Kero Kubwa za Watanzania - Changia

Goodrich

JF-Expert Member
Jan 29, 2012
2,091
1,177
Naamini timu nzima ya #WachapaKazi wa Magufuli wapo tayari kuchukua kero zetu #Watanzania na kuzifanyia kazi bila kusita.

Hivyo basi, tuweke kero za msingi hapa.

Mimi naanza na hizi;

1. Mpasuko unaosababishwa na tofauti za kiitikadi.
- Mbali ya wananchi, kuna viongozi wakubwa kabisa ambao hawajitambui. Mpaka leo bado wapo tayari kuona taifa linadidimia ili vyama vyao vistawi. Wapo tayari kutetea ufisadi wakidhani wanalinda chama. Wapo tayari kuminya uhuru wa maoni na kupata habari wakidhani wanalinda chama. Wapo tayari kukwamisha miradi ya maendeleo sehemu zenye itikadi tofauti wakidhani wanalinda chama. Wameweka maslahi ya chama kabla ya maslahi ya taifa.
- Ni wakati wa kuweka Utanzania mbele kuliko itikadi, tumeachwa !.

2. Ufisadi wa kutisha
- viporo vyote vya ufisadi vifanyiwe kazi na mfumo uimarishwe.

3. Bei Kubwa ya Umeme
- Mikataba ya umeme ipitiwe.

4. Miundombinu
- Sehemu kubwa ya Tanzania bado haina miundombinu ya barabara, maji, umeme nk.

5. Mazingira
- Mazingira yetu yanaathiriwa sana na kelele za muziki wa ma bar na vilabu, uchafu, ujenzi holela nk. Kuna jamii zinateswa sana na hii kero ya kelele ambapo inafika mahali hawawezi kufanya shughuli za uzalishaji, elimu nk. Wanashinda mahakamani na kwenye maofisi ya serikali kutafuta ufumbuzi miaka nenda rudi.
- Wizara husika ikomeshe kelele za muziki kwenye makazi ya watu.

6. Mfumo wa Uchumi
- Uchumi wetu umeshikiliwa na unanufaisha tabaka fulani la wachache na wageni kutokana na serikali kutosimamia vyema fursa zinazojitokeza.

7. Madawa ya kulevya
- Madawa ya kulevya yanaua nguvu kazi ya taifa letu.

8. (Endelea ........ )
 
Last edited by a moderator:
Changamoto ktk secta ya afya hasa ktk huduma na matibabu kwa ujumla hasa madawa
 
1-Elemu ya ufundi iboreshwe zaidi ili vijana wakimaliza wasiangalie kuajiliwa bali wajiajili. 2-ili wajiajili vijana wahitim wa vyuo serikali iangalie namna ya kuwawezesha kwa maji. 3-tuige kwa nchi zilizoendelea kama China huwa wanapeleka vijana wao kujifunza vitu ufundi kwa ajili ya taifa..na wakirudi inatakiwa output zionekane wasipoonyesha output wawajibishwe.iwe tofauti na sasa watu wanapelekwa kujifunza ujuzi wanaishia kupiga picha akiwa ulaya Matunda ndani ya nchi Hakuna.
 
(Naomba mods wa stick uzi huu kwa ustawi wa taifa letu)

Naamini timu nzima ya #WachapaKazi wa Magufuli wapo tayari kuchukua kero zetu #Watanzania na kuzifanyia kazi bila kusita.

Hivyo basi, tuweke kero za msingi hapa.

Mimi naanza na hizi;

1. Mpasuko unaosababishwa na tofauti za kiitikadi.
- Tuweke Utanzania mbele kuliko itikadi.

2. Ufisadi wa kutisha
- viporo vyote vya ufisadi vifanyiwe kazi na mfumo uimarishwe.

3. Bei Kubwa ya Umeme
- Mikataba ya umeme ipitiwe.

4. Miundombinu
- Sehemu kubwa ya Tanzania bado haina miundombinu ya barabara, maji, umeme nk.

5. Mazingira
- Mazingira yetu yanaathiriwa sana na kelele za muziki wa ma bar na vilabu, uchafu, ujenzi holela nk.

6. Mfumo wa Uchumi
- Uchumi wetu umeshikiliwa na unanufaisha tabaka fulani la wachache na wageni kutokana na serikali kutosimamia vyema fursa zinazojitokeza.

7. Madawa ya kulevya
- Madawa ya kulevya yanaua nguvu kazi ya taifa letu.

8. (Endelea ........ )
Mbona kero zote wanazijua.Ispokuwa wanapofushwa macho na chama chao! Kama unakumbuka Katibu mkuu mmoja aliwahi ghiribu watu wasiseme Rushwa bali waseme Takrima.Na tukaaminishwa hivyo.Baadhi ya wazee waliamua kukaa kimya kwasababu walikuwa wakitoa maoni yao,walikuwa wakipuuzwa.Katika hayo uliyo yataja hakuna jipya.
 
Hakuna wasichokijua.......wao wafanye.......watakachosahau tutawakumbusha.......tumechoka kuongea kila siku na hakuna kinachofanyika zaidi ya masifa........
 
Chama kujaa uongozi wa juu wa CHAMA kutoka kanda moja ya kaskazini hasa CHADEMA.Magufuli atumbue hilo jipu.
 
MADALADALA KUKATIZA RUTI HILI NI GONJWA SUGU / WAZIRI WAKE SIJUI NI YUPI?
@MAGUFURI TUSAIDIE KWA HILI WAZIRI YUPO KIMYA.
ii
 
Back
Top Bottom