Kifo cha hawara (Mkono Wa Jini)

Kifo cha hawara (Mkono Wa Jini)

UNAONA UNAVYOHANGAIKA KUNUNUA BANDO KILA SIKU? WI-FI ROUTER ZA TIGO NDO KITU PEKEEE KINGEKUSAIDIA


Kua na wi-fi router kuna faida nyingi sana, kama unajiweza kidogo, jitahidi usikose kifaa hiki.


1. Ukiwa na wi-fi unaweza kukuza biashara yako. kwasababu wateja watapenda kuja ofisin kwako wakijua kuna wi-fi, pia wewe utakua huru kupost biashara zako mtandaoni ukiwa hauhofii kuishiwa bando.





2. Kuokoa gharama za bando. Ukweli ni kua bando za kawaida zinaumiza sana mana ukipiga hesabu ya gb 1 kwa 2100 kama kwa siku unatumia gb 1 basi kwa mwezi unatumia 63000. Zidisha kwa watu wote mliopo kwenye ofisi, taasisi au nyumbani kwenye familia yako na majirani, utakuta hela ni kubwa sana mnayotumia. Kukata hizo cost zote mngechukua wi-fi router ya tigo mana inaunganisha hadi watu 64, yani watu 64 wote mnatumia bando unlimited





3. Wi-fi router za tigo zina speed kubwa na zina technology ya 5G pia hazisumbui au kukata katikati ya mwezi, speed kuanzia 20mbps hadi 200mbps hivyo utakua na stable internet connection mda wote.





4. Kifaa ni portable yani kinabebeka kirahisi unaweza kuhamisha, mfano kutoka ofisini kwenda nyumbani kwenye gari unaweza kutembea nacho huku wi-fi ikiwa inafanya kazi. Pia kifaa kinasambaza wi-fi eneo kubwa, zaidi ya mita mia.





UTARATIBU WA MALIPO MARA YA KWANZA.
Mara ya kwanza unalipia kiasi cha sh.250,000, kiasi hicho ni kwaajili ya kupatiwa kifaa(router) pamoja na bando unlimited lenye speed ya Mbps 100. Pia utapewa offer mwezi unaofuata hautalipia, kwahiyo ukishatoa hiyo 250000 miezi miwili yote utatumia wi-fi router yako bila kulipia, utaanza kulipia mwezi wa tatu na kuendelea. Pia kuna router ndogo za 130,000 bando lake ni unlimited pia. Ukitaka unlimited bando kwenye lain yako tu utumie bila wifi router ni laki moja kwa miez 3


UTARATIBU WA KULIPIA KILA MWEZI MARA YA PILI NA KUENDELEA!


Uzuri wa huduma hii ni kua unaweza kulipia kidogo kidogo kila mwezi hadi umalize, kikubwa ndani ya mwezi ukamilishe kulipia 100k


KUFIKISHIWA KIFAA(DELIVERY)
ukishafanya malipo kupitia menu ya mix by yas, utaniambia sehem ulipo popote Tanzania utatumiwa kifaa bila kutoa gharama za usafiri yani free delivery. Hutajuta kujiunga na huduma hii.


Mawasiliano: 0717700921
 
KIFO CHA HAWARA (mkono wa jini)
SEHEMU YA HAMSINI
MTUNZI: Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA AROBAINI NA TISA : hata lile lengo la kushirikiana nae nililiona halifai, japo nilisha panga kushirikiana nae bila yeye kujuwa mimi ni nani, na nina fanya nini, “mzee mimi naitwa Eric Frank, ni mwalimu wa taaluma, lakini nimekuja hapa kwaajili ya kuomba msaada na ushauri pengine maono juu ya kitabu ambacho ninakiandika kuhusu maisha ya binadamu, na viumbe vinavyoitwa majini” nilimueleza insp Aroub, huku nikijaribu kusoma uso wake kwamba atalipokea ombi langu au laa….….ENDELEA….
Ukweli insp haroub alishtuka kidogo, baada ya kusikia hoja yangu na kunitazama kwa mshangao, nilihisi mambo mawili, moja ni kwamba pengine jambo alilotoka kuongea na mzee Mohamed linahusiana na kifo cha jana cha yule mfuasi wa Ussi, au anafahamu jambo kuhusu mchezo unao chezwa na muuwaji anae singizia jini, “kijana unadhani umekuja sehemu sahihi kuomba huo msaada?, mimi kazi yangu ni polisi, sasa nahusiana vipi na majini?” aliuliza insp Aroub, huku ananitazama kwa macho fulani yaliyo jaribu kuchangamka toka kwenye mshangao, huku macho yake yakiwa kama yananikagua hivi, wakati huo yule polisi koplo alikuwa anaondoka zake na kutuacha sisi wawili pale langoni.
Hapo nikaona kuna uwezekano wa kukosa kile nilichokitaka, hivyo nikatakiwa kujiongeza, kwanza nilianza kwa kucheka kidogo, “mzee nyie polisi mnakumbana na mengi, pia alieniambia nije nikuone sidhani kama alikosea, niwazi anautambua uwezo wako mkubwa wakupambana na kesi zinazo husu vitu kama hivi” nilimueleza bwana Aroub, huku nikijichekesha kidogo, hapo insp alitulia kidogo kama vile anawaza jambo, kisha akainua uso wake na kunitazama huku anatabasamu, “bwanaaaa nani vile?” aliuliza insp Arob, kama vile amekubari kunisikiliza, na mimi nikamjibu kwa haraka, “Eric, naitwa Eric Frank” nilimjibu na kutega sikio kusubiri kusikia anachotaka kusema, “ok! Hebu nifuate, na ninakupa dakika tano tu, maana kuna report nahitaji kuikamilisha haraka sana itumwe dar es salaam” alisema insp Aroub, huku anaogoza kuelekea upande wa maegesho ya magari.
Naam!!! baada ya kutembea hatua kadhaa, insp akaanzisha maongezi, “haya bwana Eric, hebu niambie, unatokea kampuni gani na unaulizia majini kwa maana ipi?” aliuliza insp Aroub, huku tukitembea taratibu kuelekea upande ule ule wa maegesho ya magari usawa wa lile Toyota spacio tulilokuja nalo.
Ukweli sikutaka tulisogelee, kwa sababu sikutaka Jessenia asikie ninachoongea na insp huyu mtu mzima, ambae lengo langu ni kushirikiana nae bila yeye kujuwa kuwa na mimi mpelelezi, “labda nianze kujitambulisha tena, naitwa Eric, toka Mbogo Publishers iliyopo dar es salaam” nilisema hivyo huku natoa kitambulisho fake, ambacho tunatumia dar es salaam, maana kampuni yetu ya upelelezi ni ya siri, japo inatambuliwa na serikali akakichukuwa na kukitazama, alitumia muda mfupi sana kukitazama, “mnajihusisha na nini?” aliuliza insp Aroub huku ananirudishia kitambulisho changu, “tuna jihusisha na uuzaji wa vifaa vya maofisini na uchapishaji wa makala na vitabu, pia mimi nina degree ya mipangilio za Tarakishi (computer softwere/program) na sasa nipo hapa Pemba, nime ajiliwa kwa muda kufundisha computer hapo shule ya sekondali ya Fider Castor, mwalimu wa computer” hapo Arobu akanitazama kama vile ananifananisha na maneno ninayosema, “hoooo! kumbe upo vizuri eeh, sasa wewe umesomea computer zipi, yale makubwa au zile ndogo?” aliuliza mzee huyu, ambae niligundua kuwa uelewa wake juu ya computer ni mdogo sana, “mzee unapozungumzia computer, ziwe tarakilishi za mezani na zile mpakato au za mnara, zote zina mifumo ya kufanana tofauti maumbile na matoleo, pia uwezo kupokea mipangilio (program), uhifadhi pia na uzalishaji” nilifafanua na hapo nikamuona tena Aroub ananitazama kwa namna ile ile ya kunikagua, “ok! sasa kwanini msomi kama wewe unaanza kuulizia habari za majini?” insp Aroub aliniuliza swali ambalo nilikuwa nalitamani sana, kwanza tulicheka kwa pamoja, kabla sijamfafanulia, “ni kwamba mzee wakati nikiwa namaliza kidato cha sita, nilikuwa nimeshaanza kuandika kitabu changu kinachoitwa Maisha unapande wa giza, nikijaribu kuandika kuhusu viumbe ambavyo kuna baadhi ya watu wanatoa ushuhuda kuwa wamekutana navyo, na baadhi wanaisi, kuwa ni mambo ya kufukilika, asa kuhusu viumbe vinavyoitwa jinni” nilimueleza insp Arob, ambae sasa alionekana kuanza kuniamini, maana alikubaliana na mimi kwa kichwa, huku ananitazama tena, “ok! sasa kwangu unataka nini maana mimi sio mganga wala mtabiri?” aliuliza insp Aroub, huku tuna ingia kwenye eneo la maegesho na bahati nzuri ni kwamba tulililenga gari moja la polisi ambalo lilionekana halija tembea muda mrefu kidogo, ni kutokana na nyasi chache kwenye matairi yake, “ni kwamba mzee, ujuwe hii project niliisimamisha kwa muda mrefu sana, maana nilikosa dondoo muhimu kuhusu viumbe hivyo, lakini nilipofika hapa pemba nikasikia matukio mawili yanayohusishwa na jini, moja lilitokea week kama mbili zilizopita, na moja nimesikia leo asubuhi, nilipoulizia namna ya kupata hizi habari nikaambiwa nikuone wewe kwa sababu wewe ndie unae chunguza kuhusu vifo hivyo” nilimaliza ufafanuzi na kumuachia Aroub aamue kama kuninyima ushirikiano au kunieleza anacho kijuwa ambacho ndio kitu cha kwanza nilicho kitaka kwa mzee huyu ili niweze kumsoma anachoelewa juu ya matukio haya ya kupangwa na mtu wa kawaida, au kama anafahamu juu ya kinacho endelea.
Insp Aroub, alitulia kidogo kama anawaza jambo fulani, kisha akainua uso wake, “kijana kwanza hongera sana kwa hiyo makala ambayo umeibuni, maana itatoa elimu nzuri sana kwa kizazi cha sasa, ila nikuambie kitu kimoja, ungekuwa umenijulisha ujio wako ungekuwa umefanya jambo zuri sana, maana kwa sasa nitakueleza kwa kifupi, ila ukipata nafasi utakuja tena kupata mengine zaidi, ila kwa sasa wacha nikueleze kwa kfupi” alisema insp Aroub, akionyesha wazi kuniunga mkono katika kuandaa hiyo makala fake.
Mzee Aroub akaendelea kunieleza huku akisimulia mambo mengi niliyosimuliwa, yaani ambayo nilisha yasikia na kuyafanyia uchunguzi, “ukweli kijana haya mambo ni mapana sana, aliekueleza kwamba uje kwangu hakukosea, maana ni mwaka wa tano sasa na chunguza kesi hii ambayo bado sijaipatia ufumbuzi, kuna kiumbe kinachosadikiwa kuwa ni jini, kina fanya mauwaji mara kwa mara tena kwa wanaume tu, mwanzo tulidhania vijana wawili wanafunzi walikufa kwa kuumwa na nyoka, lakini vipimo vilikataa kabisa, hata tulipopeleka sampuli dar es salaam, nao walikosa majibu ya chanzo cha vifo vile, lakini kwa upande wa wazee na wenye elimu ya majini wakasema kuwa vifo kama hivyo hutokea sana kwa watu wanao uliwa na majini ya bahari” alieleza insp Aroub, huku nikijitahidi kumchunguza kama anaficha jambo au anasema anacho kijuwa, “lakini hapa karibu mashuhuda wanasema kuwa marehemu kama wawili hivi waliokutwa na janga hilo la jini, walionekana wakiongozana na mwanamke anae shabihiana, kwa maana maelezo yana mlenga mwanamke mmoja mrefu mwenye umbo la kuvutia, anaevaa baibui na niqab nyie watu wa bara munaita ninja, muda mfupi kabla hawaja uwawa” alisema insp Aroub, na hapo nikamuwahi, “lakini mzee, unadhani huyo mwanamke ndie jini mweyewe?” nilimuuliza insp, ambae alishusha pumzi ndefu, kama vile alichotaka kunieleza hata yeye hajakiafiki, “ndivyo tunavyo amini, maana hatuna viwezeshi kama tungekuwa na vifaa kama ulaya, nadhani tungeweza kulinasa hata tukio la jana usiku, ambapo huyu kijana ameuwawa hadharani kabisa” alisema mzee Aroub, na hapo nilitamani kuamini kuwa haegemei upande wowote, lakini hapo hapo nikakumbuka kuwa muda mfupi uliopita alikuwa na mzee Juma Mohamed, mtu ambae nashuku kuwa anahusika juu ya kila kitu kinachoendelea, “samahani mzee, hivi huyo jamaa alie uwawa naweza kukutana na ndugu zake, pengine anaweza kupatikana mmoja ambae alimuona akiwa na mwanamke au hilo jini” nilimuuliza insp kama mtego, maana nilijuwa fika kuwa lazima mzee Juma alikuja kumuona insp kuhusu kifo cha kijana wa Ussi.
Hapo insp Aroub nikawa kama nime mkumbusha jambo, “huyo kijana ni mgeni hapa Pemba, aliajiriwa na mtoto wa mzee mmoja hivi kama ulimuona niliongozana nae wakati ule ulitaka kumsukuma, ndiyo nilimuita nimueleze hilo jambo, na yeye ndio kwanza anasikia hizo taarifa, hivyo anaenda kufanya utaratibu kama ni kuachia hospital izike au laa, maana amesema kuwapata ndugu zake itakuwa ngumu” alisema insp Aroub, na hapo nikagundua kuwa, insp hakuwa anaelewa chochote juu ya mchezo unao endelea, “hooo! yule mzee niliwahi kumuona mara moja, kwenye msiba wa Vuai hapo msingini” nilimuambia insp Aroub nikijaribu kumleta kwenye ushawishi wa kujiweka wazi kama ni mshirika au la, maana kushiriki sio lazima awe muuwaji, ila akijuwa na kuficha nako ni kuhusika pia, “yah! na yeye anaishi pale msingini, na hao ni vijana wake wa pale mtaani umri wa Vuai ni kama wa kijana wake Ussi” alisema insp Arobu, na hapo nikamchomekea swali tangulizi kabla sijaenda kwenye swali husika, “samahani mzee kwa usumbufu ila naona maswali yanazidi kunijia kichwani, hivi unadhani huyo jini anauwa kwa sababu gani, maana katika dodosa yangu, ni kwamba jini huwa hauwi bila sababu, na kama angekuwa jini korofi basi mimi na wewe pia tunge kuwa hatarini” nilimuuliza mzee Aroub, ikiwa ni njia ya kutambua kama anafahamu ukweli au la, “mh! ukweli ilo ndilo linalotushangaza hata sisi, maana tumewahi kusikia visa vingi vya majini, kama vile popo bawa, jini Chongo, na mengine, huwa yanatokea kwa sababu fulani na kuuwawa watu linalowahitaji kama huyu anavyo fanya, lakini mpaka sasa hatuja pata sababu au kitu ambacho kilitokea na kumnkasirisha” alisema insp Aroub, ambae bado niliona kuwa hakua na muelekeo wa kuwa anatambua ukweli wa jambo hili, hapo nikacheka kidogo, kiasi cha yeye kunitazama kwa macho ya kuuliza, lakini kabla hajauliza lolote nikamuwahi, “samahani mzee unajuwa hili jambo kwa sisi ambao hatuja kumbana na jini huwa tunaona kama hadithi za mbogo edgar, ila mlijaribu kuweka mtego wowote au kuwashuku watu fulani fulania kuhusika na matukio haya?” nilimuuliza mzee Aroub ambae alitabasamu kidogo……… ENDELEA.


