Kifo cha CCM kimetimia

Kifo cha CCM kimetimia

Anguko la CCM ni la kishindo na historia ya CCM itapotea kabisa kwenye vinywa vya wananchi zaidi kutaja mabaya yaliyofanywa na CCM.
Kila nikizungumza na mtu awe mwanafunzi, mkulima,mfanyakazi n.k CCM inalaumiwa sana,hii ni kutokana na maisha kuwa magumu.Lakini wao(CCM) wanasema wameleta maendeleo,sijui ni maendeleo yapi? Kazi kujisifia tu,wakati hakuna lolote.
Ukitaka kujua kuwa serikali ya CCM haijafanya kitu,tumia mfano huu; Enzi za mwalimu Nyerere hawa viongozi wote walisoma bure toka chekechea hadi chuo kikuu.
Lakini leo,gharama za kusoma ni juu ya mzazi,halafu wanasema tumeendelea. Ukiwauliza watakwambia idadi ya wanafunzi ni kubwa. Ok ni kubwa lakini mbona tumeendelea? Hayo maendeleo yanakwenda wapi?
Enzi za mwalimu hapakuwepo na uchimbaji madini,lakini watu walikuwa wanasoma bure.Leo hii,madini yanachimbwa faida hakuna,wawekezaji kibao faida hakuna.
Sasa,hayo maendeleo ni ya nani? Au mnavyojenga nyumba,barabara n.k ndio maendeleo? Maendeleo yanapimwa qualitatively(standard of living) and Quantitatively(physical assets like roads,buldings).Sasa ndugu zangu CCM wakiona majengo makubwa,barabara ndiyo basi wanajisifia!,Ndugu,bila kuondoa umaskini barabara,maghorofa n.k ni bure.Watu hawali barabara au majengo.
Narudi kwenye mada ya msingi,anguko la CCM litakuwa la kutisha.Wanachama wengi wa CCM,wako kimaslahi na kwa sasa wako njia panda baada ya kuona CCM imeshikwa pabaya.Ukizungumza nao wanasema CCM ikipigwa chini,sisi(wao) wanahamia chama tawala.Sasa najiuliza,CCM siku imeshindwa itabaki na nani? Au Nnape na Mwigulu ndiyo watabaki?
CCM,wanajifariji sana kuwa tuna wanachama vijijini,vyuo vikuu,wanajidanganya! Kwanza ukisema mtaani/chuoni kuwa niko CCM wanakucheka na kukuona mshamba.
CCM ikishindwa uchaguzi ujao na ninaamini inashindwa,haitakuwepo tena na jina la CCM litapotea, zaidi watu watakuwa wanaikumbuka kwa ufisadi,kubambikiza kesi na uzushi wa aina mbalimbali.
Na siku CCM imepigwa chini kuna watu watazimia,watahama nchi na wengine sura zao sijui watazificha wapi?
Mtu hana cheo wala wadhifa wowote CCM,maisha magumu kama mimi hapa,lakini anaisifia ccm na kuitabiria ushindi,ivi umerogwa na nani? Au ni njaa inakusmbua?
Kama ni kijana humu JF,hakuna haja ya kuishabikia wala kuwa CCM,kwani sina hakika kama CCM itatawala miaka 50 ijayo. Viongozi walio na miaka 60+ baada ya miaka 50 kuanzia sasa sio wenzio umri wao umekwenda,wewe ndiyo unakua,ni hatima yako kwa miaka hamsini ijayo? Hao mawazir sio wenzio,ukiendelea kuwafuata wanakuambukiza element za ufisadi kitu ambacho kitameza hata kizazi chako,
Vijana tubadilike hii nchi si ya watu wenye umri wa miaka 60+,bali ni ya kwetu.
 
hakika na kweli mkuuu umenena!!!!! Maandiko yanasema aliye na masikio na asikie sasa Bwana awaambia mataifa.
 
Mamanda wazidishe mapambano tu, hata enzi za Idd Amin wakati wa vita ya Kagera Idd Amin aliendelea kutangaza kwamba majeshi ya Tanzania yanapigwa vibaya sana, na kwamba wote walioingia katika ardhi ya Uganda hawatarudi kwao salama watakuwa chakula cha mamba kwenye mto Nile.

Sasa mnataka Kinana, Nepi Mnawaye, na makada wengine waseme nini? Si unaona wanamfungia Murji ndani kwa sababu eti anachochea wananchi.

Ikimbukwe kwamba hata enzi za kutafuta uhuru wa Afrika ya Kusini Mandela aliitwa Mchochezi hapa Tanzania Nyerere, Karume, kule Kenya Kenyatta wote waliitwa wachochezi SASA MNASHANGAA NINI CCM kuwaita watetea haki na raslimali kuitwa wachochezi.

ALUTA CONTINUA
Tafakari!!!!!!!!!!!
 
Ikiwa ni muda mrefu umepita,tokea watanzania tupate uhuru, tukiwa chini ya utawala wa TANU, hatimaye CCM bado mabadiliko makubwa hayajafanyika kuonesha malengo ya kulipatia taifa letu maendeleo. Awamu ya kwanza ilianza vyema, lakini mawazo ya Mwalimu JK Nyerere yalipoanza kukiukwa katika awamu ya pili, ya tatu na hatimaye ya nne ndio sasa watanzania tunaona tuko katika jehanamu iliyojaa chuki,njama,ufisadi, na umaskini uliokithiri.

Ni ukweli usiofichika CCCM na uongozi wake wote imeshindwa kutatua matatizo yanayotukabili, na niseme imekuwa ikituongezea tabu kila kukicha. Nianze na MGOMO WA MADAKTARI, AJALI ZA ZANZIBAR, SUALA LA MUUNGANO,KILIMO n.k vyote vinatabiri kifo cha CCM, kwa kuzingatia kuongezeka kwa machafuko nchini.

Watanzania walio wengi wenye akili timamu na hekima nadhani tayari wameshajiandaa kufanya mabadiliko makubwa 2015 ,na namini itakuwa ndio mwisho wa utawala wa kidhalimuna dhaifu wa CCM!

NA HICHO NDICHO KIFO CHA CCM 2015!
Mamanda wazidishe mapambano tu, hata enzi za Idd Amin wakati wa vita ya Kagera Idd Amin aliendelea kutangaza kwamba majeshi ya Tanzania yanapigwa vibaya sana, na kwamba wote walioingia katika ardhi ya Uganda hawatarudi kwao salama watakuwa chakula cha mamba kwenye mto Nile.

Sasa mnataka Kinana, Nepi Mnawaye, na makada wengine waseme nini? Si unaona wanamfungia Murji ndani kwa sababu eti anachochea wananchi.

Ikimbukwe kwamba hata enzi za kutafuta uhuru wa Afrika ya Kusini Mandela aliitwa Mchochezi hapa Tanzania Nyerere, Karume, kule Kenya Kenyatta wote waliitwa wachochezi SASA MNASHANGAA NINI CCM kuwaita watetea haki na raslimali kuitwa wachochezi.

ALUTA CONTINUA
Tafakari!!!!!!!!!!!
 
Kama rasimu ya katiba mpya itapendekeza haya yafutayo yawepo kwenye katiba mpya,nashuhudia anguko la ccm na serikali yake;
1.Tume huru ya uchaguzi.
Hapa kwa uzoefu wa ccm wao wa kuiba kura utakuwa umefika mwisho

2.Muundo wa serikali tatu.
Hapa tutashuhudia/ naona kitu ambacho nina uhakika nacho kuwa rais wa Tanganyika(Tanzania bara) lazima atoke upinzani.Hili liko wazi,kwani kura ambazo ccm walikuwa wanashinda ilikuwa ni ziada ya kura kutoka Znz.Sasa,hii kwao itakuwa ngumu kwani Znz hawana nguvu tena,pia upande wa bara ccm wananchi hawaitaki tena.

3.Spika na Naibu spika kutokuwa wabunge.Hapa tutashuhudia makubwa,kwani ule utaratibu wa kulinda serikali na chama chake hautakuwa na nafasi tena.

4.Wananchi kuwawajibisha wabunge/kuwa na mamlaka ya kuwaondoa wabunge wazembe.
katika hili,wabunge wataibana serikali vya kutosha,mbunge hawezi kuondolewa kizembe kizembe.kwa hiyo issue ya kukilinda chama tawala na serikali yake haitakuwepo tena.

5.Mbunge akifukuzwa uanachama anaendelea kuwa mbunge.
Katika hili, mbunge yeyote hasa wa chama tawala (ccm) japo sina uhakika asilimia 100 kama wataendelea kutawala,hataogopa kuivua nguo serikali na chama chake kwa kuhofia kufukuzwa uanachama.

Haya yanadhihirishia anguko kuu la CCM,hata kama watabahatika kuwa madarakani mwaka 2015-2020 ndio mwisho wao,ambapo 2021 ni mwaka wa neema kwa Tanzania,kwa kutokuwepo na utawala wa CCM.

