Kenya yafunga mipaka yake na Tanzania na Somalia. Zuio la kutotoka ndani laongezwa kwa siku 21

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,809
11,973
1C04ECEF-E83E-4D0B-8258-0CE06DF2942C.png


Rais Uhuru Kenyatta ametangaza kufungwa kwa mipaka yake na Mataifa ya Tanzania na Somalia kuanzia usiku wa leo kwa siku 30 zijazo

Rais Kenyatta amesema kuwa ni madereva wa magari ya kubeba mizigo pekee ambao wataruhisiwa kuingia nchini Kenya baada ya kupimwa COVID19 na kupatikana kuwa hawana

Amesema kuwa amechukua hatua hiyo baada ya madereva wa malori ya kubeba mizigo 78 raia wa kigeni kunyimwa kibali cha kuingia nchini Kenya baada ya kukutwa na virusi hivyo

Kenya aidha imeongeza muda wa marufuku ya kutoka nje kwa siku 21 zijazo hadi Juni 6
 
Uchawi ni pale mtu anakwambia "Endeleeni kuchapa kazi, nipo pamoja na nyie" wakati kiuhalisia amejificha huku watu wake wakiangakizwa na Corona! Huo ni uchawi namba moja duniani.
Habari ndio hiyo! Hii nchi ina wachawi wazawa wengi kama wewe. Ulitaka awabie watu wakifungie alafu wakiwnza lalamika shida mpate pa kushika. Aendelee kuwanyoosha! Kenya wamefunga mpaka kwa maelezo yako, SO WHAT! Tena usiku saa sita.
 
Kenya yafunga mipaka yake ya upande wa Tanzania na Somalia kwa kipindi cha muda wa siku 30.

Marufuku hiyo ya kuzuia watu kutoka Tanzania na kuingia nchini Kenya inaanza usiku wa leo saa 6 na kuruhusu mizigo tu kupita.

Na kwa upande wa Somalia masharti ni hayo hayo, mizigo peke yake ndio itaruhusiwa.

Aidha madereva watakaoingia nchini Kenya kuleta mizigo watatakiwa kupima corona kwanza.

Kenya imeongeza tena muda wa marufuku ya kutoka nje kwa muda wa siku 21.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom