Kifo cha CCM kimetimia

Kifo cha CCM kimetimia

Hali inasikitisha kwamba kila unakokwenda leo ndani nchi yetu, CCM inaonekana kama Chama Cha Mafisi. Wananchi wanafika hatua ya kumwambia Bosi Wangu Edo kwamba, asaidie kupinga ufisadi ili angalau wananchi wapate auheni ya maisha. Viongozi wa Chama na Ndani ya Serikali ya CCM wanafananishwa na na Ukoo wa Fisi ambao wanakula kila kitu hadi mzoga ilimradi ni nyama.

Viongozi wetu ndani ya CCM wanatafuna kila kitu, yaani hadi kutengeneza madawa ya kulevya ni CCM, ufisadi ni CCM, uonevu ni CCM,mauji ya tembo ni viongozi wa CCM. utoroshaji wa wanyama hai ni CCM. CCM tumekuwa janga. Mwarobaini ya mafisi haya ni Jembe Edward Lowasa. Kiongozi anayechukia ufisadi na mchapa kazi
 
samaki mmoja akioza tenga zima limeoza hakuna wa kutetewa wala kupona!!!
 
Mkuu umefanya reasech?

Ndio nimefanya research kaka. Chama kinapewa majina ya kila aina. Chama cha Majambasi, Chama Cha Wauza Sembe, Chama Cha Wachina, Chama Cha Mafisi....Aibu tupu inabidi tujipange....

Mkombozi wa CCM ni Lowassa Tu !
 
Dawa ya chama kilicho choka ni kupumzika. Nakishauri hicho chama cha ma....(majina mengi) kijikongoje kisifie njiani bado mwendo wa miezi 25 ya safari ili chama kingine kikipokee.
 
CCM wameamua wao wenyewe kutuachia ikulu yetu baada ya kuipoka kwa miaka mingi.Hii inatokana na 'kutengeneza' mazingira ya vyama vya upinzani kuungana kupinga madudu yake.Umati wa maelfu ya watanzania uliohudhuria jana viwanja vya jangwani haijawahi kutokea na wote wanasema NO TO CCM! 2015 ccm kwa heri,ahsanteni kwa kutufikisha hapa tulipo.
 
CCM wameamua wao wenyewe kutuachia ikulu yetu baada ya kuipoka kwa miaka mingi.Hii inatokana na 'kutengeneza' mazingira ya vyama vya upinzani kuungana kupinga madudu yake.Umati wa maelfu ya watanzania uliohudhuria jana viwanja vya jangwani haijawahi kutokea na wote wanasema NO TO CCM! 2015 ccm kwa heri,ahsanteni kwa kutufikisha hapa tulipo.
Maranyingi mtu akiwa na matatizo ya akili hawaze kujijua mpaka watu wamwambie jiangalie mkuu.
 
Chama tu kinawashinda ije kuwa serikali nyie mnaweza kupigana tu hakuna jipya,mbowe na sugu wanapigana bungeni ikulu siwataifanya dangulo.
 
Sure Mkuu. Hebu watafakari Kinana, Nape, na Mwigulu kwa makini ukiwa umetulia mithili ya ku-meditate. Itafakari CCM kwa utulivu wa hali ya juu; tafakari mambo mbalimbali ambayo yamefanyika chini ya utawala wa hawa jamaa. Kisha rudisha mawazo yako pale Bungeni; mtafakari Job Ndugai, Speaker Makinda, Lukuvi, Werema, Lusinde, Nkamia, na wabunge wote wa magamba na majibu ya dharau ya mawaziri.

Kisha taratibu rudisha mawazo yako kwa makada wao waliotapakaa nchini kuanzia ngazi ya shina hadi taifa na mbwembwe zao za kijinga - CCM ina wenyewe na itatawala "milele" na dharau zao.

Kisha itafakari hatma ya Tanganyika chini ya hali hii; watoto na watoto wa watoto wetu sisi maskini watakuwa wageni wa nani tena ndani ya ardhi yao wenyewe! Utafikia conclusion moja tu - CCM has to go!
 
Chama tu kinawashinda ije kuwa serikali nyie mnaweza kupigana tu hakuna jipya,mbowe na sugu wanapigana bungeni ikulu siwataifanya dangulo.
hoja zenu nyepesi zinaonyesha jinsi mlivyo na mawazo finyu,na kadri mnavyotoa hoja nyepesi na zisizokuwa na tija ndivyo mnavyowakatisha tamaa wanachama wenu wa ccm maana hata wao wanagundua kwamba hamna hoja zaidi ya mizaa tu,
 
Chama tu kinawashinda ije kuwa serikali nyie mnaweza kupigana tu hakuna jipya,mbowe na sugu wanapigana bungeni ikulu siwataifanya dangulo.

4.jpeg

View attachment 113181

Hivi katika vyama ambavyo ngumi ni kila kukicha ni kipi ndugu yangu yaani unashindwa kuelewa yanayotokea CCM kwa sababu tu na wewe ni mmoja wao.
 
Mimi naona bado. Kama hawa watu kwenye picha bado ni huru machoni mwa watanzania.Angalia picha hii.
 

Attachments

  • 1379870840055.jpg
    1379870840055.jpg
    142.7 KB · Views: 111
Sure Mkuu. Hebu watafakari Kinana, Nape, na Mwigulu kwa makini ukiwa umetulia mithili ya ku-meditate. Itafakari CCM kwa utulivu wa hali ya juu; tafakari mambo mbalimbali ambayo yamefanyika chini ya utawala wa hawa jamaa. Kisha rudisha mawazo yako pale Bungeni; mtafakari Job Ndugai, Speaker Makinda, Lukuvi, Werema, Lusinde, Nkamia, na wabunge wote wa magamba na majibu ya dharau ya mawaziri.

Kisha taratibu rudisha mawazo yako kwa makada wao waliotapakaa nchini kuanzia ngazi ya shina hadi taifa na mbwembwe zao za kijinga - CCM ina wenyewe na itatawala "milele" na dharau zao.

Kisha itafakari hatma ya Tanganyika chini ya hali hii; watoto na watoto wa watoto wetu sisi maskini watakuwa wageni wa nani tena ndani ya ardhi yao wenyewe! Utafikia conclusion moja tu - CCM has to go!
Moto utawawakia sana tu nyie chadema ikulu mtaisikia kwenye bomba bakini uchocholoni mfanye uchafu wa kisiasa lakini ikulu si mahala penu.
 
hoja zenu nyepesi zinaonyesha jinsi mlivyo na mawazo finyu,na kadri mnavyotoa hoja nyepesi na zisizokuwa na tija ndivyo mnavyowakatisha tamaa wanachama wenu wa ccm maana hata wao wanagundua kwamba hamna hoja zaidi ya mizaa tu,
Hoja zenu nzito ni zipi kuandamana na kupigana bungeni ndiyo hoja za maana? Tumia akili mkuu siyo kuvimba mashavu halafu unajiona wa maana.
 
Hatuiombei kifo CCM lakini tunasema miaka 50 inatosha, hali ni mbaya kiasi kwamba haivumiliki zaidi ya kuiondoa CCM madarakani, mfano:Kanali wa JWTZ wa bandia kakamatwa. polisi wa usalama barabarani wa bandia kakamatwa,daktari wa bandia kakamtwa Muhimbili, dawa za mamilioni ya shilingi za bandia zimekamatwa,kituo cha afya cha bandia kimefungwa, dawa za kupunguza makali ya ugonjwa wa ukimwi za bandia zimekamatwa,mbolea ya ruzuku ya bandia imekamatwa, madawa ya mifugo ya bandia yamekamatwa, dawa za kuua wadudu za bandia zimekamatwa, barabara kuanzia Chalinze hadi Mlandizi ya bandia, barabara kati ya Dar es Salaam na Mtwara halijakamilika tangu miaka ya 90, askari magereza wamekamatwa na nyama ya twiga!? askari wa kituo cha Oysterbay wamekamatwa na pembe za ndovu huko Kisarawe, askari wa kituo cha Dumila wamekamatwa na kifuu cha binadamu kwenye mfuko wa rambo, askari wa Arusha wamekamatwa na magunia 18 ya bangi, walimu wanaidai serikali zaidi ya sh bilioni 30, matokeo yake asilimia 94 ya wanafunzi waliofanya mtihani wa kidato cha nne mwaka jana wamefeli, mafuta ya treni zinazoenda bara kuliko kusafirishwa na treni yanasafirishwa na maroli ya kukodi (badala ya mafuta kusafirishwa na treni zenyewe wenzetu hawa wanakodi malori),Mzungu mmoja huko bandarini ameweka bomba lake linalochota mafuta kutoka kwenye bomba la serikali, majambazi wamevamia kituo cha polisi cha kati Mwanza, fimbo ya dhahabu ya IGP imeibwa, wazee zaidi ya miaka 60 wameahidiwa matibabu bure kutoka hospitali yeyote ya umma lakini dawa hakuna, Watanzania hawaaminiki tena popote duniani kwa sababu ya kujihusisha na madawa ya kulevya, Dar es Salaam kwa sasa inaaminika kuwa ndiyo njia kuu ya kupitisha madawa ya kulevya Afrika Mashariki, wananchi wanaendelea kuumizwa na tindikali, hakuna mahali unapoweza kupata huduma ya kuridhisha bila kutoa rushwa.Listi ni ndefu, sasa katika hali kama hii chama kile kile, serikali ile ile, viongozi wale wale, tutatokaje hapa, hapana tunahitaji mabadiliko. Naomba kutoa hoja.
 
Back
Top Bottom