Kifanyike kipi kuboresha Mikopo kausha damu iwe na manufaa kwa wakopaji?

Half american

JF-Expert Member
Sep 21, 2018
26,133
68,444
Habari wakuu, nmeona kipindi cha ripoti maalum ITV kuhusu mikopo kausha damu.

Malalamiko ni mengi sana licha ya kuwepo kwa uhitaji wa mikopo na wengine kufikia hatua ya kuomba hii mikopo isitishwe.

Dhamana zinazowekwa na kiasi cha mkopo haviendani kabisa.

Kwa maelezo ya wanawake wengi wanaochukua mikopo wanadai ina madhara makubwa kuliko faida, na wengi wanachukua bila kuwashirikisha waume zao, hii ni hatari zaidi.

Serikali inajinadi kutoa mikopo kwa makundi mengi ya kijamii hasa kwa wanawake lakini ina mlolongo mrefu na ndio chanzo cha wengi kukimbilia kausha damu kupata mkopo kwa haraka.

Kipi kifanyike kuboresha hii mikopo inayoonekana inawaumiza wengi na uhitaji wake bado ni mkubwa?

Taasisi za fedha kama mabenki hamuoni hii fursa kwa kuweka utaratibu mzuri wa kuwafikia watu wa matabaka ya chini kupitia vikundi? (tatizo hapa ni mlolongo mrefu mpaka kupata mkopo)

Wanawake wanadhalilika sana na hii mikopo ya kausha damu. Mtu una mikopo zaidi ya minne kausha damu lazima utadhalilika tu, huwezi kutoka shimoni kwa kuendelea kuchimba shimo.

NB: DAWA YA DENI NI KULIPA.

Screenshot_20240222_113558.JPG
 
Serikali ikopeshe kwa riba na fuu wapunguze vigezo vya lazima vijana wajiunge makundi.
 
waache tu kukopa utakuwa mwishonwake tatizo lipo Kwa wakopaji wakibanwa na matatizo wanaenda kimyakimya BAADA ya kutuma vibaya wanaanza kuitaka serikali ikomeshe mikopoo hiyo
 
Huko ni kufeli Kwa serikali Kuna mikopo ya halmashauri wengi hawaijui hata mashari yake pia lazima yazingatie hali ya wakopaji. Lakini vipi taasisi za serikali zinazo simamia mambo ya fedha
 
Mkopo wenyewe kausha damu, halafu unatarajia uwe na manufaa kwa wakopaji......what a contradiction!
 
Wakati wa kukopa watu huwa very anxious; hata kujiridhisha huona kama vile wanapoteza muda hivyo kujikuta wanakopa hata kwenye maeneo ambayo hayana usajili na hayako kisheria.

Pia kuna hulka ya wakopaji kukopa hovyo-hovyo. Unakuta mtu ana mikopo sehemu zaidi ya moja bila sababu ya msingi kulingana na aina ya biashara anayofanya. Hii upelekea kuelemewa na mikopo na hivyo kufanya marejesho inavyotakiwa (Na hapo ndipo kelele na malalamiko huwa mengi wakati tatizo ni mkopaji).

Wako pia wanaodhani wanaenda kukopa kwenye NGO (Hawa ni wale wapenda vya mteremko). Ukikopa ni sharti ulipe. Hili utaliona pia hata kwa baadhi ya wakopaji wanaopata mikopo ya Halmashauri (Kurudisha huwa ni changamoto).
 
Back
Top Bottom