Wastaafu wanateswa sana na mikopo ya kausha damu wasaidiwe

Tlaatlaah

JF-Expert Member
May 18, 2023
8,184
11,607
Kausha damu ni mikopo ya yenye urahisi sana upatikanaji wake. Ina vigezo na masharti nafuu sana yanayowezekana kwa wakopaji wengi.

Kwa upande moja inasaidia sana watu wenye shida na malengo ya kujiunua kiuchumi, na wanafanikiwa bila wasiwasi.

Kwa upande mwingine ni mateso, vilio na kusaga meno kwa hiari yao na kwa kujitakia. Aibu, fedheha na dhahama zinawapata wahusika zinatukumba pia tusio husika.
Maana vilio vya shida zisizoisha, malalamiko, manung'uniko na majuto vinasikitisha sana.
Na kiubinadamu tunasaidia kadiri tunavyo jaaliwa na Mungu.

WALIMU wa shule za Msingi wanao elekea kustaafu wamekwama hapa kausha damu. Wanateseka sana.
Kadi za benki, vitambulisho na nyaraka zao muhimu za kazi zimehodhiwa na maofisa kausha damu, kama dhamana kutokana na malimbikizo ya marejesho na riba walizokosa kuzilipa huko nyuma na zinaongezeka kadiri mkopaji anavyochelewa kurejesha.

Muda wa kustaafu ukifika, afisa wa kausha damu na mwalimu mustaafu mguu kwa mguu kufanya clearance za mafao. Na baada ya hapo kausha damu anamkomba vizuri sana mstaafu huyu malimbikizo ya marejesho na riba, na akimuachia pumzi kidogo ya kupigia miyayo kwa muda mfupi tu ujao...

Watu hawa wasaidiwe, kustaafu sio tiketi ya kufa. Bado wanastahili kuishi kwa furaha na Amani ndugu zetu hawa.
 
Kausha damu ni mikopo ya yenye urahisi sana upatikanaji wake. Ina vigezo na masharti nafuu sana yanayowezekana kwa wakopaji wengi.

Kwa upande moja inasaidia sana kuwasaidia watu wenye shida na malengo ya kujiunua kiuchumi, na wanafanikiwa bila wasiwasi.

Kwa upande mwingine ni mateso, vilio na kusaga meno kwa hiari yao na kwa kujitakia. Aibu, fedheha na dhahama zinawapata wahusika zinatukumba pia tusio husika.
Maana vilio vya shida zisizoisha, malalamiko, manung'uniko na majuto vinasikitisha sana.
Na kiubinadamu tunasaidia kadiri tunavyo jaaliwa na Mungu.

WALIMU wa shule za Msingi wanao elekea kustaafu wamekwama hapa kausha damu. Wanateseka sana.
Kadi za benki, vitambulisho na nyaraka zao muhimu za kazi zimehodhiwa na maofisa kausha damu, kama dhamana kutokana na malimbikizo ya marejesho na riba za walizokosa kuzilipa na zinaongezeka kadiri mkopaji anavyochelewa kurejesha.

Muda wa kustaafu ukifika, afisa wa kausha damu na mwalimu mustaafu mguu kwa mguu kufanya clearance za mafao. Na baada ya hapo kausha damu anamkomba vizuri sana mstaafu huyu malimbikizo ya marejesho na riba, na akimuachia pumzi kidogo ya kupigia miyayo kwa muda mfupi tu ujao...

Watu hawa wasaidiwe, kustaafu sio tiketi ya kufa. Bado wanastahili kuishi kwa furaha na Amani ndugu zetu hawa.
Wamelazimishwa ? Kama hiari yao shida yako wewe iko wapi ? Serikali ifanyeje sasa ? Iwalipie hayo madeni ?
 
Wamelazimishwa ? Kama hiari yao shida yako wewe iko wapi ? Serikali ifanyeje sasa ? Iwalipie hayo madeni ?

shida yangu na huruma yangu nimeieleza vizuri sana ndani ya bandiko..

wala hakuna mahali nimeilaumu serikali...

wala sijashauri serikali ifanye nini..

ni raia yangu ikiwa una ndugu, jamaa, rafiki ama vinginevyo anaeweza kua miongoni mwa wanapitia sahibu hizi za kausha damu, help him njia njema za kutoka salama humo na Mwenyezi Mungu Atakubariki sana ...
 
shida yangu na huruma yangu nimeieleza vizuri sana ndani ya bandiko..

wala hakuna mahali nimeilaumu serikali...

wala sijashauri serikali ifanye nini..

ni raia yangu ikiwa una ndugu, jamaa, rafiki ama vinginevyo anaeweza kua miongoni mwa wanapitia sahibu hizi za kausha damu, help him njia njema za kutoka salama humo na Mwenyezi Mungu Atakubariki sana ...
Kupanga ni kuchagua.....shika jembe ukalime .....panda miti matunda...utanishukuru baadae
 
Kupanga ni kuchagua.....shika jembe ukalime .....panda miti matunda...utanishukuru baadae
ushauri mujarabu na wa maana sana huu

For sure ni bidii, subra na ustahimilivu unatoka vizur sana pande izo aise
 
Kausha damu ni mikopo ya yenye urahisi sana upatikanaji wake. Ina vigezo na masharti nafuu sana yanayowezekana kwa wakopaji wengi.

Kwa upande moja inasaidia sana watu wenye shida na malengo ya kujiunua kiuchumi, na wanafanikiwa bila wasiwasi.

Kwa upande mwingine ni mateso, vilio na kusaga meno kwa hiari yao na kwa kujitakia. Aibu, fedheha na dhahama zinawapata wahusika zinatukumba pia tusio husika.
Maana vilio vya shida zisizoisha, malalamiko, manung'uniko na majuto vinasikitisha sana.
Na kiubinadamu tunasaidia kadiri tunavyo jaaliwa na Mungu.

WALIMU wa shule za Msingi wanao elekea kustaafu wamekwama hapa kausha damu. Wanateseka sana.
Kadi za benki, vitambulisho na nyaraka zao muhimu za kazi zimehodhiwa na maofisa kausha damu, kama dhamana kutokana na malimbikizo ya marejesho na riba walizokosa kuzilipa huko nyuma na zinaongezeka kadiri mkopaji anavyochelewa kurejesha.

Muda wa kustaafu ukifika, afisa wa kausha damu na mwalimu mustaafu mguu kwa mguu kufanya clearance za mafao. Na baada ya hapo kausha damu anamkomba vizuri sana mstaafu huyu malimbikizo ya marejesho na riba, na akimuachia pumzi kidogo ya kupigia miyayo kwa muda mfupi tu ujao...

Watu hawa wasaidiwe, kustaafu sio tiketi ya kufa. Bado wanastahili kuishi kwa furaha na Amani ndugu zetu hawa.
Dawa ni moja tu.Kuwalaani kwa nguvu zote kila kukicha mpaka mungu aseme nao
 
Back
Top Bottom