Kifo cha CCM kimetimia

Kifo cha CCM kimetimia

Utasubiri sana tu!

Hivyo ndivyo huwa mnajidanganya wauza madawa ya kulevya nyie!! mwisho wenu utakuwa mbaya kuliko wa ghadafi, Sadam Hussein au hata HITLER.Kumbukeni hakuna marefu yasiyo na mwisho.mpende msipende mwisho wenu umekaribia. tunacho fanya sasa ni kuweka kumbukumbu sawa nani wanahusika katika kuliangamiza Taifa hili kiuchumi, kisiasa na kijamii.
 
Hakuna cha kuingusha CCM miaka ya hivi karibuni. Chama cha mapinduzi bado kiko imara!
 
Kama wamejifunza au hawajajifunza pale Serena au Blue peal basi ni viwavi.
 
dalili za mvua ni mawingu, nimeangalia mjadala wa jana kweli niliwahurumia sana wajumbe wa ccm, nidhahiri kwamba wananchi wengi wako nyuma ya ukawa, nilishangaa juzi kumuona Zitto akiwa pia upande wa UKAWA ktk kipindi cha asbh Star TV aliposema UKAWA sio wajinga kususia bmk
 
Katika masuala kama haya historia ina nafasi yake pia. Hakuna dola yoyote duniani iliyowahi kutawala milele. Angalia dola kama za Kirumi, Babeli, Sulemani, Hitler, Mussolin, Soviet Union, Napoleon, nk; zilikuwa na nguvu nyingi, lakini ziko wapi leo! Unadhani Marekani unayoiona leo itakuwa juu ya dunia milele? Mfano wa dola iliyotawala milele uko wapi?

Kwa hiyo suala la kuanguka CCM kama ilivyo leo halielekei kuegemea sana Chadema, Ukawa, kura za wananchi, nk; CCM ni zaidi ya hapo. CCM itahukumiwa na wakati kama walivyohukumiwa wababe wenzake waliotangulia.
 
Hadi sasa, UKAWA ni muungano wa wadau wanaotaka bunge la katiba lijadili rasimu ya katiba iliyoandaliwa na tume ya jaji warioba. Na si kupenyeza rasimu isiyokuwa na utaalamu wowote. Hii ni hatua muhimu katika maandalizi ya katiba mpya.

Sasa wewe unasemaje katika haya. Rasimu ya Jaji warioba ijadiliwe na kuboreshwa ama iachwe kando? Naomba jibu bila jazba wala matusi tafadhali.


mtasubir sana na UKAWA wenu
 
Nakuunga mkono 100%. Mimi nilikuwepo kwenye mdahalo wa leo pale Blue Pearl Ubungo kimsingi hali ilikuwa tete sana kwa wanaccm. Nilichoshuhudia ni kwamba the majority ya waliohudhuria hawakutaka kbs kusikia chochote kinachojadiriwa nje ya Rasimu ya pili (maoni ya wananchi) yaani km vile serikali mbili. Ndiyo maana wanaccm wengI waliposoma upepo huo waliamua kuficha utambulisho wao pamoja na kutochangia kbs.
Ni kweli mkuu mwigulu alikuwapo akakauka.
 
Hata KANU bado WaPo imara mpaka Leo

Acha kufananisha kifo na usingizi. Upinzani wa Tanzania bado hauko imara kama ule wa jirani zetu ulioiondosha KANU.
Watanzania walio wengi bado wana imani kubwa na CCM.
 
Acha kufananisha kifo na usingizi. Upinzani wa Tanzania bado hauko imara kama ule wa jirani zetu ulioiondosha KANU.
Watanzania walio wengi bado wana imani kubwa na CCM.
Endelea kujiaminisha hivyo kama hao wakuu wa chama chenu wanavyojiaminisha. Upepo wa kisiasa kwa sasa unavuma kivingine kabisa. Hasa hili suala la katiba linaweza kuwanyongea mbali kabisa. Nilitegemea mdau kama wewe ungekua mstari wa mbele kuwashauri wakuu wa chama chenu kupima upepo unavyobadirika lakini matokeo yake na wewe unapotezea kama wao. Au mkuu ushagua pa kuahamia?
 
iangushwe na UKAWA wanaozomea???
hakuna mwananchi anaetaka fujo
 
Acha kufananisha kifo na usingizi. Upinzani wa Tanzania bado hauko imara kama ule wa jirani zetu ulioiondosha KANU.
Watanzania walio wengi bado wana imani kubwa na CCM.

Msalani hivi uwa unafikiria kabla ya kujibu au uwa unakurupuka tu?Hivi nani anayefanya upinzania wa Tanzania usiwe imara?
 
Msalani hivi uwa unafikiria kabla ya kujibu au uwa unakurupuka tu?Hivi nani anayefanya upinzania wa Tanzania usiwe imara?

Wapinzani wenyewe wameshindwa kujiimarisha kwa sababu ya tabia zao za ulafi, ubinafsi, ukabila na udini.
 
Wapinzani wenyewe wameshindwa kujiimarisha kwa sababu ya tabia zao za ulafi, ubinafsi, ukabila na udini.

Utakuwa siyo Muungwana usipo kitaja chama chako CCM ambacho kila uchwao wapo busy kuwarubuni wapinzania ili waendelee kutawala siyo kwamba ccm ni bora
 
Back
Top Bottom