KIFO CHA HAWARA (mkono wa jini)
SEHEMU YA HAMSINI NA MOJA
MTUNZI: Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA HAMSINI : alisema insp Aroub, ambae bado niliona kuwa hakua na muelekeo wa kuwa anatambua ukweli wa jambo hili, hapo nikacheka kidogo, kiasi cha yeye kunitazama kwa macho ya kuuliza, lakini kabla hajauliza lolote nikamuwahi, “samahani mzee unajuwa hili jambo kwa sisi ambao hatuja kumbana na jini huwa tunaona kama hadithi za mbogo edgar, ila mlijaribu kuweka mtego wowote au kuwashuku watu fulani fulania kuhusika na matukio haya?” nilimuuliza mzee Aroub ambae alitabasamu kidogo……… ENDELEA……
Ni kama vile aliniona ninazungumza kitu ambacho yeye alisha kifanya, “unajuwa nilikuwa na mawazo kama ya kwako, kwamba kuna mtu anafanya matukio haya halafu anasingizia jini, lakini hatukufanikiwa kupata mshukiwa, na juzi kwenye tukio la kifo cha Vuai, nilipigiwa na watu wa jirani wa Vuai, kuwa ile nyumba ina security, kama tunaweza kuzikagua na kuona jinsi tukio lilivyo kuwa, na kwamba tuangalie kama kweli muuwaji ni jini au binadamu anae uwa kwa mtindo wa kipekee unao fanana na mauwaji ya jini, lakini bahati mbaya tulikuta mfumo wote wa camera ulikuwa mbovu” alijibu insp Aroub, na hapo nilimshangaa kimoyo moyo, “kwanini unasema mfumo ulikuwa mbovu” nilimuuliza insp Aroub kwa sauti tulivu, sikutaka aone mshangao wangu, “yah! tuliona kwa macho Vifaa vilikuwa vimeharibika haikuhitaji kuangalia mara mbili ili kuona” alisema insp, na hapo nilishindwa kuvumilia, “samahani mzee ilikuwa ni mibovu au iliharibiwa” swali langu lilimfanya insp Aroub anitazame kwa macho ya kunikagua, lakini safari hii hakukaa kimya, “kijana wewe ni mwalimu au mpelelezi?” aliuliza insp Aroub, ambae kiukweli, alinishtua na kunifanya nihisi kuwa ninaenda kuumbuka muda mfupu ujao.
Hapo nikajichekesha kibwege, huku nawaza ni mjibu nini ili kumuondoa kwenye hisia zake, lakini wakati nawaza nimjibu nini, insp Aroub akaniwahi “maana una maswali ya kipelelezi, ambayo hata mimi sikuwahi kuyafikiria hapo kabla, ila sishangai sana, waandishi wengi wanakuwa kama wapelelezi” alisema insp Aroub huku anacheka kidogo, “hooo! kumbe nafaa kuwa mpelelezi eeh?” nilimuuliza insp kwa kumzuga ili asigundue kama nilishtuka kwa swali lake, insp Alicheka kidogo, “yah! unamaswali mazuri, naimani kama ningekuwa na wewe toka hapo mwanzo ningefanikiwa kupata jibu sahihi, na pengine ningekuwa nimesha fanikiwa kumuona huyo jini” alisema mzee Aroub, ambae aliendelea kwa kusema kuwa, ukweli mazingira waliyo yakuta yalionyesha kuwa ile computer iliyobeba hard disc ilikuwa imevunjwa na kioo hakikuonyesha kitu, “sasa mzee tufanye marehemu alivunja mwenye security na kutoa hard disc, lakini sasa tujiulize alifanya hivyo kwasababu gani, si angeifungua na kutoa Hard disc, na kama kuna mtu alifanya hivyo ni nani, na kwanini, maana sidhani kama jini ana haja ya kuharibu mfumo wa camera za ulinzi ili kufanya jambo lake” nilimueleza insp Aroub, ambae sasa alikuwa amesha sahau kama anakazi kule ofisini maana tulikuwa tumesimama kwa zaidi ya dakika ishirini.
Insp Aroub alitulia kwa sekunde kadhaa, kama vile anawaza jambo kwa kina, kisha akavuta pumzi ndefu na kuishusha kwa nguvu, “yani hapa najiuliza ni kwanini wakati mwingine tusiwe tuna angalia vipaji kama hiki cha kwako na kuja kufanyia kazi ndani ya jeshi, maana unachokiongea ndicho nilichotakiwa kukichunguza mwanzo, hasa muda ule ambao tulikuwa tumetoka kuchukuwa mwili wa Vuai” alisema Aroub kama mtu anae jilaumu kwa kukosa kuliwaza hilo.
Kama ninge kuwa wewe msomaji, japo ninge mfumbulia fumbo ilo la camera, lakini ukweli lazima ningeingia kwenye matatizo, au kushukiwa katika nafasi ya kwanza, ila sikushindwa kutoa msaada, “ila mimi naona jujachelewa, unaweza kupata jibu ambalo litatusaidia wote, wewe katika upelelezi wako, na mimi katika kukamilisha kitabu changu” nilimueleza insp Aroub, kama vile natania, nikatulia kusubiri aniulize swali, “mh! sidhani kama naweza kupata chochote kwasasa, maana zimeshapita week mbili?” ujuwe kuna raha yake pale unapo kuwa na jibu, halafu unakaa kusubiri swali, “kwani unachotakiwa kujuwa ni kitu gani, mimi nadhani ni kufahamu kama camera zime haribika kabla au baada ya tukio, kama ni baada ya tukio nina uhakika kuwa huyo sio jini ni mtu kabisa ambae anafahamu madhara ya camera hizo endapo zitafika mikononi mwako” nilimueleza insp, ambae aliitikia kwa kichwa kukubaliana na mimi, “sasa nitaanzia wapi unadhani” swali hilo lilonyesha wazi kuwa mzee huyu alianza kuamini kuwa mawazo yangu yana mchango mkubwa sana kwenye kazi yake.
Hapo nikajifanya nawaza kidogo, kama natafuta jibu ambalo tayari nilikuwa nalo, nilitumia kama nusu dakika, kisha nikajifanya nimepata wazo, “hivi hakuna vijana wa karibu ambao walikuwa wanafahamiana na marehemu Vuai huko mtaani kwake?” nilimuuliza insp nae akacheka kidogo, “unaona basi hata hilo wazo sikuwa nalo, yupo kijana ambae muda wa tukio alimpisha Vuai aingie na mwanamke na ndie wa kwanza kugundua kuwa Vuai ameuwawa, nafanya mpango wa haraka sana kumpata kijana huyo” alisema insp Aroub huku anajiandaa kuondoka pale tulipokuwepo, nilitamani kumuongezea wazo jingine la kumpata kijana mwingine wa Ussi, lakini nikasita kwa kuonekana ninafahamu mambo mengi kwa wakati mmoja.
Lakini nilimuona insp Aroub, kama vile amepata hamu ya kufanya kazi muda huo huo, “kijana naona tumeongea mengi, ila nahitaji kumpata yule kijana haraka sana, sitoweza kupeleka report dar es salaam pasipo kupata jibu la camera, hivyo chukuwa namba yangu ya simu, utanipigia kuona kama tunaweza kupata muda zaidi wa kupeana habari zitakazo patikana” alisema mzee Aroub, ambae sasa alionekana kuwa na haraka sana, akanitajia namba za simu, na mimi nikazihifadhi kwenye simu yangu, na mpaka namaliza kusave namba tayari Aroub alikuwa anatembea kwa mwendo wa haraka kuelekea kwenye jengo lao la polisi, nilitabasamu kidogo kwa kuona kuwa mzee huyu hakuwa anafahamu lolote juu ya kilichokuwa kinaendelea.
Nilitembea zangu taratibu kulifuata gari tulilokuja nalo, ambalo ndani yake alikuwepo Jessenia, ambae sasa niliweza kumuona ananitazama huku anatabasamu, tayari nilisha anza kuhisi njaa, maana hata nilipotazama muda kwenye simu yangu ilisha karibia saa tano za asubuhi, “we Eric, yule insp Aroub unafahamiana nae, maana naona mnaongea kirefu haswaa?” aliuliza Jessenia mara baada ya mimi kuingia ndani ya gari, “niliagizwa kwake, ndio akawa ananieleza kuwa, mjomba wako alikuja hapa kuna mtu ameuwawa jana usiku, vipi umeisikia hiyo?” nilimuuliza Jessenia, ili nijuwe kama na yeye alikuwa anajuwa kuhusu mfanya kazi wa kaka yake kuuwawa jana usiku, wakati huo nawasha gari, “hapana sijasikia, wamesema ameuliwa na nani?” aliuliza Jesse kwa mshangao na uoga, “ameuliwa na jini” nilimueleza Jessenia huku naondoa gari taratibu, “weeee! usiniambie, sasa mjomba yeye anahusiana nini?” aliuliza Jeseenia, wakati huo tunaingia barabara kuu nakushika uelekeo wa chake, “insp ameniambia kuwa alie uwawa ni mmoja kati ya wafanyakazi wa Ussi” nilimueleza Jessenia ambae alishtuka sana, “mamaaaaaa tayari mangeu amesha anza sasa, ndio maana mimi nakuambia tuondoke Eric tukaishi kwenu huko bara” alisema Jessenia kama alie pagawa, na mimi nikajifanya namshangaa, huku namuwekea mkono begani kwake, “kwani sisi inatuhusu nini Jesse, we tulia mimi nimalize kazi zangu nakuja kujitambulisha kwenu kisha tunaondoka zetu” nilimueleza jesse huku nampapasa begani, “yaani mimi nina wasi wasi na wewe na hivi mjomba ndio ameanza kukataa, yani nazidi kuchanganyikiwa kabisaaa” alisema Jessenia, kwa sauti fulani ambayo licha ya kuwa katika unyonge wa kujidekeza lakini ilikuwa tamu sana, hilo usiliwaze Jesse, cha msingi ni wewe kukubali kuolewa na mimi” nilimueleza hivyo huku natoa mkono wangu na kuongeza mwendo kuingia mjini chake chake, “Jesse, hapa chake kuna sehemu ya kupata supu” nilimuuliza Jessenia, “unasikia njaa eeh?” aliuliza Jessenia huku ananitazama “ndiyo sijala toka jana” nilimjibu kwa sauti ya msisitizo huku natazama kwenye eneo la mapaja yake, ambayo licha ya kuwa ndani ya gauni pana lakini niliweza kuona jinsi yalivyojaa na kutuna vyema, “kwani sasa tunaenda wapi si nyumbani kwako, kwanini usiende kula vitongoji?” aliuliza Jessenia na mimi kwa haraka haraka nikaona wazo lake halikuwa zuri, maana lazima nisinge kuta kitu ninacho hitaji kule vitongoji, “mh! sidhani kama itakuwa wazo zuri, maana kule wanamaliza mapema sana” nilimueleza Jessenia ambae tayari alikuwa amesha niondolea uvumilivu wa moyo na akili kwa rangi yake ya mdomo na wanja kwenye nyusi na kope zake za macho, na yeye akanielekeza mgahawa mmoja, uliopo njia ya markiti, kwa kuwa tulisha karibia chake chake, nilipunguza mwendo kidogo huku namtazama mschana huyu, ambae kiukweli siwezi kukuficha, mpaka hapo nilikuwa natamani kama ninge kuwa getoni nafanya kile ambacho nilimfanya jana, na leo nilipania kumfanyia vitu vingi ninavyo vijuwa, hakika sikutaka ajifunze kwa mwingine halafu anitukane wakiwa wanapeana dudu, maana kuna kisa kimoja nilipenda nikudokeze wakati natafuta maegesho hapa chake chake barabara ya marikiti maana ni finyu sana, je unajuwa ilikuwaje.… ITAENDELEA..
 
UNAONA UNAVYOHANGAIKA KUNUNUA BANDO KILA SIKU? WI-FI ROUTER ZA TIGO NDO KITU PEKEEE KINGEKUSAIDIA


Kua na wi-fi router kuna faida nyingi sana, kama unajiweza kidogo, jitahidi usikose kifaa hiki.


1. Ukiwa na wi-fi unaweza kukuza biashara yako. kwasababu wateja watapenda kuja ofisin kwako wakijua kuna wi-fi, pia wewe utakua huru kupost biashara zako mtandaoni ukiwa hauhofii kuishiwa bando.





2. Kuokoa gharama za bando. Ukweli ni kua bando za kawaida zinaumiza sana mana ukipiga hesabu ya gb 1 kwa 2100 kama kwa siku unatumia gb 1 basi kwa mwezi unatumia 63000. Zidisha kwa watu wote mliopo kwenye ofisi, taasisi au nyumbani kwenye familia yako na majirani, utakuta hela ni kubwa sana mnayotumia. Kukata hizo cost zote mngechukua wi-fi router ya tigo mana inaunganisha hadi watu 64, yani watu 64 wote mnatumia bando unlimited
Asanteh kwa elimu yako hila huku kwetu kenya tangu mwaka juzi tunatumia safaricom mifi-router.
 
KIFO CHA HAWARA (mkono wa jini)
SEHEMU YA HAMSINI NA MBILI
MTUNZI: Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA HAMSINI NA MOJA : uliopo njia ya markiti, kwa kuwa tulisha karibia chake chake, nilipunguza mwendo kidogo, huku namtazama mschana huyu, ambae kiukweli siwezi kukuficha, mpaka hapo nilikuwa natamani kama ninge kuwa getoni, nafanya kile ambacho nilimfanya jana, na leo nilipania kumfanyia vitu vingi ninavyo vijuwa, hakika sikutaka ajifunze kwa mwingine alafu anitukane wakiwa wanapeana dudu, maana kuna kisa kimoja nilipenda mnikudokeze wakati natafuta maegesho hapa chake chake barabara ya marikiti maana ni finyu sana, je unajuwa ilikuwaje. ……… ENDELEA…..
Kuna binti mmoja wa kipemba (jina sitoweza kulitaja, sababu sijaomba kibali cha kusimulia) ila anaishi kengeja huko huko pemba, alijaliwa kumiliki mwili mdogo mdogo na sura nzuri kweli kweli, japo alikuwa na miaka ishirini na mbili kwa kipindi hicho, lakini ungeweza kusema alikuwa na miaka kumi na nane, hakutokea kwenye familia ya kitajiri lakini alijaaliwa usafi na uzuri wa asili, mschana huyu mara baada ya kumaliza kidato cha sita alibahatika kupata mchumba na kuolewa nae, hakujali ufaulu wake wa daraja la tatu akatulia na mume wake kwa mwaka mmoja, kabla hajapata wazo la kwenda kusoma ili kujiendeleza kielimu na kusaidia familia yake iliyoongozwa na mume wake aliekuwa anaishi kwa kutegemea banda dogo la kuuza urojo, ndipo alipo anza kuomba kwa mume wake huyo ambae alimkatalia kata kata, hili nalo lilikuwa tatizo kubwa kwa wenzetu wa kisiwa hicho, hawakutaka wake zao wafanye kazi au kujiendeleza kielimu, hata kama ingekuwa na manufaa kwao, sijajuwa sasa hivi ipoje, mzee baba alitoa mashariti ya kuwa kama mke wake ataondoa mguu wake pemba kwenda kusoma, basi ajuwe kuwa talaka inahusika, hapo bidada akawa mpole na kuendelea na maisha ya ndoa.
Maisha yaliendelea, maisha yakiwa yanazidi kudidimia kwa kukosa vitu muhimu, mfano aliwahi kuishi akibadili nguo mbili tu za ndani, yaani akifua hii wakati anaenda kuoga basi angeifua aliyovaa na kuvaa nyingine ambayo angeifua kesho wakati wakuoga, ndipo mschana huyo alipoamua kuanza tena wazo lake la kumuomba kwenda kusoma, lakini mzee baba akasimamia msimamo wake ule ule, hakuna kusoma, kama vipi bidada achague kati ya kusoma au taryaka, bi dada ambae alikuwa anathamini ndoa na elimu, akatoa ushauri wa kwamba mume wake aoe mke wa pili, na pia muda wowote anaweza kumtembelea dar, na yeye atakuwa anaenda pemba kila likizo, na kwamba yeye kama yeye akimaliza chuo na kupata ajira serikalini, angehudumia familia yote, yaani mume bi mdogo na watoto wa bi mdogo endapo ange fanikiwa kuzaa, lakini hiyo haikusaidia lolote, jamaa akasimika hapo ndipo bidada alipoamua kukubali taraka, na bi dada akapewa taraka mbili na yeye kuondoka zake kuelekea dar es salaam kusoma chuo, pia mtanisamehe sitokitaja, maana kinaweza kutumika kama utambulisho kwa wale wanao mfahamu.
Naam maisha ya chuo yalikuwa mazuri kwake, upepo wa dar ukazidi kumng’arisha na kumfanya azidi kuwa mzuri, akichangia na uvaaji wake wa kistaarabu magauni marefu na hijab, huku vyakula vya bara vikineemesha na kuanza kufichua vile vilivyo vichika, kuna jambo naomba niweke sawa, ujuwe kwa wenzetu pemba,l chakula kigumu kuliko vyote ni wali, ambao ungeliwa mchana, tena mara moja moja, (ugali kuna watu hawaufahamu kabisa, kama jamaa yangu asivyo ifahamu biriyani) zaidi ya hapo ni chai mkate, au supu ya dagaa mchele, muhogo kwa samaki, au masheri sheri yaliyo ungwa kwa nazi, pia urojo na vyakula vingine laini, tofauti na bidada alipoingia dar na kukutana na ugali kila mchana, na ubwabwa kila jioni, vitu ambavyo mwanzo vilimpa shida lakini baadae alizoea na kufanya hips na makalio yake kuanza kuchomoza sehemu zake, na kuzidi kumpendesha na kumfanya awe mmoja kati ya waschana waliokuwa wanatajwa sana midomo mwa watu, japo wenzake waliponzwa na uzuri wao na kujikuta wakitumikisha vitumbua vyao kila kukicha, tofauti na bi dada wakipemba, ambae mpaka miaka miwili inakatika alikuwa hajaruhusu dudu ya mwanaume yeyote kupenya kitumbuani kwake, sio kwamba hakutamani au kuhitaji dudu, hapana bidada alikuwa na kiukali sana ya dudu, lakini kutokana na malezi aliyolelewa kule kwao aliweza kujihifadhi na kutunza heshima yake, japo alianza kusikia tetesi za kuwa mume wake anatoka na mwanamke mwingine na yupo mbioni kupeleka barua ya posa.
Lakini mwishoni mwa mwaka wa tatu ambao ni mwaka wa mwisho pale chuoni, pasipo kuona dalili za kurudiana na mume wake, ambae alikuwa katika pilika za kupeleka barua kwa mwanamke mwingine, ndipo bi dada akashindwa kuvumilia na kujikuta akijilegeza kwa kijana mmoja wa kimakonde, hawa jamaa sijui wana nini, maana jamaa baada ya kumnasa mtoto wa kipemba, na hivi alikuwa na uhakika kuwa yupo mwenyewe, dah! akamaliza ufundi, japo siku ya kwanza ilikuwa ni zaidi ya ushawishi ili wafanikishe zoezi.
Hadithi inasema kuwa, siku ya kwanza bi dada kuingia guest flani kule magomeni mapipa, ilikuwa ni mida ya saa mbili za usiku, walipanga watumie lisaa limoja tu, kisha kila mmoja aende kwake na ile wanaingia tu, bidada bila kuchelewa alisaula nguo zake na kulala chali, “fanya basi tuwahi kuondoka, kiza kisha ingia” alisema bi dada, huku anatanua miguu yake na kujaribu kumtazama kijana huyu toka umakondeni huko newala, ambae hakuonyesha kuwa na haraka yoyote, “usijali nitakupeleka mpaka kigamboni (alikokuwa anaishi bidada)” alijibu kijana wa kingoni, huku ana mshika mkono mschana yule na kumuinua toka kitandani, kisha wakaelekea bafuni ambako walioga kwa pamoja na kufanyiana usafi kila kona yenye kujificha ficha.
Baada ya hapo walirudi chumbani na kujibwaga kitandani, huku bidada kama kawaida yake akajilaza chali na kujiweka mkao wa kupokea muwa, akitarajia kuona mpenzi wake mpya akija juu yake na kulenga chombo ndani ya chombo, lakini akaja kushangaa kuona mwenzie anapelaka uso katikati ya mapaja yake mwanzo alidhania ananusa kama ni sehemu safi au laa, kwahilo alikuwa anajiamini, hakuwa na wasi wasi, ndio kwanza akatanua miguu, kutoa nafasi kwa kijana huyu, huku akiamini kuwa ni utaratibu wake au wao waliojiwekea huko kusini mwa Tanzania.
Lakini haikuwa hivyo, maana mara baada yakijana kusogeza uso karibu na papuchi, huku akitegemea kumuona kijana yule akiinuka toka kwa bibi na kupeleka dudu, baada yake akahisi ulimi wa kijana yule ukigusa mashavu ya kitumbua chake na toka chini, na kuanza kupaluza kuta za kitumbua chake upande wa ndani wa kitumbua, “weee bwana weee, khaaaa wanlamba lamba ka jibwa?” aliuliza bi dada kwa ile sauti ya kipemba, huku akijaribu kubana mapaja yake kumzuia kijana wetu, ilibakia kidogo kijana wangu aangue kicheko kule kitumbuani, lakini akaona ni vyema akiongeza ufundi ili bidada atulie, hapo adumbukiza kikunde mdomoni, na kuanza kumung’unya kama pipi sukari, kitu ambacho kilimfanya bidada akose ujasiri wa kubana mapaja na kujikuta akitanua mapaja kama anataka kujifungua, huku anakamata kichwa cha kijana wa kingoni na kukindamiza kitumbuani, huku akizungusha kiuno cha kimakonde, ambacho hata yeye bi dada hakujuwa wala kuelewa aliko jifunzia kiuno hicho, “haassss! wajuwa kunlamba weye, wanlamba kajibwa” yalimchomoka maneno bi dada wa kipemba, kwa lafundi yake ya kipemba, huku kiuno kikiendelea kuzungushwa, hapo kijana wetu akaona ni wakati wa kujaribu kama amefanikiwa.
Hivyo akasitisha kidogo, na kuinua uso wake toka kwenye kitumbua na kumtazama bidada usoni, ambae alikuwa amefumba macho huku mdomo ameulegeza, “vipi hupendi kulambwa?” aliuliza jamaa kwa sauti nzito ya taratibu, “we nlambe tu, nasikia uroda mwenzio” alisema bidada kwa lafudhi yake ile ile ya kipemba, huku anakandamiza kichwa cha kijana wetu, kukirudisha kwa bibi, ambako kijana wetu hakufanya ajizi, aliendelea kulamba lamba kama jibwa, akitumia muda mrefu sana na kufanya mtoto wa kipemba avunje dafu hewani, hata muda walipopeana dudu, bidada alionekana kufurahia sana, na kitu ambacho huwezi amini, bidada alighairi kabisa kurudi kigamboni, alilala pale Magomeni usiku kucha wakipeana dudu, kwa mitindo mbali mbali, huku kila wakati walipoanza tendo akiomba kulambwa kitumbua.
Mapenzi haya kuishia hapo, yaani bidada hakuweza kupitisa hata siku tatu kabla hajamtafuta kijana wetu toka kule kwa kila munu avena kwao, amfanyie kile ambacho alifanyiwa usiku wa kwanza kulala na kijana wetu, na wakati mwingine walifululiza siku kadhaa wakilala pamoja huku wakipeana dudu kisawa sawa, bidada akisahau kama yeye ni mke wa mtu ana anatalaka mbili, kwamba muda wowote anaweza kurudiana na mume wake, alikuja kukumbuka hilo, mara baada ya kumaliza chuo na kurudi pemba, ambako alifika kama mwanamke asie na mume, huku bahati ikiwa kwake baada ya kupatiwa kazi serikalini, akiwa ni mmoja wafanyakazi wa idara ya fedha, katika kiwanda fulani cha zao muhimu na maarufu pale kisiwani, huku kila mwanaume aliemuona bidada alikubali na kuvutiwa na muonekano mpya wa bidada, kitu ambacho kilisababisha salamu kuwa nyingi sana kwa bi dada, hata mume wake wa zamani hakubaki nyuma aliweza kuanza kupitia pale nyumbani kwa kina bidada, mara kwa mara akiwa na zawadi mbali mbali, ikiwa ni nazi au samaki, kama sio dagaa mchele, mihogo au masheri sheri, na embe bolibo, hakujari kama tayari alikuwa na mwanamke mwingine ambae alitarajia kumuoa….. ITAENDELEA
 
