CCM ni sawa na kanisa katoliki duniani namna lilivyojiwekea mizizi na kuwa na waumini wengi dunia kushinda madhehebu mengine yote!
Kuna wahumbiri mbalimbali wanajitokeza na huwa wana vuma sana ila baada ya muda huwa wanapotea na makanisa yao yanageuka kuwa magofu (white elephant) wakati huo kanisa katoliki linazidi kuimalika na waumini wake wanazidi kuongezeka! Hii inatokana na misingi ya mafundisho yao yanayoendana na uhalisia wake!
Hivyo hivyo kwa CCM ndivyo inavyozidi kuimalika kutokana na chama hicho kuamua kusimamia misingi yake ambao vyama vingine vinazidi kuporomoka kutokana na ubabaishaji na utapeli uliojifisha ndani yake!
nimegundua kitu kuna watu hawapendi ccm ifanye mambo mazuri kwa watanzania raha yao ni kusikia ccm inafanya vibaya! ccm imejisahihisha na watanzania wengi wanaendelea kuiunga mkono! mshindwe wote mnaoichulia ccm!
ukome tena ukome kabisa kulinganisha KANISA KATORIKI na chama chenu cha mafisadi, CCM hamfai kabisa ktk jamii ya watanzania wa sasa wanaoteseka na serikali LEGELEGE inayotokana na chama chenu cha mbogamboga, kafie mbali kabisa!
Mambo ya kanisa yanaingiaje tena kwenye siasa hebu usichanganye dini na siasa.
Usirudie kulinganisha uozo uliojaa ufisadi na uonevu wakinyama usiokuwa na aya mbele za mwanadam na Mungu Baba kwa ujumla na kuulinganisha na maswala ya kiroho hata km ulikuwa na nia nzuri usirudie unaweza ukajikuta unatenda dhambi kwa kutokujua sasa nimekuondolea huo ujinga be aware , kanisa ni watu watakatifu nasio ujinga wa watu na mbinu zao za ulafi ulinganishe na imani za watu. Usirudie pia uchambuzi wako uwe na mipaka.
Kumbukeni mwisho wa siku...kichwa kimoja, kura moja...unlike hapa JF kichwa kimoja kinaweza kuwa na ID zaidi ya 10 (mkakati wa Chadema) ili kuonyesha jamii kuwa mmeteka majority ya watanzania. Karibu October...Kichwa kimoja, kura moja!
Kitabu cha maombolezo kiko lumumba tukapigane vikumbo ku sign?Umezaliwa na makadirio ya maisha ya Mtz ndio yanayoonyesha umefikia mwisho wa uhai wako ,tulikupenda ila bwana amekupenda zaidi na hatutasahau wala kuwacha kukumbuka ,uzee wako umeiwachia Tanzania maafa ya aina yake na kupigiwa mfano duniani ,ajali zinazowamaliza waTz zimekuwa zikikusindikiza bila ya wewe mwenyewe kujua ,CCM hakuna lisilo na mwisho ,dalili la jina lako CCM (Chukua Chako Mapema) limeshika kasi kwa viongozi walioshika bendera za chama chako wakizidi kuwahi ,wakijua wasipowahi leo kaburini hakuna kitu.
Ondoka kwa salama ,ingawa viashiria vinaonyesha dalili ya kifo chako ,yaani utakufa kwa kupapatika vibaya sana na kukuru kakara zitashinda kishindo cha mwendawazimu wa malaria ,ila vyombo vya dola havitakaa mbali nawe ili usisababishe maafa makubwa ,na vitakuwahi kwa kukufunga kamba za miguu na mikono na hata madaktari watakudunga sindano za kukuvunja nguvu ili ufariki kwa taratibu sana,
Poleni wafiwa,