Kazi za Kujitolea: Kwanini Ufanye, Umuhimu wake, na madhara ya kuzichukulia kwa wepesi

Kaka Pekee

JF-Expert Member
Apr 3, 2018
336
559
Habari Wadau.

Naomba kufungua mazungumzo haya kuzungumzia Suala la Kazi za Kujitolea na Umuhimu wake sambamba na madhara yake unapochukulia kwa wepesi nafasi hizi pindi unapozipata. (Kutokana na uzi huu kutokuwa maandiko matakatifu, ninaweza kurekebishwa, unaweza kutoa mchango chanya na kutoa taarifa jengefu ili kusaidia kuwafumbua macho vijana wenzetu juu ya fursa za kujitolea hususan wanaosubiria Ajira rasmi na wanafunzi wanaokuwa likizo ndefu na fupi)

1.) KAZI ZA KUJITOLEA NI NINI?
Kazi za kujitolea zina maanisha kufanya Shughuli/kazi isiyotegemea malipo (Ujira/Mshahara) ambapo mtu anatoa muda wake kusaidia shughuli/kazi za kijamii, kupitia taasisi au mtu asiyehusiana nae.
Badala ya kutegemea malipo ya pesa (Ujira/ Mshahara) hupata uzoefu na kutengeneza Mtandao (Network) unaoweza kumsaidia katika kazi/taaluma yake hapo baadaye. Baadhi ya Taasisi kulingana na sera zao na majukumu husika hutoa Posho kidogo ya nauli kuwawezesha wafanyakazi wao wa kujitolea (Volunteers)

2.) UMUHIMU WA KAZI ZA KUJITOLEA!

Kazi za kujitolea zina Tija kubwa sana kuliko tunavyofikiria, hii ni katika pande zote BINAFSI, na KIJAMII.

KIBINAFSI : Mtu anayefanya kazi hizi za kujitolea hujiongezea ufahamu na ujuzi zaidi wa shughuli anayoifanya nje ya ajira rasmi, hii inaweza kuwa ni kupitia maombi binafsi ya kujitolea kwa nafasi husika, au kupitia maombi maalum yanayotumwa kwa niaba ya mhusika kupitia Taasisi za elimu ya Juu na Vyuo.( Field Work)

  1. WASIFU-Kujiongezea Ufahamu na Ujuzi zaidi wa shughuli/Kazi humsaidia mhusika kuongeza thamani katika wasifu wake (CV) katika ushindani wa nafasi za kazi.
  2. USHINDANI KATIKA AJIRA- Waajiri wengi siku hizi huangalia Vyeti na Uzoefu pindi unapotuma maombi ya kazi, kupitia hizi hizi kazi za kujitolea unaweza kupenya katika uchaguzi wa awali (Screening) na kuzingatiwa kwa hatua ya Usahili wa ana kwa ana (Personal Interview).
  3. UBOBEZI- Kazi za kujitolea husaidia Mhusika kujiamini zaidi katika uwanja wake wa kazi sababu ya kuwa mbobezi/ mzoefu kutokana na muda wa kufanyia kazi vile alivyojifunza kwa vitendo zaidi, kupata muda wa kufanya makosa na kujirekebisha.
  4. MTANDAO-Pia Mtu anayefanya kazi za kujitolea huwa na wigo mpana wa kufahamiana na watu katika fani, tasnia husika hivyo kutengeneza Mtandao (Network) ambayo huweza kuwa na manufaa baadaye iwapo utautumia vizuri. Watu unaokutana nao hutathimini na kuona utendaji, wanaweza kuwa washauri, walezi wako na kuwa rahisi kwao kukutambulisha kwa wadau wengine zaidi au hata kukupa ajira rasmi...lakini pia hata kuwa rahisi kufanya nao kazi kutokea nje ya taasisi husika iwapo utakuwa na uhitaji.
KIJAMII : Iwapo utakuwa unafanya kazi za kujitolea, faida za jumla zinazoweza kupatikana kijamii ni pamoja na;
  1. MTAZAMO NA KUFANYA MAAMUZI- Kusaidia kumjenga mhusika kimawazo na kimtazamo, kumfanya awe na tija kwa jamii (Mawazo atakayokuwa akitoa huakisi yale anayoyafahamu na watu wanaomzunguka hivyo akifahamu mengi zaidi kwa nadharia na vitendo kutamfanya afikiri na kutoa mawazo chanya, na kushiriki katika kutoa maamuzi) pia kupitia kujishughulisha na kazi kutampunguzia kujihusisha na makundi yasiyo na tija na kumfanya awe Productive.
  2. KUWA SEHEMU YA MAENDELEO- Kazi za kujitolea zinazohusisha jamii husaidia kusukuma mbele gurudumu la maendeleo. Taasisi/ Jumuiya zinazofanya kazi za kujamii humuwezesha kijana anayefanya kazi hizo kuwa sehemu ya maendeleo na kusaidia kufanikisha Maendeleo chanya. (Hata Ukiamua kufanya kazi ya kujitolea kufanya usafi, kuhamasisha vijana kupima nk. inakuwa ni mchango mkubwa sana kijamii)
MADHARA YA KUTOFANYA KAZI ZA KUJITOLEA:

KIBINAFSI:

Hebu Fikiria kuwa umeenda kuomba nafasi ya kazi sehemu (Fresh From College/ Uni) ukiwa na vyeti na sifa zinazostahili kitaaluma kwa nafasi husika halafu unaambiwa huwezi kuchaguliwa sababu huna uzoefu na kazi.
NB: Baadhi ya Taasisi zilizoendelea pia huwa wana utaratibu wa kuchagua Experience Over Academic Qualification kwa sababu mbalimbali.
5 Reasons Why Experience Matters More Than Education

KIJAMII :
Athari inayoweza kupatikana ni kuwa na vijana wengi wasiojishughulisha mtaani na kupelekea makundi yasiyo na tija, sambamba na kudumaza maendeleo kutokana na jamii kuwa tegemezi kwa kukosa watendaji kazi wa kutosha, au hata watoa mawazo jengefu yanayoakisi hali halisi ya kijamii na kiutendaji ili kufanikisha maendeleo.

TATIZO LA KUCHUKULIA KWA WEPESI SUALA HILI:
Iwapo suala la kujitolea likichukuliwa kwa wepesi, na vijana wasipokuwa na muamko wa kujitolea na kuonyesha mfano suala la maendeleo binafsi na kijamii haliwezi kufanikiwa.

Kwa wale wanaopata fursa hizi za kujitolea wanapozitendea haki ni rahisi kufanya Mashirika,taasisi na Jumuiya zetu za kijamii kuona umuhimu wa kuendelea kutoa nafasi zaidi kwa vijana wengine na kufanya nao kazi na kuwa endeleza kupitia ushiriki wao katika mazingira halisi ya kazi.
(Baadhi ya wanaopata kazi hizi za kujitolea huzembea nafasi hizo na kuharibu sifa za wengine ambao ni wachapa kazi na wenye nia ya dhati ya kujifunza wanaotafuta fursa hizi- Unapopata Wasaa wa kufanya shughuli hizi Fanya kwa Moyo na Jitihada zote huenda hapo ndipo utapokuja kupata ajira, kuzoa uzoefu na kuwa bora zaidi au kutengeneza Network zenye manufaa zaidi baadae).

SUALA LA MUDA na WAPI UTAFANYA KAZI ZA KUITOLEA:
Changamoto nyingi za Vijana wenzangu utasikia "Tatizo sina Muda Unaba, sina muda wa kutosha Kufanya kazi za Kujitolea" au "Wapi naweza kwenda Kujitolea?"

Kujitolea hata kwa saa Moja au Mbili tu Kila siku kama upo sehemu sahihi na unafanya kilichokupeleka ina COUNT, mfano: Unajitolea saa moja kuwa kiongozi kanisani, kushiriki katika Vikao vya maendeleo, au Kusaidia Kufundisha katika kituo cha Watoto Yatima mtaani nk. kwako hiyo ni BIG STEP!
Mbali na kufanya kazi za kujitolea, kutana na watu, Ongea nao vizuri badilishana nao mawazo hapo unaweza kuongeza au kupata kitu cha ziada pia.

Iwapo ni Mwanafunzi kipindi cha Likizo unaweza kuomba kushiriki kazi za kujitolea katika kikundi rasmi cha vijana Mtaani kwako/ Serikali ya mtaa au Taasisi iliyo karibu na wewe kisha give it 100% hiyo inaweza kukuinua na kuongeza wigo wa Ufahamu wa mambo pamoja na kujuana na watu wa Tabaka, Rika, Taaluma na Utashi tofauti kisha ukajifunza au wao kujifunza jambo kutoka kwako.

Inafahamika kuwa Kujitolea kuna umiza katika suala la nauli iwapo sehemu ya kazi ni mbali na ulipo ukiwa bado huna chanzo cha uhakika cha mapato na hususani kama sehemu unayofanyia kazi haina utaratibu wa Posho/nauli, ufanikiwa kujiwezesha katika hili hesabu kama ni Investment kwa ajili ya future yako.

Naomba kuwasilisha na karibuni kwa Maswali, Maoni na Ushauri wa kujenga zaidi ili kuangaza jamii yetu Vijana katika kushika hatamu ya maendeleo

Kaka Pekee!
0677679339
 
Habari Wadau.

Naomba kufungua mazungumzo haya kuzungumzia Suala la Kazi za Kujitolea na Umuhimu wake sambamba na madhara yake unapochukulia kwa wepesi nafasi hizi pindi unapozipata. (Kutokana na uzi huu kutokuwa maandiko matakatifu, ninaweza kurekebishwa, unaweza kutoa mchango
Kujitolea kufanya kazi kwa muda usiozidi mwaka mmoja na kuwa na malengo c ujinga bali kujitolea kufanya kazi kwa zaidi ya miaka miwili bila ujira ni upumbavu kwa upotevu wa rasilimali muda
 
Kwa sahiz Bora ,uuze genge lako mtaani baada ya mwaka utaniambia,unaweza jitolea miaka miwili ukaishia kumaliza soli ya kiatu,alafu Alie Anza mishe akawa mbali na vice versa,kwahiyo angalia upepo pia solo la ajira gum
 
kujitolea kufanya kazi kwa muda usiozidi mwaka mmoja na kuwa na malengo c ujinga bali kujitolea kufanya kazi kwa zaidi ya miaka miwili bila ujira ni upumbavu
Hakika, Kuna ambao wakijishikiza sehemu hususani zinazotoa posho kidogo anaridhika napo, kubweteka na kusahau kuwa na ndoto kubwa za kukua zaidi. ni Lazima Ujitolee kwa malengo ya Muda na kuyasimamia
 
Kwa sahiz Bora ,uuze genge lako mtaani baada ya mwaka utaniambia,unaweza jitolea miaka miwili ukaishia kumaliza soli ya kiatu,alafu Alie Anza mishe akawa mbali na vice versa,kwahiyo angalia upepo pia solo la ajira gum
Unaweza pia kujitolea na Kujiajiri baada ya hapo na watu uliofanya kazi kwao wakawa wateja binafsi wa biashara, kazi yako baada ya kutengeneza network nzuri na wao ambao usingewafahamu bila kufanya nao kazi kwa kujitolea. Tuelewe kuwa Kufanya kazi ya kujitolea sehemu hakumaanishi kuwa utaajiriwa hapo, tengeneza mtandao na watu (connection) zoa Ujuzi, practice ulichojifunza kisha angalia malengo mengine.
 
Habari Wadau.

Naomba kufungua mazungumzo haya kuzungumzia Suala la Kazi za Kujitolea na Umuhimu wake sambamba na madhara yake unapochukulia kwa wepesi nafasi hizi pindi unapozipata. (Kutokana na uzi huu kutokuwa maandiko matakatifu, ninaweza kurekebishwa, unaweza kutoa mchango chanya na kutoa taarifa jengefu ili kusaidia kuwafumbua macho vijana wenzetu juu ya fursa za kujitolea hususan wanaosubiria Ajira rasmi na wanafunzi wanaokuwa likizo ndefu na fupi)

1.) KAZI ZA KUJITOLEA NI NINI?
Kazi za kujitolea zina maanisha kufanya Shughuli/kazi isiyotegemea malipo (Ujira/Mshahara) ambapo mtu anatoa muda wake kusaidia shughuli/kazi za kijamii, kupitia taasisi au mtu asiyehusiana nae.
Badala ya kutegemea malipo ya pesa (Ujira/ Mshahara) hupata uzoefu na kutengeneza Mtandao (Network) unaoweza kumsaidia katika kazi/taaluma yake hapo baadaye. Baadhi ya Taasisi kulingana na sera zao na majukumu husika hutoa Posho kidogo ya nauli kuwawezesha wafanyakazi wao wa kujitolea (Volunteers)

2.) UMUHIMU WA KAZI ZA KUJITOLEA!

Kazi za kujitolea zina Tija kubwa sana kuliko tunavyofikiria, hii ni katika pande zote BINAFSI, na KIJAMII.

KIBINAFSI : Mtu anayefanya kazi hizi za kujitolea hujiongezea ufahamu na ujuzi zaidi wa shughuli anayoifanya nje ya ajira rasmi, hii inaweza kuwa ni kupitia maombi binafsi ya kujitolea kwa nafasi husika, au kupitia maombi maalum yanayotumwa kwa niaba ya mhusika kupitia Taasisi za elimu ya Juu na Vyuo.( Field Work)

  1. WASIFU-Kujiongezea Ufahamu na Ujuzi zaidi wa shughuli/Kazi humsaidia mhusika kuongeza thamani katika wasifu wake (CV) katika ushindani wa nafasi za kazi.
  2. USHINDANI KATIKA AJIRA- Waajiri wengi siku hizi huangalia Vyeti na Uzoefu pindi unapotuma maombi ya kazi, kupitia hizi hizi kazi za kujitolea unaweza kupenya katika uchaguzi wa awali (Screening) na kuzingatiwa kwa hatua ya Usahili wa ana kwa ana (Personal Interview).
  3. UBOBEZI- Kazi za kujitolea husaidia Mhusika kujiamini zaidi katika uwanja wake wa kazi sababu ya kuwa mbobezi/ mzoefu kutokana na muda wa kufanyia kazi vile alivyojifunza kwa vitendo zaidi, kupata muda wa kufanya makosa na kujirekebisha.
  4. MTANDAO-Pia Mtu anayefanya kazi za kujitolea huwa na wigo mpana wa kufahamiana na watu katika fani, tasnia husika hivyo kutengeneza Mtandao (Network) ambayo huweza kuwa na manufaa baadaye iwapo utautumia vizuri. Watu unaokutana nao hutathimini na kuona utendaji, wanaweza kuwa washauri, walezi wako na kuwa rahisi kwao kukutambulisha kwa wadau wengine zaidi au hata kukupa ajira rasmi...lakini pia hata kuwa rahisi kufanya nao kazi kutokea nje ya taasisi husika iwapo utakuwa na uhitaji.
KIJAMII : Iwapo utakuwa unafanya kazi za kujitolea, faida za jumla zinazoweza kupatikana kijamii ni pamoja na;
  1. MTAZAMO NA KUFANYA MAAMUZI- Kusaidia kumjenga mhusika kimawazo na kimtazamo, kumfanya awe na tija kwa jamii (Mawazo atakayokuwa akitoa huakisi yale anayoyafahamu na watu wanaomzunguka hivyo akifahamu mengi zaidi kwa nadharia na vitendo kutamfanya afikiri na kutoa mawazo chanya, na kushiriki katika kutoa maamuzi) pia kupitia kujishughulisha na kazi kutampunguzia kujihusisha na makundi yasiyo na tija na kumfanya awe Productive.
  2. KUWA SEHEMU YA MAENDELEO- Kazi za kujitolea zinazohusisha jamii husaidia kusukuma mbele gurudumu la maendeleo. Taasisi/ Jumuiya zinazofanya kazi za kujamii humuwezesha kijana anayefanya kazi hizo kuwa sehemu ya maendeleo na kusaidia kufanikisha Maendeleo chanya. (Hata Ukiamua kufanya kazi ya kujitolea kufanya usafi, kuhamasisha vijana kupima nk. inakuwa ni mchango mkubwa sana kijamii)

MADHARA YA KUTOFANYA KAZI ZA KUJITOLEA:

KIBINAFSI:

Hebu Fikiria kuwa umeenda kuomba nafasi ya kazi sehemu (Fresh From College/ Uni) ukiwa na vyeti na sifa zinazostahili kitaaluma kwa nafasi husika halafu unaambiwa huwezi kuchaguliwa sababu huna uzoefu na kazi.
NB: Baadhi ya Taasisi zilizoendelea pia huwa wana utaratibu wa kuchagua Experience Over Academic Qualification kwa sababu mbalimbali.
5 Reasons Why Experience Matters More Than Education

KIJAMII :
Athari inayoweza kupatikana ni kuwa na vijana wengi wasiojishughulisha mtaani na kupelekea makundi yasiyo na tija, sambamba na kudumaza maendeleo kutokana na jamii kuwa tegemezi kwa kukosa watendaji kazi wa kutosha, au hata watoa mawazo jengefu yanayoakisi hali halisi ya kijamii na kiutendaji ili kufanikisha maendeleo.

TATIZO LA KUCHUKULIA KWA WEPESI SUALA HILI:
Iwapo suala la kujitolea likichukuliwa kwa wepesi, na vijana wasipokuwa na muamko wa kujitolea na kuonyesha mfano suala la maendeleo binafsi na kijamii haliwezi kufanikiwa.

Kwa wale wanaopata fursa hizi za kujitolea wanapozitendea haki ni rahisi kufanya Mashirika,taasisi na Jumuiya zetu za kijamii kuona umuhimu wa kuendelea kutoa nafasi zaidi kwa vijana wengine na kufanya nao kazi na kuwa endeleza kupitia ushiriki wao katika mazingira halisi ya kazi.
(Baadhi ya wanaopata kazi hizi za kujitolea huzembea nafasi hizo na kuharibu sifa za wengine ambao ni wachapa kazi na wenye nia ya dhati ya kujifunza wanaotafuta fursa hizi- Unapopata Wasaa wa kufanya shughuli hizi Fanya kwa Moyo na Jitihada zote huenda hapo ndipo utapokuja kupata ajira, kuzoa uzoefu na kuwa bora zaidi au kutengeneza Network zenye manufaa zaidi baadae).

SUALA LA MUDA na WAPI UTAFANYA KAZI ZA KUITOLEA:
Changamoto nyingi za Vijana wenzangu utasikia "Tatizo sina Muda Unaba, sina muda wa kutosha Kufanya kazi za Kujitolea" au "Wapi naweza kwenda Kujitolea?"

Kujitolea hata kwa saa Moja au Mbili tu Kila siku kama upo sehemu sahihi na unafanya kilichokupeleka ina COUNT, mfano: Unajitolea saa moja kuwa kiongozi kanisani, kushiriki katika Vikao vya maendeleo, au Kusaidia Kufundisha katika kituo cha Watoto Yatima mtaani nk. kwako hiyo ni BIG STEP!
Mbali na kufanya kazi za kujitolea, kutana na watu, Ongea nao vizuri badilishana nao mawazo hapo unaweza kuongeza au kupata kitu cha ziada pia.

Iwapo ni Mwanafunzi kipindi cha Likizo unaweza kuomba kushiriki kazi za kujitolea katika kikundi rasmi cha vijana Mtaani kwako/ Serikali ya mtaa au Taasisi iliyo karibu na wewe kisha give it 100% hiyo inaweza kukuinua na kuongeza wigo wa Ufahamu wa mambo pamoja na kujuana na watu wa Tabaka, Rika, Taaluma na Utashi tofauti kisha ukajifunza au wao kujifunza jambo kutoka kwako.

Inafahamika kuwa Kujitolea kuna umiza katika suala la nauli iwapo sehemu ya kazi ni mbali na ulipo ukiwa bado huna chanzo cha uhakika cha mapato na hususani kama sehemu unayofanyia kazi haina utaratibu wa Posho/nauli, ufanikiwa kujiwezesha katika hili hesabu kama ni Investment kwa ajili ya future yako.

Naomba kuwasilisha na karibuni kwa Maswali, Maoni na Ushauri wa kujenga zaidi ili kuangaza jamii yetu Vijana katika kushika hatamu ya maendeleo

Kaka Pekee!
0677679339
Mwisho wa siku lengo la kila mtu kusoma ni kujifunza ila pamoja na hilo ni kuweza kutengeneza mazingira ya kuhakikisha anapeleka chochote kwenye meza ya chakula ya watu wake.

Kujitolea ni very risky attempt unless ufanye hilo ukiwa na dhamira ya ku pass time. Wapo watu wanajitolea for years na waliishia kutoswa ila imagine unajitolea unapewa hela ya kujikimu sawa tu na mshahara maybe laki 8 kila mwezi utaacha?

Sote tunahitaji pesa mkuu hayo uliosema yako practical ikiwa volunteer analipwa stipend vinginevyo ni utani!
 
Mwisho wa siku lengo la kila mtu kusoma ni kujifunza ila pamoja na hilo ni kuweza kutengeneza mazingira ya kuhakikisha anapeleka chochote kwenye meza ya chakula ya watu wake.

Kujitolea ni very risky attempt unless ufanye hilo ukiwa na dhamira ya ku pass time. Wapo watu wanajitolea for years na waliishia kutoswa ila imagine unajitolea unapewa hela ya kujikimu sawa tu na mshahara maybe laki 8 kila mwezi utaacha?

Sote tunahitaji pesa mkuu hayo uliosema yako practical ikiwa volunteer analipwa stipend vinginevyo ni utani!
Ukitoa saa moja au mbili katika shughuli zako kufanya kujitolea on something is Investment ukikubali hilo kwanza unaweza kuangalia ni muda gani kila siku mtu anashinda kijiweni kupiga stori/ vijiwe vya kahawa na ubishi wa siasa na kuto invest kwenye future yake.
 
Ukitoa saa moja au mbili katika shughuli zako kufanya kujitolea on something is Investment ukikubali hilo kwanza unaweza kuangalia ni muda gani kila siku mtu anashinda kijiweni kupiga stori/ vijiwe vya kahawa na ubishi wa siasa na kuto invest kwenye future yake.
Sasa utaenda ofisini kwa mtu for 2hours?
 
Sasa utaenda ofisini kwa mtu for 2hours?
Yes unaweza kaka call it Hour Bank, Depends na unaenda kufanya shughuli gani/ Aina ya kazi. hata kama si kila siku unaweza ku spend 1 or 2 days a week. Prior agreement ndio msingi ujue majukumu yako na wafahamu uhitaji wao kwako. Iam a living Example nilipotoka 12 years ago
 
Yes unaweza kaka call it Hour Bank, Depends na unaenda kufanya shughuli gani/ Aina ya kazi. hata kama si kila siku unaweza ku spend 1 or 2 days a week. Prior agreement ndio msingi ujue majukumu yako na wafahamu uhitaji wao kwako.
Ni rahisi mkuu kama una mishe ya kukusongesha
 
Ni rahisi mkuu kama una mishe ya kukusongesha
YES kaka, Kujitolea sio Kazi ya Kuitegemea... ni sahihi kuwa na Mishe nyingine au kufanya kazi sawa na hiyo unayojitolea kwa kampuni fulani kama chanzo cha mapato.
Mfano: Unafanya kazi ya Kujitolea kupiga picha kwenye taasisi fulani kila siku kwa 3Hours, au wanakuita wanapokuhitaji kwa ajili ya (Vikao, Mikutano n.k) Unaweza pia kufanya kazi nyingine au hiyo kuwa rasmi nje ya muda wao na kuitegemea kuwa chanzo cha mapato. ikitokea nafasi ya wao kukuajiri, au kupata kazi sehemu nyingine wao wanaweza kuwa referees wako.
 
Habari Wadau.

Naomba kufungua mazungumzo haya kuzungumzia Suala la Kazi za Kujitolea na Umuhimu wake sambamba na madhara yake unapochukulia kwa wepesi nafasi hizi pindi unapozipata. (Kutokana na uzi huu kutokuwa maandiko matakatifu, ninaweza kurekebishwa, unaweza kutoa mchango chanya na kutoa taarifa jengefu ili kusaidia kuwafumbua macho vijana wenzetu juu ya fursa za kujitolea hususan wanaosubiria Ajira rasmi na wanafunzi wanaokuwa likizo ndefu na fupi)

1.) KAZI ZA KUJITOLEA NI NINI?
Kazi za kujitolea zina maanisha kufanya Shughuli/kazi isiyotegemea malipo (Ujira/Mshahara) ambapo mtu anatoa muda wake kusaidia shughuli/kazi za kijamii, kupitia taasisi au mtu asiyehusiana nae.
Badala ya kutegemea malipo ya pesa (Ujira/ Mshahara) hupata uzoefu na kutengeneza Mtandao (Network) unaoweza kumsaidia katika kazi/taaluma yake hapo baadaye. Baadhi ya Taasisi kulingana na sera zao na majukumu husika hutoa Posho kidogo ya nauli kuwawezesha wafanyakazi wao wa kujitolea (Volunteers)

2.) UMUHIMU WA KAZI ZA KUJITOLEA!

Kazi za kujitolea zina Tija kubwa sana kuliko tunavyofikiria, hii ni katika pande zote BINAFSI, na KIJAMII.

KIBINAFSI : Mtu anayefanya kazi hizi za kujitolea hujiongezea ufahamu na ujuzi zaidi wa shughuli anayoifanya nje ya ajira rasmi, hii inaweza kuwa ni kupitia maombi binafsi ya kujitolea kwa nafasi husika, au kupitia maombi maalum yanayotumwa kwa niaba ya mhusika kupitia Taasisi za elimu ya Juu na Vyuo.( Field Work)

  1. WASIFU-Kujiongezea Ufahamu na Ujuzi zaidi wa shughuli/Kazi humsaidia mhusika kuongeza thamani katika wasifu wake (CV) katika ushindani wa nafasi za kazi.
  2. USHINDANI KATIKA AJIRA- Waajiri wengi siku hizi huangalia Vyeti na Uzoefu pindi unapotuma maombi ya kazi, kupitia hizi hizi kazi za kujitolea unaweza kupenya katika uchaguzi wa awali (Screening) na kuzingatiwa kwa hatua ya Usahili wa ana kwa ana (Personal Interview).
  3. UBOBEZI- Kazi za kujitolea husaidia Mhusika kujiamini zaidi katika uwanja wake wa kazi sababu ya kuwa mbobezi/ mzoefu kutokana na muda wa kufanyia kazi vile alivyojifunza kwa vitendo zaidi, kupata muda wa kufanya makosa na kujirekebisha.
  4. MTANDAO-Pia Mtu anayefanya kazi za kujitolea huwa na wigo mpana wa kufahamiana na watu katika fani, tasnia husika hivyo kutengeneza Mtandao (Network) ambayo huweza kuwa na manufaa baadaye iwapo utautumia vizuri. Watu unaokutana nao hutathimini na kuona utendaji, wanaweza kuwa washauri, walezi wako na kuwa rahisi kwao kukutambulisha kwa wadau wengine zaidi au hata kukupa ajira rasmi...lakini pia hata kuwa rahisi kufanya nao kazi kutokea nje ya taasisi husika iwapo utakuwa na uhitaji.
KIJAMII : Iwapo utakuwa unafanya kazi za kujitolea, faida za jumla zinazoweza kupatikana kijamii ni pamoja na;
  1. MTAZAMO NA KUFANYA MAAMUZI- Kusaidia kumjenga mhusika kimawazo na kimtazamo, kumfanya awe na tija kwa jamii (Mawazo atakayokuwa akitoa huakisi yale anayoyafahamu na watu wanaomzunguka hivyo akifahamu mengi zaidi kwa nadharia na vitendo kutamfanya afikiri na kutoa mawazo chanya, na kushiriki katika kutoa maamuzi) pia kupitia kujishughulisha na kazi kutampunguzia kujihusisha na makundi yasiyo na tija na kumfanya awe Productive.
  2. KUWA SEHEMU YA MAENDELEO- Kazi za kujitolea zinazohusisha jamii husaidia kusukuma mbele gurudumu la maendeleo. Taasisi/ Jumuiya zinazofanya kazi za kujamii humuwezesha kijana anayefanya kazi hizo kuwa sehemu ya maendeleo na kusaidia kufanikisha Maendeleo chanya. (Hata Ukiamua kufanya kazi ya kujitolea kufanya usafi, kuhamasisha vijana kupima nk. inakuwa ni mchango mkubwa sana kijamii)
MADHARA YA KUTOFANYA KAZI ZA KUJITOLEA:

KIBINAFSI:

Hebu Fikiria kuwa umeenda kuomba nafasi ya kazi sehemu (Fresh From College/ Uni) ukiwa na vyeti na sifa zinazostahili kitaaluma kwa nafasi husika halafu unaambiwa huwezi kuchaguliwa sababu huna uzoefu na kazi.
NB: Baadhi ya Taasisi zilizoendelea pia huwa wana utaratibu wa kuchagua Experience Over Academic Qualification kwa sababu mbalimbali.
5 Reasons Why Experience Matters More Than Education

KIJAMII :
Athari inayoweza kupatikana ni kuwa na vijana wengi wasiojishughulisha mtaani na kupelekea makundi yasiyo na tija, sambamba na kudumaza maendeleo kutokana na jamii kuwa tegemezi kwa kukosa watendaji kazi wa kutosha, au hata watoa mawazo jengefu yanayoakisi hali halisi ya kijamii na kiutendaji ili kufanikisha maendeleo.

TATIZO LA KUCHUKULIA KWA WEPESI SUALA HILI:
Iwapo suala la kujitolea likichukuliwa kwa wepesi, na vijana wasipokuwa na muamko wa kujitolea na kuonyesha mfano suala la maendeleo binafsi na kijamii haliwezi kufanikiwa.

Kwa wale wanaopata fursa hizi za kujitolea wanapozitendea haki ni rahisi kufanya Mashirika,taasisi na Jumuiya zetu za kijamii kuona umuhimu wa kuendelea kutoa nafasi zaidi kwa vijana wengine na kufanya nao kazi na kuwa endeleza kupitia ushiriki wao katika mazingira halisi ya kazi.
(Baadhi ya wanaopata kazi hizi za kujitolea huzembea nafasi hizo na kuharibu sifa za wengine ambao ni wachapa kazi na wenye nia ya dhati ya kujifunza wanaotafuta fursa hizi- Unapopata Wasaa wa kufanya shughuli hizi Fanya kwa Moyo na Jitihada zote huenda hapo ndipo utapokuja kupata ajira, kuzoa uzoefu na kuwa bora zaidi au kutengeneza Network zenye manufaa zaidi baadae).

SUALA LA MUDA na WAPI UTAFANYA KAZI ZA KUITOLEA:
Changamoto nyingi za Vijana wenzangu utasikia "Tatizo sina Muda Unaba, sina muda wa kutosha Kufanya kazi za Kujitolea" au "Wapi naweza kwenda Kujitolea?"

Kujitolea hata kwa saa Moja au Mbili tu Kila siku kama upo sehemu sahihi na unafanya kilichokupeleka ina COUNT, mfano: Unajitolea saa moja kuwa kiongozi kanisani, kushiriki katika Vikao vya maendeleo, au Kusaidia Kufundisha katika kituo cha Watoto Yatima mtaani nk. kwako hiyo ni BIG STEP!
Mbali na kufanya kazi za kujitolea, kutana na watu, Ongea nao vizuri badilishana nao mawazo hapo unaweza kuongeza au kupata kitu cha ziada pia.

Iwapo ni Mwanafunzi kipindi cha Likizo unaweza kuomba kushiriki kazi za kujitolea katika kikundi rasmi cha vijana Mtaani kwako/ Serikali ya mtaa au Taasisi iliyo karibu na wewe kisha give it 100% hiyo inaweza kukuinua na kuongeza wigo wa Ufahamu wa mambo pamoja na kujuana na watu wa Tabaka, Rika, Taaluma na Utashi tofauti kisha ukajifunza au wao kujifunza jambo kutoka kwako.

Inafahamika kuwa Kujitolea kuna umiza katika suala la nauli iwapo sehemu ya kazi ni mbali na ulipo ukiwa bado huna chanzo cha uhakika cha mapato na hususani kama sehemu unayofanyia kazi haina utaratibu wa Posho/nauli, ufanikiwa kujiwezesha katika hili hesabu kama ni Investment kwa ajili ya future yako.

Naomba kuwasilisha na karibuni kwa Maswali, Maoni na Ushauri wa kujenga zaidi ili kuangaza jamii yetu Vijana katika kushika hatamu ya maendeleo

Kaka Pekee!
0677679339
Mkuu; Nakazia: Kwa Kijana msomi na Asiye na ajira; Mwenye masikio na ASIKIE na KUZINGATIA uliyoandika hapo juu.👆
Hongera sana Bro. kwa kuwafunulia mang'amuzi uliyonayo vijana wengine 👍👍
Vijana wasomi wakumbuke kwamba kwa Kutokufanya shughuli inayoendana na fani uliyosomea, Fani yako hiyo itaendelea kudorora na hatimaye ita Expire kabisa(Itapitwa na wakati jumla)
 
Kujitolea mwisho ni miaka miwili, na lengo liwe ni kupata ujuzi sio kuweka mategemeo ya kukumbukwa kwenye ajira, nje hapo ni suicide mission
Sawa; Naboresha zaidi: Lengo liwe ni pamoja na kupata UJUZI na UZOEFU KAZINI lakini pia kung'arisha zaidi CV yako esp. ikiwa utapewa/utapata A Letter of Appreciation and Competence kutoka Ofisi/Taasisi uliyokuwa unajitolea na zaidi pia kukuepusha kuwa Idle.
 
Habari Wadau.

Naomba kufungua mazungumzo haya kuzungumzia Suala la Kazi za Kujitolea na Umuhimu wake sambamba na madhara yake unapochukulia kwa wepesi nafasi hizi pindi unapozipata. (Kutokana na uzi huu kutokuwa maandiko matakatifu, ninaweza kurekebishwa, unaweza kutoa mchango chanya na kutoa taarifa jengefu ili kusaidia kuwafumbua macho vijana wenzetu juu ya fursa za kujitolea hususan wanaosubiria Ajira rasmi na wanafunzi wanaokuwa likizo ndefu na fupi)

1.) KAZI ZA KUJITOLEA NI NINI?
Kazi za kujitolea zina maanisha kufanya Shughuli/kazi isiyotegemea malipo (Ujira/Mshahara) ambapo mtu anatoa muda wake kusaidia shughuli/kazi za kijamii, kupitia taasisi au mtu asiyehusiana nae.
Badala ya kutegemea malipo ya pesa (Ujira/ Mshahara) hupata uzoefu na kutengeneza Mtandao (Network) unaoweza kumsaidia katika kazi/taaluma yake hapo baadaye. Baadhi ya Taasisi kulingana na sera zao na majukumu husika hutoa Posho kidogo ya nauli kuwawezesha wafanyakazi wao wa kujitolea (Volunteers)

2.) UMUHIMU WA KAZI ZA KUJITOLEA!

Kazi za kujitolea zina Tija kubwa sana kuliko tunavyofikiria, hii ni katika pande zote BINAFSI, na KIJAMII.

KIBINAFSI : Mtu anayefanya kazi hizi za kujitolea hujiongezea ufahamu na ujuzi zaidi wa shughuli anayoifanya nje ya ajira rasmi, hii inaweza kuwa ni kupitia maombi binafsi ya kujitolea kwa nafasi husika, au kupitia maombi maalum yanayotumwa kwa niaba ya mhusika kupitia Taasisi za elimu ya Juu na Vyuo.( Field Work)

  1. WASIFU-Kujiongezea Ufahamu na Ujuzi zaidi wa shughuli/Kazi humsaidia mhusika kuongeza thamani katika wasifu wake (CV) katika ushindani wa nafasi za kazi.
  2. USHINDANI KATIKA AJIRA- Waajiri wengi siku hizi huangalia Vyeti na Uzoefu pindi unapotuma maombi ya kazi, kupitia hizi hizi kazi za kujitolea unaweza kupenya katika uchaguzi wa awali (Screening) na kuzingatiwa kwa hatua ya Usahili wa ana kwa ana (Personal Interview).
  3. UBOBEZI- Kazi za kujitolea husaidia Mhusika kujiamini zaidi katika uwanja wake wa kazi sababu ya kuwa mbobezi/ mzoefu kutokana na muda wa kufanyia kazi vile alivyojifunza kwa vitendo zaidi, kupata muda wa kufanya makosa na kujirekebisha.
  4. MTANDAO-Pia Mtu anayefanya kazi za kujitolea huwa na wigo mpana wa kufahamiana na watu katika fani, tasnia husika hivyo kutengeneza Mtandao (Network) ambayo huweza kuwa na manufaa baadaye iwapo utautumia vizuri. Watu unaokutana nao hutathimini na kuona utendaji, wanaweza kuwa washauri, walezi wako na kuwa rahisi kwao kukutambulisha kwa wadau wengine zaidi au hata kukupa ajira rasmi...lakini pia hata kuwa rahisi kufanya nao kazi kutokea nje ya taasisi husika iwapo utakuwa na uhitaji.
KIJAMII : Iwapo utakuwa unafanya kazi za kujitolea, faida za jumla zinazoweza kupatikana kijamii ni pamoja na;
  1. MTAZAMO NA KUFANYA MAAMUZI- Kusaidia kumjenga mhusika kimawazo na kimtazamo, kumfanya awe na tija kwa jamii (Mawazo atakayokuwa akitoa huakisi yale anayoyafahamu na watu wanaomzunguka hivyo akifahamu mengi zaidi kwa nadharia na vitendo kutamfanya afikiri na kutoa mawazo chanya, na kushiriki katika kutoa maamuzi) pia kupitia kujishughulisha na kazi kutampunguzia kujihusisha na makundi yasiyo na tija na kumfanya awe Productive.
  2. KUWA SEHEMU YA MAENDELEO- Kazi za kujitolea zinazohusisha jamii husaidia kusukuma mbele gurudumu la maendeleo. Taasisi/ Jumuiya zinazofanya kazi za kujamii humuwezesha kijana anayefanya kazi hizo kuwa sehemu ya maendeleo na kusaidia kufanikisha Maendeleo chanya. (Hata Ukiamua kufanya kazi ya kujitolea kufanya usafi, kuhamasisha vijana kupima nk. inakuwa ni mchango mkubwa sana kijamii)
MADHARA YA KUTOFANYA KAZI ZA KUJITOLEA:

KIBINAFSI:

Hebu Fikiria kuwa umeenda kuomba nafasi ya kazi sehemu (Fresh From College/ Uni) ukiwa na vyeti na sifa zinazostahili kitaaluma kwa nafasi husika halafu unaambiwa huwezi kuchaguliwa sababu huna uzoefu na kazi.
NB: Baadhi ya Taasisi zilizoendelea pia huwa wana utaratibu wa kuchagua Experience Over Academic Qualification kwa sababu mbalimbali.
5 Reasons Why Experience Matters More Than Education

KIJAMII :
Athari inayoweza kupatikana ni kuwa na vijana wengi wasiojishughulisha mtaani na kupelekea makundi yasiyo na tija, sambamba na kudumaza maendeleo kutokana na jamii kuwa tegemezi kwa kukosa watendaji kazi wa kutosha, au hata watoa mawazo jengefu yanayoakisi hali halisi ya kijamii na kiutendaji ili kufanikisha maendeleo.

TATIZO LA KUCHUKULIA KWA WEPESI SUALA HILI:
Iwapo suala la kujitolea likichukuliwa kwa wepesi, na vijana wasipokuwa na muamko wa kujitolea na kuonyesha mfano suala la maendeleo binafsi na kijamii haliwezi kufanikiwa.

Kwa wale wanaopata fursa hizi za kujitolea wanapozitendea haki ni rahisi kufanya Mashirika,taasisi na Jumuiya zetu za kijamii kuona umuhimu wa kuendelea kutoa nafasi zaidi kwa vijana wengine na kufanya nao kazi na kuwa endeleza kupitia ushiriki wao katika mazingira halisi ya kazi.
(Baadhi ya wanaopata kazi hizi za kujitolea huzembea nafasi hizo na kuharibu sifa za wengine ambao ni wachapa kazi na wenye nia ya dhati ya kujifunza wanaotafuta fursa hizi- Unapopata Wasaa wa kufanya shughuli hizi Fanya kwa Moyo na Jitihada zote huenda hapo ndipo utapokuja kupata ajira, kuzoa uzoefu na kuwa bora zaidi au kutengeneza Network zenye manufaa zaidi baadae).

SUALA LA MUDA na WAPI UTAFANYA KAZI ZA KUITOLEA:
Changamoto nyingi za Vijana wenzangu utasikia "Tatizo sina Muda Unaba, sina muda wa kutosha Kufanya kazi za Kujitolea" au "Wapi naweza kwenda Kujitolea?"

Kujitolea hata kwa saa Moja au Mbili tu Kila siku kama upo sehemu sahihi na unafanya kilichokupeleka ina COUNT, mfano: Unajitolea saa moja kuwa kiongozi kanisani, kushiriki katika Vikao vya maendeleo, au Kusaidia Kufundisha katika kituo cha Watoto Yatima mtaani nk. kwako hiyo ni BIG STEP!
Mbali na kufanya kazi za kujitolea, kutana na watu, Ongea nao vizuri badilishana nao mawazo hapo unaweza kuongeza au kupata kitu cha ziada pia.

Iwapo ni Mwanafunzi kipindi cha Likizo unaweza kuomba kushiriki kazi za kujitolea katika kikundi rasmi cha vijana Mtaani kwako/ Serikali ya mtaa au Taasisi iliyo karibu na wewe kisha give it 100% hiyo inaweza kukuinua na kuongeza wigo wa Ufahamu wa mambo pamoja na kujuana na watu wa Tabaka, Rika, Taaluma na Utashi tofauti kisha ukajifunza au wao kujifunza jambo kutoka kwako.

Inafahamika kuwa Kujitolea kuna umiza katika suala la nauli iwapo sehemu ya kazi ni mbali na ulipo ukiwa bado huna chanzo cha uhakika cha mapato na hususani kama sehemu unayofanyia kazi haina utaratibu wa Posho/nauli, ufanikiwa kujiwezesha katika hili hesabu kama ni Investment kwa ajili ya future yako.

Naomba kuwasilisha na karibuni kwa Maswali, Maoni na Ushauri wa kujenga zaidi ili kuangaza jamii yetu Vijana katika kushika hatamu ya maendeleo

Kaka Pekee!
0677679339
Hii mambo ya kujitolea ina faida na hasara

kwa upande wa serikalini hakuna shida lakini bila udhibiti sekita binafsi zitafanya kujitolea kama ndiyo mfumo wa ajira.

watatumia watu wa kujitolea na kuwalipa pesa kidogo inayoitwa posho na watakuwa wanafanya hivyo tu.

hivyo kujitolea siyo jambo la kuhamasisha kwa kuangalia personal gain kuwa mtu anaongeza ujuzi lakini kama waajiri wataacha kuajiri na kuanza kutegemea watu wa kujitolea itakuwaje?
 
Back
Top Bottom