Kero: Tabia ya ajabu Mbeya kuchangisha pesa za misiba imezidi mno

sky soldier

JF-Expert Member
Mar 30, 2020
5,408
19,038
Binafsi niweke wazi kabisa kwamba napenda kuishi kijamii na wala sinaga tatizo na misiba ila hali ya mbeya imezidi sana

Sasa kwa huku Mbeya hali ya misiba imekuwa tofauti sana, watu hawajali kushiriki kwako msibani hawakwambii hata msiba ulipo mpaka uwauilze na hata hawajali ukaribu wako na mfiwa, kinachopewa kipaumbele ni mchango wako pesa, na huna budi inabidi uchange tu kukwepa lawama kwamba hauna ushirikiano kwenye jamii.

Kisingizio huwa ni pale wanakwambia inakubidi uchangie lasivyo siku ukipata msiba watakususia..Huu ni upuuzi mkubwa, hivi mtu ninayemchangia ambaye hata sijaenda kwenye mazishi yake na hatujuani kweli ndio nitegemee awe tegemeo kuu kwenye msiba wangu, hapana! Watu naowategemea kwenye msiba wangu ni wale ambao hata wao wakipata misiba huwa inailazimu kupangua ratiba yangu ili niende kuhudhuria msibani, nazungumzia wanafamilia, ndugu, jamaa, marafiki na watu wa karibu, na hata kama ni mtu wa sokoni basi akiwa ni mtu wangubwa karibu ama rafiki wala sihitaji kupitishiwa daftari, ntaenda kuhudhuria msiba au ntampelekea hela mkono kwa mkono au kwa mpesa nikiwa mbali.

Huku maofisini kuna unafuu maana waajiriwa wamechanganyika, Shughuli ipo mitaa yenye wazawa wengi wa Mbeya, maderva wa bajaji, kwenye frem za maduka, n.k

Nina frem yangu pale soko kuu la Mwanjelwa nimemweka binti yani kwa wiki ni mara 4, niliwahi pia kushinda hapo na kweli nikajiridhisha, wanakuja watu wa sokoni pale pale (ni wazawa wa Mbeya) kama watatu moja kashika picha, mwengine peni na daftari mwengine anawasindikiza, inabidi uchangie tu.

Na bora ingekuwa ni mtu aliyefariki ni mwenye frem, yani unakuta mtu aliyefariki ni ndugu yake mwenye frem na kama mnavyojua wenzetu Wanyakyusa ni kawaida kuwa na ndugu hata 150.

Kuna baadhi ya misiba nimeshuhudia watu wanaingia hadi barabarani wanaomba michango huku msiba unaendelea, hasa misina ya Makunguru, Ilolo, Isanga, n.k.

Pia kwa upande wa bajaji naonaga sana hii, pale pale Mwanjelwa kuna viongozi wao kila siku lazima kuwe na mchango wa msiba.

Hii ni kero sasa.

Hitumisho:michango ifanywe kwa wahusika wenyewe sio kila mtu ahusike kwenye msiba usiomuhusu...
 
Yaani mtu akifariki huo msiba unakuwa kama wa eneo lote.

Hii nmeiona sana mitaani, kwa maderva wa bajaji, kwenye frem za maduka, n.k...
Hayo mbona ni mambo ya kijamii .Sema pia mchango wa msiba au harusi siku zote siyo lazima,isipokuwa kama ni michango ya ujenzi wa madarasa au zahanati.

Siku ukiona umechoshwa unawambia tuu kwamba huhitaji usumbufu.ili na wewe siku ukifiwa unapiga zako kimya tuu wala husumbui watu.unachofanya unapotea tuu kimya kimya kuhudhuria msiba,wakikuuliza mbona ulipotea,unawambia nilienda msibani nilifiwa niliona siyo busara kupitisha bakuli na picha ya marehemu kuwa sumbueni kwa michango ya kijinga.
 
Yaani mtu akifariki huo msiba unakuwa kama wa eneo lote.

Hii nmeiona sana mitaani, kwa maderva wa bajaji, kwenye frem za maduka, n.k...
Kuna wanaochangisha misiba kwa upendo na wengine wanafanya kwa manufaa yao.

Kama mna uongozi wenu hapo soko la mwanjelwa, basi wekeni taratibu za jinsi ya kuchangia. Taratibu hizi zitaainisha nani wa kuchangiwa na kiasi gani. Lazima kila msiba wa kuchangiwa upitie kwa mwenyekiti kwa utambuzi.

Lakini pia, unaweza ukaamua kuchangia sawa sawa na baraka za Mungu zinavyokufikia ilimradi usiwe unaibiwa.
 
Tunapenda kuishi kijamii lakini sasa huwa kuna mambo yanapitiliza, binafsi msiba wa rafiki, ndugu, mwanafamilia, au mtu wa karibu huwa sina shida nayo na huwa sitoi hela tu bali huwa nafunga safari kabisa kwenda huko msibani....
Usiwalaumu ndugu yang, hiyo tabia ya kuomba omba na kuchangishana kila wakati wameiga kutoka chadema. Kumbuka Mbeya ni moja ya ngome za chadema na wengi wanaishi kwa kufuata misingi na tabia za viongozi wa chama.
 
Mbeya jiji la kijinga Sana!! Watu wanaishi maisha ya kijima enzi hizo bado tukiwa nyani sijui sokwe hutujabadilika na kuwa watu,

Wanyakusya hovyo sana , michango ya kijinga kijinga mingi .

Badilikeni nyie
 
Usiwalaumu ndugu yang, hiyo tabia ya kuomba omba na kuchangishana kila wakati wameiga kutoka chadema. Kumbuka Mbeya ni moja ya ngome za chadema na wengi wanaishi kwa kufuata misingi na tabia za viongozi wa chama.
Acha kuleta ajenda zako za kijinga mkuu, inhekuwa hivi basi huko Moshi, Arusha, Mara, n.k wangekuwa na hizi tabia.
 
Changia na uache kulia lia
Siku ukipata msiba watakususia..
Ndio wanavosemaga hivi hivi ila hii point haina uzito kabisa.

Binafai huwa mahudhuria na kuchanga misiba ya wanafamilia, ndugu, jamaa, marafiki na watu wa karibu, hawa wananitosha sana tu maana huwa nahudhuria kabisa misiba yao, michango inakuaga ishu za ziada tu
 
Hayo mbona ni mambo ya kijamii .Sema pia mchango wa msiba au harusi siku zote siyo lazima,isipokuwa kama ni michango ya ujenzi wa madarasa au zahanati.

Siku ukiona umechoshwa unawambia tuu kwamba huhitaji usumbufu.ili na wewe siku ukifiwa unapiga zako kimya tuu wala husumbui watu.unachofanya unapotea tuu kimya kimya kuhudhuria msiba,wakikuuliza mbona ulipotea,unawambia nilienda msibani nilifiwa niliona siyo busara kupitisha bakuli na picha ya marehemu kuwa sumbueni kwa michango ya kijinga.

Yupo sahihi kabisa maana wengine wanaochangisha ni matapeli na wavuta bangi, hata hiyo pesa haifikishwi kunakohusika! Mitaa ya barabara za Makunguru hadi sokoni Mwanjelwa ni mtindo wa kila siku. Wanazuia hadi magari barabarani, ukionekana hutaki kusimama wanapiga mawe vioo vya gari! Kwa kweli ule ni ushamba kabisa!
 
Kweli kabisa hii tabia imezidi hasa maeneo ya Isanga huko yaani hujui msiba ni wapi ila kila siku wanapita kuchangisha.
Dah mbeya bhana😠😠😠
 
Nakuunga mguu mia kwa mia! Hii tabia inakera sana pale Mbeya! Mwenyewe nimeishi Mby na nimeshuhudia ujinga huu sanaa! Hasa ile barabara ya Makunguru! Na fedha nyingi zinazochangishwa zinasimamiwa na vibaka, hadi wengine wanakuonyesha picha kumbe mtu alikufa miaka mitatu iliyopita au hata wanakurupua tu lipicha la mtu huko studio na kutembeza kuwa ni marehemu! Shenzi kabisa hawa!
 
Yupo sahihi kabisa maana wengine wanaochangisha ni matapeli na wavuta bangi, hata hiyo pesa haifikishwi kunakohusika! Mitaa ya barabara za Makunguru hadi sokoni Mwanjelwa ni mtindo wa kila siku. Wanazuia hadi magari barabarani, ukionekana hutaki kusimama wanapiga mawe vioo vya gari! Kwa kweli ule ni ushamba kabisa!
ohoo! kumbe ni kwa style hiyo,huo ni uharifu mkuu! Serikali iko wapi sasa? hata tuuharifu twa namna hii nato tunahitaji tamko la akamanda Simon Nyakoro Siro?
 
Back
Top Bottom