakati huo huo nikaona mwanga wa taa ya pikipiki ukija kwa kasi nyuma yetu, mwanzo sikuitilia mashaka ile pikipiki, lakini baada ya kufika njia panda ya wawi ambapo tuliifuata ile bara bara ya vitongoji na ile piki piki kutufuata ndipo nilipoitilia mashaka, hapo nikapunguza mwendo ili niitazame kama ni pikipiki ya Mandevu au la.
Ukweli Mandevu hakuwa na umakini wakufuatilia mtu, maana alikuja karibu yetu na kupunguza mwendo akiwa mita kama ishirini nyuma yetu, hapo nikaweza kumuona vyema kabisa kuwa ni yeye Mandevu, “simuachi huyu mjinga” nilisema hivyo huku naongeza mwendo, nikamuona Jessenia nae anatazama nyuma kutazama nani anae tufuata, kwa kuwa nilikuwa nimesha sogea mbali kidogo hakuweza kumuona kutokana na mwanga wa taa wa ile Vesper.…. ENDELEA..

KIFO CHA HAWARA (mkono wa jini)
SEHEMU YA SABINI
MTUNZI: Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA SITINI NA NANE: Ukweli Mandevu hakuwa na umakini wakufuatilia mtu, maana alikuja karibu yetu na kupunguza mwendo akiwa mita kama ishirini nyuma yetu, hapo nikaweza kumuona vyema kabisa kuwa ni yeye Mandevu, “simuachi huyu mjinga” nilisema hivyo huku naongeza mwendo, nikamuona Jessenia nae anatazama nyuma kutazama nani anae tufuata, kwa kuwa nilikuwa nimesha sogea mbali kidogo hakuweza kumuona kutokana na mwanga wa taa wa ile Vesper.…. ENDELEA
“Ni nani huyo” aliuliza Jessenia, huku ananitazama kwa macho yaliyojaa wasi wasi, yule jamaa mwenye mandevu ulie sema ni mfanyakazi kwenye majahazi ya Ussi” nilimuambia Jessenia huku nazidi kuongea mwendo, “kha sasa kwanini anatufuata” aliuliza Jessenia, huku anageuza shingo yake kutazama tulikotoka, yaani nyuma na kwa kupitia kioo cha nyuma aliweza kuona mwanga wa pikipiki kwa mbali ukionyesha kwamba mwendesha pikipiki alikuwa anajitahidi kutufuata kwa kasi, hapo sikumjibu Jessenia, nikazidi kukanyaga mafuta huku kichwani nikiwa nimesha panga kitu cha kumfanyia, “sasa nime shajuwa kwanini mjomba alikuwa anajuwa kila tunachofanya, kumbe anawatuma watu wananifuatilia” aisema Jessenia kwa sauti ya ung’amuzi iliyosheheni hasira za hali ya juu, bado sikusema lolote, maana nilijuwa ingezuwa maswali mengi na kuchochea kumueleza kile ambacho nilitakiwa kumueleza baadae, maana kwa sasa nilikuwa na kazi ya kufanya na huyu bwana Mandevu, “umejuwaje kama ni yeye na anatufata sisi?” aliuliza Jessenia, ambae wasi wasi wake ulizidi mara dufu, “toka jana asubuhi, na pia kuna wengine walikuwa wanatufuatilia toka siku ya kwanza ulipokuja huku kwangu” nilimjibu, huku napunguza mwendo kuingia kona ya ngerengere, ambayo ni kona kali sana, nilipoimaliza nikakanyaga mafuta kwa nguvu na kulifanya gari likimbie kwa speed mia ishirini kwa saa, huku nikichungulia kwenye side mirror sikuona dalili ya mwanga wa taa za pikipiki, niwazi kuwa tulikuwa tumemuacha mbali, niliendesha gari kwa speed kali sana mpaka tulipofika eneo linaloanza kijipori kidogo nilizima taa za gari na kupunguza mwendo kisha nikaingiza gari pembeni ya barabara nikigeuza nilikotoka, lakini nikiwa nje ya barabara, “Eric, unataka kufanya nini, akituona ataenda kumuambia Ussi” alisema Jessenia huku akionyesha wasi wasi mwingi, “kwani unaogopa akimuambia?” niliuliza kwa kumtega ili kujuwa anaelewa nini juu ya kilicho tutokea mida ile, wakati huo gari lina unguruma lakini nilikuwa nimezima taa zote na gia nimeweka P, sikuweka hand brake, maana sikutaka aone taa yoyote, “kwani we hujamuona Ussi alivyotaka kunipiga na panga, yupo na wale wageni wao” alisema Jessenia na hapo nikajuwa kuwa tayari amesha anza kuona hatari iliyopo mbele yake, na kwamba sitokuwa na kazi ngumu kujieleza mbele yake, “hivi wale wengine ndio wageni toka Unguja?” nilimuuliza Jessenia, “ndiyo ni hao hao, nimewaona kwa macho yangu, na Ussi ndie alitaka kunikata na panga, nimegundua pale tulipo wamulika na taa za gari” alisema Jessenia, akimaanisha kuwa alimtambua mtu alietaka kumkata na panga kuwa ni Ussi, baada ya kumuona akiwa hajajiziba uso, wakati ule tukiwa kwenye gari la Mwasenga, “unadhani kwanini Ussi alitaka kukukata na panga?” nilimuuliza swali la pili la kumtega Jessenia, ambae bado alikuwa na wasi wasi na hofu kuu moyoni mwake, “yeye na mjomba watakuwa wamechukia nilivyo kataa kuolewa na Mussa, halafu pia wamechukia waliponiona nipo na wewe, ndio maana hata walituita wezi” alisema Jessenia, na wakati huo huo tukaona mwanga wa taa ya piki piki, yani jicho moja ukija kwa kasi sana upande wetu, “huyooooo anakuja, Eric wapigie simu wanajeshi waje wamkamate, wanaweza kutuuwa hawa” alisema Jessenia huku anachukuwa begi langu toka seat ya nyuma kwa lengo la kupekuwa ili atoe simu, “Jesse unaweza kutulia kwajili yangu, amini siwezi kuruhusu mtu akuguse” nilimueleza Jessenia nae akaacha begi na kutulia, akiitazama Piki piki.
Naam nilihesabu mwendo wa pikipiki, ambayo ilikuwa inakuja kwa kasi sana, na ilipokaribia kwetu kwa umbali wa mita mia moja nikaingiza gia ya kuendeshea yani D, halafu nikahesabu, moja mbili tatu, huku Vesper ikiwa inakuja kwa kasi na kubakiaza kama mita ishirini, nikawasha taa zote yaan full, ambao ulimpiga usoni Mandevu na kumchanga kidogo, halafu kama haitoshi nikakanyaga mafuta kwa nguvu kama naingia barabarani, halafu nikasimama, hapo nikamuona Mandevu akishika brake za ghafla, ambazo zilimyumbisha na kumfanya akose uelekeo na kujibwaga kwenye lami, kisha kuseleleka akisota juu ya lami hiyo sambamba na piki piki yake, kwa msoto wamita kama ishirini hivi, wakati huo tayari nilikuwa nimesha shuka, toka ndani ya gari, nikiwa nimezima taa za gari, na kukimbilia upande ilipoelekea pikipiki ambako kulikuwa na giza maana hata taa ya pikipiki ilikuwa imesha zima, nadhani kwaajili ya ule mdondoko.
Nilipokaribia niliweza kumuona Madevu akijichomoa toka kwenye pikipiki iliyomkandamiza mguu mmoja wa kulia na kufanikiwa kusimama huku akiwa anachechemea na aliponiona namfuata akasimama na kunitazama kwa hasira, “unaweza kuniambia ni kwanini munafanya mauwaji kwa wanaume wanaotaka kumuoa Jesse?” nilimuuliza yule jamaa, yani Madevu kwa sauti tulivu, huku nazidi kumsogelea Mandevu ambae alionekana kuwa katika maumivu makali sana ya mguu, ambao niliona ukiwa unavuja damu kwa mchupuko mkubwa ulioupata, Mandevu hakujibu lolote zaidi alijipapasa kwenye paja la mguu wa kushoto, ambao haukuwa umeumia kama ule wa kulia, kisha akaingiza mkono kwenye upido wa nusu suruali yake maeneo ya kiunoni na kuibuka na kisu kirefu kinachong’aa kwa makali yake.
Ushikaji wa kisu wa Mandevu, haukuwa wakipiganaji, ushikaji ambao nilisha juwa atakitumia vipi kunishambulia, alishika kama vile anataka kukata mua, “ni vyema kama unge achana na hicho kisu halafu unijibu maswali yangu” nilimueleza Mandevu kwa sauti tulivu kama mwanzo, sauti hii ni silaha kubwa sana, hasa unapo pambana na mtu hatari, maana huonyesha wazi kuwa unajiamini, lakini haikusaidia kitu, niliweza kumuona Mandevu akivuta kisu chake kwa nguvu na kukileta kwangu kwaspeed kali sana, hapo niliudaka mkono wake kwaharaka na mkono wangu wa kushoto, huku naachia ngumi moja nzito kwa kumkono wangu wa kulia , ambayo ilitua usoni kwake usawa wa kati ya pua na mdomo, ambayo ilimlegeza na kumfanya ayumbe kidogo, lakini bado aling’ang’ania kisu chake ambacho kilishikwa na mkono wake wa kulia niliokuwa nimeushika kwa nguvu, hapo nikamvuta kwangu na kumzungusha kwa nguvu mfano wa mtu anaecheza music wa charanga na mpenzi wake, nae akaja usawa wa kifua changu akiwa ametazama kule nakotazama mimi, huku kisu alicho kishika mwenyee kikipita shingoni mwake na kuanza kurusha damu kwa nguvu, ilikuwa rahisi kumuuwa mandevu, lakini yenye kuhitaji moyo mgumu kama vile kumuibia kipofu, yaani ni rahisi sana, ila ukiwa na moyo wa huruma huwezi kufanya hivyo.
Nilipomuachia Mandevu nikamuona akipepesuka kama mlevi, kisha akajibwaga chini karibu na piki piki yake, hapo nikarudi kwenye gari haraka, na kuondoa gari kuelekea Vitongoji, sikuwasha taa mpaka tulipompita Mandevu na Piki piki yake sikutaka Jessenia ajuwe kilichotokea, “mbona amelala pale, kwani ameumia sana alivyoanguka?” aliulizaJessenia wakati tuna pita alipolala Mandevu, “achana nae ameshindwa hata kunieleza chochote” nilimjibu Jessenia, huku nakanyaga mafuta na kuwasha taa za gari, maana tayari tulikuwa tumeshapita eneo lile, lenye picha ya kutisha ya Mandevu aliechinjwa kama mbuzi, picha ambayo kama Jessenia angeiona sidhani kama tungeweza kuelewana kwa muda huu, “lakini Eric unakumbuka babu Mangeu alisema tukalale Mantariff, yaani huku kwako lazima watatufuata tu” alisema Jessenia kwa sauti ya uoga, “huku kuna vitu naenda kuchukuwa, kisha twende zetu Mantariff” nilimueleza Jessenia.
Ilikuwa hivyo, green house nilitumia muda mchache sana nikichukuwa lap top na vifaa vyote vya kazi, ikiwa kisu nguo chache, viatu na fedha za kutosha, japo nyingine alisha nipatia babu Mangeu, nilitandika kitanda vizuri na kuzima taa za ndani, nikafunga mlango kisha tukaondoka zetu nikiwa nimevaa tisht nyingine maana lile la mwanzo lilikuwa limechafuka damu za Mandevu, lakini sikuliacha nililihifadhi ndani ya begi kwenye mfuko wa pembeni.
Tulitoka kwa mwendo wa speed lengo langu likiwa ni kuwahi kupita pale Ngerengere, kabla watu hawajaona mwili wa Mandevu na kuita Polisi, lakini haikusaidia lolote, maana tulipokaribia eneo lile nikaona kuna mwanga wa taa za gari, na mbaya zaidi tulikuwa kama mita mia moja tu kufikia pale kwenye tukio, hivyo nikapunguza mwendo na kutembea mwendo wa kawaida kusogelea eneo la tukio, “watu wameenda kumsaidia” alisema Jessenia, kwa sauti ambayo bado ilikuwa na hofu, ni baada ya kuanza kuona watu wakiwa wamezunguka eneo lile ambalo lilikuwa linamulikwa na taa za gari, lakini mimi tayari nilisha gundua kuwa wale mbele yetu ni polisi, “Jesse nenda seat ya nyuma” nilimueleza Jessenia kwa sauti ya chini, huku nazidi kupunguza mwendo, japo tulikuwa tunazidi kusogelea eneo lile, ambapo nilimuona polisi mmoja mwenye cheo cha constable, akisogea barabarani na kutupungia mkono kutusimamisha, hapo nikapunguza mwanga wa taa za gari huku nasimama, wakati huo Jessenia akiwatayari amesha hamia seat ya nyuma.
Yule askari alisogelea kwenye mlango wa dereva, ambako nilikuwa nimekaa, nikashusha kioo , “habari kaka naona mupo kazini” nilimsemesha yule polisi kabla hajaniambia chochote, ndiyo kamanda si unajuwa kazi zetu ni sawa tu na nyie” alijibu yule polisi, akidhania kuwa na mimi ni askari wa jeshi la ulinzi, “unadhani mimi nikamanda basi, mimi ni mwalimu, sema ninakaa kambini” nilijibu huku tazama pale chini, ambapo tayari walisha uondoa mwili wa Mandevu na pikipiki yake na kabla yule polisi hajajibu kitu, akaongezeka askari mwingine , hapo moyo wangu ukalipuka kwa mshtuko, “Ticha Eric, afadhari nimekuona” ilikuwa ni sauti ya insp Aroub, ambae alikuwa amekuja moja kwa moja kwenye mlango wa gari, sasa walikuwa wawili, “salama tu mzee, naona leo upo busy sana” nilimjibu Aroub ambae kiukweli sikutamani mzee huyu agundue kama Jessenia yupo ndani ya gari, au kufungua mdomo wake kuongea lolote juu ya uchunguzi wetu na sikutaka Jessenia apate wazo la kumshitakia Ussi kwa insp Aroub, “busy kweli kweli, lakini ilikuwa muhimu tuonane, alienipa moyo ni Malambo, ambae alisema kuwa lazima ungekuja pale Mess kwa chakula cha jioni” hapo nilishaona dalili za maongezi ya muda mrefu, ambayo yange haribu mambo….…. ENDELEA..
 
KIFO CHA HAWARA (mkono wa jini)
SEHEMU YA SABINI NA MOJA
MTUNZI: Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA SABINI: “salama tu mzee, naona leo upo busy sana” nilimjibu Aroub ambae kiukweli sikutamani mzee huyu agundue kama Jessenia yupo ndani ya gari au kufungua mdomo wake kuongea lolote juu ya uchunguzi wetu, na sikutaka Jessenia apate wazo la kumshitakia Ussi kwa insp Aroub, “busy kweli kweli, lakini ilikuwa muhimu tuonane, alienipa moyo ni Malambo, ambae alisema kuwa lazima ungekuja pale Mess kwa chakula cha jioni” hapo nilishaona dalili za maongezi ya muda mrefu, ambayo yange haribu mambo….…. ENDELEA..
Hivyo nilitakiwa kutumia akili kufupisha maongezi yale, “hooo! kumbe, basi wacha nikuache umalie jukumu hilo, mimi natangulia tutaonana baadae pale mess” nilimueleza Aroub, huku napachika gia na kuanza kuondoka taratibu, “sawa mwandishi, ila kuwa makini bwana, kipindi cha uchaguzi mambo huwa hovyo sana, si unaona hapa tumekuta mtu amechinjwa kabisaaaa” alisema mzee Aroub, hapo sikujibu lolote nikakanyaga mafuta na kuondoka, huku nikimuona Jessenia akichugulia nje kwa umakini mkubwa, kama angeona chochote nadhani aliona damu ambazo zilikuwa zimetapakaa kwenye lami, hapo nikamuona Jessenia akiwa kimya kabisa kule kwenye seat ya nyuma ya gari lile dogo, “unaweza kurudi huku mbele” nilimsemaesha Jessenia, ambae alionekana kuwa katika mawazo mazito sana, “huku kunatosha” alijibu akiwa katika hali ya uoga mara dufu ya ule mwanzo, hapo sikumsemesha tena mpaka tulipofika Wawi Mess ambapo palikuwa na watu wengi kiasi, hasa waschana wengi waliotokea bara mkoa wa Tanga, usinge amini kuwa ni kisiwa cha pemba, ungedhania kuwa ni moja ya kumbi za starehe za Tanzania bara.
Nilisimamisha gari kwenye maegesho ya pale mess palipojaa magari mengi ya serikali, “nisubiri nakuja sasa hivi” nilimuambia Jessenia, aliekuwa amekaa seat ya nyuma, ambae sikumsikia akijibu lolote na mimi bila kujiuliza sababu ya Jessenia kukaa kimya nikashuka toka kwenye gari na kuelekea kwenye lango la ukumbi, lakini kabla sijafikia lango la ukumbi, Mwasenga akanidaka, “ticha vipi ndio unasepa au?” aliuliza Mwasenga, huku anajitoa kwa wenzake ambao pia walivalia sale za kazi na kunisogelea, na wezake pia walinisalimia wakiwa pale waliposimama, niliitikia na kumjibu Mwasenga, “ndiyo kaka ila nataka nionane na Malambo kwanza” nilimueleza Mwasenga, ambae aliniambia kuwa Malambo hakuwa amekaa ndani ya ukumbi, “yeye na wenzake wamekaa kul….” kabla hajamaliza kunieleza akasita kidogo, huku akitazama upande alio ukusudia, “tena yule pale anataka kuingia ukumbini” alisema Mwasenga huku anaonyesha kule alikokuwepo Malambo, nikachomka haraka kumuwahi bwana Malambo, ambae kiukweli aliponiona alishtuka vibaya sana, “huuu Ticha, afadhari nimekuona upo salama” alisema Malambo huku ananishika mkono na kusogeza pembeni zaidi, nikajuwa amesha pata habari za kule Msingini, “kuna nini Malambo, mbona kama umeshtuka sana” nilimuuliza ili kumchochea aseme anacho kijuwa, “kuna taarifa zilifika hapa kuptia jeshi la polisi, kwamba kuna mtu anae sadikiwa kuwa ni mwizi amekimbizwa mitaa ya msingini karibu na kwa yule demu wako, hapo moja kwa moja nikakufikiria wewe isije kuwa Ussi amefanya mchezo flani ili ushambuliwe kwaajili ya wivu wake, maana namjuwa vizuri yule jamaa hatakagi kuona mtu yupo na Seni, na isitoshe mpaka sasa hajaingia hapa Mess, na mbaya zaidi inasemekana kuna mtu amekutwa ameuwawa huko ngerengere” alinieleza Malambo, ambae alisema kuwa na sasa alikuwa ameitwa na mkuu wa kambi, “nadhani anataka akaniambie swala hilo hilo” na mimi ambae sikutaka kutumia muda mrefu mahali hapa nikamueleza Malambo kuwa ninahitaji kwenda sehemu na Jessenia, lakini sitaki mtu mwingine ajuwe, “nitakueleza kesho jinsi ilivyokuwa” nilimuambia Malambo, ambae alishangaa na kushtuka zaidi, baada ya kugundua kuwa mimi ndie niliekimbizwa huko Msingini.
Hakukuwa na maongezi mengi, hivyo tuliagana na mimi nikarudi kwenye gari kwaajili ya kuanza safari, lakini nilichokikuta kilinishtua kidogo, “Jesse mbona umeshuka kwenye gari, huoni kama ni hatari kwako endapo watakuona watu wanaotumwa na mjomba wako wakufuatilie?” nilimuuliza Jessenia kwa sauti ya chini, ambae nilimkuta ameshuka toka kwenye gari na kusimama nje ya gari na viatu vyake mkononi, “Eric, siingii ndani ya gari mpaka uniambie wewe ni nani na unafahamiana vipi na mzee Mangeu, na nini kinaendelea kuhusu wakina Ussi” alisema Jessenia, kwa sauti ambayo haikuwa na dalili hata chembe ya utani, nikatazama kushoto na kulia, kama kuna mtu karibu yetu, hakika hakuwepo hata mmoja, “Jesse ni hatari kwako, hebu twende nitakueleza kila kitu, siwezi kukuficha hata moja” nilimueleza Jessenia, kwa sauti tulivu ya kubembeleza, lakini haikusaidia, “hatari ni ipi Eric, watu walionilea toka utotoni au wewe usie eleweka, mara Pross mara Eric, mara mwalimu, mara mwandishi, mara ukae kwenye nyumba za jeshi, mara unamfahamu Aroub, mara unamfahamu Mangeu, unapigana na watu saba, unamchinja m…” hapo nikawahi na kumziba mdomo asimalizie kuongea maana alikuwa anazidi kupandisha sauti kila sekunde, “ok! ngoja nikueleze Jesse, hao ulio wataja hakuna hata mmoja anae nifahamu mimi ni nani, na wote nimefahamiana nao kwa sababu yako wewe ulienifanya nije Pemba” nilimueleza Jessenia ambae nilimuona akitoa macho kwa mshangao, “mimi nimekufanya uje pemba?” aliuliza huku anatabasamu kwa dharau, aliona kama nina mdanganya kitoto, “ndiyo jesse nimekuja Pemba kwaajili yako” nilimuambia jesse huku nacheka kidogo, alinifurahisha kwa uulizaji wake, “najuwa wanaume hudanganya ili kuvutia hisia za mwanamke, lakini ni vyema kwanza tukilimaliza hili ndio uanze upuuzi wako, naomba unieleze ninachotaka kujuwa, vinginevyo nitaenda kujipeka kwa polisi, inaweza kuwa ndiyo sehemu salama kwangu” alisema Jessenia, huku akionyesha baadhi ya polisi waliokuwepo pale mess kwaajili ya wageni wao waliokuja kupata burudani, nikamtazama Jessenia kwa sekunde kadhaa, kisha nikaanza kumueleza, “ok! mimi naitwa Eric Frank, ni mpelelezi wa shirika binafsi, ambae nimetumwa kuja kuchunguza mauwaji yanayoendelea yanayo sadikika kuwa yanafanywa na jini” nilimueleza Jessenia, ambae alionekana kunitazama kwa jicho la mshtuko na mshangao, “siku ya kwanza kukuona, ndio ilikuwa siku ya kwanza mimi kufika Pemba” nilimueleza Jessenia kila kitu pasio kumficha kitu chochote, kuanzia nilivyo anza uchunguzi na mpaka yeye akaja kunieleza kuwa ndie mwanamke ambae anahisiwa kuwa ni jini, pia nikamueleza jinsi nilivyokuwa nafuatiliwa na mzee Mangeu, na wale jamaa wa Ussi, ambao walijaribu kuniuwa mara kadhaa, na jinsi walivyokuwa wanachungulia pale Green house, pia nikamueleza jinsi nilivyopambana na wale jamaa wa Ussi na mmoja akameza sindano yenye sumu na kukauka, kisha mwili wake kwenda kutupwa Migombani, “unataka kuniambia mjomba na Ussi ndio wanao wauwa watu wote hao” aliuliza Jessenia ambae sasa alikuwa amesha fungua mlango wa nyuma wa gari na kukaa kwenye seat lakini miguu yake peku peku ikiwa chini, “sio hao tu na sasa wanataka kutuuwa mimi na wewe, na pengine Mangeu” nilimueleza Jessenia, ambae hapo alipata swali, “sasa kwanini wanafanya hivyo, na Mangeu anahusikaje katika maisha yangu?” aliuliza Jessenia, ambae bado alikuwa katika mshangao mkubwa sana, “mjomba wako na Ussi wanafanya mauwaji ili usiolewe na mtu mwingine, zaidi ya yule ambae wao watamtaka” nilimueleza Jessenia, ambae alikuwa na maswali mengi sana, “kivipi Eric, mbona sikuelewi” aliuliza Jessenia, “mwanzo familia ya mzee Juma walitaka uolewe na Ussi ilikupata kila ulichonacho, ndio maana mara ya kwanza waliwaachia nyumba nzima wakakunywesha wine na wewe ukaenda kujifungia chumbani, hapo uliharibu mpango, ndipo walipokupeleka kwa mganga na kukuambia mizimu inataka uolewe na binamu yako, na wewe binamu pekee unaemfahamu ni Ussi, lakini hapo ikawa ngumu, maana tayari mipango yao ilisha gunduliwa na kuzuiliwa” nilimueleza Jessenia, ambae alicheka kidogo, tena kicheko cha dharau, “Eric, unaweza kuacha kunitania na kunieleza ukweli, niolewe na Ussi ili wapate nilicho nacho nini, Uchi wangu, maana ndio pekee nilicho nacho” alisema Jessenia kwa sauti yenye kuchoshwa na uongo, huku anainuka na mimi nikawahi kumzuia, “subiri nikueleze Jesse” nilimweleza huku namrudisha pale alipokuwa amekaa, “naomba usinizungushe Eric, nitaenda kujisalimisha kwa wale polisi” alisema Jessenia, na hapo nikaona kuwa sikuwa na sababu ya kumzungusha, maana nikichelewa ataharibu mambo na kunifanya nikose kukamilisha ushahidi na kuwakamata wakina Ussi kwa mauwaji waliyo yafanya, “Jesse mzee Juma Mohamed sio mjomba wako, na kila unacho kiona anakimiliki ni mali yako, kuanzia nyumba mpaka magari kimetokana na fedha yako, haya sasa umeelewa?” nilimuuliza Jessenia, ambae alikuwa anitazama kwa macho yakunishangaa, kisha akaachia kicheko cha ghafla, ambacho kilidumu kwa dakika nzima, kisha ghafla akatisha kicheko chake na kunitazama kwa macho yenye hasira, “hivi unajaribu kunifanya mimi mpuuzi Eric, naomba uniambie ukweli Eric, nakupa nafasi ya mwisho?” alisema Jessenia, kwa sauti ya ukali……….…. ENDELEA..

KIFO CHA HAWARA (mkono wa jinni)
SEHEMU YA SABINI NA MBILI
MTUNZI: Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA SABINI NA MOJA: “Jesse mzee Juma Mohamed sio mjomba wako, na kila unacho kiona anakimiliki ni mali yako, kuanzia nyumba mpaka magari kimetokana na fedha yako, haya sasa umeelewa?” nilimuuliza Jessenia, ambae alikuwa anitazama kwa macho yakunishangaa, kisha akaachia kicheko cha ghafla, ambacho kilidumu kwa dakika nzima, kisha ghafla akatisha kicheko chake na kunitazama kwa macho yenye hasira, “hivi unajaribu kunifanya mimi mpuuzi Eric, naomba uniambie ukweli Eric, nakupa nafasi ya mwisho?” alisema Jessenia, kwa sauti ya ukali….…. ENDELEA..
Hapo nikaona Jessenia anakaribia kuharibu mambo, dawa nikuweka wazi kila kitu, “nakuambia ukweli Jesse, familia ya kina Ussi sio ndugu zako, anaemfahamu marehemu mama yako ni mzee Zidadu peke yake, ambae ndie alieokoa maisha yako, huku mama yako akifariki, kabla ya kufika hospital” nilimueleza Jessenia, kuhusu historia halisi ya wazazi wake na mzee Mangeu, mpaka kufikia mama yake kupata ujauzito nakuzaliwa yeye, huku mzee Mangeu akimpa kila msaada uliohitajika katika kuokoa maisha ya mama yake “mama yako yani bi Aisha ambae jina lake harisi ni Celine alishambuliwa na mke wa Abdulkarim ni mwarabu toka oman, ambae ndie baba yako” nilimueleza Jessenia jinsi mzee huyo alivyojitolea kushambuliwa mpaka kumuokoa yeye na kumpatia mfanyakazi wa nyumba aliyoinunua kwaajili ya Aisha na mtoto wake yaani yeye Jessenia, ambae jina alilopewa na mama yake ni Josephiner, saa tatu na nusu ilitukuta hapo nikimaliza kumsimulia, Jessenia historia hiyo, “ina maana babu Mangeu ndie ndugu wa peke nilie nae kwa sasa?” aliuliza Jessenia ambae machozi yalikuwa yanamtiririka mshavuni” na wakati huo nikaliona gari la Ussi linakata kona kuingia pale Mess, “Jesse ni vyema ukiingia ndani ya gari kwa usalama wako, ni jukumu langu kuhakikisha hupatwi na tatizo lolote” nilimuambia hivyo huku namsogeza miguu yake ndani ya gari kisha nikafunga mlango, nashukuru hakuwambishi.
Na mimi nikaingia ndani ya gari na kutulia kidogo, tukilitazama gari la Ussi likiingia pale Mess na kwenda kupaki pembeni ya gari la pili toka kwenye gari letu, na wakati huo huo nikaliona gari la polisi likiingia, ni lile ambalo alikuwa nalo kule kwenye eneo la tukio la bwana mandevu, nae akaenda kuegesha upande wa pili wa eneo lile, ambalo leo limetumika kama maegesho pia, na tukiwa tunaendelea kuwatazama wakina Ussi, tuliwaona wakishuka saba toka ndani ya gari lile, huku wakiwa wamevaa vile vile kama walivyokuwa kule msingini wakati wanatushambulia.
Waliposhuka nikawaona wanaelekea kwenye lango la ukumbi, ambapo sasa music ulikuwa unasikika kwa sauti ya juu, lakini kabla hawaja lifikia lango Ussi akamuona Mwasenga na kumfuata, hapo nikajuwa sasa hivi mambo yana badilika na kugeuka uwanja wa mapambano, hivyo nikawasha gari na kuondoka pale taratibu, huku tukiwa kimya, huku mimi nikitazama kwenye side mirror na kumuona Ussi na wenzake wanarudi kwenye gari haraka haraka, “Eric fanya haraka wanaingia kwenye gari” alisema Jessenia, hapo nikagundua kuwa na yeye alikuwa anawatazama wakina Ussi kupitia kioo cha nyuma ya gari, “usiwe na wasi wasi, wameshachelewa” nilijibu kwa sauti tulivu isiyo na wasi wasi, huku napunguza mwendo na kuwasha taa za kuelekeza kuwa naingia upende wa kulia, ambako ni uelekeo wa Vitongoji, yaani Ali Khamis Camp, “unaenda wapi Eric, Ussi anakimbiza sana gari atatukuta sasa hivi, halafu wana mapanga wale” alisema Jessenia kwa sauti yenye wasi wasi, huku anatazama nyuma kuwatazama wakina Ussi, ambao sasa walikuwa wanalifikia gari na kuanza kufungua milango, maana tayari alishailock, mpaka wanaingia ndani ya gari mimi nilikuwa nimesha ingia barabara kuu na kukanyaga mafuta kwa nguvu, ndani ya sekunde kumi tayari nilikuwa ni speed mia moja kwa kwa saa, ungesema ninaenda mbali sana, hata wakati tunaikamata njia panda ya Vitongoji na kule nyumba za kijiji tukaona mwanga wa taa za gari linaingia barabarani na kuja upande wetu, hapo nikapunguza mwendo kidogo na kuingia kushoto kuelekea Vitongoji na kupotea kabisa machoni pao, hapo sikuenda hata mita ishirini, “jishikilie Jesse” nilimueleza Jessenia kisha nikakanyaga blake za ghafla na kupunguza kabisa mwendo kisha nikaingiza gari pembeni ya barabra na kuegesha gari nje ya nyumba moja, kati nyingi zilizokuwepo pale, halafu nikazima engine ya gari pamoja na taa.
Naam haikupita hata dakika, tukaanza kusikia ngurumo ya gari na sekunde chache baadae tukaona mwanga wa taa za gari ukija upande wa barabara ya vitongoji, ikifuatiwa na gari lililokuwa katika speed kali sana kuelekea vitongoji, na hapo nikawasha gari na kulipa cha uwani, nilipoikamata barabra nikalipa D na kukanyaga mafuta kuelekea upande wa macho mane, yani kurudi tulikotoka, wakati huo huo nikasikia simu inaita, nilipoitazama alikuwa ni Mwasenga, nikaipokea, “hoya ticha umewaona hao wanakufuatilia?” aliuliza Ussi ambae siwezi kumlaumu, maana hakuwa anajuwa undani wa mambo yale, yeye alichojuwa ni kuwa ulikuwa ni wivu wa Ussi tu, “sijawaona maana mimi niliingia njia ya nyumba za kijiji, lakini sasa nageuka” nilimueleza Mwasenga, ambae nilimueleza kuwa nitampigia baadae, sasa nilikuwa naendesha gari, nae hakuwa mbishi akakata simu na mimi nikaiweka kwenye seat ya pembeni yangu, maana Jessenia alikuwa seat ya nyuma, tuka pita wawi mess.
Naam tulikatiza wawi na kwenda kusimama Macho Manne, ambapo nilitumia dakika chache sana kununua chakula na nguo kadhaa za Jessenia, yaani gauni mbili, hijab, na chupi, halafu nikatoka na kununua chakula kisha nikaingia ndani ya gari na kuliondoa taratibu kama vile hatukuwa na safari ya mbali, lakini nilipoikamata barabara ya Wete, ndipo nilipoongeza mwendo.
Safari ilikuwa kimya kimya Jessenia akiwa seat ya nyuma, ni wazi alikuwa anatafakari kile nilicho msimulia juu ya kuwa mzee Juma sio mjomba wake, na hawana undugu wowote, na kwamba mzee Mangeu mzee ambae siku zote anahisiwa na kuchukuliwa kuwa ni mtu hatari na mbaya, Jessenia ambae hata mjomba na shangazi yake walisha muonya juu yake ya kwamba ni mtu asiefaa katika jamii, kumbe ndie mtu aliepigania maisha yake, huku akiharibu uso wake mwenyewe, pengine alikuwa anawaza kuhusu jinsi alipoteza wanaume anao wapenda, akidhania kuwa anatatizo la kuwa na jini, ambalo halitaki aolewe wala kuwa karibu na mwaume, au anawaza juu ya mimi kuwa ni mpelelezi.
Sikutaka kumsemesha, maana ukweli sikuwa na uhakika alichokuwa anakiwaza, nakumbuka tukiwa tumeshaiacha wete, mji ambao ulikuwa kimya mida ile, nilipokea simu toka kwa babu Mangeu, “vipi Eric mupo wapi sasa hivi?” aliuliza Mangeu, kwa sauti ya chini, ikionyesha kuwa alikuwa sehemu ambayo haikuhitaji kelele, “tupo mtambwe tunaeleka Jando” nilimjibu Mangeu, huku naendelea kukanyaga mafuta kwenye barabara ambayo haikuwa nzuri sana, “ok! nimesha fanya malipo hotelini, ukifika pale muone bwana Alex Kinka, yeye ndie aliepewa maelekezo ya ujio wenu kama watalii toka Dar es salaam” alisema Mangeu, ambae pia aliuliza kuhusu usalama wetu na kama kuna lolote lilitokea baada ya kuachana.
Na mimi nilimsimulia kama ilivyokuwa, “mimi bado nipo hapa, nimejibanza mita chache pembeni ya nyumba yangu, nimejiandaa kweli kweli, nina panga kubwa na pia nina pinde na mishale, maana siwezi kuondoka pasipo kuhakikisha usalama wa Seni” alisema Mangeu, “ok! mimi nitakuja kesho kuna kitu lazima tukipate hapo kwa Ussi ili kukamilisha ushahidi na kuwatia nguvuni” nilimuambia Mangeu, kabla hatujaagana na kukata simu, na safari ikaendelea huku nikianza kusikia kitu kama kilio cha kwi kwi toka kwa Jessenia, mwanzo nilijuwa analia kwa kuona kuwa aliodhania kuwa ndio ndugu zake kumbe ndio maadui zake, sikutaka kumsemesha kwa lolote maana isinge saidia kumtuliza, hivyo nilimuacha alie ili apunguze machungu.
Baada ya hapo hatukutembea kwa muda mrefu, mala simu ya Jessenia ikaita, akaitazama na kuiweka pembeni, “nani anapiga simu?” nilimuuliza Jessenia ambae hakunijibu chochote, huku simu ikiendelea kuita, “Jesse mbona hunijibu, au kuna tatizo?” niliuliza kwa sauti ya kujifanya nashangaa, lakini bado Jessenia hakujibu kitu, na mbaya zaidi ndiyo kwanza akazidi kulia kwa sauti ya chini, wakati huo tayari tulisha anza kuona taa za majengo ya Mantariff Lodge, nikaona itakuwa vyema kama nikinaanza kumtuliza Jessenia ili usiku wangu na yeye uwe mzuri, “Jesse, mbona hunijibu kuna baya nimefanya kwako?” nilimuuliza kwa lengo la kumchokoza, ili aweze kusema kile kinacho kwaza, “Eric siwezi kukuongea na wewe mpaka ujibu swali langu” alisema Jessenia kwa sauti ambayo ilikuwa dalili za mtu anaelia, “swali gani ambalo nitashindwa kukujibu Jesse, niulize tu nitakujibu” nilimueleza Jessenia kwa sauti tulivu, huku napunguza mwendo kuingia kwenye lango la kuingilia hapa hotelini.
Hapo Jessenia hakunipa hata nafasi ya kupumua, akanipa swali alilo kusudia kuniuliza, “Eric naomba unieleze utauweka wapi upendo wangu, ambao nimekupa nikiamini kuwa unanipenda toka moyoni, kumbe unapeleleza?” aliuliza Jessenia, kwa sauti ambayo ukweli haikuwa na hata chembe ya utani na hakika alihitaji jibu kwa haraka…….…. ITAENDELEA..
 
KIFO CHA HAWARA (mkono wa jini)
SEHEMU YA SABINI NA TATU
MTUNZI: Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA SABINI NA MBILI: Hapo Jessenia hakunipa hata nafasi ya kupumua, akanipa swali alilo kusudia kuniuliza, “Eric naomba nieleze utauweka wapi upendo wangu, ambao nimekupa nikiamini kuwa unanipenda toka moyoni, kumbe unanipeleleza?” aliuliza Jessenia kwa sauti ambayo ukweli haikuwa na hata chembe ya utani na ni hakika alihitaji jibu kwa haraka…….…. ENDELEA..
Hapo nilipunguza mwendo kabisa na kusimamisha gari kwenye maegesho ya hoteli ile ya kisasa, ambayo ilikuwa na magari machache sana, ambayo yaliashiria wateja hawakuwa wengi sana pale hotelini, ikiwa ni pamoja na mabusy madogo mawili, ambayo hubeba watalii hapa hotelini, music ulikuwa unasikika kwa mbali, huku watu kadhaa ambao ni wafanyakazi wakikatiza katika eneo lile wakiendelea na kazi zao.
Nilishuka toka kwenye gari na kufungua mlango wa nyuma wa gari, yaani kule alikokuwa Jessenia, kisha nikakaa karibu yake, wakati huo simu yake ilikuwa imekatika, “Jesse, nadhani unakumbuka nilikupenda hata kabla sijajuwa wewe ni nani na unahusikaje na swala hili, na bado nakupenda sana Jesse, siwezi kukuacha kwaajili ya kile kilichotokea, niliahidi kwa mzee Mangeu kuwa sitokuacha hata baada ya kumaliza jukumu..” hata kabla sijamaliza kuongea, akanikumbatia kwa nguvu, “asante Eric, wewe ndie mtu ambae nitaenda kuanzisha nae familia, nakupenda Eric, nilikupenda toka siku ya kwanza nilipokuona pale chake chake” alisema Jessenia, akiwa bado amenikumbatia, huku anajifutia machozi kwenye tishet langu maeneo ya kifuani, kiukweli maneno yake yalinigusa “sitokuacha mpenzi wangu, na wala sitofikiria kukuacha, nakupenda sana” nilimueleza Jessenia huku nampapasa mgongoni mwake, yani papasa yenyewe ni ile ya kubembeleza, nikasikia sauti ya kicheko flani cha furaha, kilicho ambatana na kuvuta kamasi nyepesi kwa Jessenia, ambae alikuwa ameacha kulia muda mfupi uliopita, na wakati huo huo simu yake ikaanza kuita tena, mimi ndie nilieichukuwa na kutazama jina la mpigaji alikuwa ni mjomba.
Ukweli swala hili lilisha ingia katika hatua mbaya ya kuweka kila kitu wazi, lakini kuna kitu nilikuwa nakihitaji toka kwa Ussi na njia pekee ya kukipata ni Jessenia ambae anaweza kuingia na kuchukuwa kitu hicho ambaho ni hard disc ya camera za ulinzi iliyoibiwa toka nyumbani kwa Vuai, “sikia Jesse, unatakiwa kupokea simu na usiongee kama umegundua lolote juu ya njama zao” nilimueleza Jessenia, kisha nikampatia simu, “sasa niwaambiaje wakati nimemuona Ussi anataka kunikata na panga?” aliuliza Jessenia, na hapo kweli niliona kuna kikwazo.
Nilitumia sekunde chache kupata jibu la swali la Jessenia, “sikia wewe wasikile watakachosema, maana lazima watahitaji kukudanganya ili uwaamini, na jifanye unawaamini, maana kuna kitu lazima kesho ukakichukue nyumbani kwenu” nilimueleza Jessenia ambae alijiweka sawa na kupokea simu na kuweka loud speeker “asalam aleykum” alisalimia Jessenia kwa sauti tulivu ya upole, “waleykum salam Seni, upo wapi wewe mbona unatia mashaka we mtoto, si unajuwa kuwa wageni wapo hapa nyumbani pamoja na mchumba wako?” ilikuwa ni sauti ya mjomba wake Jseenia, ambayo ilionekana kuwa na wasi wasi na hofu nyingi sana, lakini kwa nilivyo msikiliza, ule wasi wasi na hofu yake ilikuwa ni kama ya kuigiza, “nipo na mchumba wangu” alisema Jessenia na kunishtua kidogo, maana hilo sidhani kama lilikuwa kwenye makubaliano yetu, “mchumba ina maana bado tu umeng’ang’ania kuwa na yule kijana toka bara?” aliuliza mjomba kwa sauti ambayo ukiisikiliza kwa haraka, ungeamini kuwa mzee Juma Mohamed alishtuka sana kusikia vile, lakini kwa jinsi nilivyoisoma sauti ile ilikuwa na mshtuko bandia, ni wazi alikuwa anajuwa mpwa wake yupo na mimi, “mjomba nilishakueleza kuwa, huyu ndie mwanaume niliekubaliana nae atanioa, na ndie pekee niliempenda” alisema Jessenia kwa sauti tulivu ya upole, bila hata kunitazama usoni, lakini bado alikuwa kifuani kwangu, “sawa nimekuelewa Seni, kama kweli anania ya kukuoa, we rudi nyumbani sasa tuongee vizuri juu ya swala hilo na tuone tunafanya je” alisema Mjomba wake Jessenia kwa sauti tulivu ambayo ilionyesha amekubaliana na uchumba wangu na Jessenia.
Hapo Jessenia akanitazama usoni, huku anazuia kicheko, maana ni wazi kabisa maneno ya mjomba wake yalikuwa ni danganya toto, “mjomba kwa kweli leo utanisamehe, siwezi kurudi, yaani wakati narudi hapo nyumbani nimekutana na watu wanataka kunikata na panga” alisema Jessenia, hapo tuka tulia kusikia mjomba atasema nini, “weeeee usiambie Seni, ilikuwaje mpaka wakakufanyia hivyo, kwanini hukutupigia simu, na vipi uliwatambua hao washenzi?” aliuliza maswali kadhaa mjomba akionyesha kushtuka sana, lakini mshtuko wake ulikuwa ni wa bandia, “sijawajuwa hata mmoja, yaani kosa Eric ningekuwa nimesha kufa” alisema Jessenia na kumsimulia ilivyokuwa, huku akimficha kama tulisaidiwa na babu Mangeu, na kama tuliwaona wakina Ussi na wageni wao toka unguja, “basi jitahidi kesho uwahi nyumbani ili tujuwe la kufanya, naomba kuongea na huyo kijana aliekusaidia” alisema mzee Juma Mohamed, na hapo Jessenia akanitazama, nikamuonyesha ishara ya kukataa, “yupo bafuni anaoga” alisema Jessenia, huku bado ananitazama, “sawa, utamwambia nashukuru sana kwa msaada aliokupa ila kuweni makini” alisema mjomba wake Jessenia, ambae kabla hajakata simu ni kama alikumbuka jambo, “eti Seni, subiri kwanza usikate” alisema mjomba wake, na mimi nikamuonyeshea Jessenia ishara ya kwamba asikate simu, “ndiyo mjomba nakusikia” alisema Jessenia, “nilisahau kuuliza, kwani sasa mupo wapi?” aliuliza mjomba, na hapo nikatabasamu kidogo huku nikimueleza Jessenia kwa ishara namna ya kutoa jibu, “tulikuwa mess sasa hivi ndio tumeingia vitongoji nyumbani kwake hapa Ali Khamis Camp” alijibu Jessenia huku amenitolea macho, “hooo! kwahiyo …. ho! sawa usiku mwema, hakikisha unakuwa mbali na Mangeu, pengine yeye ndie alietuma watu wakudhuru” alisema mzee Juma na kukata simu, hapo wote tukacheka kidogo kwa ile kauli yake ya mwisho, “unadhani kwanini mjomba wako ameuliza sasa tupo wapi?” nilimuuliza Jessenia, huku tukiwa tumekaa ndani ya gari, si alitaka ajuwe sehemu tulipo” alijibu Jessenia, ambae sasa alikuwa amejitoa kifuani kwangu, “swali lina onyesha kwamba, alishaambiwa kuwa hatupo Green house, na sasa anataka ajuwe sehemu tulipo, na pengine kuwa julisha wakina Ussi watufuate kuja kutimiza lengo lao” nilimuambia Jessenia, ambae alitulia kidogo kutafakari jibu langu, kisha akauliza tena, “sasa kama ni hivyo, sasa kesho si wataniulia humo humo ndani, au unataka kunitoa chambo?” aliuliza Jessenia huku ananitazama kwa macho ya kunitilia mashaka, “siwezi kutuhusu baya lolote likukute Jesse, niamini nitakacho kuambia, mambo yote yataenda vizuri, na utakuwa na ulinzi mkubwa sana” nilimueleza Jessenia, nikimaliza kwa kumvuta kwangu na kukiss kwenye paji la uso.
Wakati huo huo tukasikia vishindo vyepesi vikisogelea gari, nikatazama upande ule vinakotokea nikamuona mschana mmoja mrembo alievalia suruali nyeusi na shati jeupe, akiwa hatua chache toka kwenye gari akija usawa wa gari letu, “habari za jioni jamani, karibuni” alisema yule mschana, huku anaachia tabasamu laini, hapo nikamuona Jessenia ananitazama kwa macho ya kipelelezi, kama nimelipokeaje lile tabasamu, “asante dada, tumesha karibia” nilijibu huku natoka nje ya gari, kisha nikaanza kumsaidia Jessenia kutoka nje ya gari, ambae alitanguliza begi langu dogo, akifuatia mfuko mdogo wenye nguo zake nilizonunua pale macho manne, “nikusaidie tafadhari, alisema yule yule dada muhudumu, huku akiachia tabasamu pana lenye ukarimu mwingi sana, akihitaji kutupokea begi na ule mfuko wa Jessenia, “hapana usijari tunakuja wenyewe, wewe waweza kutangulia tu” alisema Jessenia huku anashuka toka kwenye gari na viatu vyake mkononi, nikatabasamu kidogo, maana niliona wazi Jessnia hakupenda msaada wowote toka kwa yule mwanamke, “sawa, karibu sana lakini kama kuna msaada wowote munahitaji?” aliuliza yule mwanamke, na hapo nikawahi mimi kuongea, “nahitaji kuonana na Alex Nkika, tuliweka oder ya chumba na tumesha fanya malipo” niliulizia yule jamaa ambae mzee Mandevu alinielekeza, huku nampokea Jessenia viatu na kuviweka kwenye begi, “hooo! kumbe nyie ndio watalii toka dar, ameshaacha maagizo, chumba chenu ni kule juu, chumba cha Sulta Said” alisema yule mwana dada, ambae tabasamu lilikuwa halikauki mdomoni mwake, “ok! itakuwa vyema kama utatupeleka huku” nilimueleza yule dada huku na mshika mkono Jessenia ambae alionekana kutembea kwake ni shida, kwa maana nyanyo zilishaanza kuuma, ni kutokana na kukimbia muda mrefu bila kuvaa viatu” nikamsika vizuri na kuanza kumsadia kutembea vizuri, huku sasa yule dada akitupokea begi, na safari hii Jessenia akiridhia kupokelewa begi na yule mwanamke.
Dakika kumi na tano baadae, tayari tulikuwa chumbani kwetu, chumba ambacho kilikuwa na hadhi ya Sultani kweli sikujuwa ni bei gani kwa usiku mmoja, lakini kiukweli kilikuwa ni chumb kizuri, ambacho ukiachilia vitu vingi vilivyo tengenezwa kwa sanaa ya kale ya kiarabu, pia kilikuwa na bwawa dogo la kuogelea mule mule ndani, kitanda kikubwa cha kuvutia na vitu vingi ambavyo nikitaja kimoja baada ya kingine itachukuwa kurasa kadhaa mpaka kumaliza, ila vya muhimu ni pamoja na friji kubwa tv na kuta zake zilitawaliwa na kioo kikubwa pande tatu yaani mashariki ambako kulikuwa na misitu, na bahari kwa mbali kaskazni ambako pia kulikuwa na bahari, ambayo kwa usiku huu tuliweza kuona giza nene na magharibi ambako kulikuwa na taa nyingi sana ambazo zilimulika pwani, na hapo ungweza kugundua kuwa hotel hii ipo ufukweni, na ukitazama vizuri kwa mbali ungeweza kuona taa pwani ya mombasa na tanga.
Niliagiza mahitajio yetu ya usiku ule, ikiwa ni vyakula na vinywaji, mara nikasikia simu inaita, ilikuwa ni simu toka kwa insp Aroub, “hallow mzee habari za jioni” nilisalimia mara baada ya kupokea ile simu, “upo wapi kijana, nimehangaika sana kukutafuta, ujuwe kuna mambo nahitaji unielekeze, nimekutafuta hapa mess sijakuona kabisa wala gari lako halipo” alisema mzee Aroub kwa namna ya kulalamika, “mzee samahani mzee, nilifika hapo sikukaa sana nikaondoka zangu, ila sio mbaya hata mimi mwenyewe nilikuwa nahitaji kesho mida ya saa nne za asubuhi tuonane, yani juu chini kwa namna yoyote ile” nilimueleza insp Aroub, “sawa tena itakuwa vyema maana mida hiyo tutakuwa Ali Khamis camp Rais anahutubia” alisema insp Aroub na hapo nikaona kama vile kuna kitu kitakwama, maana nilihitaji mida hiyo akampe ulinzi Jessenia pale kwa mjomba wake, ili atafute hard disc kisha tumalize kazi kabla damu ya mtu mwingine haija mwagika, “halafu mwalimu, hivi unajuwa ule mwili tulio ukuta pale ngerengere ni wa mfanyakazi wa Uss, kijana wa mzee Juma” alisema mzee Aroub akionyesha kulifahamu hilo baadae, “hooo kumbe, kwahiyo bado unaamini kuwa kifo chake kinahusiana na siasa?” nilimuuliza insp Aroub kwa kumtega, “mpaka sasa nimeingiwa na mshaka, nahisi ni mauwaji yale yale yanaendelea, hivyo nimepanga kukutana na mzee Juma kesho, maana na yeye atakuwepo kwenye hotuba ya rais kule Ali Khamis, akiwa katika kundi la wazee chama wa hapa chake chake” alisema mzee Aroub, ambae ni wazi bado alikuwa pale mess, hapo tukaagana na kukata simu.

Dakika kumi baadae, tayari tulisha letewa mahitaji yetu ya vyakula na vinywaji, yani wine na vyakula mbali mbali tulivyo viagiza, na kabla hatujaenda kuoga nililazimika kwanza nimfanyie massage Jessenia, ambae ni wazi lazima angehitaji huduma hii, kwaajili ya kuweka sawa mwili wake, kutokana na misuko suko iliyotukuta muda mfupi ulipita, huku muda wote nawaza juu ya kitu ambacho natakiwa kukifanya ili kufanikiwa mpango wangu pasipo kuleta madhara kwa Jessenia, hata nilipopata wazo nikajitabasamulia mwenyewe huku naendelea kufanya massage juu ya mwili laini wa Jessenia, ambae niliamini leo asingeweza kupata hamu ya dudu hata kama angejibust kwa kwa ile dawa ya kupaka ya babu mabudi, lakini haikuwa hivyo.
Maana Jessenia akiwa amelala kifudi fudi kwenye kitanda maalumu cha kufanyia massaje karibu na bwawa dogo la kuogea mule mule chumbani, akiwa mtupu kabisa kama alivyo zaliwa, msambwanda wake ukiwa umetazama juu na kumwaga hips pembeni, nilianza kutembeza mikono yangu kuanzia kwenye nyayo za miguu yake, nikinibinya binya kwa kuikanda na mafuta mazuri ya karafuu, ni mguu mmoja baada ya mwingine, nikipandisha mkono wangu taratibu juu ya ngozi laini iliyopakaa mafuta ya karafuu, mpaka kwenye magoti ambapo palianza kuleta tatizo, hasa baada ya kuanza kutembeza vidole nyuma ya goti, huku nikibinya binya taratibu, nadhani nilikuwa na mtekenya, maana japo alikuwa ametulia lakini kuna vitu vilinipa ishara kwamba kuna kitu kina mpwita……….…. ITAENDELEA
 
Hamieni jinsi Biashara ya Huba ilivyonikutanisha na Dada mrembo wa ajabu.😀😀😀😀
 
KIFO CHA HAWARA (mkono wa jini)
SEHEMU YA SABINI NA TATU
MTUNZI: Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA SABINI NA MBILI: Hapo Jessenia hakunipa hata nafasi ya kupumua, akanipa swali alilo kusudia kuniuliza, “Eric naomba nieleze utauweka wapi upendo wangu, ambao nimekupa nikiamini kuwa unanipenda toka moyoni, kumbe unanipeleleza?” aliuliza Jessenia kwa sauti ambayo ukweli haikuwa na hata chembe ya utani na ni hakika alihitaji jibu kwa haraka…….…. ENDELEA..
Hapo nilipunguza mwendo kabisa na kusimamisha gari kwenye maegesho ya hoteli ile ya kisasa, ambayo ilikuwa na magari machache sana, ambayo yaliashiria wateja hawakuwa wengi sana pale hotelini, ikiwa ni pamoja na mabusy madogo mawili, ambayo hubeba watalii hapa hotelini, music ulikuwa unasikika kwa mbali, huku watu kadhaa ambao ni wafanyakazi wakikatiza katika eneo lile wakiendelea na kazi zao.
Nilishuka toka kwenye gari na kufungua mlango wa nyuma wa gari, yaani kule alikokuwa Jessenia, kisha nikakaa karibu yake, wakati huo simu yake ilikuwa imekatika, “Jesse, nadhani unakumbuka nilikupenda hata kabla sijajuwa wewe ni nani na unahusikaje na swala hili, na bado nakupenda sana Jesse, siwezi kukuacha kwaajili ya kile kilichotokea, niliahidi kwa mzee Mangeu kuwa sitokuacha hata baada ya kumaliza jukumu..” hata kabla sijamaliza kuongea, akanikumbatia kwa nguvu, “asante Eric, wewe ndie mtu ambae nitaenda kuanzisha nae familia, nakupenda Eric, nilikupenda toka siku ya kwanza nilipokuona pale chake chake” alisema Jessenia, akiwa bado amenikumbatia, huku anajifutia machozi kwenye tishet langu maeneo ya kifuani, kiukweli maneno yake yalinigusa “sitokuacha mpenzi wangu, na wala sitofikiria kukuacha, nakupenda sana” nilimueleza Jessenia huku nampapasa mgongoni mwake, yani papasa yenyewe ni ile ya kubembeleza, nikasikia sauti ya kicheko flani cha furaha, kilicho ambatana na kuvuta kamasi nyepesi kwa Jessenia, ambae alikuwa ameacha kulia muda mfupi uliopita, na wakati huo huo simu yake ikaanza kuita tena, mimi ndie nilieichukuwa na kutazama jina la mpigaji alikuwa ni mjomba.
Ukweli swala hili lilisha ingia katika hatua mbaya ya kuweka kila kitu wazi, lakini kuna kitu nilikuwa nakihitaji toka kwa Ussi na njia pekee ya kukipata ni Jessenia ambae anaweza kuingia na kuchukuwa kitu hicho ambaho ni hard disc ya camera za ulinzi iliyoibiwa toka nyumbani kwa Vuai, “sikia Jesse, unatakiwa kupokea simu na usiongee kama umegundua lolote juu ya njama zao” nilimueleza Jessenia, kisha nikampatia simu, “sasa niwaambiaje wakati nimemuona Ussi anataka kunikata na panga?” aliuliza Jessenia, na hapo kweli niliona kuna kikwazo.
Nilitumia sekunde chache kupata jibu la swali la Jessenia, “sikia wewe wasikile watakachosema, maana lazima watahitaji kukudanganya ili uwaamini, na jifanye unawaamini, maana kuna kitu lazima kesho ukakichukue nyumbani kwenu” nilimueleza Jessenia ambae alijiweka sawa na kupokea simu na kuweka loud speeker “asalam aleykum” alisalimia Jessenia kwa sauti tulivu ya upole, “waleykum salam Seni, upo wapi wewe mbona unatia mashaka we mtoto, si unajuwa kuwa wageni wapo hapa nyumbani pamoja na mchumba wako?” ilikuwa ni sauti ya mjomba wake Jseenia, ambayo ilionekana kuwa na wasi wasi na hofu nyingi sana, lakini kwa nilivyo msikiliza, ule wasi wasi na hofu yake ilikuwa ni kama ya kuigiza, “nipo na mchumba wangu” alisema Jessenia na kunishtua kidogo, maana hilo sidhani kama lilikuwa kwenye makubaliano yetu, “mchumba ina maana bado tu umeng’ang’ania kuwa na yule kijana toka bara?” aliuliza mjomba kwa sauti ambayo ukiisikiliza kwa haraka, ungeamini kuwa mzee Juma Mohamed alishtuka sana kusikia vile, lakini kwa jinsi nilivyoisoma sauti ile ilikuwa na mshtuko bandia, ni wazi alikuwa anajuwa mpwa wake yupo na mimi, “mjomba nilishakueleza kuwa, huyu ndie mwanaume niliekubaliana nae atanioa, na ndie pekee niliempenda” alisema Jessenia kwa sauti tulivu ya upole, bila hata kunitazama usoni, lakini bado alikuwa kifuani kwangu, “sawa nimekuelewa Seni, kama kweli anania ya kukuoa, we rudi nyumbani sasa tuongee vizuri juu ya swala hilo na tuone tunafanya je” alisema Mjomba wake Jessenia kwa sauti tulivu ambayo ilionyesha amekubaliana na uchumba wangu na Jessenia.
Hapo Jessenia akanitazama usoni, huku anazuia kicheko, maana ni wazi kabisa maneno ya mjomba wake yalikuwa ni danganya toto, “mjomba kwa kweli leo utanisamehe, siwezi kurudi, yaani wakati narudi hapo nyumbani nimekutana na watu wanataka kunikata na panga” alisema Jessenia, hapo tuka tulia kusikia mjomba atasema nini, “weeeee usiambie Seni, ilikuwaje mpaka wakakufanyia hivyo, kwanini hukutupigia simu, na vipi uliwatambua hao washenzi?” aliuliza maswali kadhaa mjomba akionyesha kushtuka sana, lakini mshtuko wake ulikuwa ni wa bandia, “sijawajuwa hata mmoja, yaani kosa Eric ningekuwa nimesha kufa” alisema Jessenia na kumsimulia ilivyokuwa, huku akimficha kama tulisaidiwa na babu Mangeu, na kama tuliwaona wakina Ussi na wageni wao toka unguja, “basi jitahidi kesho uwahi nyumbani ili tujuwe la kufanya, naomba kuongea na huyo kijana aliekusaidia” alisema mzee Juma Mohamed, na hapo Jessenia akanitazama, nikamuonyesha ishara ya kukataa, “yupo bafuni anaoga” alisema Jessenia, huku bado ananitazama, “sawa, utamwambia nashukuru sana kwa msaada aliokupa ila kuweni makini” alisema mjomba wake Jessenia, ambae kabla hajakata simu ni kama alikumbuka jambo, “eti Seni, subiri kwanza usikate” alisema mjomba wake, na mimi nikamuonyeshea Jessenia ishara ya kwamba asikate simu, “ndiyo mjomba nakusikia” alisema Jessenia, “nilisahau kuuliza, kwani sasa mupo wapi?” aliuliza mjomba, na hapo nikatabasamu kidogo huku nikimueleza Jessenia kwa ishara namna ya kutoa jibu, “tulikuwa mess sasa hivi ndio tumeingia vitongoji nyumbani kwake hapa Ali Khamis Camp” alijibu Jessenia huku amenitolea macho, “hooo! kwahiyo …. ho! sawa usiku mwema, hakikisha unakuwa mbali na Mangeu, pengine yeye ndie alietuma watu wakudhuru” alisema mzee Juma na kukata simu, hapo wote tukacheka kidogo kwa ile kauli yake ya mwisho, “unadhani kwanini mjomba wako ameuliza sasa tupo wapi?” nilimuuliza Jessenia, huku tukiwa tumekaa ndani ya gari, si alitaka ajuwe sehemu tulipo” alijibu Jessenia, ambae sasa alikuwa amejitoa kifuani kwangu, “swali lina onyesha kwamba, alishaambiwa kuwa hatupo Green house, na sasa anataka ajuwe sehemu tulipo, na pengine kuwa julisha wakina Ussi watufuate kuja kutimiza lengo lao” nilimuambia Jessenia, ambae alitulia kidogo kutafakari jibu langu, kisha akauliza tena, “sasa kama ni hivyo, sasa kesho si wataniulia humo humo ndani, au unataka kunitoa chambo?” aliuliza Jessenia huku ananitazama kwa macho ya kunitilia mashaka, “siwezi kutuhusu baya lolote likukute Jesse, niamini nitakacho kuambia, mambo yote yataenda vizuri, na utakuwa na ulinzi mkubwa sana” nilimueleza Jessenia, nikimaliza kwa kumvuta kwangu na kukiss kwenye paji la uso.
Wakati huo huo tukasikia vishindo vyepesi vikisogelea gari, nikatazama upande ule vinakotokea nikamuona mschana mmoja mrembo alievalia suruali nyeusi na shati jeupe, akiwa hatua chache toka kwenye gari akija usawa wa gari letu, “habari za jioni jamani, karibuni” alisema yule mschana, huku anaachia tabasamu laini, hapo nikamuona Jessenia ananitazama kwa macho ya kipelelezi, kama nimelipokeaje lile tabasamu, “asante dada, tumesha karibia” nilijibu huku natoka nje ya gari, kisha nikaanza kumsaidia Jessenia kutoka nje ya gari, ambae alitanguliza begi langu dogo, akifuatia mfuko mdogo wenye nguo zake nilizonunua pale macho manne, “nikusaidie tafadhari, alisema yule yule dada muhudumu, huku akiachia tabasamu pana lenye ukarimu mwingi sana, akihitaji kutupokea begi na ule mfuko wa Jessenia, “hapana usijari tunakuja wenyewe, wewe waweza kutangulia tu” alisema Jessenia huku anashuka toka kwenye gari na viatu vyake mkononi, nikatabasamu kidogo, maana niliona wazi Jessnia hakupenda msaada wowote toka kwa yule mwanamke, “sawa, karibu sana lakini kama kuna msaada wowote munahitaji?” aliuliza yule mwanamke, na hapo nikawahi mimi kuongea, “nahitaji kuonana na Alex Nkika, tuliweka oder ya chumba na tumesha fanya malipo” niliulizia yule jamaa ambae mzee Mandevu alinielekeza, huku nampokea Jessenia viatu na kuviweka kwenye begi, “hooo! kumbe nyie ndio watalii toka dar, ameshaacha maagizo, chumba chenu ni kule juu, chumba cha Sulta Said” alisema yule mwana dada, ambae tabasamu lilikuwa halikauki mdomoni mwake, “ok! itakuwa vyema kama utatupeleka huku” nilimueleza yule dada huku na mshika mkono Jessenia ambae alionekana kutembea kwake ni shida, kwa maana nyanyo zilishaanza kuuma, ni kutokana na kukimbia muda mrefu bila kuvaa viatu” nikamsika vizuri na kuanza kumsadia kutembea vizuri, huku sasa yule dada akitupokea begi, na safari hii Jessenia akiridhia kupokelewa begi na yule mwanamke.
Dakika kumi na tano baadae, tayari tulikuwa chumbani kwetu, chumba ambacho kilikuwa na hadhi ya Sultani kweli sikujuwa ni bei gani kwa usiku mmoja, lakini kiukweli kilikuwa ni chumb kizuri, ambacho ukiachilia vitu vingi vilivyo tengenezwa kwa sanaa ya kale ya kiarabu, pia kilikuwa na bwawa dogo la kuogelea mule mule ndani, kitanda kikubwa cha kuvutia na vitu vingi ambavyo nikitaja kimoja baada ya kingine itachukuwa kurasa kadhaa mpaka kumaliza, ila vya muhimu ni pamoja na friji kubwa tv na kuta zake zilitawaliwa na kioo kikubwa pande tatu yaani mashariki ambako kulikuwa na misitu, na bahari kwa mbali kaskazni ambako pia kulikuwa na bahari, ambayo kwa usiku huu tuliweza kuona giza nene na magharibi ambako kulikuwa na taa nyingi sana ambazo zilimulika pwani, na hapo ungweza kugundua kuwa hotel hii ipo ufukweni, na ukitazama vizuri kwa mbali ungeweza kuona taa pwani ya mombasa na tanga.
Niliagiza mahitajio yetu ya usiku ule, ikiwa ni vyakula na vinywaji, mara nikasikia simu inaita, ilikuwa ni simu toka kwa insp Aroub, “hallow mzee habari za jioni” nilisalimia mara baada ya kupokea ile simu, “upo wapi kijana, nimehangaika sana kukutafuta, ujuwe kuna mambo nahitaji unielekeze, nimekutafuta hapa mess sijakuona kabisa wala gari lako halipo” alisema mzee Aroub kwa namna ya kulalamika, “mzee samahani mzee, nilifika hapo sikukaa sana nikaondoka zangu, ila sio mbaya hata mimi mwenyewe nilikuwa nahitaji kesho mida ya saa nne za asubuhi tuonane, yani juu chini kwa namna yoyote ile” nilimueleza insp Aroub, “sawa tena itakuwa vyema maana mida hiyo tutakuwa Ali Khamis camp Rais anahutubia” alisema insp Aroub na hapo nikaona kama vile kuna kitu kitakwama, maana nilihitaji mida hiyo akampe ulinzi Jessenia pale kwa mjomba wake, ili atafute hard disc kisha tumalize kazi kabla damu ya mtu mwingine haija mwagika, “halafu mwalimu, hivi unajuwa ule mwili tulio ukuta pale ngerengere ni wa mfanyakazi wa Uss, kijana wa mzee Juma” alisema mzee Aroub akionyesha kulifahamu hilo baadae, “hooo kumbe, kwahiyo bado unaamini kuwa kifo chake kinahusiana na siasa?” nilimuuliza insp Aroub kwa kumtega, “mpaka sasa nimeingiwa na mshaka, nahisi ni mauwaji yale yale yanaendelea, hivyo nimepanga kukutana na mzee Juma kesho, maana na yeye atakuwepo kwenye hotuba ya rais kule Ali Khamis, akiwa katika kundi la wazee chama wa hapa chake chake” alisema mzee Aroub, ambae ni wazi bado alikuwa pale mess, hapo tukaagana na kukata simu.

Dakika kumi baadae, tayari tulisha letewa mahitaji yetu ya vyakula na vinywaji, yani wine na vyakula mbali mbali tulivyo viagiza, na kabla hatujaenda kuoga nililazimika kwanza nimfanyie massage Jessenia, ambae ni wazi lazima angehitaji huduma hii, kwaajili ya kuweka sawa mwili wake, kutokana na misuko suko iliyotukuta muda mfupi ulipita, huku muda wote nawaza juu ya kitu ambacho natakiwa kukifanya ili kufanikiwa mpango wangu pasipo kuleta madhara kwa Jessenia, hata nilipopata wazo nikajitabasamulia mwenyewe huku naendelea kufanya massage juu ya mwili laini wa Jessenia, ambae niliamini leo asingeweza kupata hamu ya dudu hata kama angejibust kwa kwa ile dawa ya kupaka ya babu mabudi, lakini haikuwa hivyo.
Maana Jessenia akiwa amelala kifudi fudi kwenye kitanda maalumu cha kufanyia massaje karibu na bwawa dogo la kuogea mule mule chumbani, akiwa mtupu kabisa kama alivyo zaliwa, msambwanda wake ukiwa umetazama juu na kumwaga hips pembeni, nilianza kutembeza mikono yangu kuanzia kwenye nyayo za miguu yake, nikinibinya binya kwa kuikanda na mafuta mazuri ya karafuu, ni mguu mmoja baada ya mwingine, nikipandisha mkono wangu taratibu juu ya ngozi laini iliyopakaa mafuta ya karafuu, mpaka kwenye magoti ambapo palianza kuleta tatizo, hasa baada ya kuanza kutembeza vidole nyuma ya goti, huku nikibinya binya taratibu, nadhani nilikuwa na mtekenya, maana japo alikuwa ametulia lakini kuna vitu vilinipa ishara kwamba kuna kitu kina mpwita……….…. ITAENDELEA
Yuko poa mwandishi sioni tatizo lolote👍👍
 
Mkuu tangu uzamie humo hotelini na Sania umesahau kazi ya upelelezi iliokuleta na bosi anangoja report.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom