Kifo cha CCM kimetimia

Kifo cha CCM kimetimia

bado hujaeleweka. Ni juzi tu mlisema kuwa ccm haichukui maamuzi magumu. Leo mnakuja na story ya kuwazuia baadhi ya watu wao kugombea uongozi
 
Kutokana na yanayo endelea kutokea ndani ya chama cha mapinduzi yanaonyesha chama kinapumulia mashine chukulia ya fuatayo kuzuiwa kugombea uongozi kwa baadhi ya makata wake kwa kipindi cha mwaka mmoja na hii hoja ya kutaka kumpata mgombea mapema bila kufuata katiba ya chama sio dalili ya kukizika chama?

Dada yangu ni yepi yanayo endelea ndani ya CCM?
Kikwete kasema wanaCCM wasiwe wanyonge!
 
CCM ishakufa siku nyingi - tunachokisuburi watanzania ni kifo rasmi pale Dodoma wakati wa nominations za candidates wa URAIS kupitia CCM.

So far mtifuano huu wote mnaushuhudiia, watu tayari wameshalimwa kadi za njano wasijihusishe na mambo yoyote ya kimtandano, kitu ambacho kimetabiriwa na wachambuzi wa mambo ya kisaisa kwamba ni kujichimbia kaburi kwa chama hiki kikonge kilichotawala nchi hii miaka nenda rudi.

Tatazo lililopo ndani ya chama ni ile nidhamu ya woga iliyojengeka ndani ya chama hiki tangu enzi za mwalimu sasa imekwisha - tunausuburi mtifuano huu kwa hamu kuu.
 
CCM haiwezi kusimama tena. Hata kuwawajibisha hawa akina Lowassa ni kuiga toka CDM japo bado hawajafikia viwango vya CDM hata robo tu.
 
CCM ishakufa siku nyingi - tunachokisuburi watanzania ni kifo rasmi pale Dodoma wakati wa nominations za candidates wa URAIS kupitia CCM.

So far mtifuano huu wote mnaushuhudiia, watu tayari wameshalimwa kadi za njano wasijihusishe na mambo yoyote ya kimtandano, kitu ambacho kimetabiriwa na wachambuzi wa mambo ya kisaisa kwamba ni kujichimbia kaburi kwa chama hiki kikonge kilichotawala nchi hii miaka nenda rudi.

Tatazo lililopo ndani ya chama ni ile nidhamu ya woga iliyojengeka ndani ya chama hiki tangu enzi za mwalimu sasa imekwisha - tunausuburi mtifuano huu kwa hamu kuu.

chadema bana! Huku wakifanya jitihada kumfukuza Zitto kwa kuonesha nia ya kugombea nafasi ya mwenyekiti wa chama, wanailaumu ccm kwa kuwachukulia hatua baadhi ya makada wao wanaokiuka kanuni za chama
 
CCM haiwezi kusimama tena. Hata kuwawajibisha hawa akina Lowassa ni kuiga toka CDM japo bado hawajafikia viwango vya CDM hata robo tu.

mkuu, kwako yale matokeo ya chopa tatu kata tatu unayachukuliaje? Pia kumbuka maneno ya kitila kuwa ccm inaimarika, chadema inasinyaa. Nini tafsiri yake?
 
nasema kweli ccm wakimpitisha sitta watashinda,wapinzani wengi wanampenda sitta na huyo mzee hana makuu,anafaa kuiongoza nchi na kuipa hathi yake.
 
Ah! Kumbe ni ndoto za mchana za Slaa! Hayo ni mawazo potofu ya tamaa za fisi, anapoona mkono wa binaadamu unatembea kwa kurembua, anangoja ukatike autake! Mtangoja saana na kumbe kinachokufa ni chagadema! R.I.P chagadema!
 
chadema bana! Huku wakifanya jitihada kumfukuza Zitto kwa kuonesha nia ya kugombea nafasi ya mwenyekiti wa chama, wanailaumu ccm kwa kuwachukulia hatua baadhi ya makada wao wanaokiuka kanuni za chama
Bwana Songoro wewe jaribu kujirithisha mashamba ya baba yako mzazi akiwa hai na tena bila kufuata taratibu za kifamilia - kitakachokupata njoo hapa utoe ushuhuda.
 
Mzimu wa posho walitesa Bunge la Katiba

Siku mbili baada ya kuanza kwa Bunge hilo, baadhi ya wajumbe wametaka waongewe posho kwa maelezo kuwa kiasi wanachopewa sasa cha Sh300,000 kwa siku hakiwatoshi kutokana na kupanda kwa gharama za maisha Dodoma.
 
mkuu, kwako yale matokeo ya chopa tatu kata tatu unayachukuliaje? Pia kumbuka maneno ya kitila kuwa ccm inaimarika, chadema inasinyaa. Nini tafsiri yake?

Kuwa specific kada wa magamba, sasa wewe mategemeo yako makuu ulitaka Chadema ichukue hata kata za CCm? Hata hivyo angalia mazingira waliyopambana nayo CDM katika uchaguzi huo. Watu wameumizwa wengine Viongozi kusotea ndani bila sababu yoyote bali njama za ccm ishinde kupitie Policcm.
 
HILI NI BUNGE LA POSHO MPYA AU BUNGE LA KATIBA MPYA ?
Kwa vyovyote na kwa hali yeyote ile sikubaliani kabisa kuwa eti posho katika bunge la katiba ziongezwe.Ni aibu kwa mbunge yeyote aliyeteuliwa au aliyepo bungeni kusimama na kutoa hoja isiyo ya msingi kama hii. Hoja hii imelenga nini hasa? Ikiwa mjumbe mmoja analipwa laki tatu [ Tshz 300,000/=] kama posho kwa siku moja, unataka nini zaidi hapo? Mtanzania wa chini ambaye anajaribu kuweka imani katika bunge hili kwamba katiba aminifu itapatikana hapa, je aliamini vipi tena bunge hili ikiwa limegeuza malengo toka katiba aminifu au mpya kwenda posho mpya? Kila mwanadamu ana mahitaji lakini kuyapata mahitaji hayo inategemea na kipato chake kwa siku. Ikiwa ewe mjumbe unaingiza sh. 300,000 kwa siku na unaishi TANZANIA, je haitoshi wewe kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa hilo? Kama wewe wataka zaidi ya hapo na upo bungeni mpaka sasa, hakika hiyo ni DHAMBI na unapaswa kutubu kwa hilo.
Najua na natambua wapo wajumbe wa bunge la katiba ambao kimsingi na kiuwazi wameenda kwa nia moja tu ya kutetea yale maoni ya wananchi na si kitu kingine katika kuhakikisha katiba aminifu inapatikana niseme tu mchango wao na kazi yao inatambulika na itakumbukwa katika taifa hili. Lakini BAADHI ambao wamekosa utu, ambao wamekosa heshima na adabu hakika jamii itawaadabisha katika hili. Ni maisha gani magumu zaidi yaliyopo DODOMA hata posho hiyo isimtoshe mbunge? Ukiachilia mbali malipo mengine? Ni mbunge yupi au nani aliyeteuliwa na raisi ambaye hali yakeni kama za watanzania wengi masikini hapa nchini? Ni kwa sababu gani mtu kama huyo ambaye ameenda kuchuma pesa anastahiki kuwepo bungeni hadi sasa? Hakika ni hoja dhulumishi, hafifu na iliyokosa utu iliyoweza kutolewa katika kipindi hiki ambacho tegemeo kubwa la wengi ni katiba mpya na katiba aminifu kupatikana.
Siku zote nimekuwa nikiamini katika UTU, HAKI NA USAWA. Lakin utakubaliana name kuwa nchi hii imefika wakati ipate kiongozi ambaye ni zaidi ya hata alivyokuwa GADAFFI[DICTATOR]. Kwa kuwa wapo baadhi ya viongozi mfano wabunge wanaodai posho kama hizi, wananchi tungenufaika na viongozi wa mabavu kama huyu. Ifike mahali tupate mtu atakayekemea, na kuchukua hatua stahiki mara moja pindi masuala ya ajabu na aibu yanapotokea katika taifa letu. Wapo watakaosema ni ukiukaji wa haki za binadamu kutumia nguvu katika hili lakini niseme tu kila kitu kina faida na hasara na pindi faida inapoonekana basin a kitumiwe kwa manufaa ya taifa. Zimekuwepo shutuma nyingi za UCHOCHEZI kwa baadhi ya viongozi , Lakini niseme tu huu ndio uchochezi wa wazi kabisa kuwahi kufanyika. Kwa nini nasema hivyo ni kwa sababu kwa hoja kama hii, kwanza wananchi watagawanyika, wajumbe watagawanyika, katiba itagawanyika, na hatimaye taifa litagawanyika kwani wapo watu wanaosimama katika haki na kweli na wapo wale wanyonyaji na wakandamizaji wa haki ambao mfano mzuri ni hao watakaokubali POSHO ZIONGEZWE.
Mwisho niseme tu “HAKUNA HAKI PASIPO NA HAKI” RAISI litazame hili kwa makini na ufanye maamuzi kwa manufaa ya wengi kwani wapo wengi waliokwisha tenda MAOVU NA MABAYA mengi sana kwa kuwakandamiza wananchi lakini kwa kutenda HAKI kwa siku za mwisho wao walilinda heshima yao na kukumbukwa japo kwa HAKI ya siku moja katika muda wa MADARAKA YAO.

“BUNGE LA KATIBA LISIWE SEHEMU YA KUCHUMIA MALI NA UMAARUFU”
 
nadhani tokea mwaka 2010 mpaka sasa kila mtanzania aliyepima hali ya siasa kwa umakini atakuwa ana jibu la TANZANIA ijayo siku za usoni
 
Demokrasia ni mhimu katika nchi yoyote hapa duniani, Lakini kama nchi inafinyanga Demokrasia hiyo sio nchi hata kidogo bali ni kundi linalojiita nchi .

Nasema ivyo kwa kuwa ccm wanazani watabakia madarakain milele , Hawapon hata chembe kwa kizazi hiki cha shule walizoleta ambazo hazina walimu , shule ambazo hazina majengo wala nyumba za kutosha za walimu. Ccm ni Bomu ambalo tunapaswa kuliondoa haraka sana
 
Kombe alikwenda Malawi Mkuu na ndo nadhani akachuklua jina la huyo presida na kuibatiza shule yake
 
Komba alikwenda Malawi Mkuu na ndo nadhani akachuklua jina la huyo presida na kuibatiza shule yake
 
Back
Top Bottom