Kifo cha hawara (Mkono Wa Jini)

Kifo cha hawara (Mkono Wa Jini)

KIFO CHA HAWARA (mkono wa jini)
SEHEMU YA SITINI NA MOJA
MTUNZI: Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA SITINI: “hujakosea boss nimemnasa mtoto mkali kinyama nadhani utahusika kuja kupeleka barua” nilimueleza mkurugenzi ambae alishindwa kuzuwia kicheko, japo hakikuwa kikali sana, “acha upuuzi, sikukupigia simu unipe hiyo taarifa yako ya uzinzi, hebu niambie ulipo pata ile sumu ya hatari uliyoituma” alisema mkurugenzi kwa sauti ambayo ilikuwa imeshaondoka kwenye utani, “nieleze kwanza ni sumu ya aina gani, na inafanyaje kazi” nilimuuliza mkurugenzi, ili anipe jibu lake….…. ENDELEA……
Nililinganishe na lile la maabara ya hospital ya chake chake, “ni sumu aina ya synanceia, inayo fisha kwa muda mfupi sana, ambayo hupatikana kwenye kiumbe cha baharini, kijulikanacho kama stone fish, sumu ambayo hukausha maji maji yote pamoja na damu ipatikanayo ndani ya binadamu, au kiumbe chochote kitakacho patwa na sumu hiyo, ok! unaweza kuniambia ulivyo ipata?” aliuliza mkurugenzi, na hapo sikuona sababu ya kumficha, “hiyo ndiyo sumu inayo tumiwa na muuwaji, na kuwapumbaza raia na polisi, kuwa mauwaji yana fanywa na jini, jana usiku nilivamiwa na watu wawili, ambao walijaribu kunidunga hiyo sumu, lakini niliwawahi na kuwakabiri mmoja wao alijidunga sumu hiyo, na kukutwa na umauti, nadhani hata wewe uliniambia asubuhi juu ya kifo chake, nimethibitisha mwenyewe kwa macho yangu hospital ya chake chake, na kijana mwenzie aliesalia amekutwa ameuwawa jioni ya leo, nadhani wanajaribu kuficha ushahidi” nilimueleza mkurugenzi, huku nikiwa naendesha gari taratibu na wakati mwingine nikitazama side mirror, ambapo sasa niliweza kuona mwanga wa taa mmoja ukija nyuma yangu, ni wazi ilikuwa pikipiki, “duh! we kiboko, hivi unajuwa ni miaka mingapi wamehangaika kusaka chanzo cha mauwaji, ni zaidi ya miaka sita Eric, upo vizuri sana, hebu niambie mipango yako kwa sasa” alisema mkurugenzi, akionyesha kuwa mwenye furaha na kujivunia, “siwezi kukupa mipango yangu kwa sasa, ila nitakupa lengo langu, ni kwamba nina tafuta ushahidi ili muuwaji awekwe chini ya ulinzi” nilimueleza mkurugenzi, huku nikitazama kwa mara nyingine kwenye kioo cha kutazamia nyuma nikaiona ile pikipiki ikiwa karibu yangu, lakini sikuweza kujuwa kama anae ni fuatilia ni yule mandevu au babu mangeu ambae tulikubaliana tukutane sehemu nyingine, lakini nyuma ya pikipiki hiyo kulikuwa na gari nalo linakuja, nikaongeza mwendo na wapikipiki akaongeza mwendo, “ok! sawa kijana nakutakia kazi njema” alisema mkurugenzi na kukata simu, nikaiweka simu kwenye seat ya pembeni, halafu nikatazama side mirror, nikaiona ile pikipiki inakuja kwa mwendo wa kasi sana nyuma yangu, na gari la polisi nalo likiwa linakuja kwa speed kama yetu, hapo nikapunguza mwendo ghafla.
