Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 23,288
- 33,882
- Thread starter
- #41
Kizibao,Kuzunguka kama pia ni kwa kule kwetu ZNZ ni Neno ambalo hutumika kwa kumtanabahisha mtu anafanya/anaongea kitu kile kwa kujirejea sasa sijui wapi nimekuvunjia staha.Tuje historia ya mapinduzi na huko kwa bamkwe mimi babu yangu mzalia baba ni mtumbatu na alikuwa akiuza nyama marikiti darajani pale...na unajua wakati wa alfajiri wanaenda pale na habari za mapinduzi alizisikia wakati yupo marikiti na alikuwa ni HIZBU mkubwa sana alienda kutolewa kwenda masanduku ya kuhifadhia nyama alikojificha na hakuiona familia yake kwa miaka 4. Sasa hizo historia ya ba mkwe na mapinduzi Nimezipata kutoka kwake..lakini hii leo ukiniuliza je ninayakubali mabadiliko yale.. basi jibu langu ndiyo hasa ukizingatia jamii ya kizanzibar iliyokuwa wakati ile basi mabadiliko yalikuwa ni ya lazima ijapokuwa babu yangu alikuwa ni victim wa mabadiliko yale. I'm sorry ya kuwa kuna watu hawana hatia walikufa na wengine wakafungwa na wengine wakakimbia nchi yao. Ukija kuhusu ubaguzi wa uchotara, mama yangu binafsi ni chotara na yeye ni mpemba wa ziwani na mkanyageni..kwa hivyo siongei haya kutokana na chuki yangu binafsi ya machotara au vp. Ubaguzi wa rangi znz upo na utaendelea kuwepo kwani watu wanajisifia Zaidi makabila ya babu zao.. (pengine ni 1/8 ni muarabu) kuliko uzanzibar wao na hao wanajiona wao wako noble Zaidi kuliko watu wengine.Na tuje ubaguzi mwengine wa upemba na uunguja huu watu wanafikiria umeenza baada ya vyama vingi but kusema kweli huu ubaguzi upo tangu zamani na nimeweza kuuushuhudia tangu nikiwa mdogo kwani kuna kipindi Fulani nililelewa na babu/bibi kwa mama yangu. Na mpaka 1995 nilikuwa mfuasi mzuri wa CUF mpaka ilipotokea event moja kuanzia hapo nikaona hichi chama hakifai kwa wazanzibar kwani ilikuwamanifestation yake ni Pembas movement na hao wengine wote ambao si wapemba just si wasindikizaji tu na siyo priority. Kwa hivyo kama unataka kuongelea suala la ubaguzi znz usisome kwenye magazeti au kuangalia vyombo vya habari nenda znz na kaa na ile jamii ya kizanzibari na utaona jinsi gani ubaguzi unavyoivuruga nchi.. tena kwa pande zote mbili... na ndiyo maana mimi ni muumini mkubwa wa muungano kwanibila ya muungano znz ni somali
Umekuja na mengine kabisa na mimi nakushukuru kwa hilo.
Mimi kama wewe napenda muungano kwani umoja una faida nyingi sana.
Kuhusu kuja Zanzibar mie sina haja ya kuja.
Zanzibar ni kwetu pia yaani ''second home.''
Hili sikuanza mimi.
Baba yangu alikuwa rafiki mkubwa wa Jaha Ubwa na Abdulaziz Twala katika
1950s wakati huo wote ni vijana.
Mimi nina marafiki-ndugu Zanzibar.
Nadhani tumeelewana.