Umeona udhaifu wa shahidi vizuri kabisa. Anaulizwa kwanini baada ya kukiri makosa yake hawakumpeleka kwa mlinzi wa amani. Anajibu: hatukutaka kupoteza muda tulikuwa tunataka kuhakikisha ugaidi hautokei. Anasahau hata shahidi mwenzake aliulizwa kama kuna taarifa zozote kwa wakuu wa polisi wa maeneo lengwa, jibu hakuna. Kama walengwa (Sabaya) walifahamishwa kuhusu kutafutwa kwao kutendwa ubaya, hapana. Kama walitoa taarifa kwa kamati za usalama za wilaya au mkoa, hapana. Sasa sijui ni hawa watu wanne tu walikuwa na jukumu la kuzuia ugaidi nchi nzima???
Tuna polisi wa ajabu sana. Na bahati mbaya huyu shahidi nae amesimamishwa kazi kwa kubambikizia mtu kesi!!