KIFO CHA HAWARA (mkono wa jini)
SEHEMU YA HAMSINI NA TATU
MTUNZI: Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA HAMSINI NA MBILI: akiwa ni mmoja wafanyakazi wa idara ya fedha, katika kiwanda fulani cha zao muhimu na maarufu pale kisiwani, huku kila mwanaume aliemuona bidada alikubali na kuvutiwa na muonekano mpya wa bidada, kitu ambacho kilisababisha salamu kuwa nyingi sana kwa bi dada, hata mume wake wa zamani hakubaki nyuma aliweza kuanza kupitia pale nyumbani kwa kina bidada, mara kwa mara akiwa na zawadi mbali mbali, ikiwa ni nazi au samaki, kama sio dagaa mchele, mihogo au masheri sheri, na embe bolibo, hakujari kama tayari alikuwa na mwanamke mwingine ambae alitarajia kumuoa….. ENDELEA NAYO
Hazikupita hata week mbili, kabla ugeni hauja fika nyumbani kwao bidada, ukitaka suluhu ya kufuta talaka mbili zilizo tolewa na mume wa bidada, ambae licha ya kuwa katika harakati za kuoa mke mwingine lakini alilazimika kughairi na kutaka kumrudia mke wake, baada ya wazee kusimamia swala hilo, bidada akakubali kurudi kwa mume wake, sasa unajuwa nini kilifuatia, ndicho hicho ambacho mimi sikutaka kinitokee, hata wewe kama una mchumba au mke usije ukaombea likukute, hebu nikueleze kwa kifupi.
Ilikuwa ni siku ya pili asubuhi, toka bidada arudi kwa mume wake, kiliitishwa kikao cha dharula, upande wa kike na wakiume, kila mmoja aliambiwa alete wawakilishi kwenye kikao, ambacho mume wa bidada alikuwa anasisitiza kuwa hawezi kuendelea tena na mke wake, na kwamba sasa anampa talaka, tena talaka ya tatu ambayo kwa sheria haruhusiwi kumuoa tena mpka aolewe na mume mwingne na amuache kwa hiyari yake, “kijana ni vyema ungekaa na kufikiria juu ya uamuzi huo taraka imeandikwa kuwa itatolewa, lakini sio jambo zuri” alisema mzee mmoja, ambae ni wa upande wa mume wa Bi dada, “jamani naomba mnielewe sina cha kufikiria, siwezi kuendelea kuishi na huyu mwanamke” alisema jamaa, akionyesha ni kweli hawezi kuendelea na bi dada, “basi utuambie tatizo nini, mpaka unafikia hatua ya talaka ya tatu” alisema mzee mwingine, lakini haikusaidia, “nilisema mimi huyu asiende huko bara, sasa mnaona?” aliuliza jamaa bila kufafanua tatizo nini, na mpaka uamuzi wa talaka una pitishwa na talaka zinatolewa, jamaa hakusema kilicho msibu, lakini najuwa una hamu ya kujuwa kilicho tokea katika usiku na kusababisha jamaa atoe talaka ya tatu kwa mke wake.
Ilikuwa hivi, Usiku ule wa kwanza wa wanandoa kurudiana, kila mmoja alikuwa na hamu na mwenzie, hivyo walipanda kitandani mapema sana, huku kila mmoja akiwa kama alivyo zaliwa, jamaa ndie alikuwa na hamu sana mke wake huyo, hasa baada ya kuuona ule mwili uliotuna sehemu za mapaja na makalio ya mke wake, ambae alipopanda kitandani alilala kitandani akiwa chali, na kutanua miguu yake ili kumkaribisha mume wake, ambae hakuhitaji kuambiwa kwa maneno, alipanda juu ya mke wake na kujiweka kati kati ya mapaja manene ya bidada, huku anakamata dudu yake na kuisogeza kwenye kitumbua na kuingia ndani, kisha akaanza kupiga nje ndani, mfano wa mtu anae twanga mpunga kwenye kinu huku bidada akiwa amelala kama gogo ana guna guna kwa lawama, kama kuna kitu kina kosewa katika upeanaji wa dudu, mwanzo mzee baba hakuelewa, yeye aliendelea kupiga nje ndani nakufanya dudu itembee ndani ya kitumbua mfano wa msumeno mkubwa juu ya gogo la mninga.
Tendo lile ambalo lilionekana kuto kumfurahisha bidada liliendelea kwa dakika tatu, ndipo na yeye bi dada akaonekana kuanza kuchezesha kiuno chake ili aonyesha kwamba ameanza kufurahia tendo, lakini tendo lile halikuendelea hata kwa sekunde thelathini, maana mzee baba akashusha watoto na kujibwaga pembeni ya mke wake akiwa hoi, “mke wangu siku hizi umekuwa mtamu” alisema jamaa huku anahema kama bata dume, lililotoka kundinya, “yaani umesha maliza” aliuliza bidada kwa sauti ya upole, huku moyoni akiwa hajaamini kilicho tokea, yaani yeye anaanza safari mwenzie amesha maliza, “sasa je unadhani kwa utamu huo nitasubiri nini?” alisema mzee baba huku akijiinua na kueleka uwani, na ile anatoka tu akakutana na mke wake mlangoni nae anaenda uwani, ambako alitumia kama dakika tano hivi, kisha akarudi na kumkuta mume wake akiwa anaanza kusinzia kutokana na uchovu wa kushusha watoto, “haya sasa na mimi unisaidie” alisema bidada huku analala chali na kutanua miguu, ukweli jamaa alishaangaa, kwanza alitazama kitumbua cha mke wake, kisha akamtazama usoni, akamuona anatabasamu kwa aibu, “mwenzio si nime maliza, nikusaidieje sasa?” aliuliza kwa hamaki na mshangao, “kwani hujui unanisaidiaje, wenzio bara wanailamba hii” kauli hiyo ilimshtua sana mzee baba, ambae mwanzo alidhania hajasikia vizuri, “eti unasema wanaifanyeje?” aliuliza kwa mshangao mzee baba, hapo bi dada alicheka kwa aibu ya kike, “wenzio wairamba hiyo kama tende, tena wanaimung’unya haswaaa kama pelemende, inakuwa burudani kabisa” kusikia hivyo mzee baba akainuka na kujifunga msuri, halafu akachukuwa simu na kutoka nje ya nyumba, akimuacha bidada anashangaa kilicho msibu mume wake alietoka nje huku sura ime mvimba kwa hasira, ambayo bi dada hakuitambua imetokana na nini.
Bidada alisubiri kwa muda mrefu pale kitandani, akitegemea kwamba anakuja kulambwa lambwa, lakini lilipita lisaa lizima pasipo kumuona mume wake akirudi ndani, aliendelea kumsubiri mpaka alipo pitiwa na usingizi, hakujuwa mume wake alirudi saa ngapi kitandani, ila alishtuka saa nane usiku na kumuona mume wake yupo macho anachezea simu yake, ni kama alikuwa anawasiliana na mtu kwa njia ya sms, hakuhitaji kumsumbua tena mume wake, japo alikuwa ametamani kulambwa kama jibwa, jibu la kwamba alikuwa anawasiliana na nani, alilipata asubuhi mara baada ya kuamka, hakumuona mume wake ila alikuta ujumbe kwenye simu yake kuwa wakutane nyumbani kwao bi dada, kwamba kuna kikao cha talaka nyumbani kwao, kisa na sababu ya taraka ikishindwa kutamkika mdomoni kwa mzee baba, “Eric unaweza kuegesha hapa chake hotel, maana hiyo sehemu ya kula ni hapo mbele tu” alisema Jessenia ambae anakatisha story yetu ya bi dada aliemwambia mzee baba kuwa wenzio bara wailamba lamba kama tende.
Naam eneo hili la Chake hotel upande wa pili wa barabara ya markiti kulikuwa na watu wengi sana waliokuwa kwenye maduka, na wengine wakipita barabarani wakichangia na magari na pikipiki, wakiingia au kutoka upande wa sokoni, na kutokana na ufinyu wa barabara ya markiti nili unga mkono wazo la Jessenia la kuegesha gari kwenye maegesho ya chake chake hotel, kisha nikazima gari na kujiandaa kushuka, lakini nilipomtazama Jessenia sikuona dalili ya kushuka toka kwenye gari, nadhani nae alijishtukia, “kwani na mie nashuka?” aliuliza Jessenia kwa lafudhi ya kipemba, huku anacheka kidogo, kicheko ambacho kilimfanya azidi kuwa mzuri na kunisababishia hamu ya kutenda zambi ya uzinifu, “kama upo tayari niende peke yangu sawa” nilisema kwa sauti ya kama nina mtahadharisha, kwamba ninaweza kutamaniwa na waschana wengine, “mh! twende wote” alisema Jessenia huku anajiweka sawa, “na mimi ndie nilie tangulia kushuka toka kwenye gari, na kuanza kutembea kuzunguka gari, kuelekea upande wa mlango wa kushoto wa mbele kule alikokaa Jessenia.
Lakini wakati nikiwa usawa wa bonet la gari, nikamuona jamaa mmoja anaegesha pikipiki yake aina ya Vesper, pembeni kidogo ya gari letu, kilichoni vutia kwa jamaa huyu, ambae muonekano wake ni wa mtu wenye asili ya bara, kuna kitu ambacho sikumbuki kama nimekueleza, ila wacha nikueleze tena, ni kwamba, nilijifunza kuwatambua watu wenye asili ya kisiwa hiki, ni kwamba walikuwa na vichogo mfuto (flat) sio kama vichogo vya watu toka sehemu nyingine za Tanzania bara, ambao tulijaliwa vichogo vya aina mbali mbali, na kufanya vichogo vyetu viwe kama utambulisho, maana baadhi ya wenyeji wa kisiwa hiki hutuita machogo, hivyo basi huyu jamaa licha ya uvaaji wake wa suruali fupi iliyo kwamia chini kidogo ya magoti, pia alikuwa amevaa shat refu lililofika usawa wa mapaja, chini alivalia sendo, kichwani akimaliza kwa baraghashia chakavu kidogo, kwa haraka ungesema ni Mpemba, lakini huyu jamaa niliweza kumtambua kwa haraka kutoka na kichwa chake, kitendo chake cha kunitazama kwa macho ya udadisi, na kuyakwepesha mara tu nilipomtazama na macho yetu kukutana, akazuga anaitazama Vesper yake na kuwa kama anaikagua kagua, sikumjali sana, nilitembea taratibu mpaka kwenye mlango wa kushoto wa gari, kisha nikaufungua mlango na kumtazama Jessenia, ambae ni kama alikuwa ananisubiri ili aniambie kitu fulani, maana licha ya kunitazama nilimuona akitabasamu pia, “Eric, unaweza kuniruhusu nishuke bila niqab” aliuliza Jessenia, huku ananitazama usoni kwa sura yake ya tabasamu.
Ukweli nililipenda sana swali au ombi la Jessenia, maana ukiachilia mpango wangu wa kujionyesha hadharani nikiwa na Jessenia, pia nilijisikia raha kuongozana na mwanamke mzuri kama huyu, lakini nilijifanya kama nampa changuo, “siwezi kukukatalia kile ambacho unakipenda Jesse” nilimueleza kwa sauti tulivu, na hapo Jessenia ambae tabasamu alikukauka usoni mwake, alinipa mkono kama kuomba usaidizi wa kushuka toka kwenye gari, na mimi nikamshika na kumpa usaidizi huo, na alipotoka nikaufunga mlango, lakini wakati naulock mlango, nikakumbuka kumtazama yule jamaa mwenye ile vesper, na kwa bahati nikakutana nae macho kwa macho akiwa ananitazama, hapo akakwepesha macho yake ghafla, na kutoa simu mfukoni. ….. ITAENDELEA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom