Sharbel
JF-Expert Member
- Feb 20, 2020
- 1,076
- 2,242
Hivi karibuni, kumetokea na wimbi kubwa la taasisi, mashirika na makampuni mbalimbali kutoa nafasi za kujitolea kufanya kazi.
Kimsingi huo ni unyonyaji tu maana wao unawazalishia alafu wanakupa ujira mdogo au kutokukulipa kabisa.
Vijana wengi wameingia huko labda wanadhani kujitolea pengine inaweza kukupatia nafasi ya kupata ajira, lakini wanajikuta miaka inaenda na ajira hamna.
Zipo taasisi asilimia 60% ya wafanyakazi wake ni wakujitolea tu, yaani wao wanaingiza pesa na huku kutolipa chochote kwa hao wafanyakazi wao.
Mwisho nimeshangaa sana wizara ya afya inatoa nafasi za kujitolea katika hospital ya maweni kigoma na kuwalipa asilimia 50% ya mshahara wao, ilhali inao uwezo wa kutoa hizo ajira.
Kijana kataa kujitolea,
Kujitolea ni utumwa,
Kujitolea ni laana,
Kujitolea ni wizi,
Kujitolea ni utapeli,
Kujitolea ni unyonyaji,
Kataa kujitolea,
Kataa kujitolea.
Kimsingi huo ni unyonyaji tu maana wao unawazalishia alafu wanakupa ujira mdogo au kutokukulipa kabisa.
Vijana wengi wameingia huko labda wanadhani kujitolea pengine inaweza kukupatia nafasi ya kupata ajira, lakini wanajikuta miaka inaenda na ajira hamna.
Zipo taasisi asilimia 60% ya wafanyakazi wake ni wakujitolea tu, yaani wao wanaingiza pesa na huku kutolipa chochote kwa hao wafanyakazi wao.
Mwisho nimeshangaa sana wizara ya afya inatoa nafasi za kujitolea katika hospital ya maweni kigoma na kuwalipa asilimia 50% ya mshahara wao, ilhali inao uwezo wa kutoa hizo ajira.
Kijana kataa kujitolea,
Kujitolea ni utumwa,
Kujitolea ni laana,
Kujitolea ni wizi,
Kujitolea ni utapeli,
Kujitolea ni unyonyaji,
Kataa kujitolea,
Kataa kujitolea.