Kifo cha CCM kimetimia

Kifo cha CCM kimetimia

Huu udanganyifu una mwisho kwa kuwa huwa unaenda na kizazi chake! ndo maana Mke wa Mwenyekiti wa CCM alisema hawa vijana wamepewa nini mbona hawaitaki CCM!!
umeongea kugaidi gaidi kweli. ccm itazidi kuwa mwalimu wenu kwa mda mrefu sana ujao
 
Ujumbe wa picha ni mkubwa zaidi wa maneno, mtoa mada nakushukuru sana, mwenye macho haambiwi tazama, imani yangu ni kwamba mwisho wa nyinyiemu umeishafika, tunasubiri kutangaziwa matokeo tu. CHADEMA NDO MUAROBAINI WA HAYA YOTE.
mwisho wa ccm ni 2090. hiyo chadamu yako peleka huko
 
i love chama cha mapinduzi, hutaki unaacha au koroga sumu ya panya unywe
 
user-online.png
Elineema J Mosi

Today 11:46
JF Senior Expert MemberArray


Join Date : 17th May 2013
Location : ARUSHA
Posts : 618
Rep Power : 437
Likes Received94
Likes Given0


[h=2]
icon1.png
Re: Ccm hivi ndivyo mnavyowarubuni ndugu zetu!!? [ona picha], na hii ndio busara yenu!!?[ ona picha][/h]

quote_icon.png
By h.imani
kidumu chama cha mapinduzi? ''kimetobokaaaaaaaaaaaaaaaaaa''
wape ukweli hao





wape ukweli hao​


  • multiple IDs, wrongly commented


 
Kumekuwa na matukio mengi yanayofanywa na jeshi la Polisi kwa kisingizio cha kulinda amani, matukio hayo mengi yameelekezwa kwa wanasiasa wa upinzani hususan Chadema. Wakati Fikra za Polisi(Wakuu) ni kuisaidia ccm hali ni tofauti kwa wananchi hasa katika matendo ya wazi yanayotafsiriwa kuwa ni uonevu na vitisho vya moja kwa moja kwa wapinzani.mfano ulio hai ni kitendo cha jeshi hilo mkoani Iringa kuamua kumkamata Mwenyekiti wa Chadema na Wenzake kwa tuhuma za kufanya vitendo vinavyoashiria kuvunja amani kwa Mujibu wa Polisi 1 kushindwa kuanza mkutano katika muda walioomba,katika maeneo yote mkoani Iringa,kutumia muda mfupi wa kuhutubia hata baada ya kuchelewa kuanza mikutano na kuwepo kwa amani hata baada ya mikutano kumalizika na kukosekana mtu aliyedhuriwa.Kwa mazingira hayo jeshi likaona kuna sababu ya msingi ya kuwakamata Mbowe na Wenzake kwa ajili ya kuamsha emotion zaidi kwa wananchi wa maeneo mengine wajue jinsi jeshi la Polisi lisipoingilia mikutano hiyo uvunjifu wa amani hautotokea
 
CCM haifi utakufa wewe na baba yako bahati yako mama yako yeye al iisha kufa naye angekufa nyambafuuuuu zakoooo.
 
Kama wameshindwa kumwelewa Mzee Warioba, inawezekena kabisa.
 
Ili chama kiweze kuongoza dola kwa ufanisi; vinahitajika vitu viwili vikubwa.


(i) Kukalia ofisi (kushika dola) (ii) kukubalika na wananchi.



Kuhusu kukalia Ofisi; chama kinaweza kuwa madarakani iwe kwa kuchaguliwa au kwa njia yeyote ila kikawa hakikubaliki kwa wananchi walio wengi wakati huo kikiwa madarakani kwa sababu mbalimbali. Katika mazingira hayo ni vigumu sana kwa chama hicho kuongoza dola .Rejea kesi ya Muslim Brother hood ya Misri.



Kuhusu kukubalika na wananchi; Chama chochote kinapokuwa madarakani , ni lazma kitafute mbinu ya kukifanya kikubalike na wananchi ili kiendelee kuwepo.Njia kubwa zinazotumika huwa ni mbili;



(I) Chama kinaweza kujitahidi kutekeleza ilani na majukumu yake mengine na wananchi wanapoona jitihada hizo ; moja kwa moja hukikubali chama bila kushinikizwa na mtu.



(II) Kutumia propaganda.



Tukianza na mbinu ya kwanza; Tunaona wazi kwamba CCM imeshindwa kutekeleza majukumu yake ya kuisimamia serikali kufanya mambo yenye tija kwa wananchi. Kushindwa huko kunasababishwa na mambo mbalimbali miongoni ikiwa ni pamoja na kushindwa kabisa kufanya siasa za kisayansi na kuwa na migongano ya kimaslahi miongoni mwa wana CCM wenyewe. Kwa mfano mdogo tu; Tarehe 27/08/2013, (ndani ya bunge) Mh. Israel Natse (mbunge CHADEMA) alitaka "Serikali itoe kauli ni kwa nini Rais na miongoni mwa viongozi wa nchi hii wanasema wana orodha ya wafanyabiashara ya madawa ya kulevya lakini hawawataji?". Katika kujibu hoja hiyo kwa niaba ya serikali; Waziri Lukuvi alisema "Tukiamua kuwataja; wengi wenu hapa bungeni mtatajwa". Hii ni dhahiri kwamba CCM na serikali yake haiwezi tena kuvuta utashi wa wananchi kuikubali kwa kutenda mambo yanayotamaniwa na wananchi kwa sababu ya migongano ya kimaslahi ndani ya viongozi wa ccm wenyewe kwa wenyewe. Katika mazingira kama hayo CCM hulazimika kuwekeza nguvu kubwa zaidi katika propaganda ili kuwafanya wananchi waikubali.




Tukija kwenye Propoganda; Propaganda ni taarifa, mawazo, itikadi au jitihada maaluum zinazofanyika ili kuathiri fikra, hisia na hata tabia ya umma kwa manufaa ya mdhamini wa propaganda yenyewe. Propaganda zinaweza kuwa za aina kuu mbili .



(i) Propaganda safi; Inayolenga kuupa umma matumaini ya kuvutia kama wakikiunga mkono chama chenye dola.

(ii) Propaganda chafu; Hizi kwa kiwango kikubwa hulenga kuutisha umma .Hapa umma hujazwa hofu nyingi kwamba kama wakionesha kutokukubali chama chenye dola basi wanaweza kudhuriwa vibaya.



Propaganda safi mara nyingi hutumiwa na huleta ufanisi wakati ambapo chama tawala hakijachukiwa sana na kupoteza imani kabisa kwa umma. Kwa Mfano CCM; Walitumia propaganda safi kama ifuatavyo na kujifanikiwa kuwavuta watu wengi kipindi cha nyuma.
Mfano;Walianza na " Ari mpya kasi mpya na nguvu mpyaa!" Wakavuta watu wakawaamini hata hivyo matarajio ya umma yakawa tofauti. Wakabadili wakaja na "Kasi zaidi, ari zaidi na nguvu zaidi", safari hii matokeo yakawa mabaya zaidi na uungwaji mkono kutoka kwa umma nao ukapungua. Wakaja na "Maisha bora kwa kila mtanzania!". Nayo ikawa kinyume kabisa. Wakaja na "Idumu CCM mpya!" Upya ambao haukuonekana mpaka leo. Katika mazingira hayo ilikuwa ni vigumu sana kwa CCM kupata propaganda nyengine chanya (safi). Basi wakachagua kuzama kwenye propaganda chafu.




Maurice Tugwell Kwenye kitabu chake "Terrorism and Propaganda" (2010), anasema; inapotokea chama tawala kimekosa kukubalika na upinzani unapata uungwaji mkono mkubwa; basi mbinu inayoweza kutumika ni kutumia propaganda ya kuwatisha watu ili waunge mkono chama tawala/utawala wowote kwa sababu ya woga. Maurice anasema mara nyingi njia ya kuwahusisha wapinzani na ugaidi hutumika. Kulifanikisha hilo, Mdhamini wa propaganda huweza kuua watu wasiokuwa na hatia na kisha akawasingizia wapinzani wake. Lengo linakuwa ni kutengeneza hali ya woga katika jamii kwa ujumla wake.



Ni sahihi kujiaminisha kwamba matokeo ya kudhuru yenye muelekeo wa kisiasa nchini yamefanywa na CCM kwa sababu tajwa hapo juu.Hii ni kwa sababu ; licha ya kwamba katika matukio yote , Waliokuwa wamepelekwa mahakamani ni wapinzani, wapinzani walishinda kisheria.Sasa ikiwa wapinzani walishinda kisheria, na wakati huo huo matukio ya kudhuru kwa lengo la kuutisha umma yalifanyika ni sahihi kusema waliokuwa wameyafanya ni CCM , nawalifanya kama sehemu ya propaganda ( propaganda chafu baada ya kukwama kwenye propaganda safi).



Kwenye kikao cha CC ya CCM Kilichomalizika 26/08/2013, CCM wanasema wamekubaliana kufanya mabadiliko makubwa ndani ya chama; mabadiliko ambayo safari hii hawakuyataja. Nina uhakika CCM wenyewe hawana uhakika kwamba ni mabadiliko gani wanataka kuyafanya. Kadhalika hakuna mbinu nyengine yeyote ya kisayansi iliyobakia ambayo inaweza kuisaidia CCM kukubalika tena kwa umma.Katika hili naamini wote tutakubaliana. Kwa sababu hiyo basi tutarajie kuona CCM wakiendelea kutia aibu kwenye hii miaka miwili iliyobakia.
 
Eti wanajidai na kujifariji kuwa ni chama kinachoongoza Dola. Hivi ufisadi, ujangili wa akina tembo dentist, madawa ya kulevya hadi nyumbani kwa mwenyekiti, uasherati wa kutisha miongoni mwao, na wake zatu, kuuwa watz kwa mabomu makisani na kwenye mikutano, kujipa ajira kwa watoto wao tu huku wengine wakisaga soli kila kukicha, matusi ya nguoni ya akina mwingulu na wenzake na....na....... endeless evils...... NDIO KUONGOZA DOLA? Mijamaa haina hata aibu inafikiri tukiyaona kwenye hayo magreen tunafurahi, kumbe nyongo zinataka kupasuka.
 
siamini hayo mnayo yasema cz hamja fanya reseach na msomi unajua (no reseach no rigth to say)
Ni kweli ccm bado haijafanya vizuri ktk uongoz wake lakin hoja mnayoijenga kuwa ndo mwisho wa uongoz wake 2015 sio wako watu wanojua kusimamia nchi kama lowassa ambaye hata wapinzani wanakubali utendaji wake.
Kwa iyo hoja zenu sio za msingi kuweni makini na hoja mnazozijenga.
Nakumbuka lowasa alizuia viwanja vya mnazi mmoja visiuzwe kipindi akiwa waziri wa aridhi na kuzuia nyumba za taifa zisibinafsishwe leo hii mnasema mwisho wa ccm yuko jembe lowassa tunamwaminiu kwa kuthubutu.
 
Nikiangalia kwa makini matukio, mengi na CCM na ubabe hata ndani ya chama, this thing is a dying horse.
 
Katika dunia ya leo hakuna kitu kibaya kama kuishi kwa mazoea kwani wakati wenzako wanapiga mbio wewe utabaki palepale ukiendelea kupiga miayu tu! Na hili si siri tena kwa chama chetu CCM. Zamani CCM ndiyo ilikuwa imeshika hatamu na ndiyo iliyokuwa na semi ya mwisho katika maamzi ya utawala wan chi hii! Tofauti na sasa ambapo kila mtu anaweza kusimama na kupaza sauti.

Sasa ukija kuangalia hali ilivyo kwa sasa ni kuwa CCM imeachwa nyuma kabisa na haijitambui kuwa ipo nyuma ya wakati. Nasema kuwa zamani ilikuwa inatembea barabarani kutokana na kuwa na nguvu ya kufanya maamzi yoyote bila kuhojiwa na mtu, na sisi tuliosalia kubaki tukipiga makofi tu!

CCM ilikuwa ikiamini hata kama itafumba macho watu watakuwa wamejipangta kando ya njia na kuifikisha kule inakotaka hata kwa lazima! Tofauti na sasa CCM imeondolewa barabarani na sasa inaonekana kama msanii wa mtaani ambaye hujipatia riziki kwa kufanya onesho la kutembea juu ya waya! Hatakiwi kufumba macho, kwani akifanya hivyo lazima atadondoka chini na kuharibu radha nzima ya onesho. Tatizo la CCM hawajajielewa kuwa kwa sasa wanafananishwa na mtu huyo.


AMKENI LA SIVYO MTAANGUKIA PUA.
 
This time nimekuwa nikifikiria sana, Juu ya hatma ya chama tawala chama chamapinduzi ccm pale nguvu ya uma itakapotumika kukiondoa madarakani. Mimi ni kati ya mamilioni ya watanzania ambao maisha yeto yametobolewa matundu ya risasi za magumu ya maisha, achilia mbali risasi zile zilizotoboa kwenye miili ya ndugu zetu waliotangulia mbele za haki, au risasi silizo piga miili ya wanyonge na kuwasababishia vilema na majeraha ya kudumu. Mrundikano wa madai ya wananchi na jamii kwa ujumla, kesi na malalamiko dhidi ya serikali na chama nijambo ambalo huwa nikilifikiria ninaona kwa taswira ang'avu kabisa jinsi viongozi wa chama tawala na serikali watakavyokuwa katika wakati mgumu kabisa kihistoria barani Afica kukubali kukubaliana na maamuzi ya wananchi ya kubadilisha utawala wa nchi, na hili ndio linadhihirisha wazi kuwa watakuwa tayari kwa gharama yoyote pengine hata kwa kumwaga damu kama kawaida ili kuhakikisha hawakiachii kiti cha kuwa madarakani.

Hii ni kwasababu kitendo cha kubadilisha utawala kitatoa fulsa sawa ya kila mmoja kufidiwa Dosari iliyowekwa kwenye maisha yake kwa haki na usawa, Sasa Hoja yangu ipo hapa; Je Utawala huu utaweza kulipa kila jeraha la mwananchi ambalo imeliweka tangu 1964? Roho za watu waliouwawa na jeshi la polisi zitafidiwa na nini? Kunajinsi ya kumrudishia Dk Ulimboka meno yake aliyopewa na mwenyezi mungu badala ya yale ya wazulu? kama hakuna nini itakuwa fidia stahiki?, Pamoja na kwamba naumia sana na ukatili na unyanyaswaji ambao tumekuwa tukiendelea kufanyiwa, wizi na ubadhilifu ambao tunaendelea kutendewa ila siku zote naamini kila mhusika atalipa, Sio raisi wala waziri wala mbunge, sio jaji wala hakimu, hakuna mkuu wa wilaya wala diwani. Tukishaweka serikali tunayoiamini madarakani kila mmoja lazima atalipa kila nukta ya baya alilotenda. Nani atasalimika......... Mengine sina uhakika huwa nasikia tu, lakini kama ni kweli, babu seya akikata rufaa mchezo mchafu aliochezewa ukabainika, Mh Atapona?
Wananchi tumesha choka, CCm ni lazima itambue kuwa 2015 ni kufa au kuolewa, Either iibe sana kura na kupiga mpaka kuua kila mwananchi na mwanaharakati atakaepigania uchaguzi huru na wahaki kama ilivyodesturi za mataifa yetu ili iendelee kubaki mdarakani, au ikubali kuachia madaraka kidemocrasia na kuanza kulipa na kuwajibika kwa kila tundu la risasi iliyo weka kwenye maisha ya watanzania.

CCM 2015 ni kufa au Kuolewa

Msamiati.
 
mtahangaika sana ila ccm ni kisiki cha mpingo, inakubalika na itazidi kushinda chaguzi zote hapa nchini
 
kidumu chama cha mapinduzi. ccm oyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom