Kichekesho cha siasa za Ugozi Zanzibar

Kichekesho cha siasa za Ugozi Zanzibar

Hata mimi ninapoingia JF Siingii kuzungumza na mtu mmoja bali naingia kuzungumza na wengi wenye uelewa mdogo na mkubwa...kama nilivyojaliwa na mwana wa Mungu yesu kristu!!

Na kwa jina la Yesu maelezo yangu hueleweka kwa wengi ukiacha maruhani wachache!

HOJA HUJIBIWA KWA HOJA NA SIO KILIO AU VIHOJA!
Hiyo kitu ekundu wasiliana na kahtaan.
 
Msamehe huyo hajui alisemalo, hajui kama CCM haishindwi na haitashindwa kwa vipande vya karatasi. Maisha ni ushindi tena wa vishindo tu labda Ma-Jecha wasiwepo. CCM mbele kwa mbele
Unamkejeli au unamfurahisha?😀😀
 
Kuzunguka kama pia ni kwa kule kwetu ZNZ ni Neno ambalo hutumika kwa kumtanabahisha mtu anafanya/anaongea kitu kile kwa kujirejea sasa sijui wapi nimekuvunjia staha.Tuje historia ya mapinduzi na huko kwa bamkwe mimi babu yangu mzalia baba ni mtumbatu na alikuwa akiuza nyama marikiti darajani pale...na unajua wakati wa alfajiri wanaenda pale na habari za mapinduzi alizisikia wakati yupo marikiti na alikuwa ni HIZBU mkubwa sana alienda kutolewa kwenda masanduku ya kuhifadhia nyama alikojificha na hakuiona familia yake kwa miaka 4. Sasa hizo historia ya ba mkwe na mapinduzi Nimezipata kutoka kwake..lakini hii leo ukiniuliza je ninayakubali mabadiliko yale.. basi jibu langu ndiyo hasa ukizingatia jamii ya kizanzibar iliyokuwa wakati ile basi mabadiliko yalikuwa ni ya lazima ijapokuwa babu yangu alikuwa ni victim wa mabadiliko yale. I'm sorry ya kuwa kuna watu hawana hatia walikufa na wengine wakafungwa na wengine wakakimbia nchi yao. Ukija kuhusu ubaguzi wa uchotara, mama yangu binafsi ni chotara na yeye ni mpemba wa ziwani na mkanyageni..kwa hivyo siongei haya kutokana na chuki yangu binafsi ya machotara au vp. Ubaguzi wa rangi znz upo na utaendelea kuwepo kwani watu wanajisifia Zaidi makabila ya babu zao.. (pengine ni 1/8 ni muarabu) kuliko uzanzibar wao na hao wanajiona wao wako noble Zaidi kuliko watu wengine.Na tuje ubaguzi mwengine wa upemba na uunguja huu watu wanafikiria umeenza baada ya vyama vingi but kusema kweli huu ubaguzi upo tangu zamani na nimeweza kuuushuhudia tangu nikiwa mdogo kwani kuna kipindi Fulani nililelewa na babu/bibi kwa mama yangu. Na mpaka 1995 nilikuwa mfuasi mzuri wa CUF mpaka ilipotokea event moja kuanzia hapo nikaona hichi chama hakifai kwa wazanzibar kwani ilikuwamanifestation yake ni Pembas movement na hao wengine wote ambao si wapemba just si wasindikizaji tu na siyo priority. Kwa hivyo kama unataka kuongelea suala la ubaguzi znz usisome kwenye magazeti au kuangalia vyombo vya habari nenda znz na kaa na ile jamii ya kizanzibari na utaona jinsi gani ubaguzi unavyoivuruga nchi.. tena kwa pande zote mbili... na ndiyo maana mimi ni muumini mkubwa wa muungano kwanibila ya muungano znz ni somali
Hongera kwa maoni mazuri kabisa. Matatizo ya Znz si ya vyama vya siasa bali ni ubaguzi baina ya jamii za kizanzibari. Amani iliyopo Znz, inatokana na muungano, kwa hiyo si amani ya kweli. Badala ya wazanzibari kuhangaika na muungano na kero zake, watafute kwanza ufumbuzi wa ubaguzi unaoitafuna jamii ya wazanzibari. Kinyume cha hapo naiona Ivory Coast jirani kabisa ikiwa muungano utatoweka.
 
Miaka ya nyuma nilibahatika kwenye masomoni katika mojawapo ya nchi za ulaya mashariki. Kule tulikwenda wanafunzi wengi kutoka bara na visiwani. Kilichokuwa kikinishangaza ni kuona kuwa zile sherehe za mwisho wa mwaka, kunakuwepo na utengano wa dhahiri. Wanafunzi kutoka Tanzania bara wanafanya sherehe ya mwaka mpya katika ukumbi fulani wa hostel ya chuo ambacho kina watu wengi wa bara. Wale wa kutoka Unguja na Pemba wanakusanyika katika hostel nyingine wakifurahia peke yao. Lakini ukikaa sehemu na mwanafunzi kutoka Unguja anawaponda sana wale kutoka Pemba. Ingawa wakati wa sherehe za mwaka mpya muunguja huyo huyo anasherehekea pamoja na mpemba. Na anapokuja afisa wa serikali ya muungano wa Tanzania kwa ajili ya kuwatembelea wanafunzi wa kitanzania, wote kwa pamoja yaani watu wa bara na wale wa visiwani, mnakusanyika pamoja kwa ajili ya mkutano.

Haifai pia kuwasema sana wenyeji wa Unguja na Pemba, hata huku bara tunao ubaguzi mbaya pia. Unakuta kwenye sherehe ya mwaka mpya inayoandaliwa na wajumbe wa jumuia fulani ya kikatoliki, labda tuseme mbezi beach, kunakuwepo na wachaga na wahaya kama ndio asilimia 95 ya wanajumuia. Wakati sherehe ikiwa inaendelea, taratibu utawaona wahaya wanajitenga na kukaa peke yao na wachaga nao watajitenga na kukaa peke yao huku wakiongea mambo mbalimbali ya kimaisha. Lakini hao wachaga na wahaya wote ni wanajumuia, wanaokutanishwa na lengo moja.

Nachojaribu kusema ni kwamba kinachopaswa kupingwa kwa nguvu zote ni ile roho ya kibaguzi, kwani ni ya kupigwa vita. Ubaguzi uliopo miongoni mwa waunguja na wapemba, ndio huwa mara kwa mara unajitokeza miongoni mwa wahaya na wachaga. Ndio huo huo unajitokeza kati ya wafugaji wa kimasai na wenyeji wa Morogoro. Ubaguzi una madhara makubwa lakini siku zote huachiwa taratibu, pengine kwa kupuuzwa tu.
 
Kitu gani kinakufanya udhani kuna siasa za kikabila na kikanda?

Kama zipo, kwa nini unadhani zinawalenga wenyeji wa Kilimanjaro na Arusha?

..ccm baada ya kuona cdm inaanza kukubalika kwa kasi, wakaamua kuwazushia kwamba ni chama cha Wachaga.

..baadaye wakaja na msamiati wa "wa kaskazini" wakilenga wa-Tz wenyeji wa mikoa ya Kilimanjaro, Manyara, na Arusha.

..hata mtoto wa Raisi Kikwete, ambaye ni mbunge wa Bagamoyo, amewahi kunukuliwa akitoa kauli za kibaguzi kwamba Tanzania haiwezi kuongozwa na mtu wa "kaskazini", akilenga wa-Tz wenyeji wa mikoa hiyo niliyoitaja.

..Mh.MOHAMED SEIF KHATIB, mjumbe wa kamati kuu ya ccm, na mratibu wa zoezi la kutafuta mgombea Uraisi wa CCM, amewahi kuandika makala mbaya sana ya kibaguzi dhidi ya wa-Tz anaowaita " wa kaskazini ". Yeye alikwenda mbali hata kuwananga wana-CCM wazaliwa wa mikoa hiyo ya Kaskazini.

..Ukija kwenye kampeni za CCM napo ubaguzi ulikuwa waziwazi. Watu walipanda majukwaani kwa niaba ya Dr.Magufuli na kutoa kauli za kibaguzi hazijawahi kutolewa wakati wowote ule ktk uhai wa taifa hili.

cc Nguruvi3, Mohamed Said
 
CCM haitaki Machotara

CCM haitaki wachaga

CCM hii hii ndiyo kinajiita chama cha waafrika...Yaani watu weusi...aiseee
 
Aliyesema CCM imeshindwa Uchaguzi Zanzibar ni nani na kwa mamlaka gani...hivi ukiitwa mchochezi utasema unaonewa?Tuchunge kauli zetu hata kama tunatawaliwa na itikadi zetu!

Makala yako umeiharibu hapo chini tu...

wakati mwingine uwe unaficha hata kidogo huo upumb.avu wako
 
..ccm baada ya kuona cdm inaanza kukubalika kwa kasi, wakaamua kuwazushia kwamba ni chama cha Wachaga.

..baadaye wakaja na msamiati wa "wa kaskazini" wakilenga wa-Tz wenyeji wa mikoa ya Kilimanjaro, Manyara, na Arusha.

..hata mtoto wa Raisi Kikwete, ambaye ni mbunge wa Bagamoyo, amewahi kunukuliwa akitoa kauli za kibaguzi kwamba Tanzania haiwezi kuongozwa na mtu wa "kaskazini", akilenga wa-Tz wenyeji wa mikoa hiyo niliyoitaja.

..Mh.MOHAMED SEIF KHATIB, mjumbe wa kamati kuu ya ccm, na mratibu wa zoezi la kutafuta mgombea Uraisi wa CCM, amewahi kuandika makala mbaya sana ya kibaguzi dhidi ya wa-Tz anaowaita " wa kaskazini ". Yeye alikwenda mbali hata kuwananga wana-CCM wazaliwa wa mikoa hiyo ya Kaskazini.

..Ukija kwenye kampeni za CCM napo ubaguzi ulikuwa waziwazi. Watu walipanda majukwaani kwa niaba ya Dr.Magufuli na kutoa kauli za kibaguzi hazijawahi kutolewa wakati wowote ule ktk uhai wa taifa hili.

cc Nguruvi3, Mohamed Said
Mkuu CCM wanapandikiza mbegu mbaya sana ya chuki. Walianza na udini, sasa ni ukanda
Wamejenga chuki dhidi ya wananchi wa kanda nyingine.

CCM haina tatizo la rangi, wenye matatizo ni watu wa rangi waliomo ndani ya CCM asili
Hivi leo wanajisikiaje wakiwa na CCM inayotambua na kubagua uchotara?

Hivi wananchama wa CCM walio na rangi wanajiasikiaje!!!

Shein analalamika uchaguzi, hakulaani bango la uchotara.
Leo halioni tatizo kesho itakuwaje?

Talaa watoto wa hao wazawa wakakioa au kuolewa na 'chotara' maana yake wajukuu watapoteza uzawa wao!!

Hizi siasa muflisi sijui zinamsaidia nani! Watu hawaoni umbali zaidi ya pua zao!
 
Hongera kwa maoni mazuri kabisa. Matatizo ya Znz si ya vyama vya siasa bali ni ubaguzi baina ya jamii za kizanzibari. Amani iliyopo Znz, inatokana na muungano, kwa hiyo si amani ya kweli. Badala ya wazanzibari kuhangaika na muungano na kero zake, watafute kwanza ufumbuzi wa ubaguzi unaoitafuna jamii ya wazanzibari. Kinyume cha hapo naiona Ivory Coast jirani kabisa ikiwa muungano utatoweka.
Ubaguzi wenyewe unachochewa na muungano vyereje ukivunjika hakuna amani?
Una lelewa na chama cha muungano, miungano ni ccm ..sio watu ..
 
Aliyesema CCM imeshindwa Uchaguzi Zanzibar ni nani na kwa mamlaka gani...hivi ukiitwa mchochezi utasema unaonewa?Tuchunge kauli zetu hata kama tunatawaliwa na itikadi zetu!

Makala yako umeiharibu hapo chini tu...
Kwa uwezo wako mkubwa wa kufikiria hilo bango la machotara na hii kauli ya mwandishi ipi ya kichokozi? Try just a sec to use your brain to think abt that pls
 
Aliyesema CCM imeshindwa Uchaguzi Zanzibar ni nani na kwa mamlaka gani...hivi ukiitwa mchochezi utasema unaonewa?Tuchunge kauli zetu hata kama tunatawaliwa na itikadi zetu!

Makala yako umeiharibu hapo chini tu...
Wewe ni nani hadi uhukumu kuwa makala yake kaharibu?kama mchochezi mgemshitaki kwanza huyo mnaye mgwaya seif sharifu ndiye aliyejitangaza kuwa kashinda kwa kutoa mchanganuo wa kura kwa upande wa zanzibar wacha kuendekeza ujinga kila wakati
 
Jingalao,
Mwaka wa 2011 nilishiriki katika kipindi cha Meza ya Duara kinachoendeshwa na
Sauti ya Ujerumani.

Washiriki wengine wenzangu walikuwa Salehe Feruzi wa CCM Zanzibar, Ahmed Rajab (London),
Dr. Harith Ghassany (Washington DC) na mimi nikizungumza kutoka Tanga.

Mwenyekiti alikuwa Othman Miraj kutoka Bonn aliyetuunganisha kwa simu.

Nilimwambia Salehe Feruzi hayo niliyoeleza hapa kuwa CCM Zanzibar hawajapatapo kushinda
uchaguzi.

Bwana Feruzi akaniomba ushahidi kama unavyoniomba wewe hii leo.
Nikamwambia kuwa inasikitisha kuwa yeye kiongozi wa juu wa CCM Zanzibar lakini hajui hilo.

Nikamuongozea kitu kingine.

Nikamwambia kuwa CCM Zanzibar wanaogopa uchaguzi na nikamweleza yale wanayofanya
kuwazuia wafuasi wa CUF kujiandikisha katika daftari la wapiga kura.

Baada ya haya ndipo nikamkumbusha barua ya Ali Ameir katika uchaguzi wa mwaka wa 1995
baada ya CCM kushindwa waliyakataa matokeo.

Haya yote niliyosema hapa ni kweli wala si ushabiki.
Tujadili haya kabla hatujakwenda mbele katika chaguzi zilizofuatia.
Mkuu naona humjui jinga lao maana kama unge mjua wala husinge poteza muda na nguvu zako kumjibu mambo yoote hayo,kifupi huyo ni vuvuzela tu wa lumumba hata useme ukweli gani hatakuelewa tu
 
Mkuu hebu kuwa muungwana...mada yako inahusu ubaguzi ni mada nzuri sana...lakini umeingiza ushabiki kwa kusema ccm Zanzibar haijashinda ...sielewi umetumia utafiti gani na kama ni sahihi kutumia utafiti kutangaza kuwa ccm haijashinda...labda ungesema kwa mujibu wa CUF ...CCM haijashinda nisingekutaka ufute hiyo kauli.

kuna muda tuweke ushabiki pembeni...hata mimi siwezi kusema mshindi kwa kuwa mwenye mamlaka hayo hajatangaza mshindi!!

Hata huku bara wafuasi wa UKAWA wanaamini wameshinda lakini NEC ndiye aliyetutangazia mshindi.

Nakushauri ufute hiko kipengele halafu turejee kwenye mjadala wa ubaguzi kulingana na ushahidi' ulioleta
Wewe nani eti nakushauri ufute kipengele fulani,huo ndio upuuzi wa lumumba mtu husiposifia ccm basi wewe ni mnafiki,ukiisifia ccm hata kwa uongo mtupu unapigiwa vigeregere
 
Mkuu naona humjui jinga lao maana kama unge mjua wala husinge poteza muda na nguvu zako kumjibu mambo yoote hayo,kifupi huyo ni vuvuzela tu wa lumumba hata useme ukweli gani hatakuelewa tu
Mmawia,
Juu ya hayo yote kuhusu hawa ndugu zetu mimi bado naamini kuwa
tuna wajibu wa kuwaeleza ukweli wa mambo.

Asakheri katika hili huenda tija ikapatikana.
 
Mmawia,
Juu ya hayo yote kuhusu hawa ndugu zetu mimi bado naamini kuwa
tuna wajibu wa kuwaeleza ukweli wa mambo.

Asakheri katika hili huenda tija ikapatikana.
Wapo watu wa kuwaelimisha sawa lkn siyo huyo jingalao
 
Back
Top Bottom