Kifo cha CCM kimetimia

Kifo cha CCM kimetimia

Wewe ni maiti msukule,monchwari ni chadema ,dr.wa monchwari ni katibu mkuu wako.
 
Malumbano na minyukano yanayoendelea ndani ya ccm ni ishara tosha kuwa ccm mwaka 2015 itakuwa chama cha upinzani. Kwanza dharau kubwa iliyoonyeshwa na mh kikwete kwa kudharau viongozi wa chama chake kuhusu mawaziri mizigo. Pili mbio za kupata mgombea urais itakuwa hatari sana kwani kuna mh Lowasa, Benard Membe, Samwel Sitta, na Asharose Migiro. Kwa jinsi inavyo jionyesha mbio za kugombea urais zitakuwa na uhasama mkubw kiasi kwamba atakayeshinda hataungwa mkono na wale walioshindwa. Na hapo ndipo itakapo pelekea ccm kwenda vipande vipande na mgawanyiko huo utakuwa mtaji kwa wapinzani. Fikiria kama El akipata fursa ya kupeperusha bendera ya ccm, je Membe, Sitta, Mwakyembe, na makundi yao watakubali kumuunga mkono?. Kwa muonekano Lowasa amechanja mbuga mbali sana na kuwaacha wenzake kwa mbali. Hii inadhihirisha kabisa kuwa lowasa atashinda kupitia ccm lakini akashindwa kupitia uchaguzi mkuu kwani hatapata sapoti kupitia mahasimu wake wa kisiasa wenye ushawishi mkubwa kwenye kanda zao. Hivyo ndivyo chama cha mapinduzi kitakavyo poteza maisha 2015.
 
Acha utoto....chama ni taasisi kuna wakati tofauti zinawekwa kando ili kufikia lengo. OK?
 
Acha utoto....chama ni taasisi kuna wakati tofauti zinawekwa kando ili kufikia lengo. OK?
yaani kama ni utoto wewe ndo umezaliwa yaani chama kimejaa uchafu wa kila aina ufisadi, ujangili wa meno ya tembo, uuzaji wa madawa ya kulevya, utesaji, mawaziri mizigo na uchafu mwingi tu hata mkiweka tofauti pembeni ni nani atawachagua????
 
Umemsahau william ngeleja,ambaye ameshaanza kujipitisha ukanda wa kigoma.

Mf:alishaenda kibondo na kasulu kwa kutuma wajumbe wake.
 
kinachonisikitisha nu baba wa taifa mwl julius kambarage Nyerere kufa na chama cha mapinduzi ccm.hili linadhihirishwa na mwenendo mzima wa ccm leo na viongozi wake.
mfano kwa sasa kila mtu ni msemaji wa chama,viongizi wanapingana ktk kauli,maamuzi hayasimamiwi.
je nyerere alifanya hivi kwa madhumuni gani!
 
Wandugu; Kwa mtazamo wangu mie naona ni WAKATI ndiyo unaocheza role hii!! yaani kwa vizazi vya sasa(vipya) mambo kama haya ni kawaida.... hakuna sehemu SIASA moja iliyodumu forever!! Mfano Waalimu wa zamani tofauti na waalimu wa leo.... Uwajibikaji wa zamani ni tofauti na uwajibikaji wa sasa/leo, nk. Zamani familya moja ililazimika kutumia simu moja, Lakini sasa kila mwana familiya ana simu yake binafsi........ na uhuru wake bila kungojea amri ya kimila au wazee.
 
Najaribu kumfananisha JK Nyerere na mtu ambaye anaanzisha shule yake inakuwa na mafanikio, ktk nidhamu na ufaulu wakati yeye akiwa kiongozi ghafla anapoondoka shule ile inafurunda na kushindwa kufaulisha kijana hata mmoja kwa muda wote shule ile inakumbwa na kshfa za walimu kuiba mali za shule na hata wanafunzi wanageuka kuwa wavuta bangi nk.

kinachonisikitisha nu baba wa taifa mwl julius kambarage Nyerere kufa na chama cha mapinduzi ccm.hili linadhihirishwa na mwenendo mzima wa ccm leo na viongozi wake.
mfano kwa sasa kila mtu ni msemaji wa chama,viongizi wanapingana ktk kauli,maamuzi hayasimamiwi.
je nyerere alifanya hivi kwa madhumuni gani!
 
Chama cha mapinduzi kimeendelea kupoteza mvuto wake kutokana na sababu mbalimbali kubwa likiwa Ni hali ngumu ya maisha inayozidi kuwakumba watanzania huku vigogo wakizidi kujineemesha na mema ya nchi.

1. Elimu inaporomoka kila kukicha huku watoto wa vigogo wakisoma ulaya na marekani
2. Kilimo kinaporomoka huku vigogo wizara ya kilimo wakila viyoyozi maofisini
3. Maambukizi ya HIV yanaongezeka huku wizara ya afya ikiwekeza kwenye semina na warsha
4. Wajawazito wanalala na kujifungulia sakafuni huku vigogo wakienda kutibu mafua marekani, ujerumani na uingereza
5. Mateja wanaongezeka huku watoto wa vigogo wakifanya biashara ya sembe
6. Ujambazi na mauaji ya raia yanaongezeka huku rais akiwapandisha vyeo maafisa wa polisi
7. Wawekezaji kwenye gesi wanaongezeka huku mgao wa umeme nao ukiongezeka
8. Upanuzi wa barabara unafanyika huku foleni zinaongeka
9. Unywaji gongo unapigwa marufuku huku walevi wanaongezeka
10. Waziri anapewa wizara nyeti huku akiwa hana uzoefu wa kutosha
 
...loh chakavu kimeshakuwa maiti r.i.p ccm,hatukukupenda na kifo chako ni majibu ya maombi yetu...
 
Back
Top Bottom