Salary Slip
Platinum Member
- Apr 3, 2012
- 52,167
- 162,602
- Thread starter
- #81
Gazeti la Mtanzania Jumapili leo limeibuka na habari moja kwenye ukurasa wake wa mbele yenye kichwa cha habari:"Kibanda aliteswa na majasusi".
Katika habari hii ya leo gazeti hili limegusa idara ya usalama wa Taifa kama ilivyokuwa kwa Mwanahalisi kabla ya kufungiwa.Aya moja katika habari hii inasema hivi:"Sasa kuna kila dalili zinazoonyesha kuwa utekelezaji wa mpango wa kumteka na kumtesa kinyama Mhariri Mtendaji Mkuu wa kampuni ya New Habari(2006) LTD,Absalom Kibanda,ulifanywa na watu waliopata mafunzo wanayopewa maofisa usalama wa Taifa,Makachero wa Jeshi au wale wa Polisi,Mtanzania Jumapili linaripoti"
Sasa wadau kwa taarifa kama hii gazeti hili kweli litabaki salama?Gazeti halijatuhumu moja kwa moja idara hizo lakini limesema kitendo hicho kimefanywa na watu wanaopewa mafunzo ya maofisa usalama wa Taifa,Makachero wa Jeshi au Polisi.
Binafsi, sioni tatizo lolote katika taarifa hiyo kwani haijatuhumu moja kwa moja mtu yoyote wala idara yoyote ile ya serikali.
Swali,je hawataachwa kutishwa?
Idara husika za serikali ikiwemo Idara ya Habari na Maelezo zitakaa kimya?
Katika habari hii ya leo gazeti hili limegusa idara ya usalama wa Taifa kama ilivyokuwa kwa Mwanahalisi kabla ya kufungiwa.Aya moja katika habari hii inasema hivi:"Sasa kuna kila dalili zinazoonyesha kuwa utekelezaji wa mpango wa kumteka na kumtesa kinyama Mhariri Mtendaji Mkuu wa kampuni ya New Habari(2006) LTD,Absalom Kibanda,ulifanywa na watu waliopata mafunzo wanayopewa maofisa usalama wa Taifa,Makachero wa Jeshi au wale wa Polisi,Mtanzania Jumapili linaripoti"
Sasa wadau kwa taarifa kama hii gazeti hili kweli litabaki salama?Gazeti halijatuhumu moja kwa moja idara hizo lakini limesema kitendo hicho kimefanywa na watu wanaopewa mafunzo ya maofisa usalama wa Taifa,Makachero wa Jeshi au Polisi.
Binafsi, sioni tatizo lolote katika taarifa hiyo kwani haijatuhumu moja kwa moja mtu yoyote wala idara yoyote ile ya serikali.
Swali,je hawataachwa kutishwa?
Idara husika za serikali ikiwemo Idara ya Habari na Maelezo zitakaa kimya?