Kesi ya Lissu: Mawakili wa Jamhuri hawajarudi kwenye chumba cha Mahakamani kuendelea na Kesi

Kesi ya Lissu: Mawakili wa Jamhuri hawajarudi kwenye chumba cha Mahakamani kuendelea na Kesi

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,499
Wakuu

Inadaiwa mawakili wa Jamhuri hawajaonekana na hawajarudi Mahakamani mpaka muda huu.

Karani amesimama na kuseeleza kuwa kuna jambo limejitokeza anaenda kutafuta ufafanuzi kwa msajili wa mahakama na atarudi kuleta mrejesho.

1771930308117.png

Mwenendo wa Kesi > Kesi ya Lissu: Mahakama yatupilia mbali ombi la Jamhuri la kuongeza ushahidi

Kesi iliahirishwa leo majira ya saa nne na dakika 10 mpaka saa tano kamili ambapo ni baada ya Jamhuri kuomba muda kutafakari uamuzi mdogo uliotolewa na mahakama ambao ulikataa kupokelewa kwa notisi ya ushahidi kutokana na kwamba haikidhi sifa kwa mujibu wa Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai kifungu cha 308(1,2,3 na 4).

Mpaka hivi sasa(1:18PM) bado Mahakama haijarejea. Viongozi, wanachama, wafuasi wa Lissu wadau wa sheria bado wapo katika chumba cha mahakama kusubiri mwendelezo wa kesi hiyo.


Wananchi waliofika Mahakamani majira ya Saa saba na nusu mchana wameanza kuimba

Tunaitakaaaaa Jamhuri!…

Tunataitaka Jamhuriiiiiiii!….

Tunaitaaka Jamhuriiii!…
 
Wakuu

Inadaiwa mawakili wa Jamhuri hawajaonekana na hawajarudi Mahakamani mpaka muda huu.

Karani amesimama na kuseeleza kuwa kuna jambo limejitokeza anaenda kutafuta ufafanuzi kwa msajili wa mahakama na atarudi kuleta mrejesho.

Mwenendo wa Kesi > Kesi ya Lissu: Mahakama yatupilia mbali ombi la Jamhuri la kuongeza ushahidi

Wananchi waliofika Mahakamani majira ya Saa saba na nusu mchana wameanza kuimba

Tunaitakaaaaa Jamhuri!…

Tunataitaka Jamhuriiiiiiii!….

Tunaitaaka Jamhuriiii!…
Screenshot_20260224-131356~2.png
 
Bado naendelea kuwashauri hao mawakili, hata wao ni binadamu kama alivyo mh Lissu na watu wengineo

WANA moyo, damu na mwili, wana utashi na akili inayowapa kujitathimini ikiwa ni kweli wanachomfanyia mwenzao ambaye no ukweli, hana deni lolote kwa awaye yote, je ingelikuwa ni wao ingekuweje?

Waache Nafsi zao zitawale maamzi yao,

Iwapo wakienda na wasirudi kabisa na kesi ikafutwa, watakuwa wamejitendea haki
 
Wameamua kukimbia uwanja ingekua Lissu ndio kachelewa taarifa ingetangazwa hadi kwenye radio za mbao na kuongezewa kesi ingine..
Wanaojiona wana mamlaka ndiyo shida yao moja hiyo. Ukifanya wewe ni kosa na wanahamaki. Wao wanaweza kufanya kitu hicho hicho na wakaona ni sawa na hawataki hata uwahoji.
 
Wanapoteza muda tu ili wamshikilie muda mrefu zaidi.
 
Back
Top Bottom