Naam sijui tayari mwendesha pikipiki alishtukia jambo, maana safari hii hakupunguza mwendo ila baada yake alinipita kwa speed ile ile, na kunipa nafasi ya kumuona mwendesha pikipiki ambae alikuwa ni yule yule mandevu, aliepita kutokomea mbele, niliweka gari pembeni na lile la polisi nalo lilipunguza mwendo na kusimama nyuma yangu, kisha insp Aroub akashuka na kunifuata kwenye gari langu, kisha nikaingiza gia na kuondoa gari taratibu, huku gari la polisi likitufuata nyuma yetu nalo kwa mwendo wa taratibu, tukiachiana kwa mwendo wa mita mia moja, “kijana haya mambo ni mazito sana, inawezekana muuwaji amaesha juwa kuwa ninamfuatilia na nimesha gundua kuwa muuwaji sio jini, sasa sijui baada ya hapo inafuata hatua gani” alisema insp Aroub, akionekana kuhitaji msaada wangu, “kwani ilikuwaje unaweza kunieleza vizuri sasa?” nilimuuliza insp ambae alianza kunisimulia kuanzia alipotoka kule Fidel Castor sekondari.****
Iilikuwa hivi, mara baada ya insp Aroub kutoka Fidel Castor kuonana na mimi, alienda moja kwa moja mpaka nyumbani kwake, ambako alibadili nguo zake na kuvaa nguo nadhifu za kiraia, kisha akaenda moja kwa moja nyumbani kwa mzee Juma Mohamed, ambako kwa bahati nzuri alimkuta, “insp vipi tena ujo wako wa kheri kweli, au kuna jingine” aliuliza mzee Juma Mohamed, kwa sauti ambayo licha ya kuwa katika hali ya utani, lakini insp aliweza kuona wazi wasi wasi usoni kwa mzee huyu, “hakuna tatizo mzee wangu, ni jambo la kheri tu, kuna habari mzuri sana nimekuletea” alisema insp Aroub, huku akijichekesha kidogo, kumuondoa hofu mzee Juma Mohamed, ambae badala ya kufurahi, yeye alishtuka kidogo, japo alijitahidi sana kuzuia mshtuko wake, lakini bado macho yake yalionyesha wazi mshtuko wake, “ipi tena bwana Aroub?” aliuliza kwa sauti iliyojaa shauku mzee Juma Mohamed na wakati huo kijana Ussi alikuwa anaibukia sebuleni akitokea chumbani kwake, na kusalimia kisha akakaa pembeni, “mzee mpaka sasa nimebaini kuwa muuwaji sio jini, ila ni binadamu kabisaaaa, ndie amekuwa kifanya mchezo huo kwa muda mrefu” alisema Insp Aroub kwa sauti yenye furaha na kuchangamka, akitegemea kuona mzee Juma pia akiwa anachangamka, lakini ilikuwa ni tofauti kidogo, “weee umegundua vipi hilo jambo lililofichwa kwa miaka yote hii?” aliuliza mzee Juma Mohamed kwa sauti ya mshangao na mshtuko mkubwa, japo insp Aroub hakutambua kama mshtuko ule wa kawaida au ulikuwa na siri ndani yake, lakini akaona atumie nafasi hii kufanya kile alichoelekezwa na mimi, “ni kwamba mzee Juma, jibu tunaenda kulipata muda mfupi ujao, ni kwa mmoja wa vijana wako alie onekana na marehemu jana usiku” kauli hiyo iliwafanya mzee Juma na kijana wake Ussi, watazamane kwa macho ya mshangao na mshtuko, lakini wakajidhibiti na kurudi kwa insp, “hebu kwanza insp hii habari umeipataje pataje?” aliuliza mzee Juma, wakati huo Ussi alikuwa kimya anasikiliza maongezi, huku anachezea simu yake kama vile anaandika ujumbe, “ni story ndefu mzee Juma ila nitakuja kukueleza vizuri nikitoka kumuona huyo kijana, cha msingi naomba nielekeze wanakopatikana vijana wale wafanyakazi wako wa kwenye majahazi” alisema insp Aroub, na hapo mzee Juma akatazama Juma, ni kama alimtaka kujibu swali lile, “wanapatikana kule kule baharini” alisema Ussi, huku akijitahidi kuweka sauti yake katika hali flani ya kawaida, tofauti na baba yake ambae alionekana kuwa mwenye wasi wasi kidogo, “basi sawa wacha niende nikamuone huyo kijana” alisema insp Aroub, kabla ya kuaga, kisha akainuka na kuondoka zake.
Baada ya kutoka hapo insp Aroub akaenda moja moja pwani, yaani ufukweni, ambako alikutana na wafanyakazi watatu wa Ussi, na kuwauliza kama wanafahamu marehemu aliongozana na nani jana jioni, lakini wote walikataa kwamba hawa kumuona mtu yoyote akitoka na marehemu, “rafiki yake wa karibu ni nani au aliwahi kusema ana tembea na mwanamke flani” aliuliza insp Aroub, huku anawatazama wale jamaa kwa awamu, lakini jibu lao lilikuwa sijui, bahati nzuri insp Aroub akapata wazo jingine, ni kwenda kuwauliza wavuvi wajirani, tofauti na wale wafanyakazi wa Ussi, ambao hawakuonyesha dalili ya kueleza ukweli.
Ukweli wazo lake lilizaa mafanikio, pale alipoongea na wale wavuvi wa jirani, “jana mida ya saa moja jioni, nilimuona mrehemu akiwa na Mabusi, wapo kwenye pikipiki lao kubwa wanaelekea mjini, sasa nimeshangaa kusikia eti mwenzie amekufa” aliseme mmoja kati ya wale wawuvi, na hapo insp Aroub akajuwa kuna kitu baina ya mauwaji yale na wafanyakazi wale wa Ussi, “hapo nikaondoka zangu na kurudi kwa wale wafanyakazi wa Ussi, na kuwauliza alipo huyo mwenzao anaeitwa Mabusi, nao wakasema kuwa hawajui alipoenda” alisema Aroub, ambae hakutaka kufanya lolote la kuvuruga uchunguzi wake ulioanza kuleta mafanikio, hivyo akarudi mjini kuanza kumsaka huyo jamaa anaeitwa Mabusi, ambae alimsaka kuanzia saa nane mpaka saa kumi na moja alipopata taarifa ya kuokotwa kwa mwili wa kijana huyo, akiwa ameuwawa kwa kifo kama kile alicho uwawa mwenzie jana usiku, na wengine wakina Vuai, Abdulqadir, na wengine, waliosadikiwa kuuliwa na jini, “hapo ndipo nilipoelewa maana yako, nina hisia kuwa muuwaji ni mtu wa karibu sana na familia ya bwana Juma” alisema insp Aroub ambae alinieleza kuwa sasa lengo lake ni kutafuta ushahidi na sababu ya mauwaji, ili kuweza kumtia nguvuni muuwaji, “sasa unanishauri nifanyaje katika hatua inayofuata?” aliuliza insp Aroub, huku tukiwa tuna enda taratibu, ndani ya gari nililokuwa naendesha, “ujuwe mzee, kwanza kabisa sasa inabidi uwe makini sana, maana kuna hatari kubwa mbele yako, kwa vyovyote muuwaji amesha juwa kuwa unakaribia kumng’amua, hivyo anaweza kufanya lolote ili kupoteza ushahidi na kukwamisha juhudi za kumnasa” nilimueleza insp Aroub, na kati ya vitu ambavyo unatakiwa kuvizingatia ni usalama wa nyumbani kwako, maana baadhi ya vifo vilitokea wakati muuwaji akiwa nje na marehemu akiwa ndani” nilimtahadharisha Aroub, na yeye akakubaliana na mimi kwa kutikisa kichwa juu chini, “cha kufanya mzee, kesho nenda kawahoji tena, ikiwa ni sababu ya kuficha mtu alie ongozana na marehemu wa jana usiku, na pia waulize kama kuna mtu hakuwepo jana wakati unaongea nao zaidi ya marehemu Mabusi” ukimpata muulize kwa kina, zaidi ya hapo unaweza kupata jambo la kukusaidia” nilishauri insp Aroub, na hapo nikawa kama nimejichongea, maana wakati naweka gari pembeni ili ni mshushe aingie kwenye gari lake, akaniuliza, “kijana nikuulize kitu, hivi wewe ni mwandishi, au mpelelezi toka Tanzania Secret Agent?” aliuliza insp Aroub, akiwa makini na uulizaji wake, ambao haukuwa na na dalili ya utani hata kidogo….…. ENDELEA.
 
KIFO CHA HAWARA (mkono wa jinni)
SEHEMU YA SITINI NA MBILI
MTUNZI: Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA SITINI NA MOJA: ukimpata muulize kwa kina, zaidi ya hapo unaweza kupata jambo la kukusaidia” nilishauri insp Aroub, na hapo nikawa kama nimejichongea, maana wakati naweka gari pembeni ili ni mshushe aingie kwenye gari lake, akaniuliza, “kijana nikuulize kitu, hivi wewe ni mwandishi, au mpelelezi toka Tanzania Secret Agent?” aliuliza insp Aroub, akiwa makini na uulizaji wake, ambao haukuwa na na dalili ya utani hata kidogo….…. ENDELEA..
lakini mimi nilicheka kidogo, “kwa hiyo mzee ninafaa kuwa mpelelezi?” nilimuuliza kwa sauti iliyojaa utani, na yeye akacheka kidogo, “nikweli waandishi ni wajuzi wa kufwatilia habari na kufichua yaliyo jificha, lakini kiukweli kwa upande wako umekuwa tofauti kidogo, maana ndani ya masaa machache nimeweza kugundua mambo mengi sana, ambayo nilishindwa kuyagundua kwa miaka mingi sana” alisema insp Aroub, wakati huo gari la polisi lilikuwa lina simama nyuma ya gari langu, “sidhani kama una sababu ya kuwaza hivyo, cha msingi fanya nilicho kuambia ili kupata majibu” nilimuambia mzee Aroub, ambae alicheka kidogo, “haya bwana Eric, nadhani kuna majibu zaidi nayahitaji, moja kuhusu muuwaji, na sababu ya kufanya mauwaji, pili nitahitaji kujuwa wewe ni nani na una kazi gani haswaa ukiachilia ualimu na hiyo ya uandishi” alisema kwa utani insp Aroub, huku anashuka toka kwenye gari langu, huku anacheka kidogo, “ndio maana mara nyingi huwa tunaogopa kulisaidia jeshi la polisi” nilimtania insp Aroub, na hapo tukacheka kwa pamoja, huku akiwa amesimama nje ya gari, na mlango bado upo wazi, “basi bwana Eric, nikuache uka pumzike, kesho asubuhi nitaenda kwanza kule pwani, kisha saa mbili asubuhi nitaungana na msafara wa RPC, kuelekea uwanja wa ndege, kuna wageni tunaenda kuwapokea” alisema Aroub, kisha akafunga mlango wa gari, na mimi nikaondoa gari langu kwa speed huku natazama kwenye side mirror, na kumuona insp Aroub anaingia kwenye gari la polisi, ambalo liliondoka na kuelekea mjini, yani tulikotoka na mimi nikakanyaga mafuta kuelekea vitongoji, lakini mpaka nafika sikuweza kumuona madevu, yaani muendesha vesper.
Naam nilipofika Green House na kuona Vesper ubavuni mwa nyumba ndipo nilipokumbuka juu ya kuwa nilikuwa na ahadi na babu Mangeu, kwamba tukutane nje ya pale Wawi Messi, na alipotazama vizuri pale kwenye Vesper, nikamuona japo palikuwa na giza nikaweza kumuona mzee Zidadu akiwa nyuma ya Vesper ananionyeshea ishara ya kuingia ndani bila kumtazama, wala kumuongelesha, hapo sikuhitaji masomo ya ziada kuelewa alicho nieleza babu huyu, moja kwa moja nikaingia ndani ya nyumba na kutokea mlango wa nyuma, kisha nikazungukia kule alikokuwepo mzee Zidadu, ambae nilimkuta ametulia anatazama upande wa barabarani, “we mzee unamtazama nani huko barabarani?” nilimuuliza babu Mangeu kwa sauti ya kunong’ona, nae akashatuka na kunionyeshea ishara ya kukaa kimya, kisha akanionyesha kule anakotazama yeye, yaani barabarani upande wa kuelekea vitongoji,
Naam baada ya kuangalia vizuri na macho kuzowea giza, nikaweza kuona kitu kama kimvuli cha mtu, aliekaa kwenye pikipiki, alikuwa umbali wa mita kama mia mbili hivi, toka pale tulipo kuwepo mimi na mzee Mangeu, “nani yule?” nilimuuliza babu Mangeu kwa sauti ya kunong’ona, japo nilikuwa nimesha gundua kuwa yule alikuwa ni yule mandevu, “ni mpuuzi mmoja anaitwa Othman, ni mfanyakazi wa Ussi, mtoto wa Juma” alijibu Mangeu, huku akitazama kwa umakini sana, “unadhani anafuata nini huku” nilimuuliza Mangeu, ili nione kama kuna jambo amesha ligundua katika sakata zima la mauwaji yanayoendelea na familia ya bwana Juma Mohamed yaani mjomba wa bandia wa Jessenia, “weee ni hatari kubwa sana, hawa vijana nadhani kuna jambo wanalifanya, na ndio maana nimekuja kukueleza ili uwe makini” alisema mzee Mangeu, na kuanza kunieleza wasi wasi wake juu ya kile alicho kigundua.
Mzee Mangeu, aliniambia kuwa jana usiku wakati ananitafuta pale Wawi Messi, aliwaona vijana wawili wa Ussi, wakiingia na pikipiki, hivyo yeye akaona isiwe kesi akanyoosha huku Green House, lakini asubuhi akasikia taarifa ya kuwa mmoja kati ya vijana wale amekutwa ameuwawa huko gombani, na mida ya jioni akasikia kuwa mwingine tena ameuwawa, “we huoni kama kuna kitu kinaendelea hapo, na wote wameuliwa na jini” alisema mzee Mangeu, kwa sauti ya kunong’ona, ambayo ilionyesha mashaka makubwa, unadhani ni kweli mauwaji yana sababishwa na jini?” nilimuuliza Mangeu, ambae alitulia kidogo kama vile anatafuta jibu, na baada ya sekunde kadhaa akanijibu, “mh! kijana hilo swali ndilo ninalo jiuliza kwa miaka mingi sana” alisema Mangeu, akionyesha kutofahamu jibu sahihi, “unadhani ametumwa na Ussi kunifuatilia?” nilimuuliza Mangeu, katika hali ya kuchunguza hisia zake juu ya kinachoendelea.
Wakati huo huo tukasikia pikipiki ikiwashwa, na tukatazama kule alikokuwepo Mandevu, tuka ona taa ya pikipiki ikiwa imewashwa, na kisha kuondoka kuelekea mjini, “huyoooo anaondoka zake mshenzi huyu, lazima Ussi amemtuma, yani ameng’ang’ania kuweka wivu kwa huyu Seni” alisema Mangeu kwa sauti iliyojaa chuki, wakati ile pikipiki ikipita usawa wa macho yetu, na kutokomea upande wa mjini, “unadhani kwanini Ussi ana kuwa na wivu sana kwa Jesse?” nilimuuliza’ mzee Zidadu, huku naanza kutembea kutoka kwenye maficho ya giza, huku mzee Mangeu akinifuata, “unajuwa ni kawaida kwa vijana wa pemba kuona wivu kwa dada zao hasa wanaotembea na vijana toka nje ya Pemba, ni angalau akiwa ametoka unguja, lakini wivu wa kijana huyu unashangaza sana, inafikia hatua nahisi bado huyu mshenzi anamtamani kutembea na Seni” alisema mzee Mangeu, akionyesha wazi kuwa hatamani kitu kama hicho kitokee, “kwani anafahamu kuwa Jesse sio dada yake?” nilimuuliza mzee Mangeu, wakati huo tulikuwa tumesimama sehemu ya mbele ya nyumba, ambayo ilikuwa inafikiwa na mwanga wa taa.
Naam kwa swali hilo, niliweza kumuona mzee Mangeu akinitazama kwa macho ya ung’amuzi, “kwanini umeniuliza swali kama hilo, au wewe ni mpelelezi?” aliuliza mzee Mangeu, kwa sauti ya mshangao huku ananitazama kwa macho ya ung’amuzi. “kwanini niwe mpelelezi, au kuna jambo unalijuwa halafu unanificha?” nilimuuliza kwa namna flani ya kumtega, ili mzee huyu alie onekana kuwa amegundua jambo aweze kufunguka anacho kujuwa, “hapana kijana, ila swali lako lime nifanya nihisi kitu, inawezekana kabisa huu ni mpango wa Juma familia yake, kwamba Seni asiolewe na mtu yoyote, au aolewe na Ussi ili mali za Seni, wabakie nazo wao, ndio maana wakati ule alitaka wawili hawa wafanye upuuzi” alisema Mangeu, ambae ungemuona wakati huu, ungefahamu kuwa alikuwa amepata jambo jipya kabisa katika maisha yake, “kwani mzee hukuwahi kufikiria hivyo toka mwanzo?” nilimuuliza mzee Zidadu, kwa sauti ya udadisi, “yaani sikuwahi kufikiria kabisa, ujuwe leo nimewaona wana hangaika sana juu ya hawa watu walio uwawa, na pia nadhani polisi wameshaanza kuwasonga songa, leo nimuona Aroub amekuja pale nyumbani” alisema mzee Mangeu, huku bado akiwa katika hali ya mshangao, “ok! sasa unafikiria nini?” nilimuuliza Mangeu, ili kusoma alichokifikiria baada ya kugundua jambo hilo, “hapo kwa kweli ni kufanya mpango ukajitambulishe haraka kama unataka kumuoa Seni, naamini hato kataa kuolewa na wewe, na baada ya hapo muondoke kuelekea dar” alisema Mangeu, nilipata jibu la kuwa bado mzee Mangeu hajajuwa kinachoendelea kwa upande wa mauwaji, lakini sikutaka kumfanya aelewe, “lakini mimi siwezi kuondoka haraka hapa Pemba, kwasababu bado sija maliza……”….…. ITAENDELEA..

KIFO CHA HAWARA (mkono wa jini)
SEHEMU YA SITINI NA TATU
MTUNZI: Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA SITINI NA MBILI:“ok! sasa unafikiria nini?” nilimuuliza Mangeu, ili kusoma alichokifikiria baada ya kugundua jambo hilo, “hapo kwa kweli ni kufanya mpango ukajitambulishe haraka kama unataka kumuoa Seni, naamini hato kataa kuolewa na wewe, na baada ya hapo muondoke kuelekea dar” alisema Mangeu, nilipata jibu la kuwa bado mzee Mangeu hajajuwa kinachoendelea kwa upande wa mauwaji, lakini sikutaka kumfanya aelewe, “lakini mimi siwezi kuondoka haraka hapa Pemba, kwasababu bado sija maliza..... ENDELEA..
Kabla sijamaliza kusema, mzee Mangeu akadakia, “kijana kumbuka kila kitu cha Seni nitakiacha mikononi mwako, hivyo Hutokuwa na Haja ya kufanya kazi ya ualimu, tena unaweza kwenda kufungua shule yako na kuajili walimu” alisema mzee Mangeu kwa msisitizo, “Huwezi kunielewa mzee, naomba nipe muda, ujuwe bado hatuja fahamu kuhusu vifo vya wanaume ambao wamekuwa wakimfuata Jesse” nilimueleza Mangeu ambae alionyesha kunielewa kidogo, “sawa ni muhimu kufahamu kwanini jambo hilo limekuwa likitokea, lakini hatuwezi kusubiri zaidi, unadhani itakuwaje kama jini litakuuwa?” aliuliza mzee Mangeu, na mimi nikamrudishia swali, “itakuwaje kama jini linatumwa kuzuia mtu asimuoe Jesse” hapo mzee Mangeu akatulia kidogo, akitafakari jambo kwa sekunde kadhaa, kabla hajavunja ukimya, “hivi inawezekana jini linatumwa na Juma na kijana wake Ussi?” aliuliza Mangeu, huku ananitazima, na mimi nikamtupia swali, “unaonaje ukihisi kuwa muuwaji sio jini ni mtu wa kawaida ambae anazuia mtu asimuoe Jesse, na pengine akaamua kukuuwa wewe au Jessen mwenyewe” nilimuuliza mzee Mangeu, ambae alionyesha kushtuka kidogo, “hilo ndilo ninalolitafuta kila siku, na ninatumia gharama kubwa ili niling’amue hilo” alisema Mangeu na hapo nikahisi jambo kuhusu huyu mzee, “unatumiaje gharama kutafuta jibu hilo? au umekodi wapelelezi wa kujitegemea?” nilimuuliza Mangeu, kwa maana ya kuhitaji kuthibiisha hisia zangu.
Hapo nikamuona Mangeu akinitazama kwa macho ya tahadhari, kama vile alishuku jambo juu yangu, “unadhani unapaswa kulijuwa hilo mapema kiasi hiki, manaa hata wao wenyewe niliowapa kazi hawanifahamu?” aliniuliza mzee Mangeu, mpaka hapo nikagundua kuwa huyu ndie alietoa kazi ofisini kwetu, tufanye uchunguzi wa mauwaji haya, yaani mmilikiwa wa Gmail, ya j_jos@gmail.com kwa maana ya John Joseph, “hoooo! kumbe, sasa unaonaje tukikutana na huyo mpelelezi, tujuwe amefikia wapi, na sisi tumpe mawazo yetu” nilimshauri mzee Mangeu ili kumpima kama anaweza kusema ukweli au laa.
Kwanza John Joseph alicheka kidogo, kicheko cha kujidharau, “kosa nililo fanya ni moja kati ya mkataba ambao nimeingia nao, ni kwamba hakuna kufahamiana majina wala kukutana, hata malipo nimefanya benk, na niliwasiliana nao kwa simu na email” nilitabasamulia ndani kwa ndani, “ok! mimi nimepata wazo, unaonaje kama na sisi tukianza upelele wetu?” nilimueleza babu Zidadu, ambae aliachia basamu pana, lililoashiria kukubaliana na wazo langu, “eti eeh, sasa tutafanyaje?” aliuliza Mangeu, na hapo sikutaka kuwa na haraka kwa kumuambia cha kufanya, maana hata mimi sikuwa na juwa la kumtuma mzee huyu, “usijari juu ya hilo, cha kufanya wewe katulie ufikilie nini kifanyike, wakati huo unafuatilia mwendeno wa mzee Juma, na mimi nitakuwa nawaza jambo la kufanya, ila kabla hujaondoka tupeane namba za simu” nilishauri kwa mzee Mangeu, ambae aliunga mkono, huku akisistiza jambo, “lakini kuwa makini Seni asijuwe lolote” alisema hivyo Mangeu kabla hajawasha pikipiki yake na kuondoka zake, huku tukiwa tumesha peana namba za simu, na tukikubaliana kukutana siku inayofuata na kuwasiliana pale tunapata habari yoyote mpya ya kutilia shaka.
Naam na mimi niliingia ndani huku natoa simu yangu na kumpigia Jessenia ili kumjulisha kuwa nimeshafika nyumbani, lakini hakupokea, nikajaribu mara ya pili, lakini ilikuwa hivyo hivyo, kwa maana Jessenia hakupokea, hapo nikaachana nae na kuingia bafuni kuoga, nilipotoka nikakuta simu inaita, na wakati huo huo niliweza kuona alama ya missed call, na mpigaji alikuwa ni Jessenia, siku subiri mpaka nivae nikaipokea mara moja, “kwanini hupokei simu zangu” niliuliza kwa mtindo flani wakujifanya nina wivu, japo nilijuwa fika kuwa alikuwa nyumbani kwao na asingeweza kutoka kwa usiku ule, “jamani Eric, acha wivu, yaani ungejuwa mwenzio niliwekwa kikao wala usingesema” alisema Jessenia na hilo halikunishtua hata kidogo, maana nilijuwa lazima iwe hivyo, kutokana na kiburi alicho kionyesha Jessenia, kwa kutokukubari maagizo ya mjomba wake ya kurudi nyumbani, na ukizingatia kuwa niwazi walikuwa wanafahamu kuwa alikuwa na mimi, na walizijuwa sehemu zote tulizokuwepo au kutembelea, ukiachilia taarifa walizopewa na Mandevu ambae sasa niliweza kulifahamu jina lake kuwa ni Othman, pia Ussi alituona kwa macho yake pale uwanjani, “dah! sasa mjomba amesemaje?” nilimuuliza Jessenia, nikijifanya kama nimeshtuka na sikutarajia kutokea kwa jambio kama hilo, “yani mjomba na shangazi wamenisema sana, toka muda ule umeniacha hapa nyumbani ndio wana maliza sasa hivi” alisema Jessenia katika hali ya uchangamfu, niwazi hakushtuliwa na gombezo la walezi wake, ambao mpaka sasa yeye alikuwa anaamini kuwa ndio ndugu zake halisi, “hee! kwahiyo walikuwa wanasemaje?” nilimuuliza nikiweka kilombwezo cha kushangaa, “wamenisema sana, eti nimeanza tabia mbaya, na nimekuwa na kiburi, nimeonekana naranda randa na mwanaume, nina waaibisha” alisema Jessenia, ambae aliendelea kunisimulia jinsi alivyoongea na walezi wake, kwamba yeye aliwaeleza kuwa, mimi nina nia ya kumuoa, hivyo yeye Jessenia aliwaomba wavumilie kidogo ili nije kujitambulisha kwao na kuanza utaratibu wa kuoa, lakini Jessenia anasema kuwa mjomba na shangazi yake walikataa katakata, kwamba hawanitaki kabisa nifike pale kwao, kwaajili ya kuoa, hapo maongezi yakawa marefu sana, Jessenia aking’ang’ania kuolewa na mimi, na walezi wake, wakisisitiza kuto kunikubaria mimi, huku wakitoa sababu ya kwamba mimi ni mtu kutoka bara, hapo bado walikuwa hawajagusia swala la dini.
Jessenia alinieleza kuwa walezi wake yani shangazi na mjomba wake, walimsema weeee, na mwisho wakamueleza kuwa kesho kuna wageni wanakuja na hato takiwa kutoka pale nyumbani hata kidogo, “inabidi ufanye mbio mbio uje kunitolea barua Eric, na uwajulishe wazazi wako huko bara” alisema Jessenia, kwa sauti ya msisitizo alipokuwa amemaliza kunieleza jinsi walivyoongea na walezi wake, “usijari Jesse, kila kitu kitakuwa sawa, si unajuwa kuwa leo ni siku yetu ya pili toka tuwe wapenzi” nilimueleza Jessenia lakini sio kwa lengo la kumkatalia kwenda kujitambulisha kwao, “una maana gani Eric, ni vyema ukaja nyumbani kujitambulisha ili mjomba ajuwe kwamba nia yako ni kunioa nasiyo kunichezea” alisema Jessenia kwa sauti ambayo ilianza kunyongea, “sikia Jesse, sina maana ya kukataa kufanya hivyo nilimaanisha wacha kwanza hasira zao zipungue kisha tufanye utaratibu na tutaongea vizuri kesho jioni tukikutana” nilimueleza Jessenia kwa sauti tulivu yenye kumpa matumaini, “kwanini iwe jioni, kwani mchana utakosa muda?” aliuliza Jessenia, kwa sauti ya kulalamika na kujidekeza, “Jesse, kwani umesahau kuwa umeambiwa kuwa kesho kuna wageni wanakuja nyumbani kwenu na unatakiwa kuwepo nyumbani?” nilimuuliza Jessenia, kwa namna ya kumkumbusha, “mimi siwasubiri hao wageni wao, kwani kuna umuhimu wowote wa mimi kuwepo” alisema Jessenia kwa sauti ambayo haikuwa na dalili yoyote ya utani, “hapana Jesse, ukionyesha kiburi watazidi kunichukia, cha msingi wewe bakia kwanza mpaka wageni watoke” nilimshauri Jessenia, ambae sasa alinielewa nia yangu, “hapo sawa, kuwa kile alichokielewa haikuwa nia yangu halisi, nia yangu ilikuwa ni mpaka nitakapo kamilisha kazi yangu, niangalie kama bado nitakuwa katika mapenzi na Jessenia, na kama yatakuwa katika kiwango hiki, basi nifanye taratibu za kumbeba jumla jumla, tena kwa kumtumia huyo huyo Mangeu, “usijari Jesse, kila kitu kitaenda sawa” nilimjibu, kabla ya kukata simu tukikubaliana tuwasiliane kesho asubuhi. ….…. ITAEENDELEA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom