ebbyramadhani
Senior Member
- Jan 5, 2017
- 101
- 109
Habari za weekend wakuu, Tusaidiane kufikisha Hii taarifa ya adha inayowakumba wakazi wa Majohe kwa muda mrefu sana kuhusiana na ubovu wa barabara kuanzia shule ya sekondary Halisi mpaka kituo cha kwa mjeshi.
Barabara hii ni mbovu mno kupelekea vyombo mbali mbali vya usafiri ikiwemo usafiri wa umma kushindwa kupita hivyo kufanya magari kukatisha ruti njiani kukwepa eneo hilo ambalo ni korofi sana.
Wananchi wanalazimika kutembea kutoka Halisi mpaka Majohe kwa Mpemba ambapo ndo dalada ilipaswa kufika hapo kama kawaida ya mwanzoni kabla ya adha hii.
Kutoka Halisi mpaka kwa mpemba kuna km takriban zisizopungua 3.
Ubovu wa eneo hili unatokana barabara kutokuwa na mitaro na madaraja kwaajili ya kuvusha maji yanayotoka mitaani Hivyo kupelekea mvua zinaponyesha eneo hili linaharibika mara kwa mara.
Jitihada kubwa zinahitajika kusaidia wananchi wa Majohe kuweza kutatuliwa kero hii.
Barabara hii ni mbovu mno kupelekea vyombo mbali mbali vya usafiri ikiwemo usafiri wa umma kushindwa kupita hivyo kufanya magari kukatisha ruti njiani kukwepa eneo hilo ambalo ni korofi sana.
Wananchi wanalazimika kutembea kutoka Halisi mpaka Majohe kwa Mpemba ambapo ndo dalada ilipaswa kufika hapo kama kawaida ya mwanzoni kabla ya adha hii.
Kutoka Halisi mpaka kwa mpemba kuna km takriban zisizopungua 3.
Ubovu wa eneo hili unatokana barabara kutokuwa na mitaro na madaraja kwaajili ya kuvusha maji yanayotoka mitaani Hivyo kupelekea mvua zinaponyesha eneo hili linaharibika mara kwa mara.
Jitihada kubwa zinahitajika kusaidia wananchi wa Majohe kuweza kutatuliwa kero hii.