Kifo cha CCM kimetimia

Kifo cha CCM kimetimia

Uzi umepitwa na Wakati huu unasema chadema kuchukua nchi wakati sasa ni UKAWA kuchukua nchi!!!
 
Ikiwa ni muda mrefu umepita,tokea watanzania tupate uhuru, tukiwa chini ya utawala wa TANU, hatimaye CCM bado mabadiliko makubwa hayajafanyika kuonesha malengo ya kulipatia taifa letu maendeleo. Awamu ya kwanza ilianza vyema, lakini mawazo ya Mwalimu JK Nyerere yalipoanza kukiukwa katika awamu ya pili, ya tatu na hatimaye ya nne ndio sasa watanzania tunaona tuko katika jehanamu iliyojaa chuki,njama,ufisadi, na umaskini uliokithiri.

Ni ukweli usiofichika CCCM na uongozi wake wote imeshindwa kutatua matatizo yanayotukabili, na niseme imekuwa ikituongezea tabu kila kukicha. Nianze na MGOMO WA MADAKTARI, AJALI ZA ZANZIBAR, SUALA LA MUUNGANO,KILIMO n.k vyote vinatabiri kifo cha CCM, kwa kuzingatia kuongezeka kwa machafuko nchini.

Watanzania walio wengi wenye akili timamu na hekima nadhani tayari wameshajiandaa kufanya mabadiliko makubwa 2015 ,na namini itakuwa ndio mwisho wa utawala wa kidhalimuna dhaifu wa CCM!

NA HICHO NDICHO KIFO CHA CCM 2015!

-------------------------------

Wapunzike kwa amani
 
Popote nitapo piga kura diwan cdm, mbunge cdm, raisi cdm kuna mwingine jaman nimemsahau hata kama cjawai enda kwenye campain si discus over hakuna ccm wakushindana na mtu yeyote hilo ni dekio lililo sha tuniwa kwenye sakafu mbovu
 
Habari wapendwa wangu? Nipo ziarani huku kijijini kwetu, kwa kweli hali niliyokutana nayo huku inasikitisha sana! Familia nyingi mlo ni taabu kweli kweli, watu wana hangaika sana, maisha magumu mno kwao, kwa kifupi wamekata tamaa kabisa ya haya maisha.

Kilichonisikitisha zaidi nimekutana na baadhi ya wastaafu, maisha yamewapiga vibaya mno. Wananiambia huu ni mwezi wa sita tangu wamestaafu, lakini mafao yao hayaeleweki yatatoka lini! Jamani CCM mmefikia hatua ya kudhurumu Wazee? Mnafikiri hawa watu wanaishije? Kwanini wasipate pesa zao kwa wakati?

Mwigulu badala ya kuhangaikia kwenda Ikulu, ungepigania hili kwanza. Fanya juu chini hawa wastaafu wapate pesa zao kwa wakati, unafikiri wanaishije na hawana mishahara tena? Wewe unaweza kuishi zaidi ya mwezi bila kipato chochote?

Wamenihakikishia walifuata taratibu zote, ikiwa ni pamoja na kuwasilisha nyaraka zao zote kwenye ofisi za PSPF, lakini hadi leo mambo hayaeleweki tu!

Mkitaka ahueni ya maisha ya kipindi cha miaka 10 ijayo, msiichague kabisa CCM ndugu zanguni, ni waharibifu sana!!
 
Nashangaa sana, ina maana Mwigulu ameshindwa kabisa kumaliza hili?
 
Back
Top Bottom