Kifo cha hawara (Mkono Wa Jini)

Kifo cha hawara (Mkono Wa Jini)

Huwa sipotezi muda kwenye story mpaka nihakikishe imeisha...sitaki arosto
Nimekuwa Mfatiliaji mzr wa huyu mwamba na hizi simuliz zake lkn sikua najua siku nitakuta story njian, leo kwa mara ya kwanza maana huwa nikianza kusoma na penda kumaliza mpk hitimisho ss hapa na kuwa mpole tuu
 
KIFO CHA HAWARA (mkono wa jini)
SEHEMU YA SABINI NA NNE
MTUNZI: Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA SABINI NA TATU: nikinibinya binya kwa kuikanda na mafuta mazuri ya karafuu, ni mguu mmoja baada ya mwingine, nikipandisha mkono wangu taratibu juu ya ngozi laini iliyopakaa mafuta ya karafuu, mpaka kwenye magoti ambapo palianza kuleta tatizo, hasa baada ya kuanza kutembeza vidole nyuma ya goti huku nikibinya binya taratibu, nadhani nilikuwa na mtekenya, maana japo alikuwa ametulia lakini kuna vitu vilinipa ishara kwamba kuna kitu kina mpwita……….…. ENDELEA..
Maana niliona akijilegeza kabisa na kulalia kifua chake vizuri, akiyaminya maziwa yake yenye ukubwa wa wastani, na mimi nikaendelea bila kumjali, nilitembeza vidole sehemu hiyo kwa kurudia rudia kabla sijapanda mpaka kwenye mapaja yake na kuanza kumkanda taratibu kuanza karibu ya magoti mpaka juu kwenye maungio ya makalio, ukweli sijafikiria pale mfanya massaje anapo mfanyia mtu ambae sio mpenzi wake, maana mpaka dakika hii tayari dudu yangu ilishaanza kushtuka na kujitutumua toka ndani ya boxer.
Niliendelea kuminya minya mapaja yake nikizungusha mkono mpaka maungoni, na mara kadhaa nikigusa kitumbua chake, ambacho sekunde chache baade kilikuwa kimeshalowa vibaya sana kwa ute wa matamanio, na yeye nikimuona anatikinyua kiuno chake kwa tuviuno mujarabu huku anabana makalio yake kama anachomwa sindano kila nilipo kuwa nagusa kitumbuani, na matukio kama hayo yaliendelea wakati namfunga kiunoni mbavuni mabegani na hata mgongoni, “Eric una mambo weye, umea
juaje kama ukinifanyia hivi nitajisikia raha” alisema Jessenia huku anacheka kivivu “najuwa mpenzi wangu anahitaji nini kwa wakati gani?” nilimjibu huku namgeuza na kumlaza chali, kisha nikamwagia mafuta, halafu nikaanza kuminya minya mikono yake, huku nikimnyoosha kama wamama wafanyavyo kwa watoto wao, baada ya hapo nikahamia kifuani, ambapo nilianza kuminya minya taratibu, nadhani unaweza kujuwa nilikuwa naminya kwenye nini.
Niliminya taratibu maziwa ya Jessenia, wakati mwingine nilichezea chuchu zake kwa kuzivuta taratibu, nikisaidiwa na utelezi wa mafuta, “huuuu! nasikia mwili unasisimka” alisema Jessenia, aliekuwa amefumba macho, huku anashusha pumzi ndefu iliyoonyesha kuwa na msisiko kweli kweli, “vipi niache?” nilimtega Jessenia, ambae alifumbua macho kidogo na kunitazama usoni, na macho yetu yalipokutana akaachia tabasamu la kivivu, “han haaa!!” ilikuwa ni sauti flani nyororo ya kivivu toka mdomoni kwa Jessenia, huku anafumba tena macho na kuweka shingo pembeni.
Hapo ni kama nilipata kibali cha kuufanyia vyema ule mwili mwololo wa mwanadada huyu nusu mwarabu, “hapa je unajisikiaje” nilimuuliza huku naminya minya tumbo lake taratibu, kwa mkono wa kulia huku mkono wa kushoto nikiutembeza chini ya kifua yaani kwenye vungu za maziwa, “vizuri” alijibu kwa sauti ya chini, nikaona kama vile hajakolea vizuri, nikashusha mkono wa kulia mpaka kwenye mapaja yake ambayo nilikanda kwa mikono yote miwili, “hapo vipi unajisikiaje?” nilimuuliza Jessenia, ambae alijibu kwa sauti ile ile ya chini, “raha” niliendelea kumkanda mapaja yake, nikitumia kama dakika tano nzima, huku akiwa ameyabana mapaja hayo, kisha nikahamisha tena mikono yangu na kuweka juu ya kinena chake, ile sehemu yenye kuota nywele, huku mkono wangu wa kushoto ukirudi kwenye maziwa yake na kuanza kutembeza taratibu mikono yote, hasa mkono wa kushoto ulicheza na ziwa la kushoto peke yake, niliminya minya chuchu zake taratibu, lakini mkono wa kulia ulikuwa unatembea taratibu pale juu ya kinena, nikishusha toka kwenye kinena mpaka kwenye kitumbua na kulaza kiganja changu juu ya kitumbua kile kama vile nimeshika mouse ya computer, yaani kidole cha kati kikilala kwenye kunde na kufanya kila napotembeza mkono nikisugue taratibu, hapo bila kuuliza Jessenia akafungua midomo yake, “hapo nasikia utamu” nilimsikia Jessenia akisema kwa sauti iliyozidiwa na hamu ya dudu, huku akitanua mapaja yake na kunipa nafasi zaidi na ulimi wake ukiilamba midomo yake, hapo nikamsogezea mdomo wangu nae akaudaka na kuanza kunyonyana mate, huku naendelea kuchezea shamba la bibi, nikaona anapeleka mkono wake taratibu kwenye dudu yangu na kuitoa ndani ya bukta, kisha akaanza kuichezea huku tunaendelea kupeana juice ya asili, kitumbua chake kilikuwa kimelowa kweli kweli tayari kummeza mwenzie.
Nadhani hakuna asie fahamu kilicho endelea mwishoni mwa massage hiyo tamu, tulitumia dakika thelathini kwa mchezo ule wa kupeana dudu na baada ya hapo tulioga na kuanza kula tukishushia vinywaji vyetu taratibu na macho yetu yakiwa ufukweni tukitazama wazungu mbali mbali waliokuwa wanafurahia maisha halisi, maana nasikia kwao mtu anaweza kuzaliwa mpaka anazeeka hajafika mazingira kama haya, japo mto wa kawaida tu asiuone, hivyo kwa kupitia kioo kikubwa sana cha upande wa magharibi, tuliweza kuwaona watu hapo toka mataifa ya mbali wakiwa nusu uchi, wanafanya michezo mbali mbali ya ufukweni, “Eric naamini nitafidia muda wote ambao nimeupoteza kwa majonzi na machungu, nitakupenda daima, naomba usiniache mpenzi wangu” alisema Jessenia huku akiniegemea ubavuni mwangu, “siwezi kukuacha Jesse, sasa wewe ni moja kati ya viungo vya mwili wangu, cha msingi tufanye juu chini kesho kazi iishe na sisi tukaanze maisha mapya dar es salaam” nilimueleza Jessenia kwa sauti tulivu, huku nazungusha mkono wangu mgongoni kwake na kushika kiuno chake, halafu nikamkiss kwenye paji lake la uso.
Tulikaa hapo kwa muda mrefu, huku tukitazama matendo ya watu wale waliokuwa ufukweni, ukiachana na burudani hiyo pia tulikuwa tuna panga mpango wa kesho ili kuipata Hard disc chumbani kwa Ussi kama itakuwepo, maana ni ushahidi pekee wa kumuweka Ussi chini ya ulinzi, mtu ambae tulimshirikisha na ilikuwa lazima mzee Mangeu ashiriki, hivyo nilimpigia na kumueleza mpango wangu na namna yeye atakavyo shiriki, “hakuna shida nitakuwepo muda huo, ila kuna jambo lazima ujuwe” alisema mzee Mangeu, ambae sasa bado alikuwa amejibanza mita kadhaa nje ya nyumba yake, ambayo alisema anakila sababu ya kuto kuicha ghafla, “nusu saa iliyopita Ussi na wenzake walikuja hapa, wamejaribu kuniita na walipoona kimya wamezunguka kila sehemu, nadhani walikuwa wananitafuta mimi, maana nilimsikia Ussi anasema kuwa “huyu mzee lazima aondoke, na bahatiu nzuri hakuna atakae mjali baada ya kifo chake” nilitamani niwashambulie kwa mishale, lakini nikaona itakuwa kosa kubwa kwangu, maana polisi wange niandama na ningekosa cha kujitetea” alisema mzee Mangeu, ambae aliendelea kueleza kuwa, baada ya kumaliza msako ule wakina Ussi waliondoka na kurudi nyumbani kwao, na dakika chache baadae wakaondoka kuelekea upande wa macho mane, wakitumia ile barabara waliyotukimbizia sisi.
Baada ya hapo nilipiga simu kwa mwalimu mkuu, ambae kabla sijamuomba ruksa ya kwamba kesho nitachelewa kufika shule, yeye ndie alienieleza kuwa kesho hakutokuwa na vipindi vya darasani, kwasababu wanafunzi wataenda Ali Khamis kusikiliza hotuba ya rais, “hivyo ukipata muda unaweza kujinga na sisi pale pale Ali Khamis camp” alisema mzee Farid Abdallah, na baada ya kumaliza kuongea na mwalimu mkuu, nikampigia mwalimu Aisha, ambae japo alichelewa kupokea simu, lakini alipopokea alionekana kuwa katika mshangao mkubwa, “Eric, mbona usiku sana, kuna usalama kweli” aliuliza Aisha, akiwa katika mang’amu ng’amu ya usingizi, “usalama upo wewe, tatizo lako una wasi wasi sana” nilijifanya kumtania ilikumtoa wasi wasi, “nani kasema nina wasi wasi, haya ongea nakusikiliza” alisema Aisha, huku akijitaidi kujiweka sawa sauti yake, kutoka kwenye wenge la usingizi, “kuna kitu nahitaji unifanyie kesho, naomba mida ya saa tatu tukutane pale napokaa” nilimueleza Aisha na yeye akakubaliana na mimi.*******
Naam usiku ulikuwa mzuri sana wetu, tulipeana utamu kama vile ilikuwa ni mwisho leo, tukija kumalizia asubuhi na sisi tuliondoka mahali pale mida ya saa mbili za asubuhi, ndio mida ambayo tulifika green house, nikiwa nimesha muacha Jessenia mjini chake chake chini ya ulinzi wa mzee wa Mangeu, waliokuwa mjini kila mmoja akiwa amekaa sehemu yake wakisubiri niwaambie cha kufanya.
Green Mess nilikuta nguo zangu zimevulugwa vulugwa, ikionyesha wazi kuna mtu au watu waliingia mule ndani usiku uliopita, nilitegemea hilo hasa baada ya Jessenia kumueleza mjomba wake juu ya kuwa tupo Green Mess, nilikagua kwa umakini sana chumba kizima, mpaka nilipojiridhisha kuwa hakukuwa na kitu kilicho tegeshwa, hapo nikafungua begi langu ambalo pia nilikuwa nimeweka nguo zangu na zile za Jessenia, yaani zile alizovaa jana na zile baadhi nilizo mnunulia pale macho mane, nilizibeba kwa makusudi.
Wakati nakagua vitu vyangu ukiachilia lap top ambayo ilikuwa inaonekana wazi wazi, nilikagua camera tape record, bastora na vinginevyo, ambavyo natumia kwenye upelelezi, mara nikaona kipande cha karatasi ambacho Yasini, mdogo wake Maimuna alinipatia jana pale uwanjani, nikakikunjua na kukisoma, maana sikuwa nimekisoma kabisa.
Ukweli kilichoandikwa mule ndani kilinifanya nitabasamu huku navuta picha ya kile ambacho Maimuna anakihitaji kifanyike, “ijumaa jioni baba na mama wanae unguja, nabakia mimi na Yasin, unaweza kunifuata usiku nije nikulala kwako mpaka asubuhi, unifaidi usiku kucha” yani kiukweli sikuweza kupata picha juu ya kile anacho Hitaji Maimuna kifanyike, maana huyu mschana mpaka hapo alikuwa bikira na alikuwa anahitaji kufanya kinyume na umbile, je kama ningekuwa na uwezo wa kufanya hivyo, hebu fikiria ingekuwaje, yaani usiku kucha kwa njia hiyo, ataamka akiwa salama kweli, na hicho chumba kitakuwaje, nikajikuta nacheka na kuelekea chooni nikiwa na kile kijikaratasi, ambacho nilikitia chooni na kukiflash, huku kichwani mwangu nikiwa nawaza juu ya jambo flani juu ya Maimuna, kwamba kwa akili zake zilivyo si ajabu nikashtukia akiwa ameshajileta mwenyewe.
Nilimpigia simu mwasenga kumuulizia ratiba akanieleza kuwa mgeni anatarajiwa mida ya saa tano atakuwa pale Ali Khamis camp maana sasa ndio wanampokea Airport, baada ya hapo ataenda kupata chai kwa mkuu wa mkoa, kisha aelekee Ali Khamis Camp, nikasema sasa naweza kupata muda wa kupumzika kidogo, maana nikisema usiku nilipata muda wa kulala ningedanganya, usiku tulishinda tukipatanisha viungo vya uzazi.
Kama nilipata usingizi, basi ilikuwa ni nusu saa tu, maana saa nne na robo nikasikia mlango ukigogwa, nikashtuka na kutega sikio, ukagongwa tena kimya kimya pasipo sauti ya mtu kuita, “nani?” niliuliza kama vile ambavyo watu hufanya nyakati za usiku, “wewe nae mbona unaishi kwa mashaka hivyo ingekuwa usiku ungefanyaje” ilikuwa ni sauti ya kike toka nje, “dah! nilidhania bado usiku, kumbe kumeshapambazuka” nilisema hivyo kwa utani huku naamka toka kitandani na kuufuata mlango kwenda kuufungua, maana nilisha gundua kuwa alikuwa ni mwalimu Aisha.
Na ile namfungulia tu, nikakutana na mashtaka “mh! halafu mwaka huu utafungwa we mwanaume, maana jana nimepigiwa simu ya kuuliziwa na shemeji yako” alisema Aisha huku anakuja kukaa kwenye kiti cha mule chumbani, “mh! alikuwa anataka nini” nilimuuliza Aisha, huku nikijifanya sielewi chochote, “alinipigia mwenzio ile umetoka kupiga tu, na yeye huyu akauliza, eti huyu mwalimu mwenzio alietokea bara yupo wapi usiku huu, nikamuambia, atakuwa nyumbani kwake jeshini au wawi mess, sasa sijui kama alikuja au laa, yani nikahisi umemtorosha Seni” alisema Aisha mwisho wote tukacheka “acha utani Aisha, ila nimekuita kwa ajili hiyo hiyo, nataka leo ujifanye mwanamke wangu” nilimueleza Aisha, ambae alishtuka sana na kunitazama kwa mshangao…….…. ENDELEA..


KIFO CHA HAWARA (mkono wa jinni)
SEHEMU YA SABINI NA TANO
MTUNZI: Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA SABINI NA NNE: “mh! alikuwa anataka nini” nilimuuliza Aisha, huku nikijifanya sielewi chochote, “alinipigia mwenzio ile umetoka kupiga tu, na yeye huyu akauliza, eti huyu mwalimu mwenzio alietokea bara yupo wapi usiku huu, nikamuambia, atakuwa nyumbani kwake jeshini au wawi mess, sasa sijui kama alikuja au laa, yani nikahisi umemtorosha Seni” alisema Aisha mwisho wote tukacheka “acha utani Aisha, ila nimekuita kwa ajili hiyo hiyo, nataka leo ujifanye mwanamke wangu” nilimueleza Aisha, ambae alishtuka sana na kunitazama kwa mshangao…….…. ENDELEA..

Ungesema nimeeleza jambo baya la kushtua, “Eric usinitafutie balaa mwenzio, umesikia wapi mtu anajifanya mtu wa mtu, kuna vitu avibipwiki hivo” alisema Aisha akionyesha wazi kuwa hayupo tayari kufanya ninacho mueleza, “kivipi Aisha, mbona kitu rahisi tu, si unajifanya mpenzi wangu kwa muda mfupi” nilijaribu kumueleza kwa lugha laini, lakini ndio kwanza nikawa kama namshangaza, “sio bara huku, mnapata njiani munaenda chumbani kufunga ndoa, mukimaliza mwaachana, na hata kama naweza kuiba, lakini siwezi kumfanyia hivyo Seni” alisema Aisha, akimaanisha anachokisema,

na hapo nikamuelewa anachomaanisha, nikaangua kicheko, “hebu acha ujinga Aisha, nani kakuambia ninataka kukugonga bwana” nilimuambia Aisha, huku nikiendelea kucheka, “kumbe wanitakia nini, hebu niambie nijifanye kivipi, na wote hapa wanafahamu na mtu wangu” alisema Aisha, akionekana kupoa kidogo, “ni hivi, kuna nguo nataka uvae, lakini utavaa na niqab pia, kisha tutaenda kwenye mkutano wa Rais, sawa?” nilimuuliza Aisha kama amesha nielewa, bahati nzuri kwangu nae alikuwa amenielewa, “hoooo kumbe hivyo tu! na vipi akikuona Seni, au ndio usha muanzia vituko umuache?” aliuliza Aisha, huku acheka kidogo, lakini alionekana kutopendezwa, kama kile alicho kifikiria ndio lengo langu, “kama ningekuwa kaka yako, ungeni ruhusu nimuache Jesse?” nilimuuliza Aisha, ambae alicheka kidogo, “tena kwa taarifa yako na limbwata ningekuwekea mwenyewe” hapo wote tukaangua kicheko, “yani ulinitisha, nilijuwa wataka kunitia, maana weye waoneka kiboko sana, umeweza kumnasa Seni wakati majabari yameshindwa pale” aliongeza Aisha, ambae bado alikuwa anaendelea kucheka, sambamba na mimi mwenyewe.
Baada ya hapo, nikaanza kumpanga na kumueleza cha kufanya, nilimuambia atokea pale Green House, aende mpaka shuleni, kisha azunguke upande wa nyuma, kwenye njia ya choon, na mimi nitampokea upande wa nyuma ya nyumba ile ndogo, yenye two in one, (mbili kwa moja) nae akiwa hajui lengo halisi la mpango ule, alitoka na kuelekea upande wa shuleni, yani Fider Castor, akiniacha mimi naandaa nguo zake, ambazo alitakiwa kuzivaa, wakati huo huo nikapokea ujumbe toka kwa Mangeu, ukisema kuwa Ussi na wenzake wapo nyumbani, na wao wawili, yaani Jessenia na mzee Zidadu, sasa wamesha toka mjini chake chake nakujibanza ndani ya kibanda cha Mangeu, wakisubiri amri ili Jessenia aweze kuingia ndani kwao, kuisaka Hard disc ambayo mpaka muda huo hatukujuwa kama itakuwa imefutwa au bado ina video ya siku ya tukio.******

Yap! mida ya saa tano kasoro, ndio mida ambayo nilikuwa nasogea eneo ambalo rais ange hutubia, wananchi wa cheke na vitongoji vyake, sambamba na kuzindua ujenzi wa majengo mapya ya makazi ya askari, nikiwa nimeongozana na Aisha ambae sio tu kuvaa nguo ndefu iliyoficha miguu yake, pia alikuwa amevaa niqab ambayo iliambatana na kitambaa chepesi kilichofunika macho yake, lakini hakikumzuia kuona mbele.

Tulitembea taratibu kwa miguu, tukitokea Green House, tukiambatana na watu wengi ambao walikuwa wanaelekea kwenye kumsikiliza rais, huku kwa ujanja na akili nyingi nikijaribu kutazama pande zote, kama kuna mtu angekuwa anatufuatilia, lakini mpaka nafika pale kwenye eneo husika hakukuwa na mtu niliembaini, “ticha mambo vipi” alinisalimia afisa utawala, yani bwana marambo, ambae alikuwa amevalia nguo sale za jeshi za rangi ya kijani, zenye kufanana juu na chini mfano wa suit na vishikizo vyenye kung'aa mfano wa dhahabu, huku mabegani kwake nyota za chuma zikiwa zina ng’aa kweli kweli “kaka leo umewaka kwa pamba nyepesi” nilimtania bwana Malambo,ambae alicheka kidogo na kumsalimia Aisha, “mambo vipi shemeji, naona umejipamba kweli kweli” alitania malambo, akiwa na maana ya kwamba amewekea maficho, kujipamba huo ni msemo wa kijeshi, pale wanapo jibadilisha umbo, au muonekano, wafanane na mazingira waliyopo, wote tukacheka huku Aisha akicheka kidogo sana, kuzuia asije akatambulika mbele ya Malambo.

Watu walikuwa wengi sana mahali pale, yani wake kwa waume, askari raia na wanafunzi na wengine walikuwa wanaendelea kuja, tena kwa wingi sana, wakisimama upande wa mbele wa jukwaa la VIP ambalo atakaa rais, huku pembeni yake kushoto na kulia kukiwa na viti ambavyo vilikaliwa na watu wa itikadi tofauti, upande wa kulia walikaa watu wa vyombo vya ulinzi na usalama, naposema hivyo nadhani unanielewa, yani namaanisha askari wa jeshi la ulinzi, polisi mafunzo (magereza) KVZ, JKU na KMKM, na wengine ambao nilishindwa kuwatambua, kutokana na kuvalia nguo za kiraia.

Upande wa kushoto, ulikuwa umekaliwa na wazee wa chake chake, pamoja na wanachama wachama tawala, “ticha unaweza kunieleza japo kifupi mambo yalivyokuwa jana, maana mkuu aliniita na kunisisitiza kuwa nihakikishe upo…” alisema Malambo na hapo nikamkatiza, “hooo niliongea nae, nitakueleza baadae, ila kila kitu kilienda freshi” nilizuga ili Aisha asielewe lolote, nadhani Malambo alinielewa kwa haraka, maana alipotezea, “ok! munaonaje mukakae pale kwa makamanda, lakini shemeji atatakiwa kutoa uninja na akitoa tu mjomba wake atamuona maana nime muona akiwa amesha ingia” alisema Malambo huku anaonyesha upande ule waliokaa wazee na wanachama, hapo mimi na Aisha, tukatazama vizuri upande ule waliokaa wazee, na watu wengine waliovalia sale za chama tawala, “mbona simuoni, amekaa sehemu gani?” nilimuuliza Malambo, ambae alinielekeza kwa alama, “mcheki mtu wa tano toka kushoto, halafu nyuma yake, yule ambae anaongea na jamaa” alisema Malambo, na mimi nikifuata kwa macho.

nilifanikiwa kumuona mzee Juma, akiwa anaelezwa jambo na kijana mmoja ambae, alikuwa anamueleza kwa mtindo wa kunong’ona maana alikuwa amuinamia sikioni mwake, kisha nikamuona mzee huyo anamueleza mzee aliekaa jirani yake, kisha akainuka na kutoka pale walipokaa wenzie, “ni kweli nimemuona, sasa hapa bro, wacha sisi tusimame pembeni kwa kule nyuma” nilimueleza Malambo, maana lengo langu ni kwamba, nifanye jambo ambalo litamfanya mzee yule atambue uwepo wangu na kuhisi kuwa nipo na Jessenia, “ok! poa aina noma, tukutane mchana kwenye chakula mess” alisema Malambo kisha tukaagana na yeye akaelekea kwa makamanda wenzake, “twende upande ule” nilimshauri Aisha, huku tuna tembea kuelekea nyuma ya kundi kubwa la watu, kule ambako mzee Juma alielekea, japo alikuwa amesha potea usoni mwangu

“lakini leo Eric umejuwa kunigeuza kituko mwenzio, yasni yule mwenzio amehisi kuwa mimi ni Seni” alisema Aisha kwa sauti ya utani, na kabla sija jibu lolote, nikashtuka nikiguswa mkono, “assalam alaykum Ticha” ilikuwa ni sauti ya kischana toka kushoto kwangu, nikageuka kumtazama alikuwa ni Maimuna, ambae alikuwa ananitazama kwa tabasamu angavu, “waaleykum salaam Maimuna, haya tafuta sehemu ukae, ili umsikilize Rais vizuri” nilimueleza Maimuna, ili aodoke mara moja maana sikutaka aongee sana na kumfanya Aisha ahisi jambo, “nimesha pata pakukaa, lakini nimekuja kukusalimia tu” alisema Maimuna, huku anajitabasamulisha kama mtoto,

yani ungemuona wakati huo usingeweza kumfananisha na kile anachotaka nimfanyie, tena kwa usiku kucha, “hoooo safi sana mwanafunzi wangu, haya nenda kakae sasa” nilisema hivyo, na bahati nzuri Mainuma akawa muelewa, akaenda kukaa sehemu aliyokuwa amekaa, “Eric kuwa makini na hako katoto, yaani kana mapepe kama nini” alisema Aisha huku tuna tembea kuelekea nyuma ya kundi lile, ambako kulikuwa na walimu kadhaa wa Fider Castor, ambao naweza kusema ni walimu wenzetu, “hata mimi nimekaona yaani dah! mpaka kanashangaza” nilisema hivyo huku naendelea kutazama kushoto na kulia kuona kama ninge muona mzee Juma, yani mjomba wake Jessenia, “nakaona kanavyo kuhangaikia, utasema ni fisi kaona banda la kuku” alisema Aisha, huku anageuka kumtazama Maimuna ambae alikuwa anatokomea kwenye kundi la wanafunzi wenzake, “lakini anawezaje kufanya hivyo, wakati nasikia waschana wa huku hawaingiliwi mpaka waolewe?” nilimuuliza Aisha swali ambalo jibu nilikuwa nalo, ila tu nilitaka kusikia maoni yake au kupata habari zaidi, “mh! misijui, labda anacho kingine cha kumpa ili kutunza bikira yake” alisema Aisha, tukimalizia kwa kicheko.

Wakati huo tayari tulisha karibia pale walipokuwa walimu wenzetu, “hoooo! ticha Eric, umemuacha wapi mwalimu Aisha, maana alisema anakuja kukupitia muje wote” aliuliza mwalimu mmoja wa kiume, nashukuru Aisha alikuwa amekaa kimya na kunipa nafasi ya kutoa jibu, “aliniambia anakimbia mara moja nyumbani kwao, kuna kitu alisahau” nilidanganya ili kuendelea kumpa maficho Aisha, “atawahi kweli au ndiyo kasha kosa hotuba?” aliuliza mwalimu mwingine wa kike, na hapo nikatoa jibu jepesi, “ametoka muda mrefu uliopita, nadhani anaweza kuwahi” nilijibu hivyo huku nageuka kutazama nyuma, ambako mita kama kumi toka nilipokuwepo, nilishangaa kumuona mzee Juma, akiwa na yule jamaa aliekuwa anamnong’oneza wakionyeshana kitu usawa wa pale niliposimama……….…. ENDELEA..


KIFO CHA HAWARA (mkono wa jini)
SEHEMU YA SABINI NA SITA
MTUNZI: Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA SABINI NA : “atawahi kweli au ndiyo kasha kosa hotuba?” aliuliza mwalimu mwingine wa kike, na hapo nikatoa jibu jepesi, “ametoka muda mrefu uliopita, nadhani anaweza kuwahi” nilijibu hivyo huku nageuka kutazama nyuma, ambako mita kama kumi toka nilipokuwepo, nilishangaa kumuona mzee Juma, akiwa na yule jamaa aliekuwa anamnong’oneza wakionyeshana kitu usawa wa pale niliposimama ENDELEA……..
Tuka kutanisha macho yetu, na yule jamaa aliekuwa na mzee Juma, niwazi alikuwa anamuelekeza kuhusu mimi.

Hapo nikatazama mbele, sikutaka wajuwe kama nime waona, “kama amefika na nakugeuza, basi ataingia sasa hivi” alisema mwalimu mwingine, ambae alimtazama Aisha, nikahisi alitaka kumsalimia, nikaamua kuwahi “anawahi nina uhakika huo” niliongea kwa haraka huku nageuka, kutazama kule walikokuwepo wakina mzee Juma, ambao niliwaona wanasogea pembeni zaidi, huku mzee Juma anabofya bofya simu yake na kuiweka sikioni, nikajitabasamulia moyoni, huku naadika ujumbe kwenda kwa mzee Mangeu, “kuweni tayari” ndivyo nilivyoandika ule ujumbe, ambao niliutuma kwenda kwa mangeu, kisha nikatulia sekunde kadhaa, kabla sijageuka kwa umakini na kutazama kule alikokuwepo mzee Juma na yule jamaa, wakati huo niliweza kuwaona makamanda mbali mbali wakiwasilina kwa simu, ni wazi rais alikuwa njiani anakuja.

Naam niliwaona wawili hawa wakitawanyika, na kila mmoja akielekea sehemu yake, mzee Juma aliekuwa anaweka simu yake kwenye mfuko wa kanzu, yeye alielekea kule kwa wazee wenzake na yule jamaa, nikamuona anakuja kwenye eneo lile tulilokaa sisi, na hapo hazikupita ata dakika tatu, nikasikia simu yangu inaita, nikaitoa haraka na kuitazama, mpigaji alikuwa ni babu Mangeu, sikujiuliza mara mbili nikaipokea haraka sana, “niambie mzee” niliongea, mara baada ya kuweka simu sikioni, “wametoka vipi aingie?” aliuliza mzee Mangeu, “una uhakika hajabakia mtu ndani” nilimuuliza Mangeu kwa sauti ya chini, ndiyo wametoka Ussi na wale wenzake sita” alijibu Mangeu.

na hapo nikamueleza chakufanya, “yeye aingie, ila wewe nenda barabarani, hakikisha unakuwa makini, ukiwaona tu, mpigie Jesse atoke haraka, na yeye mwambie asitumie muda mrefu ndani” nilipomaliza kumuelekeza hayo, nikakata simu na kutulia kama dakika tano hivi, nikivuta muda ili niondoke na Aisha akavae nguo zake, maana kazi yake ilisha kwisha.

Lakini baada ya dakika tano kutimia, kabla sijamueleza Aisha tuondoke, mara tukaanza kusikia ving’ora vya magari ya polisi yale yanayoongoza msafara vikija kwa mbali, na hata tulipotazama barabarani nikaona polisi wengine wameshaanza kusimamisha magari kupisha msafara, nikajuwa hata wakina Ussi nao watakuwa wamezuiliwa, hivyo ni vyema kama nitatoka muda huu kuelekea Green House, maana kama kuna mtu atakuwa ananifwata ni mmoja tu, nae ni huyu jamaa aliesimama mita kadhaa nyuma yetu, “Aisha hebu nifuate” nilimuambia Aisha, kisha nikaanza kutembea kutoka eneo lile, huku na yeye akinifuata, huku tukipita mita chache sana, toka aliposimama yule jamaa, ambae alijifanya kama vile hakuwa na mpango wowote na sisi.

lakini tulipo mpita tu, akageuza shingo yake kututazama, sikutaka kuonyesha kama nimemuona, hivyo tulitembea taratibu kutoka eneo lile, haikushangaza sana maana watu wengi bado walikuwa wanakuja, hivyo tulikuwa tunapishana nao na kuchangamana nao, na hakuna alie tujali zaidi ya yule jamaa, ambae alitusindikiza kwa macho mpaka tulipokaribia kupotelea barabarani ndipo nilipomuona na yeye akitoka pale mkutanoni na kuanza kuja tulikoelekea sisi.

Na wakati huo tayari ving’ora vilikuwa vina sikika kwa ukaribu zaidi, sikuyajari sana, tukaendelea kutembea kuelekea Green House, “lakini weye Eric, mbona wanisumbua hivyo, rais anaingia na sie tunatoka maana yake nini lakini” alilalamika Aisha, wakati tunaendelea kutembea, “tunageuza sasa hivi, cha msingi tukifika pale badili nguo haraka haraka” nilimuambia Aisha, kwa maana ya kumsisitiza na sikutaka kumueleza kuhusu mtu anae tufuatilia nyuma yetu, haikuwa vyema kumshirikisha moja kwa moja katika hili.
Wakati tuna endelea kutembea nikasikia simu yangu inaita, nikahisi kuwa ni mzee Mangeu ananipa taarifa fulani, lakini nilipoitoa na kuitazama nikaona jina la mpigaji kuwa ni Jessenia nikaipokea haraka, “vipi umefanikiwa” niliuliza bila kutaja jina, sikutaka Aisha ajuwe naongea na nani, “nimeona kidude kama ulicho nielekeza lakini pia kuna lap top yake hapa, niichukue” aliuliza Jessenia, na mimi nikamwambia aibebe, “usikae tena hapo toka mara moja, maana wakikukuta itakuwa hatari kwako” nilimsisitiza Jessenia kisha nikakata simu, huku tukiendelea kutembea kuelekea Green house, wakati huo tulisikia magari yakiingia pale ambapo rais alitakiwa kuhutubia.

Tulifika Green House, nibakia sebuleni na yeye akaingia chumbani kubadili nguo, huku mimi nikichungulia dirishani kumtazama yule jamaa, ambae nilimuona akiwa amesimama upande wa kuelekea Fider Castor akitazama upande wa Green House, ambako tupo sisi kule chumbani Aisha alitumia dakika tano tu, akatoka akiwa amesha vaa nguo zake, alizovaa asubuhi, “nisubiri hapa” nilimueleza Aisha anisubiri sebuleni, “naona penzi la bandia limeisha” alisema Aisha kwa utani, tukacheka huku tunapishana, mimi nikiingia mule ndani, na Aisha akinisubiri sebuleni, kama nilivyo muambia.

kule chumbani nilichukuwa begi langu dogo, pamoja na vifaa muhimu vya kazi, kama ilivyokuwa jana usiku, baada ya hapo nikachungulia tena dirishani, nikamuona yule jamaa akiwa pale pale, “mpuuzi imekula kwako” nilijisemea huku natoka na kuungana na Aisha pale sebuleni, nikamkabidhi, niqab, “vaa hii, utavulia ndani ya gari” nilimuambia Aisha, ambae alivaa niqab haraka na kisha tukaondoka zetu, nakuingia ndani ya gari kisha nikaondoa gari, kuingia barabarani.

Na ile tunaikamata barabara, nikaliona gari la Ussi lile land cluizer Prado likija kwa speed upande ule tunao tokea sisi, hivyo tukapishana, “mh! huyu sijui anavutaga bangi” aliuliza Aisha, huku anatoa niqab, “kwani ni nani huyu?” niliuliza swali ambalo jibu lake nilikuwa nalo, huku natazama kwenye side mirror, na kuliona gari lile lina geuzia pale Green house, nikajipapasa kiunoni na kugusa APG 5.2 mm, ambayo ilikuwa imetulia kimya, inasubiri mtu wa kumfanyia majaribio, “si shemeji yako mwenye wivu kuliko watu wote duniani, usikute amekuja kuhakikisha kama mimi ni Seni” alisema Aisha, kwa sauti iliyoonyesha kuchukizwa na Ussi, “tena huyooo anageuka, wacha tuegeshe gari paleee, halafu tukasikilize hotuba” nilisema hivyo huku natazama gari la kina Ussi ambalo lilikuwa limesha tukaribia, na sisi tulikuwa tunakaribia kwenye mkusanyiko wa watu, huku tukiyaona magari ya vyombo vya ulinzi na usalama, yani jeshi la ulinzi, polisi, JKU, KVZ Mafunzo na KMKM (Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo) huku watu waliovalia sare mbali za majeshi, wakiwa wamesimama kwenye magari ya vikundi vyao, japo wapo walio valia nguo za kiraia, nao walikaa kwenye magari yao meupe, yenye namba za serikali, yani SMZ, yote yakiwa yame simama pembezoni mwa barabara, pamoja na magari mengine ya kiraia ya watu binafsi, ambao walikuwa wameenda kumsikiliza muheshimiwa Rais.

Namimi nikaenda na kuegesha gari pembeni ya barabara, sambamba na yale magari mengine, kisha tuka shuka, nikafunga gari milango yote, kasoro mmoja tu wa abaria wa nyuma upande wa kushoto, ambao ulikuwa nje ya barabara, wakati huo gari la wakina Ussi likiwa linapunguza mwendo na kuja kusimama nyuma ya gari langu. …….…. ITAENDELEA..
 
KIFO CHA HAWARA (mkono wa jini)
SEHEMU YA SABINI NA SABA
MTUNZI: Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA SABINI NA SITA: Na mimi nikaenda na kuegesha gari pembeni ya barabara sambamba na yale magari mengine, kisha tuka shuka, nikafunga gari milango yote kasoro mmoja tu wa abaria wa nyuma upande wa kushoto, ambao ulikuwa nje ya barabara, wakati huo gari la wakina Ussi likiwa linapunguza mwendo na kuja kusimama nyuma ya gari langu.…. ENDELEA…..
Hapo nika tabasamu kimoyo moyo, huku naanza kutembea nyuma ya Aisha kueleka kwenye mkusanyiko wa watu na mkononi nimesha chukua simu na kumpigia Jessenia, na wakati naipiga na kuweka sikioni, nikajifanya najikuna kichwani nikatumia mwanya huo kugeukia upande lilipo gari la kina Ussi, nikamuona Ussi akiwa ameshuka toka kwenye gari na wenzake wawili, ambao ni wale wale aliokuwa nao usiku wakati wanatushambulia.

Tulipo kutanisha macho yetu na Ussi, nikampungia mkono, “niaje Ussi mambo vipi” nilimsalimia huku nikiwa nimejichangamsha, usingedhania kama nina fahamu kuwa yeye na wenzake ndio waliotaka kuniuwa jana usiku, wakati huo niliskia simu ikiwa imepokelewa upande wa pili, yaani na Jessenia, “poa mambo vipi” alijibu Ussi, kwa sauti ambayo haikuwa na uchangamfu wowote, huku yeye na wenzake wanaendelea kutembea kuelekea kule kwenye mkusanyiko wa watu, ambako sasa kulisikika sauti toka kwenye vipaza sauti zilizo kuwa zina ashiria sasa ulikuwa ni wakati wa utambulisho kwa wageni walio ambatana na raisi, “Eric vipi mbona huongei, unanichelewesha mwenzio, namalizia ili niondoke” ilikuwa ni sauti ya Jessenia toka upande wa pili wa simu, ikionyesha kuwa ni mwenye wasi wasi mwingi sana, “ina maana ulikuwa bado hujatoka hapo nyumbani” niliuliza kwa sauti ya chini kidogo, huku nikimtazama Aisha ambae alikuwa ananipa ishara fulani, ambayo mwanzo sikuwa nimeielewa, ila baada ya kuirudia mara kadhaa, nikaielewa kuwa, ilikuwa ni ishara ya kunieleza kuwa, nitazame upande wa kushoto kwangu yaani kwenye magari yale ya vikundi vya ulinzi na usalama.
Hapo mimi nikatazama upande ambao ulionyesha wazi kuwa kuna mtu alikuwa ananiita, “ndio nataka kutoka, vipi wakina Ussi wanakuja?” aliuliza Jessenia kwa sauti ile ile iliyojaa wasi wasi, “hapana ila muda wowote wanaweza kuja, cha msingi toka hapo kwenu, elekea moja kwa moja njia panda ya kuingilia hapo kwenu, hapo utamkuta mangeu” nilimuelekeza kwa sauti ya chini, huku nikiwa nimesha muona mtu aliekuwa ananiita, alikuwa ni insp Aroub, kumbe nae alikuwa miongoni mwa wale askari wa jeshi la polisi waliokuwepo kwenye yale magari, ambae sasa alikuwa anatembea kunifuata, “sawa usichelewe Eric mwenzio naogopa” alisema Jessenia na kukata simu.

Na mimi nikaiweka simu mfukoni na kutazama Aisha, “tangulia nakuja Aisha” nilimuambia Aisha, lakini lengo langu alikuwa hilo lengu langu lilikuwa ni kumtazama Ussi na wenzake watatu, ambao niliwaona wamesha fika kwenye mkusanyiko, nikaona huo ndio wakati ambao nikichomoka na gari naweza kuwaacha, japo nilijuwa kuwa kuna wengine wamebakia ndani ya gari, ambao wanaweza kuwa wanne, lakini wasinge jichukulia uamuzi wa kuondoka bila ruksa ya Ussi.

Aisha alielekea kwenye mkusanyiko, na mimi nikamfuata huku namuonyeshea ishara ya kwamba turudi kwenye gari langu, tukaongelee pale nae akafanya hivyo.

Wakati naelekea kwenye gari, nikatazama kwenye lile Prado la Ussi kwa kupitia kioo cha mbele, nilifanikiwa kuona dalili za uwepo wa watu ndani ya gari, lakini sio kwenye seat za mbele, na bahati nzuri wakati huo huo nikamuona yule aliekuwa ananifuatia akiwa anatokea upande wa Green Mess kuja huku juu kwa mwendo wa haraka, “niambie Eric, naona umekuja kujumuika na Rais kwenye uzinduzi wa ujenzi” alisema Aroub mara baada ya kunifikia mimi, ambae nilikuwa nimesha karibia gari, “si unajuwa tena mzee, ni muhimu sana kusikiliza hotuba za viongozi kama hawa, maana sisi waandishi huwa tunapenda kupata habari moja kwa moja, hata hivyo hii simu niliyopigiwa inabidi niende mjini haraka sana” nilimueleza mzee Aroub, huku tuna zunguka gari kuelekea upande wa kushoto wa gari, yani nje ya barabara, ambako mimi nilifungua mlango ule ambao niliuacha bila kuu lock na kukaa kwenye seat ya nyuma ya upande huo wa kushoto, “basi nisikupotezee muda ila nina mawili matatu nataka nikuelezee kabla hujaondoka” alisema mzee Aroub.

Ukweli sikuona sababu ya kukataa kumsikiliza huyu mzee, ambae kiukweli nitahitaji msaada wake mkubwa hapo baadae, “haina shida ni lazima baadae tuongee, maana kuna jambo nitaomba unisaidie, nadhani litakuwa zuri kwako pia” nilimueleza Aroub, ambae alitabasamu kidogo, “bado unahitaji kujuwa habari za majini licha ya kufahamu yote haya?” lilikuwa swali la utani lililo ulizwa na insp Aroub, wote tukacheka, “unadhani naweza kuacha kazi niliyoianza,l kirahisi hivyo?” nilimjibu kwa mtindo wa swali, “ok! wacha tuongee ili uwahi” alisema insp ambae alianza kunieleza kile alichotaka kunieleza.

“Unakumbuka jana tulikutana usiku hapo juu” alisema insp Aroub, huku anaonyesha upande wa ngerengere, na mimi nikaitikia kwa kichwa, kukubali, na yeye akaendelea, “nadhani nilikueleza tulicho kikuta pale, sasa yule tuliemkuta amechinjwa nimegundua kuwa sio inshu za kisiasa” alisema insp Aroub kwa sauti ya chini, “japo sijaliongea hili ofisini, lakini nimegundua kuwa yule jamaa ni mfanyakazi wa Ussi huyo aliepita hapo, nimepanga baada ya kumpeleka mheshimiwa air port ndiyo nianze kuwafanyia mahojiano kama nilivyo kuambia jana, kuwa ninahitaji kuonana na mzee Juma, kisha kijana wake Ussi” alisema mzee Aroub,

Hapo nikagauze uso na kutazama kule kwenye mkusanyiko wa watu, lakini sikuweza kuona vizuri kutokana na giza la kioo, yaani tinted, “unadhani kwa kuwahoji utafanikiwa kupata chochote?” nilimuuliza insp Aroub, nae akatulia kidogo akitafuta jibu sahihi, ambalo alilipata sekunde tano mbele, “ndio maana nimekueleza kabla sijafanya chochote ili nipate ushauri katika kuhoji” alisema insp Aroub, na hapo sikumkawiza, “hebu mtazame Ussi halafu niambie amekaaje” nilimuambia mzee Aroub, ambae alikuwa amesimama na mimi na mimi nimekaa, kwa kimo chake na ufupi wa gari aliweza kuona vyema kule kwenye mkusanyiko.

na wakati huo huo simu ikaanza kuita, alikuwa mzee Mangeu aliekuwa anapiga, “mh! sijui ameshahisi tuna mzungumzia, mbona yeye na wenzake wanatazama sana huku?” aliuliza mzee Aroub, kwa sauti ambayo ilionyesha mashaka, “tutaongea baadae juu ya hilo, wacha mimi niondoke, naomba akianza kunifuata nijulishe” nilimueleza mzee Aroub, huku nahamia seat ya mbele kupitia kule kule nyuma, kisha nikawasha gari na kumuomba anifungie mlango.

Ile mzee Aroub anafunga mlango tu, na mimi nikaondoa gari taratibu huku nachukuwa simu niipokee, lakini ikakatika na kabla sija maliza eneo lile la mkutano, huku nikitembea taratibu, simu ikaita tena, alikuwa ni Mengeu tena, nikaipokea na kabla sijasema lolote, Mangeu akaongea, “kijana tayari Seni yupo hapa anakusubiri, sasa wewe upo wapi au unataka mpaka wamkute?” aliuliza mzee Mangeu kwa sauti iliyojaa ghazab kidogo, “dakika tano nitakuwa hapo” nilijibu hivyo kisha nikakata simu na kukanyaga mafuta kwa nguvu, maana wakati huo tayari nilikuwa nimesha maliza eneo lenye mkusanyiko.

Niliendesha gari kwa speed kali sana, nikigusa speed mia moja kwa saa, lengo langu lilikuwa ni kwamba wakina Ussi ambao nilijuwa nilazima wange nifuata watakapoingia ndani ya gari na kuanza safari wawe wamesha chelewa, wakute nimesha mchukuwa Jessenia na kuondoka nae.

Lakini wakati naiacha ngerengere, nikasikia simu yangu inaita, nilipoitazama alikuwa ni insp Aroub, nikaipokea mara moja, “hallow Ticha Ussi na wenzake ndio wanatoka hapa” alisema insp Aroub na wakati huo kwa mbali nilikuwa nasikia ngurumo ya gari kupitia simu yake, ukweli kutoka hapo mpaka hapa nilipo hapakuwa mbali sana, hivyo nililazimika kuongeza mwendo na sasa nilitembelea speed mia ishirini mpaka mia thelathini kwa saa, japo isinge kuwa kitu kwa gari kama Prado, lakini kwakuwa ni safari fupi niliamini hawato nikuta.

Ni kweli, mpaka nafika kona ya macho manne, na kuikamata barabara ya kwenda chake, sikuona dalili ya uwepo wa gari la Ussi nyumba yangu, nikaongeza speed kueleke upande wa chake chake, mpaka nilipo fika sehemu ambayo niliwaambia wakina Jessenia wanisubiri, nao niliwakuta wananisubiri, huku Jessenia akiwa amesimama pembeni ya fuko kubwa la shangazi kaja, ilinishangaza sana, nikajiuliza ule mzigo mkubwa ni wanini, lakini hapakuwa na muda wa kuhoji.

ile nasimamisha gari tu, Jessenia akafungua malango wa nyuma wa abiria na mzee Mangeu aka nanyua ule mfuko, mkubwa ambao ulikuwa umejaa kweli kweli na kuuweka ndani ya gari, huku Jessenia mwenyewe akiingia ndani ya gari, “kijana oder yenu ya chumba Mantarif nimesha weka, nendeni mukajificha huko tutawasiliana” alisema mzee Mangeu na mimi sikuchelewa nikakanyaga mafuta nakuondoa gari kueleka mjini, speed kali kweli kweli, “Jesse huo mzigo wa nini, na vitu nilivyo kuagiza viko wapi?” nilimuuliza Jessenia, ambae licha ya kuwa kwenye gari lakini bado alikuwa na wasi wasi mwingi, “nimechukuwa baadhi ya nguo zangu kwa mjomba sirudi mpaka wamekamatwa” alisema Jessenia huku anageuka kutazama nyuma kwa kupitia kioo cha nyuma ambacho hakina tinted.

Unajuwa nini, licha ya fedha zote zilizopo na uzuri wa Jessenia, lakini hakuwa na begi, na hiyo yote ni kwasababu hakuwahi kusafiri kwenda mbali, wala hakufikiria kusafiri, na ukichukulia nguo zake zilikuwa zinahifadhiwa kwenye makabati ya nguo yaliyopo chumbani kwake, ndio maana leo alichukuwa nguo zake kwa hili fuko la shangazi kaja.

Hapo nilitabasamu kidogo, maana uamuzi wa Jessenia, hata mimi sikuufikiria, japo lilikuwa wazo zuri ili kuwa panikisha na kuwa fanya wazidi kujitokeza hadharani, ila kwa upande mwingine niliogopa kuwa familia yake bandia ingenigeuzia kibao kwamba nimemtorosha Jessenia,

sikuongea chochote, nilizidi kukanyaga mafuta tukipita chake chake na kuikamata madungu kisha tuka ikamata Kangani, ambapo tuliingia upande wa kuelekea air port ambapo upande huo barabara ilikuwa nyeupe, hivyo nilikanyaga mafuta mpaka kufikia speed mia arobaini, wakati huo huo nikasikia simu inaita, nikapokea na kuiweka sikioni, “kimbia unavyoweza hawa jamaa wamepita hapa, wanakuja huko mbio mbio” alisema Mangeu kabla ya kukata simu.

“nani babu Mangeu, anasemaje?” aliuliza Jessenia, ambae sikuwa na haja ya kumficha, japo alikuwa na uoga wa wazi kabisa, “anasema wakina Ussi wamesha pita chake wanakuja” nilimueleza huku naendelea kukanyaga mafuta na kutembea kwa kilomita kama mbili hivi mbele, upande wa air port, tuka ikuta njia ya mkato ya kurudi wawili, ambayo tuliifuata barabara hiyo, ambayo kwa mwaka huo wa 2005, ilikuwa bado ya vumbi na kufanya mwendo wangu uwe wa speed sabini mpaka themanini kwa saa, huku mara kwa mara nikijaribu kutazama kwenye side morror kama ningefanikiwa kuliona gari la wakina Ussi likitufuata, lakini sikuona dalili ya gari nyuma yetu.

Na wakati huo huo tukasikia simu ya Jessenia inaita, nae akaitoa mara moja na kuitazama jina la mpigaji, nikamuona anashtuka, “Ussi huyo ananipigia simu” alisema Jessenia kwa sauti iliyojaa uoga, huku ananionyesha kioo cha simu, nikaona jina kaka Ussi, “pokea msikilize anasemaje, usimuonyeshe hasira” nilimuambia Jessenia, ambae alitumia sekunde tatu, kuweka sawa sauti yake, kisha akaipokea simu ile, na kuweka loud speeker, “asalam alaykum” alisalimia Jessenia, kwa sauti tulivu, “upo wapi Seni, unajuwa baba anakutafuta sana” aliuliza Ussi kwa sauti ya ukali……….…. ENDELEA..




KIFO CHA HAWARA (mkono wa jini)
SEHEMU YA SABINI NA NANE
MTUNZI: Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA SABINI NA SABA: Na wakati huo huo tukasikia simu ya Jessenia inaita, nae akaitoa mara moja na kuitazama jina la mpigaji, nikamuona anashtuka, “Ussi huyo ananipigia simu” alisema Jessenia kwa sauti iliyojaa uoga, huku ananionyesha kioo cha simu, nikaona jina kaka Ussi, “pokea msikilize anasemaje, usimuonyeshe hasira” nilimuambia Jessenia, ambae alitumia sekunde tatu, kuweka sawa sauti yake, kisha akaipokea simu ile, na kuweka loud speeker, “asalam alaykum” alisalimia Jessenia, kwa sauti tulivu, “upo wapi Seni, unajuwa baba anakutafuta sana” aliuliza Ussi kwa sauti ya ukali……….…. ENDELEA..
iliyoashiria ugomvi, “mbona nimetoka nyumbani sasa hivi, dada kaniambia baba ameenda kumsikiliza Rais” alisema Jessenia kwa sauti tulivu sana, “kwahiyo kama hayupo na wewe ndiyo unatoka” aliuliza Ussi, wakati huo nilikuwa nimepunguza mwendo kidogo.

Ukweli swali hilo lilimshinda Jessenia, ambae alikaa kimya huku akinitazama kwa macho ambayo ni kama alikuwa ananiuliza ajibu nini, na mimi licha ya kulitambua hilo, lakini sikumueleza chochote, “si naongea na wewe Seni, haya sasa upo wapi?” aliuliza Ussi kwa sauti ya ukali zaidi, niwazi hakujuwa kama tayari Jessenia alishamtambua jana usiku wakati anajaribu kumshambulia kwa panga, na pia ameshagundua mipango yao, yaani yeye na baba yake mzee Juma Mohamed, “nipo chake kuna kitu nataka kununua” alisema Jessenia kwa sauti kama ya kulalamika, lakini iliyojaa nidhamu, “sikia Seni, usidanganyike kirahisi hivyo, huyo mwanaume unae jivunia ni tapeli tu, hivi navyo kuambia, yupo njiani sijui anaenda bandarini mkoani au anaenda air port, kwahiyo ni wazi kabisa anaondoka zake, baada ya kukutorosha jana usiku na kukusababishia umkosee adab baba” alisema Ussi, na hapo mimi na Jesse tuka tazamana huku tukizuia kicheko, “lakini kaka yeye ndie mwanaume pekee ambae nimeweza kuwanae bila kupata matatizo” alisema Jessenia, kwa sauti kama ya kuomba hivi, lakini ungemtazama uso wake kwa muda huo, ungejuwa fika anajizuia kucheka, “achana na hizo hisia, huo ni uchawi wa Mangeu tu, hebu rudi nyumba sasa hivi baba akija akukute” alisema Ussi, kama vile anatoa amri, “sawa narudi sasa hivi” alisema Jessenia, nakukata simu, halafu tukacheka kwa pamoja.

Naam mpak hapo, tayari nilikuwa nimesha gundua kuwa Ussi na wenzake hawakujuwa mimi nipo wapi, hivyo niliendesha gari kwa uhuru na kujiachia, tukienda kutokea Wawi nyumba za kijiji na kuibukia garage, tukaikamata macho mane na kushika uelekeo wa wete, nikijuwa kuwa wakina Ussi hawakuwa wanatufuata.
Njiani tuliongea na kupanga mambo mengi ya kufanya baada ya kumaliza swala lile lililopo mbele yetu, “mimi sikai tena huku, tunaondoka wote kwenda Dar, halafu babu Mangeu amesema amesha nijengea nyumba kule dar” alisema Jessenia, kwa sauti ya kudeka, huku wasi wasi ukiwa umesha ondoka moyoni mwake, “hivi Jesse unadhani ninaweza kuondoka Pemba bila wewe?” nilimuuliza Jessenia kwa sauti flani tulivu ya kubembeleza na kumliwaza iliyojaa mahaba, kiasi cha kumfanya atabasamu “sasa ole wako nikute videmu vyako vya zamani vinakusogelea” alisema Jessenia, huku akimalzia kwa kicheko cha utani.*******

Tulitumia lisaa limoja kufika Mantariff Logde, ambapo tulipokelewa kama jana na kuonyeshwa chumba chetu, ambacho kilikuwa ni kile kile cha jana cha sultan, ambacho mchana huu kilikuwa kinaangazia vyema sana nje, japo hatukuweza kuona vyema pwani ya tanga na mombasa, zaidi ya taswila flani ya giza giza iliyo onyesha milima.

Naam wakati huo, niliutumia pia kuchunguza ile Hard disc, ambayo Jessenia alisema kuwa aliikuta kwenye drow ya kitanda cha Ussi, nikaifungua lapto ya Ussi na kuipachika bahati nzuri ilifanikiwa kusoma maana tayari ilikuwa na window seven, nilifungua file kadhaa, mpaka nilipolipata lililoandikwa security camera, nikafungua na kukuta video kadhaa, zote zikiwa zimeandika serity camera, zikitofautishwa na tarehe hivyo nikatazama ile ambayo ilikuwa ya tarehe ya mwisho kabisa.

Wote wawili tukiwa tuna itazama ile video, ambayo ilikuwa inachukuwa vipande vitano vya nyumba ile, ikiwa ni upande nne za nyumba ile na eneo la sebuleni, yani upande wa ndani, nilichagua kwanza video ya nje ambayo niliianzisha pale ambapo walionekana Jessenia na Vuai wakiingia na vesper pale nyumbani, na kushuka kisha kuingia ndani, Jessenia akiwa ameziba uso kwa niqab, dakika chache baadae anaonekana mtu mwingine anakuja na vesper, namtambua kuwa ni Ussi, ambae alitoka kuniacha wawi muda mfupi kabla, sikuwa nimesahau alivyovaa na kile kijifuko mkononi.

Ussi anachuka haraka na kuchukuwa kitu mfano wa fimbo fupi sana kwenye mfuko ule, na kisha anatoa kichupa flani na kitu ambacho mwanzo hatukuweza kukiona vizuri, ila baada ya kuisimaisha (pause) ile video na kuizoom (kuikuza) tukaona akiwa ameshika kitu kama sindano ndogo sana, yenye ncha kali sana, akitia kwenye kijichupa na kukiweka ndani ya ile fimbo yenye uwazi ndani yake mfano wa filimbi, halafu akagonga mlango.

viedo inaonyesha, sekunde chache mlango unafunguliwa na pasipo kuonekana mtu yoyote, aliefungua mlango, Ussi anasogeza ile filimbi mdomoni na kupuliza, tukiwa tumeizoom, tunaweza kumuona Ussi akipuliza ile filimbi, na kile kisindano kinatoka kuelekea mlangoni kisha haraka sana Ussi anarudi kwenye Piki piki yake na kuondoka kwa speed kali sana, “kumbe kweli Ussi anahusika na mauwaji haya” alisema Jessenia kwa sauti ya mshangao na kuto kuamini.

Dakika moja baadae video inaonyesha Jessenia nae akitoka pale mlangoni huku amevaa kama alivyokuja na kutokomea upande ule ule waliotokea, “ni mchezo wa muda mrefu sana waliucheza mjomba wako na Ussi” na lengo lao lilikuwa ni kukuaminisha kuwa kuna jini halitaki uolewe ” nilimueleza Jessenia ambae alikuwa anaifuatilia kwa umakini sana ile video.

Ili kumuona mtu ambae alifungua mlango, tuna fungua video ya camera ya sebuleni, ambayo ukiachilia kuwaonyesha wawili hawa waliyokuwa wanaingia ndani na kupotela kwenye koridoni, pia dakika chache akaonekana Vuai akiwa anarudi huku amevalia bukta na tumbo wazi anaufuata mlango, kisha anaufungua na sasa anaonekana Ussi akiwa anaweka filimbi mdomoni huku Vuai akionekana kushangaa na kupiga hatua moja nyuma, lakini anachelewa kitu mfano wa sindao kina mkuta kwenye shavu lake la kushoto, anaonekana katika maumivu makali, Ussi anatoweka kwenye usawa wa camera, huku Vuai akionekana kuyumba mara kadhaa kabla ya kuanguka chini.

Dakika moja baadae anaonekana Jessenia ambae alikuwa bado katika vazi lake alilokuja nalo, baibui na hijab na uso amejiziba niqab, anamtazama Vuai kwa uoga kisha anatoka nje na kutokomea zake, hapo zinapita dakika kama sita hivi, anaonekana kijana Mahamud, ambae mwanzo alitoka mara tu walipoingia wakina Vuai, “kwahiyo wao lengo lao kubwa ni nini?” aliuliza Jessenia, ambae alionyesha mwenye hasira na chuki na wakina Ussi, “hilo ndilo ambalo tuna taka kulijuwa kabla hatuja watia mbaroni, na ili kufanikisha jambo hili jioni ya leo tunatakiwa kurudi chake” nilimueleza Jessenia, japo sikuwa na mpango wowote nilio uweka kwaajili ya kupata chanzo kamili yenye ushahidi, ila kichwani mwangu nilishahisi kuwa mali na utajiri wa Jessenia ndio chanzo halisi. “mh! kwani kuna sababu yoyote ya kutafuta ushahidi mwingine, wakati tayari tuna ushahidi?” aliuliza Jessenia, na wakati huo huo simu yangu ikaanza kuita.

Nilipoitazama niliona kuwa mpigaji alikuwa ni insp Aroub, nikaipokea, “asalam aleykum mzee” nilimsalimia insp Aroub, ambae alionekana kuwa katika sehemu iliyo changamka, “walaykum salam mwalimu, upo wapi sasa?” aliiuliza insp Aroub ambae kiukweli sikuhitaji kumueleza nilipo maana isingekuwa vyema kutaja maficho yangu ya pekee, “nipo njiani natokea mkoani, kuna mtu nilimpeleka huko” nilimdanganya insp Aroub, sisi tupo barabara mpya, rais anaweka jiwe la msingi, ili tuweze kumpeleka air port, hapo ndipo nitahitaji kukutana na wewe kabla ya mpango mwingine wowote” alisema insp Aroub, “usijari insp, we tulia mpaka jionitutakapo kutana, nakuhakikishia hili limeisha” nilimueleza insp.

Hapo nikasikia mguno hafifu toka kwa insp, “mh! Eric, unamaanisha nini, kwamba tunaenda kumpata muuwaji na ushahidi?” aliuliza insp kwa sauti iliyojaa mashaka kiasi, “kama tutaweka mipango vizuri” nilimjibu insp Aroub, nikidhania kuwa hilo ndilo swali la mwisho, lakini haikuwa hivyo, “nidokeze kidogo, kama tunahitaji maandalizi” alisema insp Aroub na hapo alibamba kidogo, maana ni kweli tulihitaji mandalizi ya mapema, “kwanza usiri, muda wote wa zoezi, wepesi wa kitendo na kuzingatia muda na maelekezo, uvumilivu wa kusubiri, mwisho ni matumizi sahihi ya nguvu, maana watuhumiwa hawana silaha za moto” nilifunguka kwa insp Aroub, ambae nilimsikia akiachia kicheko cha fadhaa, “hivi kijana unaweza kunieleza kazi yako halisi, kama ni CID (Criminal Investigation Department), CIA (Central Intelligence Agent, MS (Millitary spay) TSA (Tanzania Secret Agent) au nani haswaa?” aliniuliza insp Aroub, na kabla sijajibu swali hilo toka kwa insp, akanibandika jingine, “hii Eric, inawezekanaje ndani ya muda huu mfupi tumalize hii kazi, wakati mimi nimehangaika nayo mwaka wa saba sasa” hapo nikaona saa nimelivuruga kabla sijamaliza kazi………….…. ENDELEA..


KIFO CHA HAWARA (mkono wa jini)
SEHEMU YA SABINI NA TISA
MTUNZI: Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA SABINI NA NANE: “kwanza usiri, muda wote wa zoezi, wepesi wa kitendo na kuzingatia muda na maelekezo, uvumilivu wa kusubiri, mwisho ni matumizi sahihi ya nguvu, maana watuhumiwa hawana silaha za moto” nilifunguka kwa insp Aroub, ambae nilimsikia akiachia kicheko cha fadhaa, “hivi kijana unaweza kunieleza kazi yako halisi, kama ni CID (Criminal Investigation Department), CIA (Central Intelligence Agent, MS (Millitary spay) TSA (Tanzania Secret Agent) au nani haswaa?” aliniuliza insp Aroub, na kabla sijajibu swali hilo toka kwa insp, akanibandika jingine, “hii Eric, inawezekanaje ndani ya muda huu mfupi tumalize hii kazi, wakati mimi nimehangaika nayo mwaka wa saba sasa” hapo nikaona saa nimelivuruga kabla sijamaliza kazi…………….…. ENDELEA..

Ni vyema kama nikimtafutia jibu ambalo linaweza kumtuliza insp Aroub, lakini wakati natafuta jibu, nikamsikia anacheka, “hakika we kijana ni hatari sana, kazi ya ualimu haikufai kabisa, bora ungesomea upelelezi, yaani utadhani FBI au KGB” alisema mzee Aroub akinimwagia sifa, tatizo upelelezi una mambo mengi, lazima ujuwe kupambana na kutumia silaha” nilisema hivyo kuunga mkono utani wake.
Hapo tukaagana na kukubaliana tuwasiliane jioni ili kupeana mipango ya kukamilisha swala hili la kiuchunguzi, na mimi nilicopy zile video na kuziweka kwenye flash disc, ambayo nilitoka nayo japan, sidhani kama mwaka ule wa 2005 zilikuwa zimefika Tanzania, maana hata huko japan zilikuwa zinauzwa kwa fedha nyingi kidogo, ukubwa wa mwisho kabisa ulikuwa ni GB 4, kama hii niliyokuwa nayo mimi, nilitunza video kwenye laptop yangu na nyingine nikaiacha kwenye flash.******

Naam mchana ule tuliutumia kwa kula na kulala ili kufidia usingizi wa jana usiku, japo sijui miili yetu ina nini, maana ile kugusana tu wakati wakutafuta usingizi, tukajikuta viungoyetu vikiingiliana na kupeana walicho kusudia kupeana, sikuweza kuzuwia, japo ilikuwa ni mara mbili, lakini ilifurahisha sana, moja ilikuwa wakati tuna taka kulala, naya pili ilikuwa baada ya kuamka na kuingia kwenda kuoga, yaani tulikiamsha tukiwa bafuni, hawamuzote mbili Jessenia ndie alikuwa mchokozi, japo sikatai kuwa nilikuwa katika matamanio, lakini yeye ndie alienichokoza kwa kuonyesha dalili za wazi za kuhitaji dudu.

Mpaka saa nane mchana tayari tulikuwa tumesha oga tumesha kula, tulikuwa tuna pumzika kuvuta muda wa kurudi chake chake, lakini tayari chumba chetu tunge kikuta, maana kilisha lipiwa, ndio mida ambayo Jessenia alisikia simu yake inaita, alipoichukuwa na kuitazama nikamuona anashtuka na kunitazama usoni, “mjomba huyo” alisema Jessenia kwa sauti iliyojaa wasi wasi, hapo kwa haraka haraka nikajiuliza kuhusu maswali ambayo au maongezi ya mzee Juma Mohamed yatalenga nini, kwanza lazima yupo wapi ingekuwepo, pili lazima atakuwa amesha fika nyumbani na ameulizwa juu ya uondokaji wake nyumbani, “ulipoondoka nyumbani kuna mtu alikuona?” nilimuuliza Jessenia, ambae aliitikia kwa kichwa, akikubali kuwa kuna mtu alimuona,

“nani?” nilimuuliza Jessenia, “alikuwepo dada wa kazi” alisema Jessenia, huku simu yake bado inaendelea kuita, “ok! akikuuliza upo wapi mwambie upo mkoani” nilimuambia Jessenia, ambae aliitikia kwa kichwa na kuipokea simu, na kuweka loud speeker, “asalam aleykum” alisalimia Jessenia kwa sauti tulivu iliyojaa nidham, “Seni unashani unafanya nini, hivi kweli wewe ndie wakukimbia nyumbani, bora ungebeba nguo zako tu, sasa umeiba mpaka computer ya kaka yako, ndivyo alivyokutuma huyo kijana toka bara?” hapo Jessenia akanitazama kwa macho ya kuniuliza kama nimesikia kinacho ongelewa, “haya niambie upo wapi?” aliuliza mzee Juma Mohamed, “nipo mkoani” alijibu Jessenia kwa sauti tulivu yenye nidhamu,

“kwahiyo unataka kutoroka kwenda bara sivyo?” aliuliza mzee Juma, yani mjomba wake Jessenia, na kabla Jessenia hajajibu kitu, tukamsikia tena mjomba wake, “sasa nakuambia urudi sasa hivi, ukichelewa tu natoa taarifa polisi ukamatwe wewe na huyo mjinga mwenzio na ukijaribu kupanda boti utakamatiwa unguja, na kuhakikishia utakaa kituoni mpaka ushike adabu” aliongea mjomba kwa sauti ya ukali na kukata simu, “tutafanyaje Eric?” aliuliza Jessenia, kwa sauti iliyojaa uoga, “kwanini una wasi wasi Jesse, ushahidi wote tunao mkononi” nilimuambia Jessenia, huku natoa simu yangu na kumpigia mzee Mangeu.

Ukweli licha ya kuchelewa kupokea ile simu yake, lakini baadae akaipokea, “asalam aleykum mzee” nilimsalimia mzee Mangeu, “waleykum salama kijana, nilikuwa nimejilaza hapa na kausingizi kalikuwa kana ninyemelea, vipi kuna lolote?” aliuliza mzee Mangeu, ambae kiukweli sauti yake ilikuwa inaonyesha wazi kuwa katika uchovu flani wa usingizi, “lolote lipo tayari tuna ushahidi wa kutosha kabisa juu ya Ussi kuhusika na kifo cha Vuai, kilichobakia ni kuhakikisha tuna maliza kazi na kuwa kamatisha hao watu” nilimueleza mzee Mangeu, ambae nilimsikia akicheka kivivu, “we kijana hatari sana, boss wako hakukosea kukutuma” alisema mzee Mangeu.

ambae pia aliendelea kusema kuwa, toka tulipoachana nae mida ile, alienda nyumbani kwake ambako alitulia nje ya nyumba na kufuatilia mienendo ya nyumbani kwa kina Jessenia, baada ya kama dakika kumi na tano, akaliona gari walilokuwa nalo wakina Ussi likiingia pale nyumbani na kuingia ndani ya gate, na haikupita muda mrefu akatoka mmoja kati ya wale vijana na kusogea mpaka usawa wa nyumba yake akiwa barabaran, akatazama na kujifanya anapita njia kisha akarudi na kuingia ndani.

Kitu kama hicho kikatokea tena dakika ishirini baadae, na baada ya hapo ikawa kimya kabla mangeu hajashtuka na kutazama ghorofani, ambako aliweza kumuona Ussi akichungulia dirishani mara kwa mara mpaka yeye alipoamua kuingia kibandani kwake kujipumzisha, “kwahiyo hujamuona mzee Juma hapo kwake?” nilimuuliza mzee Mangeu, “ukweli sijajuwa kama amesha rudi” alijibu mzee Mangeu na mimi nikamueleza mzee Mangeu, maongezi ya Jessenia na huyo mjomba wake wa bandia jinsi yalivyokuwa, “kwa hiyo mzee kuwa tayari kukutana na mzee Juma mchana huu, jifanye unamuulizia Jesse, na kwamba toka jana hujamuona kabisa” jitahidi subiri nije nikuletee kinasa sauti ili tuweze kusikia kila kitu atakacho kiongea” nilimueleza Mzee Mangeu kabla hatujakata simu.*****

Saa tisa ndio mida ambayo tulitoka Panga la mtoro, kaskazini Pemba kwenye hotel kubwa ya hadhi ya juu sana ya Mantariff, tukielekea chake chake nikiwa nimevalia nguo za michezo, yaani truck tishirt na raba, njiani tulikuwa tukiongea kwa furaha, huku Jessenia akiuliza maswali mengi kuhusu dar watu wake na maisha kwa ujumla, na mimi nilimueleza huku nikipamba kweli kweli, kitu ambacho kilimpa chachu na tamaa ya kufika dar es salaam.

Saa kumi na robo ilitukutia mitaa ya gombani, ndipo nilipoiona simu yangu ikiwa inaita, nilipoitazama alikuwa ni insp Aroub, nikajuwa amesha pata habari mpya, nikaipokea mara moja, “ndiyo mzee kuna jipya” nilimuuliza mzee Aroub, huku napunguza mwendo ili niweze kuongea nae vizuri, “jipya lipo bwana mwandishi, unatakiwa kujisalimisha kituo cha polisi ukiwa na Jessenia, na vitu ulivyoiba nyumbani kwa mzee Juma Mohamed” alisema mzee Aroub kwa sauti ya ukali tofauti na nilivyo mzowea.
Kwanza nika tabasamu, kwa kuona tayari kazi imefika patamu, “mzee….” kabla sijasema lolote, tayari mzee Mohamed akanidaka, “sikia kijana hakuna porojo zaidi, sasa ni mwisho wa kuniteka akili, umenifanya mjinga kwa muda mrefu sana, mara moja acha mpango wako wakutoroka na uje haraka kituoni, maana hautoweza kushuka toka kwenye bot bandari yoyote kabla hujatiwa mbaroni” alisema insp Aroub kwa sauti ile ile ya ukali, hapo nikasimamisha gari kabisa mita chache toka uwanja wa mpira wa gombani.

Niliwaza kwa haraka ni muambie nini mzee Aroub ili tulie maana ni wazi kuwa mzee Juma, ameshaenda kituoni kutoa taarifa kama alivyo sema, na baada ya kupata jibu nikaongea kwa sauti tulivu kabisa, “mzee sina cha kukimbia, nipo pemba, tena hapa hapa chake chake…” lakini kabla sijamaliza kuongea, insp Aroub akanidaka tena, “sikia kijana sina muda wakukusikiliza cha msingi njoo kituoni madungu, wewe ni mtuhumiwa wa wizi nyumbani kwa mzee Juma Mohamed, dakika kumi kama hujafika nita kusaka mimi mwenyewe” alisema mzee Aroub, na kukata simu.

Nikashusha pumzi na kumtazama Jessenia, ambae alikuwa anitazama kwa macho ya kujiuliza nilikuwa naongea nini, mana sikuweka loud speeker, “nani huyo?” aliuliza Jessenia, “insp Aroub, mjomba wako amesha toa taarifa kituoni” nilimjibu Jessenia, huku nikiwa nina bofya simu kupiga kwa insp Aroub, ambae aliipokea mara moja, “unasemaje kijana, unadhani tuna jambo la kuongelea kwenye simu zaidi ya kuja kujisalimisha kituoni?” aliuliza insp Aroub kwa ukali, “tunalo la kuongea mzee, ni vyema kama ungenipa na….” mzee Aroub hakunipa nafasi, “kijana mpaka sasa sina uwezo wakukusikiliza tayari kesi ipo mezani, na unatakiwa kukamatwa sasa hivi, huwezi tena kuni laghai jisalimishe kabla hatuja poteza muda wetu kukusaka” alisema insp Aroub na kukata simu. ………….…. ENDELEA

KIFO CHA HAWARA (mkono wa jini)
SEHEMU YA THEMANINI
MTUNZI: Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA SABINI NA TISA: “unasemaje kijana, unadhani tuna jambo la kuongelea kwenye simu zaidi ya kuja kujisalimisha kituoni?” aliuliza insp Aroub kwa ukali, “tunalo la kuongea mzee, ni vyema kama ungenipa na….” mzee Aroub hakunipa nafasi, “kijana mpaka sasa sina uwezo wakukusikiliza tayari kesi ipo mezani, na unatakiwa kukamatwa sasa hivi, huwezi tena kuni laghai jisalimishe kabla hatuja poteza muda wetu kukusaka” alisema insp Aroub na kukata simu ………….…. ENDELEA
Ukweli nilishangazwa na msimamo wa Aroub, ambae licha ya kumpa nafasi ya kutambua ukweli juu ya vifo vya watu ambao walisadikiwa kuwa walikuwa wanauwawa na jini, lakini leo anakuwa na msimamo mgumu kama huu, na kutaka nijisalimishe kituoni pasipo kukutana nae na kuzungumzia swala hili, na kwavyo vyote hakuna hata mmoja wetu ambae angetoka salama kule kituo, lazima wote tunge dungwa sumu kwa njia yoyote na Ussi, “hataki kukusikiliza?” aliuliza Jessenia ambae wasi wasi wake nilikuwa nauona wazi wazi usoni pake, “nashangaa kwanini anakuwa hivi, au mjomba wako amempatia kitu kidogo, sasa ngoja niongee nae kwa lugha inayompata” nilisema hivyo huku na piga tena namba yake, safari hii hakupokea kabisa, nikapiga tena hakupokea, nikaiweka simu pembeni na kuondoa gari kuelekea macho manne, kichwani mwangu nikiwa nimesha ghairi kwenda chake mazoezini, baada yake nilipanga kwenda kujichimbia pwani ya mashariki kwenye fukwe tengefu ya makaani.

Lakini kabla sijafika macho manne, naona simu inaita, nikaitazama nae alikuwa ni afisa utawala wa Ali Khamis Camp, nikaipokea mara moja, huku naendesha gari, “ndiyo kaka niambie” nilisema hivyo mara baada ya kuweka simu sikioni, “ticha upo wapi, kuna taarifa nimezipata hapa toka kituo cha polisi kuwa unatafutwa kwa kosa la kumtumia Jessenia kuiba kwa mjomba wake, na sasa mupo bandarini munataka kutorokea dar” alisema bwana Malambo, hapo niakacheka kidogo, “kaka mbona nipo macho mane hapa na kuja huko wawi” nilijibu katika hali ya kawaida kabisa, na yeye akacheka kidogo, “sasa hizi habari zinatoka wapi, au Ussi ameanza mambo yake ya kuleta wivu?’ aliuliza Malambo, wakati huo nilikuwa naingia macho manne na kuifikia kona ya kuingia wawi, ambayo ipo upande wa kushoto kama unatokea wete, “nitakueleza vizuri, ila sasa nahitaji kinga ya kukamatwa, maana kila kitu kitavurugika” nilimueleza malambo, ambae mpaka muda huo hakuwa anafahamu kazi yangu halisi, huku nakata kona kushoto kuingia barabara ya kuelekea wawi.

“ok! usijari nipo na afande hapa, wacha niongee nae kisha ukija tutajuwa cha kufanya” alisema Malambo na kukata simu, na mimi nikaona sasa mambo yanazidi kuwa mazito, na ukweli nikwamba Aroub alikuwa muhimu sana kwenye hii kazi, maana yeye ndie alikuwa ameifuatilia kwa miaka mingi japo hakufanikiwa, nikaamua kumpigia tena na habati nzuri safari hii aliipokea, “nataka kusikia kuwa upo njiani unakuja kituoni we kijana” ilikuwa ni sauti ya ukali toka kwa insp Aroub, “insp tayari unaingia kwenye orodha ya washukiwa wa hii kesi, na bahati mbaya kwako, hii kesi itakuchafua sana” niliongea hivyo kwa sauti tulivu, lakini yenye amri na kuogofya, hii ni moja silaha bora sana kumtuliza mtu, “unasema…. kivipi yaani…mbona sikuelewi” alibabaika insp Aroub, huku sauti yake ikionekana kujawa na mshangao.

Hapo nikaona tayari nimesha mshika kinacho fuata ni kuzidi kumkalisha chini, “unadhani kuna mjinga ambae anashindwa kuelezwa unacho kifanya, umezuga kwa miaka saba ukichunguza kesi hii na kudanganya serikali kuwa muuwaji ni jini, na sasa ukweli unakaribia kupatikana wewe unataka kunikamata na kunifunga ili kuvuruga uchunguzi” nilisema hivyo kwa sauti ile ile yenye utulivu wa kibabe, “ticha unataka kusema nini, hao wauwaji ni wakina nani?” aliuliza mzee Aroub kwa sauti iliyopoa, “mzee kama umeweza kushawishika kirahisi hivyo na kunigeuka, sidhani kama ninapaswa kukuamini tena” nilimueleza mzee Aroub, ni kama nilimchanganya hivi.

Wakati huo nilikuwa naingia wawi messi, ambapo palikuwa na watu wacheche, akiwepo Mwasenga ambae alinionyesha ishara ya kuzungusha gari upande wa kushoto wa jengo la mess, yani kule ambako kuna ukumbi wa chakula na mimi nikafanya hivyo huku simu ipo sikioni, “Eric, unaweza kunieleza wewe ni nani haswa, na unafanya kazi chini ya nani?” aliuliza mzee Aroub, na hapo nikatabasamu kidogo, “mzee umepoteza haki ya kulijuwa hilo, jiandae kusimama kizimbani kujibu tuhuma zitakazo kukabili” nilisema hivyo kisha nikakata simu, kisha nikasimamisha gari na kushuka toka kwenye gari nikiwa na Jessenia, ambae alikuwa amevaa niqab usoni mwake tukaingia ndani simu nikiiacha ndani ya gari.

Mule ndani ya ukumbi wa chakula, tuliwakuta afisa utawala na mkuu wake wa kambi, wakitusubiri, “anaweza kutoa hiyo ninja tafadhari” alisema mkuu wa kambi, mara tu tulipoingia, na bila kuambiwa mara mbili Jessenia akatoa mwenyewe, “shikamoo mzee” nilisalimia huku namtazama mkuu wa kambi, ambae bado alikuwa amevalia sale za kazi kama ilivyokuwa kwa Malambo, huku Jessenia yeye akisalimia “asalam aleykum” huku anamtazama Malambo, “marahaba mwalimu, pole na majukumu” alisema kamanda yule mwenye cheo cha kanali, “asante mzee, lakini naamini karibu namaliza kazi” nilijibu hivyo nikiamini kuwa kwa namna moja au nyingine mzee huyu atakuwa anafununu ya ufahamu juu yangu, hasa kuhusu kazi iliyonileta pemba, “bwana Eric, ukweli nilipo pewa maelekezo na BHQ (Base Head Quarter) hawakunifafanulia juu ya kazi unayokuja kuifanya, ila walinitaka kukupa msaada wowote utakao uhitaji, sasa je naweza kukusikiliza unachohitaji kusaidiwa ili ukamilishe kazi yako, maana tumepokea taarifa ya kwamba umeiba na unatafutwa na polisi, wakikushuku kuwa upo mbioni kutoroka” alisema mkuu wa kambi, mzee mpaka hapa nimesha fikia asilimia tisini na tisa ya kazi, bado asilimia moja tu nayo kukabidhi watuhumiwa mikononi mwa vyombo vya dola, mwanzo nilifikiria jeshi la polisi, lakini sasa nao wametia mashaka” nilimueleza mkuu wakambi, huku nikimfafanulia kilicho tokea na kazi ninayoifanya.

“ok! sisi tutakupa ulinzi mda ambao utauhitaji, tunandaa askari kwaajili hiyo, maana tayari nilisha pewa kibali cha kufanya hivyo toka siku nilipopokea ujumbe wa ujio wako” alisema mkuu wa kambi, ambae alitoa maelekezo kwa afisa utawaka, kwamba awaandae askari kumi na tano, na gari moja kwaajili ya kutoa msaada nyuma yangu pale nitakapo uhitaji.

Na hapo hapo akapiga simu kwa RPC wa chake chake na kumueleza kuwa swala langu amuachie yeye, kwasababu yupo chini ya jeshi la ulinzi, na atakamatwa na jeshi la ulinzi na kupelekwa kwao polisi kama itatakiwa kufanyika hivyo, na RPC akasema kuwa atajulisha mtu aliepewa jukumu hilo, ambae ni insp Aroub, baada ya hapo nikawaaga na kuwaeleza kuwa nitawapigia baade, na kuondoka zangu nikiwaacha wanapanga mipango ya kuniwekea ulinzi.

Naam ile naingia kwenye gari nakuta simu inaita, na juu ya kioo hicho ikionekana alama ya kwamba kulikuwa na miseed call kumi na saba, na mpigaji alikuwa ni insp Aroub, nikaipokea na kuiweka sikioni, “hallow Eric, nahitaji kuonana na wewe” alisikika insp Aroub akiongea mfululizo kama amemeza CD, huku sauti yake ikiwa ya kuomboleza, “mzee unadhani unastahili kuminiwa tena, ni vipi kama una jaribu kuniweka hadharani ili maadui zangu wanipate kirahisi” nilimuuliza insp Aroub kwa sauti tulivu lakini ya kibabe, “ticha nadhani unanifahamu vyema, tumeanza vizuri tu hii kazi naomba tuimalize vizuri, unajuwa fika kuwa sihusiki, labda nimekosea kumsiliza mzee juma” alisema Aroub hakika sauti yake ilitia huruma.…. ITAENDELEA..
 
Mkula angemaliza tu tumbless ama hana mpango wa kuleta tena story apa, ujue alikuwaga na mavyeo plus manyota kama yote kutoka kwa maraia,for the very first tym jf nlituma muamala maali ili kusupport kitu ni story Za uyu mwamba, alikuwaga unique but now
Shukran mkuu kwa kutuma muamala acha tuendelee
 
KIFO CHA HAWARA (mkono wa jini)
SEHEMU YA THEMANINI NA MOJA
MTUNZI: Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA THEMANINI: “mzee unadhani unastahili kuminiwa tena, ni vipi kama una jaribu kuniweka hadharani ili maadui zangu wanipate kirahisi” nilimuuliza insp Aroub, kwasauti tulivu, lakini yakibabe, “ticha nadhani unanifahamu vyema, tumeanza vizuri tu hii kazi naomba tuimalize vizuri, unajuwa fika kuwa sihusiki, labda nimekosea kumsiliza mzee juma” alisema Aroub hakika sauti yake ilitia huruma.…. ENDELEA..

Mpaka hapo sikuona sababu ya kuendelea kumchimba sana, ila kiukweli sikutaka kumuamini tena, “ok! upo wapi sasa hivi?” nilimuliza insp Aroub, nae akaniambia kuwa yupo kituoni pale madungu, “ok! tulia hapo hapo kituoni, nitakupigia baada ya dakika kumi kukuambia tukutane wapi, na uje vipi” nilimuambia hivyo kisha nikashuka nakurudi ndani kuonana na Malambo ambae nilimuomba aniazime gari lake, yeye alikuwa na Toyota pinic, akanipatia funguo nikafunga gari letu, kisha mimi na Jessenia tukandoka zetu na gari la Malambo.

Tulikamata barabara ya macho manne huku nikimpigia mzee Mangeu na kumtaka awe macho kuwatazama wakina Ussi kama watatoka hapo nyumbani kwao, “hawa jamaa wapo hapa nyumbani kwao, tena mzee Juma ameingia muda mfupi uliopita” alisema Mangeu, wakati naongea nae, “ok! wameshaenda polisi kunitolea taarifa ya kwamba nimemtorosha Jesse, na nimewaibia pia, sasa kuwa makini kuwa fuatilia, naenda kukutana na insp Aroub” nilimueleza mzee Zidadu.

Wakati huo, tulikuwa tumesha fika njia panda ya macho manne, na kukata kona kushoto kuelekea upande wa chake, “sawa lakini kuweni makini” alisema mzee Mangeu, kisha nikakata simu na kumpigia insp Aroub, ambae aliipokea simu haraka sana, tofauti na wakati ule ananiletea ujivuni, “ndiyo mwalimu nakusikiliza tukutane wapi?” aliuliza Insp Aroub, kwa sauti ya chini kidogo, “upo wapi sasa hivi” nilimuuliza kwa sauti tulivu, “nipo hapa kituoni Madungu” alijibu insp, “ndani au nje?” nilimuuliza tena kwa sauti ile ile, “nipo nje upande wa juu” alijibu insp wakati huo na sisi ndio tulikuwa tumesha ingia chake na kukatiza moja kwa moja kuelekea madungu, ambapo ni kama kilomita mbili tu, “ok! sogea barabarani, usawa wa maegesho ya magari na usikate simu” nilimuambia insp Aroub, huku namtazama Jessenia ambae nilimuonyesha ishara ya kwamba ahamie seat ya nyuma, kisha atulie kimya kabisa, nae akafanya hivyo kwa kulaza seat kisha akapita na kuiweka sawa ile seat, sawa kijana, nilimsikia insp Aroub akisema.

Dakika moja mbele, tayari nilikuwa naibuka madungu polisi station, ambapo tulimuona insp Aroub akiwa anasogea barabarani, simu sikioni, huku anatazama upande wa kutokea chake, nadhani kusudio lake ni kutazama gari aina ya Toyota spacio la rangi ya blue, na mimi nikapunguza mwendo ili kumkadiria hatua zake tufike pamoja kwenye point.

Naam ile anafika tu na sisi tunasimamisha gari, “ingia ndani ya gari mbele yako” nilimuambia insp Aroub, kisha nikakata simu, kumbuka kipindi hicho hakukuwa na kitu kinachoitwa bando, vocha ilikuwa inaenda kama vocha.

Insp akafungua mlango wa mbele wa gari, upande wa abiria na kuingia ndani kisha nikaanza kuendesha gari taratibu kuelekea upande wa mkoani, “aslam aleykum mzee” nilimsalimia kwa mara nyingine, “waaleykum salaam” aliitikia Aroub lakini sauti yake niliona wazi ikinichukulia kama mtu tofauti kama ilivyokuwa mwanzo, “naomba uwe free mzee, chukulia kama mwanzo, ilituweze kuongea vizuri na kukamilisha mipangao yetu” nilimueleza mzee Aroub, baada ya kuona kuwa alikuwa mwenye wasi wasi mwingi sana, “sawa mwalimu, hakuna kitakacho haribika” alijibu mzee Aroub akijaribu kujichangamsha.

Naam tulipofika maeneo ya Madungu mtaani, nikagaeuza gari na kugeuza tuliko toka, “mzee najuwa umekutana na mzee Juma, vipi unaweza kunipa maelezo yake kwa kina?” nilimuuliza insp Aroub, ambae alianza kunieleza mwanzo mpaka mwisho.

Ilikuwa hivi, baada ya kutoka airport kumsindikiza rais na wageni wengine alio ambatana nao, insp Aroub alienda moja kwa moja nyumbani kwake, akiwa na lengo la kubadili nguo ili ajiandae kukutana na mimi ndipo aende kwa mzee Juma Mohamed.
Lakini kabla haja badili nguo akasikia simu yake inaita, hivyo akaipokea na kukutana na taarifa ya kuwa anahitajika haraka kituoni, kuna jambo la kushugurikia, nae akakimbilia kituon mara moja, ambako alikutana na mze Juma Mohamed, aliemueleza kuwa amekuja kutoa taarifa mbili, moja ya wizi uliotokea nyumbani kwake, baada ya kijana wake kuibiwa computer yake ya mpakato, yaani lap top, na taarifa ya pili ni ile ya kutoweka kwa binti yake Jessenia, “na mshukiwa wa matukio yote mawili ni wewe” alieleza insp Aroub, pasipo kujuwa kuwa Jessenia alikuwa seat ya nyuma yake.

insp Aroub akasema kuwa, mzee Juma akaeleza kuwa mimi nimekuwa na tabia ya kutembelea sana nyumbani kwake nyakati za usiku, na pia nimekuwa na tabia ya kumtorosha Jessenia nyakati za mchana na kwenda kufanyanae ufuska kule Green Mess, “ukweli nilipata picha tofauti kabisa na kukushuku vibaya sana, kuwa umenitumia kumfuatilia mzee Juma kwa mambo yako binafsi, huku ukitumia mgongo wa uchunguzi wa matukio ya mauwaji, yanayoendelea” alisema mzee Aroub, ambae pia akaniambia kuwa muda mfupi uliopita amepokea taarifa toka ngazi za juu, kuachana na kunikamata mimi na kwamba swala hilo litashugulikiwa na jeshi la ulinzi.

Baada ya kumaliza kunieleza mzee Aroub, na mimi nikaanza kumueleza ukweli halisi, huku tukiwa tumemaliza eneo la chake chake na kwenda kusimama njia panda ya machomane, uelekeo wa wawi, “sikia mzee ni kweli mimi nipo na Jesse, huyo hapo nyuma yako” nilimueleza mzee Aroub kwa sauti tulivu na yeye akageuka kutazama seat ya nyuma, akamuona Jessenia akiwa anamtazama, “asalam aleykum” alisalimia Jessenia, huku uso wake ukiwa katika tabasamu, mzee Aroub akatoa macho kwa mshangao, “waleykum salaam” aliitikia na kunitazama mimi, “ni kweli pia nina laptop ya Ussi, pia kuna kitu kingine ambacho hajuwi kama tayari nimekichukuwa toka kwake, ni kitunza kumbukumbu cha computer, ambacho kiliibiwa nyumbani kwa Vuai jioni ya siku aliyo uwawa” hapo ni kama nilizidi kumchanganya mzee huyu.

ambae miaka mingi amekuwa akiifwatilia hii kesi pasipo kuambulia kitu, “kwa kifupi Ussi ndie muuwaji halisi, ambae hutumia sumu aina ya synanceia, inayopatikana toka kwenye kiumbe cha baharini, maarufu kama stone fishi, au samaki jiwe, ambao binadamu huamini kuwa jini, maarufu kama chunusi” nilimueleza Aroub nae akazidi kushangaa, “na yule mwanamke anae sadikiwa kuwa ni jini, ambae kila akionekana na mwanume anauwawa ni huyu Jesse, ambae siku zote alikuwa anaamini kuwa amekuwa na bahati mbaya, kila anapopata mwanaume anauwawa katika hatua za mwanzo kabisa za mapenzi yao”

Ukweli Insp Aroub alishikwa na mshangao mkubwa sana, akamtazama tena Jessenia, “hakika alishaenda kwa waganga wengi sana, akijaribu kutolewa jini, ambalo alikuwa anaamini kuwa analo mwili mwake, na ndilo linalo uwa wanaume wake, kitu ambaacho hakikuwa kweli, alikuwa ni Ussi alieshirikiana na wafanyakazi wake wa baharini” nilimueleza mzee Aroub, ambae sasa nikama ndio anapata picha halisi, “labda nikueleze kwa kifupi kilichotokea jana usiku” nilimueleza insp na kumsimulia kila kitu, kilichotokea kuanzia yeye aliponipigia simu kwamba amemuona Ussi anapokea wageni, aliewatilia mashaka, hata mimi nikaanza kufuatilia, hapo sikumtaja mangeu kwa maana sikutaka mambo mengine ya mangeu yafahamike, hasa kuhusu uhalisia wa mzee huyu.

Nikamuelezea kuhusu shambulizi lililotokea usiku, na washambuliaji wakiwa ni wakina Ussi na wageni wake, jinsi Jessenia alivyo nusulika kushambuliwa na mapanga, huku mimi nikifanikiwa kutoroka nae na kwenda kulala ninako kujuwa, (hapo sikumueleza nililala wapi) na wao kwenda kupekuwa chumba changu kule Green house, na hata leo jinsi walivyo nifukuzia bila mafanikio mara baada ya kupewa taarifa na mzee Juma kuwa nipo pale kwenye mkusanyo wa kumsikiliza rais, pia nilimueleza juu ya kifo cha mandevu pale ngerenger nikwamba alikuwa anatufuatilia kwa nia ovu.

“kwanini Ussi afanye hivyo kwa ndugu yake mwenyewe, sababu ni nini hasa?” aliuliza insp Aroub akitilia shaka kile nilicho msimulia, “nadhani hilo ndilo swali lililonifanya nichelewe kuwafikisha Ussi na baba yake kwenye vyombo vya dola, ni muhimu tukilijuwa hilo kwanza, ndipo tumkamate” nilimueleza insp Aroub, ambae pia niliwasha computer yangu, ambayo nilikuwa nayo kwenye gari na kumuonyesha ile video iliyochukuliwa na camera za usalama za yumbani kwa Vuai, siku ya tukio mauwaji yake.

Mpaka anamaliza kutazama zile video mbili, nilimuona mzee Aroub akitoa mguno wa fadhaha, “haya nakusikiliza kijana nini kifanyike, maana hawa washenzi wanatakiwa kukamatwa kabla hawajaondoka kisiwani kurudi unguja” alisema mzee Aroub, na mimi nikaanza kumpa mpango na kitu cha kufanya ili kuweza kukamilisha kazi yetu.

baada ya hapo tuligeuza gari na kuelekea chake chake kumpeleka mzee Aroub, na wakati tunaingia barabara ya chake pale njia panda ya Macho manne, nikapokea simu ya Mangeu, ambae aliniambia kuwa ameliona gari la wakina Ussi linatoka pale nyumbani kwao, kuelekea hii njia ya juu ambayo mimi huwa napenda sana kuitumia, sikuwa na wasi wasi sana juu ya hilo, maana nilikuwa na gari ambalo asinge lifahamu kuwa ninalitumia, hivyo niliagana na Mangeu, nikimsisitiza kuwa makini na wakina Ussi, hasa nyakati hizi za jioni, nakamuahidi kuwa nitafika kwake mapema sana ili kukamilisha mpango wetu.

Wakati nakata simu ndio tulikuwa tunapita karibia ile njia panda, ya kwenda msingini, tukiwa speed kali, hapo ghafla likatokea gari la Ussi mbele yetu, na kuingia barabarani ghafla, .…. ENDELEA..



KIFO CHA HAWARA (mkono wa jini)
SEHEMU YA THEMANINI NA MBILI
MTUNZI: Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA THEMANINI NA MOJA: “haya nakusikiliza kijana nini kifanyike, maana hawa washenzi wanatakiwa kukamatwa kabla hawajaondoka kisiwani kurudi unguja” alisema mzee Aroub, na mimi nikaanza kumpa mpango na kitu cha kufanya ili kuweza kukamilisha kazi yetu.

baada ya hapo tuligeuza gari na kuelekea chake chake kumpeleka mzee Aroub, na wakati tunaingia barabara ya chake pale njia panda ya Macho manne, nikapokea simu ya Mangeu, ambae aliniambia kuwa ameliona gari la wakina Ussi linatoka pale nyumbani kwao, kuelekea hii njia ya juu ambayo mimi huwa napenda sana kuitumia, sikuwa na wasi wasi sana juu ya hilo, maana nilikuwa na gari ambalo asinge lifahamu kuwa ninalitumia, hivyo niliagana na Mangeu, nikimsisitiza kuwa makini na wakina Ussi, hasa nyakati hizi za jioni, nakamuahidi kuwa nitafika kwake mapema sana ili kukamilisha mpango wetu.

Wakati nakata simu ndio tulikuwa tunapita karibia ile njia panda, ya kwenda msingini, tukiwa speed kali, hapo ghafla likatokea gari la Ussi mbele yetu, na kuingia barabarani ghafla .…. ENDELEA..

Kama nisinge tanua upande wa kulia wa barabara basi nilikuwa naligonga kwa nyuma na bahati mzuri hii barabara ni dubble, hivyo ilimlazimu na yeye kuelekea upande wa chake, yaani kule ambako tulikuwa tunaelekea sisi, tena alikuwa katika speed kali kuliko ya kwetu, hivyo tukaweza kuliona gari la kina Ussi likichanja mbuga kueleka upande wa chake.

na lilipokaribia maeneo ya ofisi ya diving school, ambapo palikuwa na mchepusho wa kuingia barabara ya kurudi macho manne, wakaingia na kuhamia upande wa pili na kuongeza speed zaidi ya ile, niwazi kuna kitu walikuwa wanawahi kule macho mane, “kumbe huyu kijana ni wa ovyo sana” alisema insp Aroub, ambae alikuwa seat ya mbele ya abiria, “tena sio kidogo” alichangia Jessenia, wakati huo tuna watazama upande wetu wakulia, maana ndio tulikuwa tunapishana, hakika Ussi alikuwa ameniudhi sana kwa kitendo alicho kifanya, “yani kama usingekuwa makini, sasa tungekuwa tuna ongea mengine” alisema mzee Aroub.

Sikutaka kuongea lolote juu ya jambo lile, zaidi nilikuwa nawaza ile speed ya kina Ussi inaelekea wapi, kwa vyovyote kuna mtu wao amesha liona spacio kule Mess na kuwajulisha ndio maana wanawahi huko Mess, ambako wanatarajia kutukuta.

Sisi tulienda mpaka Madungu polisi, ambako tulimuacha Aroub, kisha tuka geuka kurudi Mess, lakini kwa mwendo wa tahadhari kubwa sana, maana nilijuwa kuwa lazima wakina Ussi, watakuwa pale Mess, hata nilipofika Machomane, nilipiga simu kwa Malambo kumuuliza kama anawaona wakina Ussi hapo Mess, na yeye akaniambia kuwa ametoka na gari la jeshi, kwenda kambini kwaajili ya kuandaa kile kikundi cha kunipa msaaada hapo baadae, nikapiga simu kwa Mwasenga na kumuuliza kama yupo pale Mess, “nimeingia sasa hivi na ndio natoka hapa Wawi, vipi nimeona gari hapa lakini wewe sikuoni” alisema Mwasenga, huku nasikia akifunga mlango wa gari maana ufungaji wa mlango ule ni wakubamiza.

Hapo nikajuwa kuwa anaingia kwenye gari, tayari kuondoka kama alivyo sema, “nipo hapa maeneo ya jirani” nilimjibu Mwasenga, kisha nikampachika swali jingine, “vipi unamuona Ussi hapo Mess” niliuliza hivyo, huku nikijuwa fika kuwa Ussi atakuwa pale Mess, “jamaa nime mkuta hapa, Mess, nashangaa nime msalimia lakini naona amenilia bati kinoma” alisema Mwasenga, huku upande wake nikisikia gari linawashwa, “kwahiyo bado yupo hapo Mess?” nilimuuliza Mwasenga, wakati huo naendesha gari taratibu sana kuelekea upande wa mess, ambapo tulibakisha mita chache kupafikia, pale Mess ambapo tuliweza kuiona njia ya kuingilia mess.

“yah! ametulia ndani na jamaa flani wapo kama saba kama sikosei hata jana usiku alikuwa nao” aliongea Mwasenga wakati huo mbele yangu nililona gari la jeshi aina ya land rover defender, likitoka pale mess na kuja upande wetu, yani upande wa macho manne, “kwahiyo wapo hapo nje au ndani” niliuliza tena huku nikiliangalia gari lile la jeshi, ambalo nilifahamu kuwa lina endeshwa na Mwasenga, “wapo ndani, lakini nimemuona Ussi kama mara mbili hivi, akitoka nje na kurudi ndani, ni kama anatazama kitu nje” alisema Mwasenga na wakati huo tulikuwa tunapishana, “na wewe unaelekea wapi sasa hivi?” nilimuuliza Mwasenga, ambae alisema kuwa anaelekea nyumbani kwake kujiandaa mara moja, kisha arudi kambini, “kuna kazi ya dharula nimepewa, si unajuwa kazi zetu kaka” alisema Mwasenga ambae hakuwa na wazo kuwa mimi nipo ndani ya gari analo pishana nalo.

Yap! baada ya kukata simu, na hapo nikiwa tayari nimesha juwa kuwa Ussi na wenzake wapo Mess wanasubiri kuona nitatokea njia gani, “ujuwe Ussi atakuwa ameshaambiwa kuwa gari tunalo tumia lipo hapa mess ndio maana wamekuja haraka, na sasa wanasubiri tutatokea upande gani” nilimuambia Jessenia ambae bado alikuwa seat ya nyuma, “sasa tutafanyaje gari lenye vitu vyetu vipo kwenye lile gari?” aliuliza Jessenia, huku tunakaribia kuifikia njia ya kuingilia pale Mess, ambapo sasa tuliweza kuliona gari la wakina Ussi likiwa kwenye maegesho ya pale mess na magari mengine mawili.

“usijali mambo yataenda sawa” nilimuambia Jessenia huku nakanyaga mafuta kuelekea Ali Khamis camp, huku nikimpigia simu Malambo, nikamueleza mtego wa kina Ussi pale Mess, nae akaniambia kuwa nikifika tu niede ofisini kwake.

Naam mida ya saa moja na robo, ndiyo mida ambayo tuliingia pale Ali Khamis Camp, moja kwa moja tukaingia ndani ya geti, tena upande wa maofisini na kwenda kusimama head ofisi, kisha tuka shuka nakuingia ofisini kwa afisa utawala, ambae tulimkuta anatusubiri, “ akiwa na afisa mwingine luten Komba, ambae ndie mkuu wa ile operation, upande wa back up, yani msaada, ambae pia alisema kuwa askari wapo tayari wanasubiri mpango kazi, hapo nikamueleza jinsi mpango kazi utakavyo kuwa, (nisingependa kueleza sasa hivi, maana utaufahamu wakati wa tukio) Luten Komba na Malambo waliukubali mpango wangu, ambao ulionyesha ni kiasi gani najiamini kuwa ninaweza kukabiliana na kile ambacho kinaweza kutokea endapo nitafanya makosa kidogo tu.

“ok! muda utakao ingia eneo la tukio?” aliuliza Komba, ambae alikuwa na note book ana note kila wanacho kiongea na kukipanga, “muda ni saa mbili kamili, watu tukaohusika kwa upande wangu ni watatu, yaani mimi mwenyewe, mzee Zidadu, yaani Mangeu, na Jessenia mwenyewe” nilimueleza Komba, huku Malambo na Jessenia wakifuatilia maongezi, “pia kutakuwa na insp Aroub, ambae atakuja mara moja nakuondoka, atakuwa ameambatana na askari wachache wa jeshi la polisi, maeneo ni yale yale A na B, yani nyumbani kwa mzee Juma, au bandarini kwenye sehemua ambayo Ussi anatia nanga vyombo yake, ujio wenu ni wa siri katika sehemu zote mbili, ishara ni mwanga kwenye giza, cha msingi umakini wa hali ya juu unahitajika” huo ndio ulikuwa mwisho wa mipango na mwenendo mzima.******

Yap! saa moja na dakika arobaini na tano, nikiwa na bastora yangu niliyoichimbia vyema kabisa kwenye nguo yangu ya ndani sox ya mguu wa kulia nikiifunika na truck suit, pamoja tape record ndogo sana yenye min cassate ndani yake, ambayo nilikuwa nimeiweka kwenye sox ya mguu wa kushoto, nayo nikiifunika na truck suit, nadhani umepata picha kamili.

mimi na Jessenia tulikuwa ndani ya kibanda cha mzee Mangeu, pamoja na mzee mangeu mwenyewe, mahali pale tulifika kwa msaada wa Malambo, ambae alituleta mpaka njia panda ya kuingia msingini tukiwa tumesha pita wawi mess, ambapo tuliliona gari la Ussi likiwa pale pale, maana nyepesi bado walikuwa wanasubiri kuona tutatokea upande gani ili waweze kufanya yao.

mimi na Jessenia tulitembea kwa mguu mpaka kwenye kibanda cha Mangeu, huku nikiwa nimesha wasiliana na insp Aroub, ambae aliniambia kuwa alikuwa mita chache toka kwenye nyumba ya mzee Juma Mohamed, ambayo tayari robo tatu yake ilikuwa imezingirwa na askari wa jeshi la ulinzi wenye silaha zao zilizo sheheni mikebe mitatu ya risasi, toka dakika kumi zilizo pita, hata babu Mangeu hakuwa anafahamu kabla, kuwa kuna hao jamaa ambao wakiwa kazini, mawazo yao ni kuuwa kwa asilimia mia moja, ndio maana niliwapa tahadhari kubwa sana kuwa, wasifanye lolote mpaka nitakapo toa ishara ya kuomba msaada.

Naam, hapo mara moja tukaanza mpango, ambao ulianza kwa Jessenia kupiga simu kwa mjomba wake, ambae kiukweli alipokea mara moja, “asalam aleykum” alisalimia Jessenia ambae alikuwa ameweka loud speeker na wote watatu tukawa tunasikia maongezi yale, “unasemaje we mkosa adabu, yani malezi yote haya unanitia aibu kwa kutoroka na mwanaume” alifoka mjomba wake Jessenia, “nisamehe mjomba, lakini sijatoroka nipo hapa hapa pemba” alisema Jessenia kwa sauti iliyojaa nidhamu, na heshima, “kweli bado upo pemba, upo sehemu gani, bado upo na huyo kijana?” aliuliza mzee Juma, huku sauti yake ikibadilika na kuwa yenye shauku, “nipo njiani nakuja nyumbani lakini nilitaka nikueleze kuwa nakuja na wageni” alisema Jessenia kwa sauti ile ile ya upole.
Na hapo ni kama mzee Juma alishtuka sana kusikia vile…….…. ITAENDELEA
 
KIFO CHA HAWARA (mkono wa jini)
SEHEMU YA THEMANINI NA TATU
MTUNZI: Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA THEMANINI NA MBILI: alifoka mjomba wake Jessenia, “nisamehe mjomba, lakini sijatoroka nipo hapa hapa pemba” alisema Jessenia kwa sauti iliyojaa nidhamu, na heshima, “kweli bado hupo pemba, hupo sehemu gani, bado hupo na huyo kijana?” aliuliza mzee Juma, huku sauti yake ikibadirika na kuwa yenye shahuku, “nipo njiani na kuja nyumbani lakini nilitaka nikueleke kuwa na kuja na wageni” alisema Jessenia, kwa sauti ile ile ya upole, na hapo ni kama mzee Juma alishtuka sana kusikia vile…….…. ENDELEA..


“eti! ni wageni gani hao, na wanafwata nini?” aliuliza mzee Juma kwa sauti ya mshtuko na hasira, “ni mchumba wangu anakuja kujitambulisha, atakuwa na mzee Mangeu ndie mshenga wake” hakika sikuwahi kushuhudia mshtuko wa wazi kwenye simu kama huu, leo ndiyo ilikuwa mara ya kwanza.

Maana mzee Juma alitoa mguno mkubwa wa mshangao, “eti we Seni, mbona unafanya mambo ya ajabu hivyo, unaweza kumshirikisha huyo mzee mchawi, au umesahau kilichokutokea kwa miaka mingi?” aliuliza mzee Juma na hapo nikamuona Mangeu anatikisa kichwa kwa masikitiko, “ndiyo mjomba nafahamu, lakini yeye mwenyewe ndio kamchagua huyo, naomba unikubalie” alibembeleza Jessenia, na hapo zikapita sekunde kadhaa, ni kama mzee Juma alikuwa anawaza jambo, “sawa njooni, mupo wapi kwa sasa” aliuliza mzee Juma, “tuna karibia nyumbani, tunatokea macho manne” alisema Jessenia, “sawa njooni” alisema mzee Juma na kukata simu haraka sana.

Ukataji wa simu na ukubaliji wa mzee Juma, ulinitia mashaka, mjomba wako sasa anapiga simu kwa Ussi, hivyo basi huko ndani kutakuwa na kazi mzito, inabidi muwe makini sana kufata maelekezo yangu kila nitakapo kuwa nawaeleza” niliwaeleza Jessenia na mzee Mangeu, nao wakaitikia kwa vichwa kuonyesha kuwa wamenielewa.*******

Dakika mbili baadae tulikuwa nje ya geti la kina Jessenia, ambapo Jessenia kama mwenyeji wetu ndie alie tukaribisha ndani, ambako tulipokelewa na shangazi yake Jessenia, “karibu jamani” alikaribisha shangazi, kwa sauti ambayo, usingetia shaka yoyote, huku ananitazama usoni kama vile ananikagua, “asante sana” anilisalimia kwa sauti iliyojaa nidhamu na heshima kubwa, “karibu ndani jamani” alisema tena shangazi na safari hii aliitikia mzee Mangeu, “asante jirani, leo nimekuwa mgeni wenu jamani” alisema mzee Mangeu, wakati huo mimi navua raba miguuni mwangu nikibakiza sox, ambazo zilikuwa ni ghala langu la silaha na hifadhi ya tape record, huku mzee mangeu na Jessenia wakivua viatu vyao vya wazi, bila hata kuhangaika.

Baada ya hapo tuka ingia ndani, huku nyuma yetu tukisikia ngurumo ya gari likiingia kwa fujo kwa ujuzi nilionao katika kutambua sauti na ngurmo mbali mbali, ngurumo ya gari hilo haikuwa defender, sio la polisi wala la jeshi, ila lilikuwa ni gari aina ya Parado, hivyo nikajuwa wazi kuwa Ussi alikuwa anaingia pale nyumbani kwao, nilisha yatarajia hayo hivyo siku shtuka zaidi ya kuona mpango wangu unaenda kama nilivyopanga.

Naam Jessenia ambae ndie mwenyewji wetu, alituongoza mpaka sebuleni, huku shangazi yake akibakia pale nje, ni kama alikuwa anamsubiri Ussi, hakika lilikuwa ni jumba kubwa la kifahari, lenye mahadhi ya kiarabu, muonekano wake ulipendeza kwa kweli, “karibu karibu karibu bwana Zidadu, naona sasa umeamua kumtafutia Seni mwanume ambae unaona anafaa kurithi kila kitu sio?” hivyo ndivyo mzee Juma aliekuwa amekaa kwenye zuria la manyoya akiegemea mto wa manyoa pia, ambao ni mmoja kati ya mito kadhaa iliyopo pale sebuleni, hakuna alieshangaa juu ya maneno ya mzee Juma, maana kila mmoja kati yetu alikuwa anafahamu.

Lakini licha ya hivyo, lakini mzee Mangeu akajisaisha, “jirani unaongea nini bwana, vijana wameniomba niwe muwakilishi wao, maana huyu kijana ametokea bara” alisema mzee Mangeu, huku anakaa chini, na wakati huo tukasikia vishindo vingi vya watu vinatokea nyuma yetu, kuja upande wa sebuleni, “Seni hawezi kukubali kukutumia kama mshenga au mzee wa huyu mshenzi, bila wewe kumueleza ujinga wako, najuwa Seni amekuwa akikuogopa toka utoto wake, inakuwaje leo aondoe hofu yake ghafla hivi?” aliuliza mzee Juma kwa sauti ya ukali, wakati huo nageuka kutazama nyuma ili kuona watu waliokuwa wanaingia.

Naam macho yangu yaliona kile nilicho kitarajia, yaani Ussi akiwa ameongozana na watu kama sita hivi, wakiwa na vipande vya miti na mapanga mikononi mwao, “nyie wapuuzi bora mumetupunguzia kazi, mume jileta wenyewe hapa nyumbani, hebu niambieni computer yangu ipo wapi, na kwanini muliichukuwa” alisema Ussi huku ananisukuma kwa nguvu, nikayumba kidogo na kutembea hatua kadhaa mbele kisha nikajiangausha chini makusudi, “jamani kaka Ussi, kwanini unamsukuma shemeji yako?” alisema Jessenia huku ananifuata pale nilipo jiangusha na kuchuchumaa mbele yangu.

“pole Eric, jamani vipi umeumia?” aliuliza Jessenia aliechuchumaa mbele yangu, “hapana sijaumia” nilijibu kwa sauti iliyotoa huruma, “Juma, ndivyo tunavyo wapokea wageni wetu muhimu, si unajuwa jinsi ndoa ya Jessenia ilivyo muhimu?” aliuliza Mangeu kwa sauti iliyojaa mshangao wa ghadhab, wakati huo ndio wakati nilio utumia kupeleka mkono kwenye mguu wangu wa kushoto na kubofya kitufe cha mwisho cha tape record, ambacho ni cha kurecordia, bahati nzuri nacho kikakubali.

“tulia we mpuuzi, leo ndiyo mwisho wa kila kitu, unadhani marehemu mtarajiwa anahitaji kukaribishwa vipi kwenye nyumba ya mtoa roho?” aliuliza Ussi kwa sauti ya kibabe, huku anamsukuma mzee Mangeu, ambae pia anaanguka chini kama kifurushi pale kwenye zuria, Juma mueleze kijana wako ajuwe mimi ni nani, ili aniheshimi kidogo” alisema Mangeu huku anamtazama mzee Juma, ambae kitu cha kushangaza ndio kwanza akamuona anatabasamu kwa dharau, “anajuwa kila kitu, anajuwa kuwa wewe …..” kabla hajamaliza kuongea, mara akatokea mke wa mzee Juma, yaani shangazi yake Jessenia, akiingia ndani mbio mbio, “Aroub yupo nje anahitaji kukuona” alisema mke wa mzee Juma.

Hapo mzee Juma na Ussi wakatazamana kwa macho ya hofu, “nenda kamalizane nae haraka” alisema Ussi huku anamtazama baba yake, “sawa lakini hakikisha hawa wajinga hawapigi kelele wala hawafanyi fujo yoyote” alisema mzee Juma, huku anainuka na kuelekea upande wa nje, huku nyuma Ussi alieshikapanga alinisogelea mimi na wale wengine wakigawana sisi na kutuzingira na silaha zao za jadi mikononi, wakizinyoosha kwetu, huku wakituonyeshea ishara ya kukaa kimya, hapo tukawa kimya kabisaaaa, kiasi cha kusikia hata ngurumo za magari yaliyokuwa yanapita barabarani, ambako ni umbali wa mita kama mia nne toka pale.

“hoooo! bwana Aroub, karibu sana, naona umeishia nje” tuliweza kusikia sauti ya mjomba wake Jessenia, yaani mzee Juma akiongea toka nje kwa sauti iliyo changamka, “yaan nimeishia hapa nje maana shemeji ameniambia kuwa una wageni munakamilisha jambo flani” ilikuwa ni sauti ya insp Aroub, “nikweli bwana, lakini tunaweza kuongea” alisema mzee Juma, kwa sauti ambayo usingeweza kusema kama kuna jambo ameliacha ndani, “nadhani ni vyema kama ukimaliza maongezi na wageni wako, maana nina maongezi yanayohitaji muda na utulivu mkubwa sana, ni kuhusu wizi uliotokea hapa kwako na upotevu wa binti yako” alisema insp Aroub.

Walikubaliana hivyo kisha mzee Juma akarudi ndani, nadhani insp Aroub aliondoka kama tulivyo kubaliana, lakini hakutakiwa kwenda mbali sana, “huyo mjinga amesha ondoka, sasa tuwafanyaje hawa wapuuzi?” aliuliza mzee Juma, huku anaibukia pale sebuleni, “baba mimi nadhani tufanya kama tulivyo panga, tuwauwe kisha tukawatupe baharini” alisema Ussi, huku tape record ikiendelea kuzunguka ndani ya sox ya mguu wangu wa kushoto, “bwana Juma, hii nini, ina maana umepanga kutuuwa?” aliuliza Mangeu kwa sauti iliyojaa wasi wasi, “wewe unaona nini kitatokea juu yako na huyu kifaranga chako, ambacho baada ya kukilea kwa miaka yote hiyo sasa kina jifanya kimekuwa na kujipangia mambo yake” alisema mzee Juma, kwa sauti ya kujiamini sana, “lakini Juma, kwanini ufanye hivi ndugu yangu?” aliuliza mzee Mangeu kwa sauti iliyojaa wasi wasi na kuombleza, “hivi Zidadu, unadhani baada ya yote niliyo yafanya naweza kukubali kupoteza kila kitu, kumuacha Jessenia aende na huyu mpuuzi?” aliuliza kwa sauti yenye kejeli mzee Juma.

Hapo Jessenia akatoa macho ya mshangao, kama vile hakujuwa lolote toka mwanzo, “mjomba una maana gani, una maana hutaki niolewe?” aliuliza Jessenia kwa sauti ya mshangao wakujifanyisha, maana wote walikuwa wanajuwa kinachoendelea, “sasa je mlidhania mimi mjinga” alisema mzee Juma, huku akicheka kwa dharau, kisha akamtazama Ussi, “ngoja kwanza niwaeleze kitu ambacho kitawafurahisha hawa wajinga, ambao walidhania kuwa mimi ndie mjinga” alisema mzee Juma, huku usoni mwake furaha ikiwa imeshamili na kufanya uso wake uchukize usoni pangu,
Na hapo mzee huyu, ambae hakujuwa kama narecord maongezi yake akaanza kuongea.******

Ilikuwa hivi, wakati ule mzee Zidadu, amekuja kwa mwarabu ambae alikuwa anaishi kwenye hii nyumba, ambayo mzee Juma alikuwa mfanyakazi pamoja na mke wake kwa lengo la kununua hii nyumba, lilikuwa pigo kubwa sana kwa mzee Juma, ambae alitegemea kuwa endapo angekosekana mteja basi yeye angejimilikisha nyumba pindi mwarabu yule atakapo ondoka.

Lakini bwana Juma akapata nafasi nyingine ya kucheza karata yake kwa kumchomea mzee Zidadu na bi Aisha, yaani mama yake Jessenia, ambao alimini kuwa endapo watauwawa na wao watapata kujimilikisha nyumba ile.

Ni kweli walifanikiwa kutoa taarifa kwa mke wa Abdulkarim, ambae alituma vijana wake haraka kuja kuwa shambulia na kusababisha kifo cha Aisha Mohamed, yaani mama yake Jessenia, huku mzee Zidadu akifanikiwa kumuokoa Jessenia na yeye mwenyewe akibakia na ngeu za kutosha.

Lakini bado bahati ikabakia kwa mzee Juma, ambae alikabidhiwa nyumba ile kwa shariti la kumlea Jessenia, ambae akiolewa na wao ndio mwisho wa kumiliki mali zake, licha ya hivyo mzee huyo Mangeu aliwahudumia kwa kila kitu, huku akiwafungulia biashara mbali mbali ikiwepo ile ya Ussi ya uvuvi….. ENDELEA



KIFO CHA HAWARA (mkono wa jini)
SEHEMU YA THEMANINI NA NNE
MTUNZI: Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA THEMANINI NA TATU: Lakini bado bahati ikabakia kwa mzee Juma, ambae alikabidhiwa nyumba ile kwa shariti la kumlea Jessenia, ambae akiolewa na wao ndio mwisho wa kumiliki mali zake, licha ya hivyo mzee huyo Mangeu aliwahudumia kwa kila kitu, huku akiwafungulia biashara mbali mbali ikiwepo ile ya Ussi ya uvuvi…..….. ENDELEA..

Kwa maelezo ya mzee Juma ni kwamba toka Jessenia akiwa na miaka saba, akaanza kumuweka mbali na mzee Mangeu kwa kueneza habari za kuwa mzee Mangeu ni mchawi, sifa hiyo aliieneza sio tu kwa Jessenia peke yake, bali hata kwa watu wengine wa pale msingini, ambao waliamini na kuanza kumtenga mzee huyu, ambae baadae akaanza kuandaa mazingira kwa kijana wake Ussi kuja kumuoa Jessenia, ili mwisho wa siku wamiliki mali zote za Jessenia kama mzee Mangeu alivyopanga kuwa Jessenia akiolewa ata kabidhiwa mali zake.

Pasipo kuangalia tabia chafu za Ussi, yeye na Ussi walihakikisha Jessenia hatengenezi mahusiano yoyote ya kimapenzi, waliuwa watu wengi sana, alisimulia mzee Juma akiwataja kwa majina, “kikwazo kikaja kwa huyu mpuuzi” alisema mzee Juma huku ananionyesha kwa kidole.

Mzee Juma alieleza kuwa, siku ile wakina Ussi walijaribu sana kuniuwa siku ile pale Green Mess, ni ile mida niliwaona wanazunguka zunguka dirishani, hata waliposhindwa vijana wa Ussi, baadae akaja mwenyewe nae akashindwa na ndipo alipoanza mipango ya kuniuwa, “ndio maana tuliwauwa wale wote insp Aroub aliponza kuwatilia mashaka, “sijui ilikuwaje mpaka ukamshinda Mabusi, ila leo ndio mwisho wako” safari hii aliongea Ussi, kwa sauti iliyojaa hasira, “na bahati nzuri mume turahisishia kazi, mumekuja wote watatu” alisema mzee Juma, huku anacheka kicheko cha dharau, kicheko ambacho anacheka mtu alie mnasa panya kwenye mtego.

Unajuwa kilicho fuata hapo na mimi nikaangaua kicheko huku napeleka mkono kwenye mguu wangu wa kushoto na kuzima ile tape recorder, wote wakanitazama kwa mshangao, huku Ussi ananifuata kwa hasira na kushusha teke usawa wa mgongo wangu, lakini nikalikwepa kidogo teke lake pale nilipojaa, “Ussi tulia kidogo maana unacho kitaka hukiwezi hata kwa sekunde” niliongea kwa sauti tulivu huku naendelea kucheka hata wenzake waliokuwa wanataka kunivamia pia wakatulia na kunitazama kwa mshangao, wakijiuliza kwanini najiamini, “unaongea nini we fala, leo utoke humu ndani” alisema Ussi kwa sauti ile ile ya hasira.
Nikacheka kicheko cha kumtia hasira, “hivi Ussi, wewe na baba yako mume shindwa kujiuliza kwanini tumejileta wenyewe hapa nyumbani, au munadhani mzee Mangeu anaweza kukubali, kuwa mshenga wakati yeye ndie ndugu wa Jesse” niliuliza kwa sauti ya tulivu, ungesema tupo kwenye mazungumzo ya kawaida, “kwahiyo unataka kusema nini” aliuliza Ussi kwa jazba, huku baba yake akiwa ametulia anatoa macho kwa mshangao wa tahadhari kumtazama mzee Zidadu, “Ussi unauliza nataka kusema nini ina maana hujapata jibu tu, unadhani Jesse baada ya kukuona ukimkosa kosa na panga na kukumbia siku mbili nzima halafu leo ajileta tu?” nilimuuliza tena Ussi, ambae alimtazama Jessenia kama vile kuna jibu alikuwa anataka kupata.

Lakini alipoona kuwa amekosa jibu, akamtazama baba yake, “baba mimi naona tuwauwe kisha tukawatupe, maana wameshajuwa kila kitu” alisema Ussi, kwasauti iliyoanza kuwa na wasi wasi, “Ussi usifikirie sisi kujuwa fikiria kuhusu video ambayo inaweza kuanza kusambaa mitaani ikikuonyesha unamuuwa Vuai kwa sindano yenye sumu nyumbani kwake” hapo sasa nikawa kama nimemkumbusha kitu Ussi, “baba…. baba … hard disc” alisema Ussi huku anatoka mbio kuelekea ghorofani.

Hapo mzee Mangeu akamtazama mzee Juma, ambae alikuwa amtumbua macho kama vile amesingiziwa wizi ugenini, “bwana Juma ni vyema wewe na familia yako ukajisalimisha polisi hili swala liishe kwa amani” alisema mzee Mangeu kwa sauti ya kusihi, “nyie vijana mnashangaa nini hebu wauweni hawa washenzi” alisema mzee Juma, kwa sauti ya juu na yakupayuka, hapo nikajuwa kuwa sikuwa na muda wa kuomba msaada toka nje kutokana na ukaribu wa watu wale na nikizubaa tu nimempoteza Jessenia na mzee Mangeu, hivyo haraka sana nikapeleka mkono wangu kwenye mguu wa kulia nakuibuka na AGP, ambayo sifa yake moja wapo ni kuto kutoa sauti, ambayo nikamuelekezea mmoja kati ya wale vijana aliekuwa ameinua panga lake kutandika Jesse, nikaminya kifyetulio bila kusita na kuruhusu risasi kutoka.

Kilichotokea kiliwafanya wale wangine wa tano waanze ache walichokuwa wanakifanya toka mbio kukimbilia kolidoni, kuelekea upande wa jikoni ambako sisi tulipitia, maana nilimfumua kichwa yule jamaa na kusababisha ubongo wake kutawanyika kama tikiti lililokanyagwa na fuso, “mamaaaa” Jessenia alipiga kelele, huku mzee Mangeu na mzee Juma wakitoa macho kwa mshangao nikaipiga risasi taa ya sebuleni, halafu nikaminya saa yangu ambayo inatochi maalumu kwaajili ya kusomea ramani, halafu nikaizima na kuiwasha tena, halafu nikaizima, kilikuwa ni kitendo cha haraka wakati huo huo kwa kutumia taa za kwenye ngazi za kuendea ghorofani, nikamuona Ussi anashuka mbio mbio, “baba!! baba!! wameiba ile harad disc” alisema Ussi ambae kiukweli hakujuwa kinachoendelea.

Mara ghafla akasita, ni baada ya kuona giza limetawala pale sebuleni, “Ussi usijaribu kupiga hatua hata moja, ni vyema ukijisalimisha” nilimuambia Ussi, ambae hakujuwa pale sebuleni tupo wangapi na mkononi nina nini, “mpuuzi wewe unadhania ni rahisi hivyo” alisema Ussi kwa sauti iliyojaa hasira kali, huku anavamia giza na panga lake akiwa amelipunga hewani tayari kushambulia yeyote kati yetu, hapo sikuwa na haja ya kuchapa risasi, nilimshindilia ngumi moja nzito usoni nae akajibwaga chini akiangukia kwenye damu za yule niliempasua kichwa.

Hapo Ussi akaamka kwa haraka, huku macho yake yakianza kuzowea giza, kabla haja kaa sawa nikamuongeza teke la usoni tena, ambalo lilimrudisha pale pale, “nyie mbona hamsaidii alipiga kelele Ussi, ambae hakusikia kelele za nje, “simama” ila alikuja kusikia milipuko kadhaa ya risasi, sikutaka kumuuwa Ussi wala mjomba wake, ila nilitaka wafikishwe mbele ya sheria, hivyo nilihakikisha namtandika Ussi kisawa sawa, mpaka akalegea, kuhusu baba yake sikuwa na wasi wasi, maana niliamini kwa umri ule asingeweza kufanya lolote, “mjomba ina maana wewe ndie uliesababisha kifo cha mama yangu” aliuliza Jessenia kwa sauti iliyojaa uchungu, wakati huo tulikuwa tunasikia mke wa mzee Juma, toka nje ya nyumba akiomba asifanywe chochote sababu yeye hausiku, “Seni, huwezi kufanya lolote mama yako alisha kufa zake, jibu hilo alilitoa Ussi ambae alikuwa amechafuka uso kwa damu zilizotoka kwenye mipasuko mbali mbali ya mwili wake iliyosababishwa na ngumi, na mateke.

Kitendo bila kutegemea Jessenia akanipokonya bastora yangu na kumuelekezea Ussi, huku akiminya trigger mara kadhaa, akitandika miguu yote miwili ya Ussi kwenye mapaja, ile nataka kunyang’anya nilichelewa, tayari alisha ielekezea kwa mzee Juma hapo nikafumba macho, nakusikia sauti ya kilio cha mzee huyu, nilipofumbua macho na yeye nikamuona akiwa amechakazwa miguu yake kama ilivyo kwa kijana wake.

Naam dakika chache baadae askari walikuwa wamesha ingia ndani, huku wakitoa taarifa ya kuwa walisha wauwa wale vijana wote watano waliojaribu kutoroka, baada ya hapo insp Aroub nae akaja na kuungana na sisi, akakabidhiwa wakina Ussi baba yake na mama yake, mama Ussi alipelekwa moja kwa moja kituoni, huku mzee Juma na Ussi, wakipelekwa hospital chini ya ulinzi wa jeshi la polisi.

Wakati huo upande wa pili kule pwani, askari walikamata mashua zote za Ussi na wafanyakazi wake, kisha kuwapeleka kituo cha polisi.******

Naam siku ya pili habari za kukamtwa kwa Ussi na baba yake, zilisambaa vibaya huku sababu zikiwekwa wazi kuwa ni mauwaji yaliyo tikisa kwa muda mrefu, watu wakidhania kuwa ni jinni, ndugu na jamaa za marehemu walilaani sana kitendo kile kilicho fanywa na Ussi na baba yake, wakishirikiana na mama yake, walinisifu sana Eric kwa kusababisha wauwaji kukamatwa, japo hawakujuwa kuwa mimi ni mpelelezi walinitaja kama mwalimu au mchumba wa Jessenia, nilienusurika kuuwawa.

Mwasenga na mke wake walishangaa sana, kugundua kuwa mimi ni mpelelezi, mwalimu aisha hakujuwa kama mimi ni mpelelezi mpaka nilipoondoka, Saphia alifurahi sana aliposikia kuwa mimi ndie niliewaumbua wakina Ussi, nashukuru hakukumbushia kuhusu ndoa niliyo mdang’anya, Maimuna yeye hakuweza kuonana nae.

Mwisho mimi na Jessenia tulielekea dar es salaam ambako nafanyia kazi, japo Jessenia ananyumba yake kule mbezi msakuzi, lakini anaishi kwenye nyumba yangu amefungua maduka manne ya vipodose moja kariakoo msimbazi jingine mbezi jingine mwenge na jingine kibaha maili moja, mzee mangeu alimpatia robo tatu ya mali zote alizochukuwa kwa mwarabu Jamal.

Mzee Mangeu mwenyewe sasa anaishi dar es salaam huku lile jengo kubwa pamoja shamba, amekabidhi serikalini lifanywe shule na makazi ya watoto wasio jiweza, yeye amenunua nyumba kubwa huko kigamboni, ambako amepata mwanamke mmoja mrembo kweli anaishi nae kama mke wake, na sasa ndie mtu pekee ambae tunamchukulia kama baba na ndugu wa Jessenia.

sasa tuna watoto watatu na maisha yanaendelea, ila sikuacha kuwa zawadia wakina mwasenga na mke wake, aisha malambao na wengine walionisidia kwa namna moja au nyingine kule pemba.

Mpaka hapo nimefikia mwisho wa simulizi hii ya KIFO CHA HAWARA asante sana kwa kuwa pamoja na mimi kwa hii miezi mi nne ya simulizi hii munisamehe sana kwa pale nilipowa cheleweshea ni majukumu tu ya kila siku musichoke kufuatilia simulizi nyingine zijazo hapa hapa Jamii Forums Shukran sana kwa support yenu wote na wale walioishia njiani sisi tushamaliza... AHSANTE NA KARIBUNI TENA.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom