Kifaa cha zima moto kisichohitaji maji chazinduliwa

Kakke

JF-Expert Member
Dec 4, 2010
1,883
1,482
Posted on April 25, 2012 by www.mzalendo.net
Kamishna Ali Abadalla kushoto akiangalia kifaa kipya cha kuzimia moto kijulikanacho kama DSPA 5 kutoka kwa askari wa kikosi cha Zima Moto na Uokozi katika hafla ya uzinduzi wa kifaa hicho hapo Maisara Mjini Zanzibar

KIKOSI Cha Zima Moto na Uokozi Zanzibar jana kimezindua kifaa kipya cha kisasa cha kuzimia moto kisichotumia maji kiitwacho Dry Sprinkler Powder Aerosol (DSPA5). Kifaa hicho ambacho huzima moto ndani ya dakika mbili baada ya ya kutumbuliwa nyuzi zake kwa kwa sekunde nane kina uwezo wa kutumika na kudumu kwa miaka 15 bila kuharibika bada ya kukinunua. Uzinduzi wa kifaa hicho umefanyika Maisara Mjini Zanzibar mbele ya Naibu Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, Issa Haji Ussi pamoja na makamanda mbali mbali wa vikosi vya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na makamishina kutoka vikosi vyote.

Ussi alisema kupatikana kwa kifaa hicho kutasaidia kwa kisi kikubwa majanga ya moto yanayotokea hapa Zanzibar hasa kwa kuzingatia magari ya zima moto yaliopo ni kidogo na hayakidhi haja kutokana na ukumbwa wa mahitaji.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya ‘Your Solution Tanzania LTD' ambayo imeshirikiana na AFG Group ya Uholanzi, Damian George akitoa ufafanuzi wa kifaa hicho cha DSPA alisema kuwa lengo hasa la kifaa hicho ni kuwaonesha wazanzibari na watanzania namna ya kukitumia.

Alisema DSPA ni muhimu kutumika pale inapokea janga la moto ambapo hutumika kwa kuzima moto bila ya kutumia maji ya aina yoyote na kinapofunguliwa huzima moto unaowaka.

Akiwatoa wasiwasi watu walifika kushuhudia kifaa hicho na maafisa wa serikali na vikosi vya SMZ, George alisema DSPA ni teknolojia ya kisasa ambayo haina madhara yoyote ya kiafya wakati wa uzimaji moto hata pale mtu atakapokuwa yupo ndani wakati wa uzimaji wa moto huo.

George alisema kifaa hicho kwa nchi za Afrika, Tanzania imekuwa nchi ya kwaza kufika ambacho huzima moto kwenye chumba chenye ukubwa wa mita 100 za mraba kwa DSPA 5 moja yenye uzito wa kilo moja ambapo uwezo wake wa kufanya kazi ni mkubwa na huchukua muda wa miaka 15 bila ya kuharibika.

Akitoa shukrani katika uzinduzi huo Kamishina wa kikosi hicho, Ali Abdalla alisema amefurahi sana kuwa kifaa hicho kimekuja wakati muafaka na ni njia mbadala ya kuzimia moto baada ya magari ya kawaida kutumika hapa Zanzibar.

Alisema kutokana na kuwepo kwa matukio mbali mbali ya kuwaka kwa majengo ya Serikali, taasisi za kijamii na hata baadhi ya nyumba za makaazi ya watu binafsi hivyo kifaa hicho kitakuwa muokozi wa maafa hayo iwapo yatatokea kwa sasa.

Amesema Zanzibar ni Taifa linalohitaji mabadiliko ya kidunia ili kwenda sambamba na dhana za kisasa za uokozi pale ambapo pametokea janga la moto na kwamba hakuna budi kupambana nalo bila ya kuleta maafa mengine kwa jamii na nchi.

"Ni matumaini yetu kwamba kifaa hiki kitatumika vizuri, ni kifaa muhimu kwani hakitumii maji kitasaidia kwa kiasi kikubwa nchini kwetu kwani sisi ni sehemu ya dunia" alisema Kameshina Abdalla.

Kamishna huyo alisema Zanzibar ambayo imekubwa na tatizo kubwa la maji na ukosefu wa magari ya kuzimia moto majanga yanapotokea kifaa hicho kitasaidia kwa kiasi kikubwa utoaji wa huduma hiyo ambayo haitahitaji kupatikana kwa maji.
 
Mbona kakishika kifaa chenyewe kama kinyaa?
Katumia karatasi na vidole vichache tu.

Kwani kina nini?
 
Mbona kakishika kifaa chenyewe kama kinyaa?
Katumia karatasi na vidole vichache tu.

Kwani kina nini?

Hicho alicho shika ni baada ya kuwa kimesha tumika na kilikuwa cha moto maana kilitoka kutumika dakika chache.Nilibahatika kuwepo kwenye eneo la tukio hakika DSPA 5 ni kifaa cha maana na kinahitajika mno katika nchi hii .
 
Hicho alicho shika ni baada ya kuwa kimesha tumika na nilikuwa cha moto .Nilibahatika kuwepo kwenye eneo la tukio hakika DSPA 5 ni kifaa cha maana na kinahitajika mno katika nchi hii .

Mkuu nashukuru sana.
Maana ushamba wangu uliniacha na maswali mengi.
Umenifungua.
 
Ulikua jela nini? Mbona kilizinduliwa zamani sana pale uhamiaji?

Hapana mkuu umepotosha DSPA 5 ilizinduliwa rasmi tarehe 13 March pale viwanja vya fire kona ya Morogoto Rd na UN sasa sijui kama kuna ofisi za Uhamiaji pale kaka .
 
Iseje kuwa kama ilivyokuwa ishu ya speed governer


Kuwa mtu wa kuamini science kaka lakini unaweza kuwatembelea jamaa wako

Quaality Planza West Wing , Second Floor au wapigie simu namba
0767 554433 au 0685 252525 au 0767 500545 then uwasikie wanakupa habari zipi .
 
DSPA 5 pekee haiwezi kuzima moto wa jengo kubwa, bado conventional Zimamoto itumiayo maji inahitajika.
Kuzima moto wa vyumba 10 separate unahitaji DSPA 5 kumi, that is a hidden cost.[ ULAJI]
In short it is cheap kutumia maji kuzima moto, uvivu w kufikiri ndo unatufanya tudhani hiyo Pottasium cloud ndiyo silver bullet ya kuzima moto.
Sijui kwa nini hatujaweza kutengeneza magari ya Zima moto Localy!
Kwa sababu tunaweza kutengeneza Malori ya kubeba Mafuta step inayofuata ni kuinstall powerful water pumps, pressure gauges craneladder king'ola tayari ni gari la zima moto.
Tunaweza anza na very primitive fire trucks na kuendelea kuimprove mpaka tuwafikie.

Tunachokosa ni Will power ya kufanya mambo ya kutusaidia kaa watu huru.
 
Mie sioni tofauti yake na dry powder fire extinguisher! Otherwise kama hii ina uzito wa 1kg that means uwezo wake still ni tofauti na ile ya 15kgs! Nilidhani mnaongelea gari ya zimamoto isiyotumia maji, maana hicho ndo kilio chetu. Japo kutumia maji ni cheaper option ambayo fire yetu inamudu. Wafufue fire horse stations na kuwa wakali kuzisimamia!
Hii naona kama ni promotion ya watu binafsi na biashara zao!
 
DSPA 5 pekee haiwezi kuzima moto wa jengo kubwa, bado conventional Zimamoto itumiayo maji inahitajika.
Kuzima moto wa vyumba 10 separate unahitaji DSPA 5 kumi, that is a hidden cost.[ ULAJI]
In short it is cheap kutumia maji kuzima moto, uvivu w kufikiri ndo unatufanya tudhani hiyo Pottasium cloud ndiyo silver bullet ya kuzima moto.
Sijui kwa nini hatujaweza kutengeneza magari ya Zima moto Localy!
Kwa sababu tunaweza kutengeneza Malori ya kubeba Mafuta step inayofuata ni kuinstall powerful water pumps, pressure gauges craneladder king'ola tayari ni gari la zima moto.
Tunaweza anza na very primitive fire trucks na kuendelea kuimprove mpaka tuwafikie.

Tunachokosa ni Will power ya kufanya mambo ya kutusaidia kaa watu huru.


DSPA 5 moja ambayo ni manual kwa matumizi ya kuzima moto wa ndani ambao siyo conventional ina uzito kwa 5.4kgs.Ubishi wa nini wakati wenzetu hapa Ulaya kote wame kimbilia dspa 5 ? Unaongelea maji ? Duh !!! watu wana achana na maji maana wamegundua maji yanaongeza uharibifu wa mali wakati wa kuzima moto kwa 60-70 % .Ndiyo maana sasa watu wanatumia dspa 5 kwa kuangalia mahali kama Dar mfano mara ngapi watu wa fire na maji wamewahi katika matukio ? Na elewa dspa 5 ina fight moto mkubwa kuanzia joto la 700 kwenda juu na si kama hiyo unayo ongelea.DSPA 5 unaituma na inafanya kazi kama n i manual na automatic it goes on yenyewe na kufanya kazi kubwa .Unataka science yake utapewa lakini ubishi huu hauna maana na hakuna ulaji .Mkuu ulaji ni mindset tu si kila kitu ni ulaji .
 
Back
Top Bottom