MUNGU YUKO UPANDE WA WANANCHI NAAMINI HAKUNA KITACHOBADILIKA. MAONI YANGU.
 
umenena kwel sasa saizi wanaweseka weseka eti rasimu wameipeleka kwa wanchama wakati siku hizi awana watu kabisa wameishiwa sasa hao wanachama ni wp? Nape......kwisha habari yenu
 
Kama thread zinaua chama CCM ingekuwa imekufa llongtime hata mabaki yangekuwa yashapotea, Nguvu ya Chama ni wananchi na subiri uone vumbi lake 2015 kwani Odinga alijua kuwa Katiba mpya ndo ingemmaliza?
 
Rasimu inaeza pelekea katiba ya hvo,ila kama cc wananchi hatuja amua mabadiliko ccm itaendlea kutawala
 
Hiyo ni rasimu tu wewe. Unaanza kuhesabu mayai hata kabla ya kuku hawajatotoa.

Radhia dada yangu hata kama hii ndio rasimi lakini ndo mtizamo wa wananchi na ndo inakwenda kuwa katiba kwa sababu yaliyomo mengi wananchi wanayakubali naninacho kuambia wale wazee awatakubali kabisa kutuletea katiba mbovu kwa sababu wao ndio wanamaamzi ya mwisho kwenye uchambuzi nacho kiamini katiba itakayo kidhi matakwa ya wananchi ndiyo itakayopatikana chini ya waryoba, baregu, na wengine wote
 
Hiyo ni rasimu tu wewe. Unaanza kuhesabu mayai hata kabla ya kuku hawajatotoa.

Kwanza hujielewi,mayai yanatotolewa na kuwa mayai tena? Au ni vifaranga? Umeshajijibu mwenyewe huwezi kutotoa kama hauna mayai,ni kweli najihesabia mayai kwa maana hilo umerithibitisha mwenyewe,kwani huwezi kutotoa kama hakuna mayai.
 
Kama thread zinaua chama CCM ingekuwa imekufa llongtime hata mabaki yangekuwa yashapotea, Nguvu ya Chama ni wananchi na subiri uone vumbi lake 2015 kwani Odinga alijua kuwa Katiba mpya ndo ingemmaliza?

CCM mnajifariji kama wagonjwa wa ukimwi,mgonjwa unamwambia utapona tu,wakati waliowahi kuwa na ukimwi hawajawi kupona.Mnatembea huku mmekufa.
 
Kwanza hujielewi,mayai yanatotolewa na kuwa mayai tena? Au ni vifaranga? Umeshajijibu mwenyewe huwezi kutotoa kama hauna mayai,ni kweli najihesabia mayai kwa maana hilo umerithibitisha mwenyewe,kwani huwezi kutotoa kama hakuna mayai.

Unaongea pumba wewe. Na mimi huwa sina muda na waongea pumba. Watafute waongea pumba wenzako ili mziendeleze hizo pumba zenu.
 
Kama thread zinaua chama CCM ingekuwa imekufa llongtime hata mabaki yangekuwa yashapotea, Nguvu ya Chama ni wananchi na subiri uone vumbi lake 2015 kwani Odinga alijua kuwa Katiba mpya ndo ingemmaliza?

Wewe mawazo yako ni mitizamo yako ni ya kitoto hivi unaweza ilinganisha kenya na tanzania?sisi tutaitoa ccm kama kenya walivyo itoa kanu alafu hayo mengine yafuate lakini kwa taarifa yako ccm ndo bye bye ndugu yangu
 
it is so sad watu wasiojua hata kwanini nchi wanayoitawala na kuiibia ni masikini bado wanaendelea ku force kuitwa waheshimiwa...idi...oo...t..s
 
it is so sad watu wasiojua hata kwanini nchi wanayoitawala na kuiibia ni masikini bado wanaendelea ku force kuitwa waheshimiwa...idi...oo...t..s

mkuu Mh,P.Msigwa alisema,akili ndogo haiwezi kutawala akil kubwa.Pia mh.Mnyika alisema tumefika hapa tulipo kwa sababu ya udhaifu wa mh.Rais na upuuzi wa wabunge wa ccm.
 
kunawatu huwa siwaelewi ukisema anguko la ccm na serikali yake kwani hii rasimu imeandaliwa ccm na serikali yake haya mawazo mfu hayatasaidia yawezekana mkuu unajifariji mimi ninachojua wenye maamuzi ya haya mambo ni watanzania wala siyo wewe.
 
mkuu Mh,P.Msigwa alisema,akili ndogo haiwezi kutawala akil kubwa.Pia mh.Mnyika alisema tumefika hapa tulipo kwa sababu ya udhaifu wa mh.Rais na upuuzi wa wabunge wa ccm.

hayo ni mawazo yao kwani mnyika na msigwa wananini kwenye vichwa vyao,mnyika hata shule kakimbia,sitta alisema msigwa ni mhuni wa kawaida tu.
 
Back
Top Bottom