KIFO CHA HAWARA (mkono wa jini)
SEHEMU YA SABINI NA SABA
MTUNZI:
Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA SABINI NA SITA: Na mimi nikaenda na kuegesha gari pembeni ya barabara sambamba na yale magari mengine, kisha tuka shuka, nikafunga gari milango yote kasoro mmoja tu wa abaria wa nyuma upande wa kushoto, ambao ulikuwa nje ya barabara, wakati huo gari la wakina Ussi likiwa linapunguza mwendo na kuja kusimama nyuma ya gari langu.…. ENDELEA…..
Hapo nika tabasamu kimoyo moyo, huku naanza kutembea nyuma ya Aisha kueleka kwenye mkusanyiko wa watu na mkononi nimesha chukua simu na kumpigia Jessenia, na wakati naipiga na kuweka sikioni, nikajifanya najikuna kichwani nikatumia mwanya huo kugeukia upande lilipo gari la kina Ussi, nikamuona Ussi akiwa ameshuka toka kwenye gari na wenzake wawili, ambao ni wale wale aliokuwa nao usiku wakati wanatushambulia.
Tulipo kutanisha macho yetu na Ussi, nikampungia mkono, “niaje Ussi mambo vipi” nilimsalimia huku nikiwa nimejichangamsha, usingedhania kama nina fahamu kuwa yeye na wenzake ndio waliotaka kuniuwa jana usiku, wakati huo niliskia simu ikiwa imepokelewa upande wa pili, yaani na Jessenia, “poa mambo vipi” alijibu Ussi, kwa sauti ambayo haikuwa na uchangamfu wowote, huku yeye na wenzake wanaendelea kutembea kuelekea kule kwenye mkusanyiko wa watu, ambako sasa kulisikika sauti toka kwenye vipaza sauti zilizo kuwa zina ashiria sasa ulikuwa ni wakati wa utambulisho kwa wageni walio ambatana na raisi, “Eric vipi mbona huongei, unanichelewesha mwenzio, namalizia ili niondoke” ilikuwa ni sauti ya Jessenia toka upande wa pili wa simu, ikionyesha kuwa ni mwenye wasi wasi mwingi sana, “ina maana ulikuwa bado hujatoka hapo nyumbani” niliuliza kwa sauti ya chini kidogo, huku nikimtazama Aisha ambae alikuwa ananipa ishara fulani, ambayo mwanzo sikuwa nimeielewa, ila baada ya kuirudia mara kadhaa, nikaielewa kuwa, ilikuwa ni ishara ya kunieleza kuwa, nitazame upande wa kushoto kwangu yaani kwenye magari yale ya vikundi vya ulinzi na usalama.
Hapo mimi nikatazama upande ambao ulionyesha wazi kuwa kuna mtu alikuwa ananiita, “ndio nataka kutoka, vipi wakina Ussi wanakuja?” aliuliza Jessenia kwa sauti ile ile iliyojaa wasi wasi, “hapana ila muda wowote wanaweza kuja, cha msingi toka hapo kwenu, elekea moja kwa moja njia panda ya kuingilia hapo kwenu, hapo utamkuta mangeu” nilimuelekeza kwa sauti ya chini, huku nikiwa nimesha muona mtu aliekuwa ananiita, alikuwa ni insp Aroub, kumbe nae alikuwa miongoni mwa wale askari wa jeshi la polisi waliokuwepo kwenye yale magari, ambae sasa alikuwa anatembea kunifuata, “sawa usichelewe Eric mwenzio naogopa” alisema Jessenia na kukata simu.
Na mimi nikaiweka simu mfukoni na kutazama Aisha, “tangulia nakuja Aisha” nilimuambia Aisha, lakini lengo langu alikuwa hilo lengu langu lilikuwa ni kumtazama Ussi na wenzake watatu, ambao niliwaona wamesha fika kwenye mkusanyiko, nikaona huo ndio wakati ambao nikichomoka na gari naweza kuwaacha, japo nilijuwa kuwa kuna wengine wamebakia ndani ya gari, ambao wanaweza kuwa wanne, lakini wasinge jichukulia uamuzi wa kuondoka bila ruksa ya Ussi.
Aisha alielekea kwenye mkusanyiko, na mimi nikamfuata huku namuonyeshea ishara ya kwamba turudi kwenye gari langu, tukaongelee pale nae akafanya hivyo.
Wakati naelekea kwenye gari, nikatazama kwenye lile Prado la Ussi kwa kupitia kioo cha mbele, nilifanikiwa kuona dalili za uwepo wa watu ndani ya gari, lakini sio kwenye seat za mbele, na bahati nzuri wakati huo huo nikamuona yule aliekuwa ananifuatia akiwa anatokea upande wa Green Mess kuja huku juu kwa mwendo wa haraka, “niambie Eric, naona umekuja kujumuika na Rais kwenye uzinduzi wa ujenzi” alisema Aroub mara baada ya kunifikia mimi, ambae nilikuwa nimesha karibia gari, “si unajuwa tena mzee, ni muhimu sana kusikiliza hotuba za viongozi kama hawa, maana sisi waandishi huwa tunapenda kupata habari moja kwa moja, hata hivyo hii simu niliyopigiwa inabidi niende mjini haraka sana” nilimueleza mzee Aroub, huku tuna zunguka gari kuelekea upande wa kushoto wa gari, yani nje ya barabara, ambako mimi nilifungua mlango ule ambao niliuacha bila kuu lock na kukaa kwenye seat ya nyuma ya upande huo wa kushoto, “basi nisikupotezee muda ila nina mawili matatu nataka nikuelezee kabla hujaondoka” alisema mzee Aroub.
Ukweli sikuona sababu ya kukataa kumsikiliza huyu mzee, ambae kiukweli nitahitaji msaada wake mkubwa hapo baadae, “haina shida ni lazima baadae tuongee, maana kuna jambo nitaomba unisaidie, nadhani litakuwa zuri kwako pia” nilimueleza Aroub, ambae alitabasamu kidogo, “bado unahitaji kujuwa habari za majini licha ya kufahamu yote haya?” lilikuwa swali la utani lililo ulizwa na insp Aroub, wote tukacheka, “unadhani naweza kuacha kazi niliyoianza,l kirahisi hivyo?” nilimjibu kwa mtindo wa swali, “ok! wacha tuongee ili uwahi” alisema insp ambae alianza kunieleza kile alichotaka kunieleza.
“Unakumbuka jana tulikutana usiku hapo juu” alisema insp Aroub, huku anaonyesha upande wa ngerengere, na mimi nikaitikia kwa kichwa, kukubali, na yeye akaendelea, “nadhani nilikueleza tulicho kikuta pale, sasa yule tuliemkuta amechinjwa nimegundua kuwa sio inshu za kisiasa” alisema insp Aroub kwa sauti ya chini, “japo sijaliongea hili ofisini, lakini nimegundua kuwa yule jamaa ni mfanyakazi wa Ussi huyo aliepita hapo, nimepanga baada ya kumpeleka mheshimiwa air port ndiyo nianze kuwafanyia mahojiano kama nilivyo kuambia jana, kuwa ninahitaji kuonana na mzee Juma, kisha kijana wake Ussi” alisema mzee Aroub,
Hapo nikagauze uso na kutazama kule kwenye mkusanyiko wa watu, lakini sikuweza kuona vizuri kutokana na giza la kioo, yaani tinted, “unadhani kwa kuwahoji utafanikiwa kupata chochote?” nilimuuliza insp Aroub, nae akatulia kidogo akitafuta jibu sahihi, ambalo alilipata sekunde tano mbele, “ndio maana nimekueleza kabla sijafanya chochote ili nipate ushauri katika kuhoji” alisema insp Aroub, na hapo sikumkawiza, “hebu mtazame Ussi halafu niambie amekaaje” nilimuambia mzee Aroub, ambae alikuwa amesimama na mimi na mimi nimekaa, kwa kimo chake na ufupi wa gari aliweza kuona vyema kule kwenye mkusanyiko.
na wakati huo huo simu ikaanza kuita, alikuwa mzee Mangeu aliekuwa anapiga, “mh! sijui ameshahisi tuna mzungumzia, mbona yeye na wenzake wanatazama sana huku?” aliuliza mzee Aroub, kwa sauti ambayo ilionyesha mashaka, “tutaongea baadae juu ya hilo, wacha mimi niondoke, naomba akianza kunifuata nijulishe” nilimueleza mzee Aroub, huku nahamia seat ya mbele kupitia kule kule nyuma, kisha nikawasha gari na kumuomba anifungie mlango.
Ile mzee Aroub anafunga mlango tu, na mimi nikaondoa gari taratibu huku nachukuwa simu niipokee, lakini ikakatika na kabla sija maliza eneo lile la mkutano, huku nikitembea taratibu, simu ikaita tena, alikuwa ni Mengeu tena, nikaipokea na kabla sijasema lolote, Mangeu akaongea, “kijana tayari Seni yupo hapa anakusubiri, sasa wewe upo wapi au unataka mpaka wamkute?” aliuliza mzee Mangeu kwa sauti iliyojaa ghazab kidogo, “dakika tano nitakuwa hapo” nilijibu hivyo kisha nikakata simu na kukanyaga mafuta kwa nguvu, maana wakati huo tayari nilikuwa nimesha maliza eneo lenye mkusanyiko.
Niliendesha gari kwa speed kali sana, nikigusa speed mia moja kwa saa, lengo langu lilikuwa ni kwamba wakina Ussi ambao nilijuwa nilazima wange nifuata watakapoingia ndani ya gari na kuanza safari wawe wamesha chelewa, wakute nimesha mchukuwa Jessenia na kuondoka nae.
Lakini wakati naiacha ngerengere, nikasikia simu yangu inaita, nilipoitazama alikuwa ni insp Aroub, nikaipokea mara moja, “hallow Ticha Ussi na wenzake ndio wanatoka hapa” alisema insp Aroub na wakati huo kwa mbali nilikuwa nasikia ngurumo ya gari kupitia simu yake, ukweli kutoka hapo mpaka hapa nilipo hapakuwa mbali sana, hivyo nililazimika kuongeza mwendo na sasa nilitembelea speed mia ishirini mpaka mia thelathini kwa saa, japo isinge kuwa kitu kwa gari kama Prado, lakini kwakuwa ni safari fupi niliamini hawato nikuta.
Ni kweli, mpaka nafika kona ya macho manne, na kuikamata barabara ya kwenda chake, sikuona dalili ya uwepo wa gari la Ussi nyumba yangu, nikaongeza speed kueleke upande wa chake chake, mpaka nilipo fika sehemu ambayo niliwaambia wakina Jessenia wanisubiri, nao niliwakuta wananisubiri, huku Jessenia akiwa amesimama pembeni ya fuko kubwa la shangazi kaja, ilinishangaza sana, nikajiuliza ule mzigo mkubwa ni wanini, lakini hapakuwa na muda wa kuhoji.
ile nasimamisha gari tu, Jessenia akafungua malango wa nyuma wa abiria na mzee Mangeu aka nanyua ule mfuko, mkubwa ambao ulikuwa umejaa kweli kweli na kuuweka ndani ya gari, huku Jessenia mwenyewe akiingia ndani ya gari, “kijana oder yenu ya chumba Mantarif nimesha weka, nendeni mukajificha huko tutawasiliana” alisema mzee Mangeu na mimi sikuchelewa nikakanyaga mafuta nakuondoa gari kueleka mjini, speed kali kweli kweli, “Jesse huo mzigo wa nini, na vitu nilivyo kuagiza viko wapi?” nilimuuliza Jessenia, ambae licha ya kuwa kwenye gari lakini bado alikuwa na wasi wasi mwingi, “nimechukuwa baadhi ya nguo zangu kwa mjomba sirudi mpaka wamekamatwa” alisema Jessenia huku anageuka kutazama nyuma kwa kupitia kioo cha nyuma ambacho hakina tinted.
