Nina kila sababu ya kusema kuwa ccm mwisho wao uko karibu sana.Nikiangalia historia ya viongozi wandamizi wa ccm sijawahi kukutana na vijana kama akina Nchemba na Nape,japo kuna wazee wengine hawajitambui kama wassira,Lukuvi nk nadiriki kusema huu ndio mwisho wa ccm na serikali yake. Sababu ni hizi
1.urafiki ktk uongozi.Huwezi kumkana wala kumwajibisha rafiki yako. Anaweza kufanya lolote bila kumchukulia hatua.mfano tunajua fika kuwa Membe ni swaiba au ndg yke Jk ile kauli ya maadui 11 inatekelezeka sawa kwa upande wake na kinyume kwa wananchi.na kauli zingine za kinyama mfano ya Pinda liwalo na liwe..,wapigeni tu,ya wassira kibanda ni nani..ya Nape mimi sio mchaga..ya mwigulu msipoichagua ccm mtakufa..,ya kova tukio la ulimboka ni siri ya taifa.ccm kumbukeni kuwa kauli zinanguvu kuliko hata vitendo na kila kitu kilichopo kiwe kizuri au kibaya chanzo chake ni kauli.Huwezi kuweka watu kama Nape,mwigulu,wassira nk wawe brand ya chama,hawa watu hawawezi kuuza brand ya chama fukuzeni hawa.
Urafiki pia umechangia kushindwa kuchukua maamuzi juu ya ufisadi,rushwa,mauaji,utesaji watu,unyanyasaji wa raia,wauzaji wa madawa ya kulevya nk.Hili ni anguko,na mkianguka hamuinuki tena.
2.Ahadi za uongo.Kila awamu ya uchaguzi mnakuja na kauli mbiu mpya ooh maisha bora kwa kila mtanzania,leo hii iko wapi? Maisha magumu zaid kwa kila mtanzania ndicho kilichopo,leo hii mnaona aibu hata kusema majukwaani.kila siku gharama za maisha zinapanda,bei ya vyakula juu,nauli juu,pembejeo juu au maisha bora ndio haya ya vitu kuwa na bei kubwa? Hivi sasa mmekuja na kodi ya simcard tsh 1000 kwa mwaka,huyu mtu maskini ambaye kipato chake ni cha chini mnamsaidiaje,hata kama mtapandisha bei ya mazao kama gharama ya vitu inapanda haisidii.Hili ni anguko la ccm.
Hitimisho:mwigulu na wengine wanaofanana nae wafukuzwe kwenye uongozi,ccm watimize ahadi zao,wasihangaike na upinzani(chadema), kazi ya upinzani ni kukosoa na sio kusifia.Kama sisiemu mtatimiza ahadi zenu ni nani atawakosoa? Rais Kikwete alitoa ahadi kibao,leo hii hakuna kilichofanyika,wekeni mikakati ya kutoa ahadi mnazoweza kuzitekeleza sio kuropoka tu majukwaani.