Unajuwa nini, licha ya fedha zote zilizopo na uzuri wa Jessenia, lakini hakuwa na begi, na hiyo yote ni kwasababu hakuwahi kusafiri kwenda mbali, wala hakufikiria kusafiri, na ukichukulia nguo zake zilikuwa zinahifadhiwa kwenye makabati ya nguo yaliyopo chumbani kwake, ndio maana leo alichukuwa nguo zake kwa hili fuko la shangazi kaja.
Hapo nilitabasamu kidogo, maana uamuzi wa Jessenia, hata mimi sikuufikiria, japo lilikuwa wazo zuri ili kuwa panikisha na kuwa fanya wazidi kujitokeza hadharani, ila kwa upande mwingine niliogopa kuwa familia yake bandia ingenigeuzia kibao kwamba nimemtorosha Jessenia,
sikuongea chochote, nilizidi kukanyaga mafuta tukipita chake chake na kuikamata madungu kisha tuka ikamata Kangani, ambapo tuliingia upande wa kuelekea air port ambapo upande huo barabara ilikuwa nyeupe, hivyo nilikanyaga mafuta mpaka kufikia speed mia arobaini, wakati huo huo nikasikia simu inaita, nikapokea na kuiweka sikioni, “kimbia unavyoweza hawa jamaa wamepita hapa, wanakuja huko mbio mbio” alisema Mangeu kabla ya kukata simu.
“nani babu Mangeu, anasemaje?” aliuliza Jessenia, ambae sikuwa na haja ya kumficha, japo alikuwa na uoga wa wazi kabisa, “anasema wakina Ussi wamesha pita chake wanakuja” nilimueleza huku naendelea kukanyaga mafuta na kutembea kwa kilomita kama mbili hivi mbele, upande wa air port, tuka ikuta njia ya mkato ya kurudi wawili, ambayo tuliifuata barabara hiyo, ambayo kwa mwaka huo wa 2005, ilikuwa bado ya vumbi na kufanya mwendo wangu uwe wa speed sabini mpaka themanini kwa saa, huku mara kwa mara nikijaribu kutazama kwenye side morror kama ningefanikiwa kuliona gari la wakina Ussi likitufuata, lakini sikuona dalili ya gari nyuma yetu.
Na wakati huo huo tukasikia simu ya Jessenia inaita, nae akaitoa mara moja na kuitazama jina la mpigaji, nikamuona anashtuka, “Ussi huyo ananipigia simu” alisema Jessenia kwa sauti iliyojaa uoga, huku ananionyesha kioo cha simu, nikaona jina kaka Ussi, “pokea msikilize anasemaje, usimuonyeshe hasira” nilimuambia Jessenia, ambae alitumia sekunde tatu, kuweka sawa sauti yake, kisha akaipokea simu ile, na kuweka loud speeker, “asalam alaykum” alisalimia Jessenia, kwa sauti tulivu, “upo wapi Seni, unajuwa baba anakutafuta sana” aliuliza Ussi kwa sauti ya ukali……….…. ENDELEA..
KIFO CHA HAWARA (mkono wa jini)
SEHEMU YA SABINI NA NANE
MTUNZI:
Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA SABINI NA SABA: Na wakati huo huo tukasikia simu ya Jessenia inaita, nae akaitoa mara moja na kuitazama jina la mpigaji, nikamuona anashtuka, “Ussi huyo ananipigia simu” alisema Jessenia kwa sauti iliyojaa uoga, huku ananionyesha kioo cha simu, nikaona jina kaka Ussi, “pokea msikilize anasemaje, usimuonyeshe hasira” nilimuambia Jessenia, ambae alitumia sekunde tatu, kuweka sawa sauti yake, kisha akaipokea simu ile, na kuweka loud speeker, “asalam alaykum” alisalimia Jessenia, kwa sauti tulivu, “upo wapi Seni, unajuwa baba anakutafuta sana” aliuliza Ussi kwa sauti ya ukali……….…. ENDELEA..
iliyoashiria ugomvi, “mbona nimetoka nyumbani sasa hivi, dada kaniambia baba ameenda kumsikiliza Rais” alisema Jessenia kwa sauti tulivu sana, “kwahiyo kama hayupo na wewe ndiyo unatoka” aliuliza Ussi, wakati huo nilikuwa nimepunguza mwendo kidogo.
Ukweli swali hilo lilimshinda Jessenia, ambae alikaa kimya huku akinitazama kwa macho ambayo ni kama alikuwa ananiuliza ajibu nini, na mimi licha ya kulitambua hilo, lakini sikumueleza chochote, “si naongea na wewe Seni, haya sasa upo wapi?” aliuliza Ussi kwa sauti ya ukali zaidi, niwazi hakujuwa kama tayari Jessenia alishamtambua jana usiku wakati anajaribu kumshambulia kwa panga, na pia ameshagundua mipango yao, yaani yeye na baba yake mzee Juma Mohamed, “nipo chake kuna kitu nataka kununua” alisema Jessenia kwa sauti kama ya kulalamika, lakini iliyojaa nidhamu, “sikia Seni, usidanganyike kirahisi hivyo, huyo mwanaume unae jivunia ni tapeli tu, hivi navyo kuambia, yupo njiani sijui anaenda bandarini mkoani au anaenda air port, kwahiyo ni wazi kabisa anaondoka zake, baada ya kukutorosha jana usiku na kukusababishia umkosee adab baba” alisema Ussi, na hapo mimi na Jesse tuka tazamana huku tukizuia kicheko, “lakini kaka yeye ndie mwanaume pekee ambae nimeweza kuwanae bila kupata matatizo” alisema Jessenia, kwa sauti kama ya kuomba hivi, lakini ungemtazama uso wake kwa muda huo, ungejuwa fika anajizuia kucheka, “achana na hizo hisia, huo ni uchawi wa Mangeu tu, hebu rudi nyumba sasa hivi baba akija akukute” alisema Ussi, kama vile anatoa amri, “sawa narudi sasa hivi” alisema Jessenia, nakukata simu, halafu tukacheka kwa pamoja.
Naam mpak hapo, tayari nilikuwa nimesha gundua kuwa Ussi na wenzake hawakujuwa mimi nipo wapi, hivyo niliendesha gari kwa uhuru na kujiachia, tukienda kutokea Wawi nyumba za kijiji na kuibukia garage, tukaikamata macho mane na kushika uelekeo wa wete, nikijuwa kuwa wakina Ussi hawakuwa wanatufuata.
Njiani tuliongea na kupanga mambo mengi ya kufanya baada ya kumaliza swala lile lililopo mbele yetu, “mimi sikai tena huku, tunaondoka wote kwenda Dar, halafu babu Mangeu amesema amesha nijengea nyumba kule dar” alisema Jessenia, kwa sauti ya kudeka, huku wasi wasi ukiwa umesha ondoka moyoni mwake, “hivi Jesse unadhani ninaweza kuondoka Pemba bila wewe?” nilimuuliza Jessenia kwa sauti flani tulivu ya kubembeleza na kumliwaza iliyojaa mahaba, kiasi cha kumfanya atabasamu “sasa ole wako nikute videmu vyako vya zamani vinakusogelea” alisema Jessenia, huku akimalzia kwa kicheko cha utani.*******
Tulitumia lisaa limoja kufika Mantariff Logde, ambapo tulipokelewa kama jana na kuonyeshwa chumba chetu, ambacho kilikuwa ni kile kile cha jana cha sultan, ambacho mchana huu kilikuwa kinaangazia vyema sana nje, japo hatukuweza kuona vyema pwani ya tanga na mombasa, zaidi ya taswila flani ya giza giza iliyo onyesha milima.
Naam wakati huo, niliutumia pia kuchunguza ile Hard disc, ambayo Jessenia alisema kuwa aliikuta kwenye drow ya kitanda cha Ussi, nikaifungua lapto ya Ussi na kuipachika bahati nzuri ilifanikiwa kusoma maana tayari ilikuwa na window seven, nilifungua file kadhaa, mpaka nilipolipata lililoandikwa security camera, nikafungua na kukuta video kadhaa, zote zikiwa zimeandika serity camera, zikitofautishwa na tarehe hivyo nikatazama ile ambayo ilikuwa ya tarehe ya mwisho kabisa.
Wote wawili tukiwa tuna itazama ile video, ambayo ilikuwa inachukuwa vipande vitano vya nyumba ile, ikiwa ni upande nne za nyumba ile na eneo la sebuleni, yani upande wa ndani, nilichagua kwanza video ya nje ambayo niliianzisha pale ambapo walionekana Jessenia na Vuai wakiingia na vesper pale nyumbani, na kushuka kisha kuingia ndani, Jessenia akiwa ameziba uso kwa niqab, dakika chache baadae anaonekana mtu mwingine anakuja na vesper, namtambua kuwa ni Ussi, ambae alitoka kuniacha wawi muda mfupi kabla, sikuwa nimesahau alivyovaa na kile kijifuko mkononi.
Ussi anachuka haraka na kuchukuwa kitu mfano wa fimbo fupi sana kwenye mfuko ule, na kisha anatoa kichupa flani na kitu ambacho mwanzo hatukuweza kukiona vizuri, ila baada ya kuisimaisha (pause) ile video na kuizoom (kuikuza) tukaona akiwa ameshika kitu kama sindano ndogo sana, yenye ncha kali sana, akitia kwenye kijichupa na kukiweka ndani ya ile fimbo yenye uwazi ndani yake mfano wa filimbi, halafu akagonga mlango.
viedo inaonyesha, sekunde chache mlango unafunguliwa na pasipo kuonekana mtu yoyote, aliefungua mlango, Ussi anasogeza ile filimbi mdomoni na kupuliza, tukiwa tumeizoom, tunaweza kumuona Ussi akipuliza ile filimbi, na kile kisindano kinatoka kuelekea mlangoni kisha haraka sana Ussi anarudi kwenye Piki piki yake na kuondoka kwa speed kali sana, “kumbe kweli Ussi anahusika na mauwaji haya” alisema Jessenia kwa sauti ya mshangao na kuto kuamini.
Dakika moja baadae video inaonyesha Jessenia nae akitoka pale mlangoni huku amevaa kama alivyokuja na kutokomea upande ule ule waliotokea, “ni mchezo wa muda mrefu sana waliucheza mjomba wako na Ussi” na lengo lao lilikuwa ni kukuaminisha kuwa kuna jini halitaki uolewe ” nilimueleza Jessenia ambae alikuwa anaifuatilia kwa umakini sana ile video.
Ili kumuona mtu ambae alifungua mlango, tuna fungua video ya camera ya sebuleni, ambayo ukiachilia kuwaonyesha wawili hawa waliyokuwa wanaingia ndani na kupotela kwenye koridoni, pia dakika chache akaonekana Vuai akiwa anarudi huku amevalia bukta na tumbo wazi anaufuata mlango, kisha anaufungua na sasa anaonekana Ussi akiwa anaweka filimbi mdomoni huku Vuai akionekana kushangaa na kupiga hatua moja nyuma, lakini anachelewa kitu mfano wa sindao kina mkuta kwenye shavu lake la kushoto, anaonekana katika maumivu makali, Ussi anatoweka kwenye usawa wa camera, huku Vuai akionekana kuyumba mara kadhaa kabla ya kuanguka chini.
Dakika moja baadae anaonekana Jessenia ambae alikuwa bado katika vazi lake alilokuja nalo, baibui na hijab na uso amejiziba niqab, anamtazama Vuai kwa uoga kisha anatoka nje na kutokomea zake, hapo zinapita dakika kama sita hivi, anaonekana kijana Mahamud, ambae mwanzo alitoka mara tu walipoingia wakina Vuai, “kwahiyo wao lengo lao kubwa ni nini?” aliuliza Jessenia, ambae alionyesha mwenye hasira na chuki na wakina Ussi, “hilo ndilo ambalo tuna taka kulijuwa kabla hatuja watia mbaroni, na ili kufanikisha jambo hili jioni ya leo tunatakiwa kurudi chake” nilimueleza Jessenia, japo sikuwa na mpango wowote nilio uweka kwaajili ya kupata chanzo kamili yenye ushahidi, ila kichwani mwangu nilishahisi kuwa mali na utajiri wa Jessenia ndio chanzo halisi. “mh! kwani kuna sababu yoyote ya kutafuta ushahidi mwingine, wakati tayari tuna ushahidi?” aliuliza Jessenia, na wakati huo huo simu yangu ikaanza kuita.
Nilipoitazama niliona kuwa mpigaji alikuwa ni insp Aroub, nikaipokea, “asalam aleykum mzee” nilimsalimia insp Aroub, ambae alionekana kuwa katika sehemu iliyo changamka, “walaykum salam mwalimu, upo wapi sasa?” aliiuliza insp Aroub ambae kiukweli sikuhitaji kumueleza nilipo maana isingekuwa vyema kutaja maficho yangu ya pekee, “nipo njiani natokea mkoani, kuna mtu nilimpeleka huko” nilimdanganya insp Aroub, sisi tupo barabara mpya, rais anaweka jiwe la msingi, ili tuweze kumpeleka air port, hapo ndipo nitahitaji kukutana na wewe kabla ya mpango mwingine wowote” alisema insp Aroub, “usijari insp, we tulia mpaka jionitutakapo kutana, nakuhakikishia hili limeisha” nilimueleza insp.
Hapo nikasikia mguno hafifu toka kwa insp, “mh! Eric, unamaanisha nini, kwamba tunaenda kumpata muuwaji na ushahidi?” aliuliza insp kwa sauti iliyojaa mashaka kiasi, “kama tutaweka mipango vizuri” nilimjibu insp Aroub, nikidhania kuwa hilo ndilo swali la mwisho, lakini haikuwa hivyo, “nidokeze kidogo, kama tunahitaji maandalizi” alisema insp Aroub na hapo alibamba kidogo, maana ni kweli tulihitaji mandalizi ya mapema, “kwanza usiri, muda wote wa zoezi, wepesi wa kitendo na kuzingatia muda na maelekezo, uvumilivu wa kusubiri, mwisho ni matumizi sahihi ya nguvu, maana watuhumiwa hawana silaha za moto” nilifunguka kwa insp Aroub, ambae nilimsikia akiachia kicheko cha fadhaa, “hivi kijana unaweza kunieleza kazi yako halisi, kama ni CID (Criminal Investigation Department), CIA (Central Intelligence Agent, MS (Millitary spay) TSA (Tanzania Secret Agent) au nani haswaa?” aliniuliza insp Aroub, na kabla sijajibu swali hilo toka kwa insp, akanibandika jingine, “hii Eric, inawezekanaje ndani ya muda huu mfupi tumalize hii kazi, wakati mimi nimehangaika nayo mwaka wa saba sasa” hapo nikaona saa nimelivuruga kabla sijamaliza kazi………….…. ENDELEA..
KIFO CHA HAWARA (mkono wa jini)
SEHEMU YA SABINI NA TISA
MTUNZI:
Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA SABINI NA NANE: “kwanza usiri, muda wote wa zoezi, wepesi wa kitendo na kuzingatia muda na maelekezo, uvumilivu wa kusubiri, mwisho ni matumizi sahihi ya nguvu, maana watuhumiwa hawana silaha za moto” nilifunguka kwa insp Aroub, ambae nilimsikia akiachia kicheko cha fadhaa, “hivi kijana unaweza kunieleza kazi yako halisi, kama ni CID (Criminal Investigation Department), CIA (Central Intelligence Agent, MS (Millitary spay) TSA (Tanzania Secret Agent) au nani haswaa?” aliniuliza insp Aroub, na kabla sijajibu swali hilo toka kwa insp, akanibandika jingine, “hii Eric, inawezekanaje ndani ya muda huu mfupi tumalize hii kazi, wakati mimi nimehangaika nayo mwaka wa saba sasa” hapo nikaona saa nimelivuruga kabla sijamaliza kazi…………….…. ENDELEA..
Ni vyema kama nikimtafutia jibu ambalo linaweza kumtuliza insp Aroub, lakini wakati natafuta jibu, nikamsikia anacheka, “hakika we kijana ni hatari sana, kazi ya ualimu haikufai kabisa, bora ungesomea upelelezi, yaani utadhani FBI au KGB” alisema mzee Aroub akinimwagia sifa, tatizo upelelezi una mambo mengi, lazima ujuwe kupambana na kutumia silaha” nilisema hivyo kuunga mkono utani wake.
Hapo tukaagana na kukubaliana tuwasiliane jioni ili kupeana mipango ya kukamilisha swala hili la kiuchunguzi, na mimi nilicopy zile video na kuziweka kwenye flash disc, ambayo nilitoka nayo japan, sidhani kama mwaka ule wa 2005 zilikuwa zimefika Tanzania, maana hata huko japan zilikuwa zinauzwa kwa fedha nyingi kidogo, ukubwa wa mwisho kabisa ulikuwa ni GB 4, kama hii niliyokuwa nayo mimi, nilitunza video kwenye laptop yangu na nyingine nikaiacha kwenye flash.******
Naam mchana ule tuliutumia kwa kula na kulala ili kufidia usingizi wa jana usiku, japo sijui miili yetu ina nini, maana ile kugusana tu wakati wakutafuta usingizi, tukajikuta viungoyetu vikiingiliana na kupeana walicho kusudia kupeana, sikuweza kuzuwia, japo ilikuwa ni mara mbili, lakini ilifurahisha sana, moja ilikuwa wakati tuna taka kulala, naya pili ilikuwa baada ya kuamka na kuingia kwenda kuoga, yaani tulikiamsha tukiwa bafuni, hawamuzote mbili Jessenia ndie alikuwa mchokozi, japo sikatai kuwa nilikuwa katika matamanio, lakini yeye ndie alienichokoza kwa kuonyesha dalili za wazi za kuhitaji dudu.
Mpaka saa nane mchana tayari tulikuwa tumesha oga tumesha kula, tulikuwa tuna pumzika kuvuta muda wa kurudi chake chake, lakini tayari chumba chetu tunge kikuta, maana kilisha lipiwa, ndio mida ambayo Jessenia alisikia simu yake inaita, alipoichukuwa na kuitazama nikamuona anashtuka na kunitazama usoni, “mjomba huyo” alisema Jessenia kwa sauti iliyojaa wasi wasi, hapo kwa haraka haraka nikajiuliza kuhusu maswali ambayo au maongezi ya mzee Juma Mohamed yatalenga nini, kwanza lazima yupo wapi ingekuwepo, pili lazima atakuwa amesha fika nyumbani na ameulizwa juu ya uondokaji wake nyumbani, “ulipoondoka nyumbani kuna mtu alikuona?” nilimuuliza Jessenia, ambae aliitikia kwa kichwa, akikubali kuwa kuna mtu alimuona,
“nani?” nilimuuliza Jessenia, “alikuwepo dada wa kazi” alisema Jessenia, huku simu yake bado inaendelea kuita, “ok! akikuuliza upo wapi mwambie upo mkoani” nilimuambia Jessenia, ambae aliitikia kwa kichwa na kuipokea simu, na kuweka loud speeker, “asalam aleykum” alisalimia Jessenia kwa sauti tulivu iliyojaa nidham, “Seni unashani unafanya nini, hivi kweli wewe ndie wakukimbia nyumbani, bora ungebeba nguo zako tu, sasa umeiba mpaka computer ya kaka yako, ndivyo alivyokutuma huyo kijana toka bara?” hapo Jessenia akanitazama kwa macho ya kuniuliza kama nimesikia kinacho ongelewa, “haya niambie upo wapi?” aliuliza mzee Juma Mohamed, “nipo mkoani” alijibu Jessenia kwa sauti tulivu yenye nidhamu,
“kwahiyo unataka kutoroka kwenda bara sivyo?” aliuliza mzee Juma, yani mjomba wake Jessenia, na kabla Jessenia hajajibu kitu, tukamsikia tena mjomba wake, “sasa nakuambia urudi sasa hivi, ukichelewa tu natoa taarifa polisi ukamatwe wewe na huyo mjinga mwenzio na ukijaribu kupanda boti utakamatiwa unguja, na kuhakikishia utakaa kituoni mpaka ushike adabu” aliongea mjomba kwa sauti ya ukali na kukata simu, “tutafanyaje Eric?” aliuliza Jessenia, kwa sauti iliyojaa uoga, “kwanini una wasi wasi Jesse, ushahidi wote tunao mkononi” nilimuambia Jessenia, huku natoa simu yangu na kumpigia mzee Mangeu.
Ukweli licha ya kuchelewa kupokea ile simu yake, lakini baadae akaipokea, “asalam aleykum mzee” nilimsalimia mzee Mangeu, “waleykum salama kijana, nilikuwa nimejilaza hapa na kausingizi kalikuwa kana ninyemelea, vipi kuna lolote?” aliuliza mzee Mangeu, ambae kiukweli sauti yake ilikuwa inaonyesha wazi kuwa katika uchovu flani wa usingizi, “lolote lipo tayari tuna ushahidi wa kutosha kabisa juu ya Ussi kuhusika na kifo cha Vuai, kilichobakia ni kuhakikisha tuna maliza kazi na kuwa kamatisha hao watu” nilimueleza mzee Mangeu, ambae nilimsikia akicheka kivivu, “we kijana hatari sana, boss wako hakukosea kukutuma” alisema mzee Mangeu.
ambae pia aliendelea kusema kuwa, toka tulipoachana nae mida ile, alienda nyumbani kwake ambako alitulia nje ya nyumba na kufuatilia mienendo ya nyumbani kwa kina Jessenia, baada ya kama dakika kumi na tano, akaliona gari walilokuwa nalo wakina Ussi likiingia pale nyumbani na kuingia ndani ya gate, na haikupita muda mrefu akatoka mmoja kati ya wale vijana na kusogea mpaka usawa wa nyumba yake akiwa barabaran, akatazama na kujifanya anapita njia kisha akarudi na kuingia ndani.
Kitu kama hicho kikatokea tena dakika ishirini baadae, na baada ya hapo ikawa kimya kabla mangeu hajashtuka na kutazama ghorofani, ambako aliweza kumuona Ussi akichungulia dirishani mara kwa mara mpaka yeye alipoamua kuingia kibandani kwake kujipumzisha, “kwahiyo hujamuona mzee Juma hapo kwake?” nilimuuliza mzee Mangeu, “ukweli sijajuwa kama amesha rudi” alijibu mzee Mangeu na mimi nikamueleza mzee Mangeu, maongezi ya Jessenia na huyo mjomba wake wa bandia jinsi yalivyokuwa, “kwa hiyo mzee kuwa tayari kukutana na mzee Juma mchana huu, jifanye unamuulizia Jesse, na kwamba toka jana hujamuona kabisa” jitahidi subiri nije nikuletee kinasa sauti ili tuweze kusikia kila kitu atakacho kiongea” nilimueleza Mzee Mangeu kabla hatujakata simu.*****
Saa tisa ndio mida ambayo tulitoka Panga la mtoro, kaskazini Pemba kwenye hotel kubwa ya hadhi ya juu sana ya Mantariff, tukielekea chake chake nikiwa nimevalia nguo za michezo, yaani truck tishirt na raba, njiani tulikuwa tukiongea kwa furaha, huku Jessenia akiuliza maswali mengi kuhusu dar watu wake na maisha kwa ujumla, na mimi nilimueleza huku nikipamba kweli kweli, kitu ambacho kilimpa chachu na tamaa ya kufika dar es salaam.
Saa kumi na robo ilitukutia mitaa ya gombani, ndipo nilipoiona simu yangu ikiwa inaita, nilipoitazama alikuwa ni insp Aroub, nikajuwa amesha pata habari mpya, nikaipokea mara moja, “ndiyo mzee kuna jipya” nilimuuliza mzee Aroub, huku napunguza mwendo ili niweze kuongea nae vizuri, “jipya lipo bwana mwandishi, unatakiwa kujisalimisha kituo cha polisi ukiwa na Jessenia, na vitu ulivyoiba nyumbani kwa mzee Juma Mohamed” alisema mzee Aroub kwa sauti ya ukali tofauti na nilivyo mzowea.
Kwanza nika tabasamu, kwa kuona tayari kazi imefika patamu, “mzee….” kabla sijasema lolote, tayari mzee Mohamed akanidaka, “sikia kijana hakuna porojo zaidi, sasa ni mwisho wa kuniteka akili, umenifanya mjinga kwa muda mrefu sana, mara moja acha mpango wako wakutoroka na uje haraka kituoni, maana hautoweza kushuka toka kwenye bot bandari yoyote kabla hujatiwa mbaroni” alisema insp Aroub kwa sauti ile ile ya ukali, hapo nikasimamisha gari kabisa mita chache toka uwanja wa mpira wa gombani.
Niliwaza kwa haraka ni muambie nini mzee Aroub ili tulie maana ni wazi kuwa mzee Juma, ameshaenda kituoni kutoa taarifa kama alivyo sema, na baada ya kupata jibu nikaongea kwa sauti tulivu kabisa, “mzee sina cha kukimbia, nipo pemba, tena hapa hapa chake chake…” lakini kabla sijamaliza kuongea, insp Aroub akanidaka tena, “sikia kijana sina muda wakukusikiliza cha msingi njoo kituoni madungu, wewe ni mtuhumiwa wa wizi nyumbani kwa mzee Juma Mohamed, dakika kumi kama hujafika nita kusaka mimi mwenyewe” alisema mzee Aroub, na kukata simu.
Nikashusha pumzi na kumtazama Jessenia, ambae alikuwa anitazama kwa macho ya kujiuliza nilikuwa naongea nini, mana sikuweka loud speeker, “nani huyo?” aliuliza Jessenia, “insp Aroub, mjomba wako amesha toa taarifa kituoni” nilimjibu Jessenia, huku nikiwa nina bofya simu kupiga kwa insp Aroub, ambae aliipokea mara moja, “unasemaje kijana, unadhani tuna jambo la kuongelea kwenye simu zaidi ya kuja kujisalimisha kituoni?” aliuliza insp Aroub kwa ukali, “tunalo la kuongea mzee, ni vyema kama ungenipa na….” mzee Aroub hakunipa nafasi, “kijana mpaka sasa sina uwezo wakukusikiliza tayari kesi ipo mezani, na unatakiwa kukamatwa sasa hivi, huwezi tena kuni laghai jisalimishe kabla hatuja poteza muda wetu kukusaka” alisema insp Aroub na kukata simu. ………….…. ENDELEA
KIFO CHA HAWARA (mkono wa jini)
SEHEMU YA THEMANINI
MTUNZI:
Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA SABINI NA TISA: “unasemaje kijana, unadhani tuna jambo la kuongelea kwenye simu zaidi ya kuja kujisalimisha kituoni?” aliuliza insp Aroub kwa ukali, “tunalo la kuongea mzee, ni vyema kama ungenipa na….” mzee Aroub hakunipa nafasi, “kijana mpaka sasa sina uwezo wakukusikiliza tayari kesi ipo mezani, na unatakiwa kukamatwa sasa hivi, huwezi tena kuni laghai jisalimishe kabla hatuja poteza muda wetu kukusaka” alisema insp Aroub na kukata simu ………….…. ENDELEA
Ukweli nilishangazwa na msimamo wa Aroub, ambae licha ya kumpa nafasi ya kutambua ukweli juu ya vifo vya watu ambao walisadikiwa kuwa walikuwa wanauwawa na jini, lakini leo anakuwa na msimamo mgumu kama huu, na kutaka nijisalimishe kituoni pasipo kukutana nae na kuzungumzia swala hili, na kwavyo vyote hakuna hata mmoja wetu ambae angetoka salama kule kituo, lazima wote tunge dungwa sumu kwa njia yoyote na Ussi, “hataki kukusikiliza?” aliuliza Jessenia ambae wasi wasi wake nilikuwa nauona wazi wazi usoni pake, “nashangaa kwanini anakuwa hivi, au mjomba wako amempatia kitu kidogo, sasa ngoja niongee nae kwa lugha inayompata” nilisema hivyo huku na piga tena namba yake, safari hii hakupokea kabisa, nikapiga tena hakupokea, nikaiweka simu pembeni na kuondoa gari kuelekea macho manne, kichwani mwangu nikiwa nimesha ghairi kwenda chake mazoezini, baada yake nilipanga kwenda kujichimbia pwani ya mashariki kwenye fukwe tengefu ya makaani.
Lakini kabla sijafika macho manne, naona simu inaita, nikaitazama nae alikuwa ni afisa utawala wa Ali Khamis Camp, nikaipokea mara moja, huku naendesha gari, “ndiyo kaka niambie” nilisema hivyo mara baada ya kuweka simu sikioni, “ticha upo wapi, kuna taarifa nimezipata hapa toka kituo cha polisi kuwa unatafutwa kwa kosa la kumtumia Jessenia kuiba kwa mjomba wake, na sasa mupo bandarini munataka kutorokea dar” alisema bwana Malambo, hapo niakacheka kidogo, “kaka mbona nipo macho mane hapa na kuja huko wawi” nilijibu katika hali ya kawaida kabisa, na yeye akacheka kidogo, “sasa hizi habari zinatoka wapi, au Ussi ameanza mambo yake ya kuleta wivu?’ aliuliza Malambo, wakati huo nilikuwa naingia macho manne na kuifikia kona ya kuingia wawi, ambayo ipo upande wa kushoto kama unatokea wete, “nitakueleza vizuri, ila sasa nahitaji kinga ya kukamatwa, maana kila kitu kitavurugika” nilimueleza malambo, ambae mpaka muda huo hakuwa anafahamu kazi yangu halisi, huku nakata kona kushoto kuingia barabara ya kuelekea wawi.
“ok! usijari nipo na afande hapa, wacha niongee nae kisha ukija tutajuwa cha kufanya” alisema Malambo na kukata simu, na mimi nikaona sasa mambo yanazidi kuwa mazito, na ukweli nikwamba Aroub alikuwa muhimu sana kwenye hii kazi, maana yeye ndie alikuwa ameifuatilia kwa miaka mingi japo hakufanikiwa, nikaamua kumpigia tena na habati nzuri safari hii aliipokea, “nataka kusikia kuwa upo njiani unakuja kituoni we kijana” ilikuwa ni sauti ya ukali toka kwa insp Aroub, “insp tayari unaingia kwenye orodha ya washukiwa wa hii kesi, na bahati mbaya kwako, hii kesi itakuchafua sana” niliongea hivyo kwa sauti tulivu, lakini yenye amri na kuogofya, hii ni moja silaha bora sana kumtuliza mtu, “unasema…. kivipi yaani…mbona sikuelewi” alibabaika insp Aroub, huku sauti yake ikionekana kujawa na mshangao.
Hapo nikaona tayari nimesha mshika kinacho fuata ni kuzidi kumkalisha chini, “unadhani kuna mjinga ambae anashindwa kuelezwa unacho kifanya, umezuga kwa miaka saba ukichunguza kesi hii na kudanganya serikali kuwa muuwaji ni jini, na sasa ukweli unakaribia kupatikana wewe unataka kunikamata na kunifunga ili kuvuruga uchunguzi” nilisema hivyo kwa sauti ile ile yenye utulivu wa kibabe, “ticha unataka kusema nini, hao wauwaji ni wakina nani?” aliuliza mzee Aroub kwa sauti iliyopoa, “mzee kama umeweza kushawishika kirahisi hivyo na kunigeuka, sidhani kama ninapaswa kukuamini tena” nilimueleza mzee Aroub, ni kama nilimchanganya hivi.
Wakati huo nilikuwa naingia wawi messi, ambapo palikuwa na watu wacheche, akiwepo Mwasenga ambae alinionyesha ishara ya kuzungusha gari upande wa kushoto wa jengo la mess, yani kule ambako kuna ukumbi wa chakula na mimi nikafanya hivyo huku simu ipo sikioni, “Eric, unaweza kunieleza wewe ni nani haswa, na unafanya kazi chini ya nani?” aliuliza mzee Aroub, na hapo nikatabasamu kidogo, “mzee umepoteza haki ya kulijuwa hilo, jiandae kusimama kizimbani kujibu tuhuma zitakazo kukabili” nilisema hivyo kisha nikakata simu, kisha nikasimamisha gari na kushuka toka kwenye gari nikiwa na Jessenia, ambae alikuwa amevaa niqab usoni mwake tukaingia ndani simu nikiiacha ndani ya gari.
Mule ndani ya ukumbi wa chakula, tuliwakuta afisa utawala na mkuu wake wa kambi, wakitusubiri, “anaweza kutoa hiyo ninja tafadhari” alisema mkuu wa kambi, mara tu tulipoingia, na bila kuambiwa mara mbili Jessenia akatoa mwenyewe, “shikamoo mzee” nilisalimia huku namtazama mkuu wa kambi, ambae bado alikuwa amevalia sale za kazi kama ilivyokuwa kwa Malambo, huku Jessenia yeye akisalimia “asalam aleykum” huku anamtazama Malambo, “marahaba mwalimu, pole na majukumu” alisema kamanda yule mwenye cheo cha kanali, “asante mzee, lakini naamini karibu namaliza kazi” nilijibu hivyo nikiamini kuwa kwa namna moja au nyingine mzee huyu atakuwa anafununu ya ufahamu juu yangu, hasa kuhusu kazi iliyonileta pemba, “bwana Eric, ukweli nilipo pewa maelekezo na BHQ (Base Head Quarter) hawakunifafanulia juu ya kazi unayokuja kuifanya, ila walinitaka kukupa msaada wowote utakao uhitaji, sasa je naweza kukusikiliza unachohitaji kusaidiwa ili ukamilishe kazi yako, maana tumepokea taarifa ya kwamba umeiba na unatafutwa na polisi, wakikushuku kuwa upo mbioni kutoroka” alisema mkuu wa kambi, mzee mpaka hapa nimesha fikia asilimia tisini na tisa ya kazi, bado asilimia moja tu nayo kukabidhi watuhumiwa mikononi mwa vyombo vya dola, mwanzo nilifikiria jeshi la polisi, lakini sasa nao wametia mashaka” nilimueleza mkuu wakambi, huku nikimfafanulia kilicho tokea na kazi ninayoifanya.
“ok! sisi tutakupa ulinzi mda ambao utauhitaji, tunandaa askari kwaajili hiyo, maana tayari nilisha pewa kibali cha kufanya hivyo toka siku nilipopokea ujumbe wa ujio wako” alisema mkuu wa kambi, ambae alitoa maelekezo kwa afisa utawaka, kwamba awaandae askari kumi na tano, na gari moja kwaajili ya kutoa msaada nyuma yangu pale nitakapo uhitaji.
Na hapo hapo akapiga simu kwa RPC wa chake chake na kumueleza kuwa swala langu amuachie yeye, kwasababu yupo chini ya jeshi la ulinzi, na atakamatwa na jeshi la ulinzi na kupelekwa kwao polisi kama itatakiwa kufanyika hivyo, na RPC akasema kuwa atajulisha mtu aliepewa jukumu hilo, ambae ni insp Aroub, baada ya hapo nikawaaga na kuwaeleza kuwa nitawapigia baade, na kuondoka zangu nikiwaacha wanapanga mipango ya kuniwekea ulinzi.
Naam ile naingia kwenye gari nakuta simu inaita, na juu ya kioo hicho ikionekana alama ya kwamba kulikuwa na miseed call kumi na saba, na mpigaji alikuwa ni insp Aroub, nikaipokea na kuiweka sikioni, “hallow Eric, nahitaji kuonana na wewe” alisikika insp Aroub akiongea mfululizo kama amemeza CD, huku sauti yake ikiwa ya kuomboleza, “mzee unadhani unastahili kuminiwa tena, ni vipi kama una jaribu kuniweka hadharani ili maadui zangu wanipate kirahisi” nilimuuliza insp Aroub kwa sauti tulivu lakini ya kibabe, “ticha nadhani unanifahamu vyema, tumeanza vizuri tu hii kazi naomba tuimalize vizuri, unajuwa fika kuwa sihusiki, labda nimekosea kumsiliza mzee juma” alisema Aroub hakika sauti yake ilitia huruma.…. ITAENDELEA..