Kazi ya kuweka Vinasaba (Marking) kwenye mafuta, TBS hawajui, Wabunge na Waziri Kalemani hajui chochote kinachoendelea. Je, kodi stahiki italipwa?

Mkaruka

JF-Expert Member
Feb 5, 2013
19,617
34,062
DISCLAIMER: Huu ni mtazamo wangu tu kuhusu hili suala kwa jinsi nilivyoliona na kulishuhudia. Sina maslahi yoyote na suala hili.

=========

Ni maajabu juu ya maajabu. Nchi ina maajabu sana hii.

Iko hivi:

Hivi karibuni bungeni, Mb. Shabiby na Tabasamu waliibua hoja kwamba serikali imepigwa sana pesa (Tsh 3B kila mwezi) na kampuni iliyokuwa inatumika kuweka vinasaba (marking) kwenye mafuta. Ifahamike kuwa hili siyo suala la kuweka kama walivyojaribu kupotosha wabunge pamoja na Speaker Ndugai, bali huhuhisha vipimo na utaalamu.

1- Kumbuka Uwekaji wa vinasaba (marking) hurahisisha ufuatiliaji wa mafuta yanayouzwa kwa siku ili kuweka kumbukumbu sawa za ulipaji kodi.

Na ili kurahisisha hili ndio maana serikali kupitia EWURA ikatangaza tender ya kuipata kampuni husika kwaajili ya kazi hiyo. Malipo ya kampuni hiyo yalitokana na tozo ya Tsh 17 kwa kila litre moja ya mafuta na ilipaswa kulipwa na wamiliki wa depots.

Mkanganyiko,

1: Mhe. Shabiby, Speaker Ndugai na Waziri Kalemani wanasemaje eti pesa ya serikali ilikuwa inapigwa wakati pesa inalipwa na wamiliki wa depots?

2: Hivi inakuwaje bunge lenye kamati ya kudumu ya nishati inashindwa kutembelea kampuni husika pamoja na depots na badala yake wanafanya maamuzi kwa kujishuku shuku tu?

3: Ieleweke kuwa kampuni husika iliyokuwa inafanya kazi ya vinasaba imekuwa ikipewa tender kila baada ya miaka 3. Na baada ya mkataba wao kyisha, EWURA walitangaza tender, ambayo inavyoonekana ilishinda kampuni ya Intertek.

Sasa ilikuwaje badala ya kupewa wao kazi, imepigwa U-turn wanapewa TBS?

Haya mambo ya serikali kufanya biashara yenyewe kwa yenyewe yataisha lini?

4: Unaposema ile pesa waliokuwa wanalipwa waweka vinasaba ipelekwe RUWASA na TARURA inakuwa vipi tena kuchota pesa kwa kumiliki wa mafuta na kuzipelekwa kwenye Maji na Barabara?

Je, wamiliki wa depots wakianza kuikataa hiyo tozo ya Tsh 17 itakuwaje?
Na, Je kama TBS wakiwa ndio wanafanya kazi maana watahitaji kuwa na staff wa kufanya kazi hiyo
Je, watawalipaje ikiwa pesa mnataka kupeleka RUWASA na TARURA?

5: Inakuwaje Waziri Kalemani anaongea tu kwente vyombo vya habari kwamba mafuta yote yawekewe vinasaba wakati TBS wenyewe hawana ujuzi wala hawajui kazi inafanyikaje mpaka sasa wala hawana staff wa kufanya kazi hiyo?

6: Hii kampuni iliyokuwa inafanya kazi mbona mpaka sasa bado inaendekea kufanya kazi Zanzibar kama ni ya kifisadi kama mlivyosema?
 
Hilo bunge la CCM Ndugai akiwa kiongozi wao ni mapambio tu ndio wanayojua kuimba.
 
Wacha ifanye kazi zanziba kwani huko panawatosha.

Tatizo wa tz hata kitu cha bure mtakifanya dili.

Kama mgekuwa mnatimiza wajibu wenu hayo yote yasingetokea kosa lenu ni kuanza kutoweka hizo vinasaba kwenye baadhi ya mafuta ili mnufaike zaidi.

Kila kitu mnataka mfanye dili na hilo mdio linawafanya msiaminike.

Najua wewe ni mmoja ya wamiliki wa hiyo kampuni kwa hiyo mjitathimini maana hata huko zenji bado wanawapima tu, mkikologa kazi inafutwa.
 
Wacha ifanye kazi zanziba kwani huko panawatosha.

Tatizo wa tz hata kitu cha bure mtakifanya dili.

Kama mgekuwa mnatimiza wajibu wenu hayo yote yasingetokea kosa lenu ni kuanza kutoweka hizo vinasaba kwenye baadhi ya mafuta ili mnufaike zaidi.

Kila kitu mnataka mfanye dili na hilo mdio linawafanya msiaminike.

Najua wewe ni mmoja ya wamiliki wa hiyo kampuni kwa hiyo mjitathimini maana hata huko zenji bado wanawapima tu, mkikologa kazi inafutwa.
Mkuu hujui unachosema

Mimi ni graduate tu nasubiria ajira za Rais Samia.

Kampuni iliyokuwa inafanya hiyo kazi ni kampuni kutoka Israel. Na haiko hapa tu, iko Zanzibar, Mozambique, Uganda n.k.

Soma Disclaimer yangu hapo juu.
 
Yes, kwa hakika.

Wale watu hawajui hata nini kinaendelea nchi hii.

Hata speaker hajui chochote yaani. Inasikitisha
Spika ni mweupe sana kichwani, aisee tungekuwa na spika type ya Andrea Chenge nazani tungelinga sana, Ndugani ni dhaifu haijawahi tokea
 
Spika ni mweupe sana kichwani, aisee tungekuwa na spika type ya Andrea Chenge nazani tungelinga sana, Ndugani ni dhaifu haijawahi tokea
Hivi siku hizi kamati za bunge zinafanya kazi kweli?
 
Kuna mambo mengine hayana umuhimu kulingana na hali halisi.
TRA hawakusanyi kodi kupitia vinasaba, wanadhibiti kwa njia nyingine.
EWURA yenyewe ni mzigo kwa mlaji halafu inaongeza contract isiyo na tija yoyote.
 
Kuna mambo mengine hayana umuhimu kulingana na hali halisi.
TRA hawakusanyi kodi kupitia vinasaba, wanadhibiti kwa njia nyingine.
EWURA yenyewe ni mzigo kwa mlaji halafu inaongeza contract isiyo na tija yoyote.
You know nothing about fuel marking dude.

Get your facts right.
 
We always learn from those who know.
Could you please write what you have in mind?
Kindly please prove that you have some knowledge.
Read the masterpiece above. I can't keep curating the same thing over and over again.
 
Hapa nasimama na Shabiby ni kwamba kazi hiyo walopewa hiyo tender na EWURA inaweza kufanywa na TBS na kwakuwa serikali haifanyi biashara basi wazo likaja kuwa Tozo hiyo ya Tsh.17 @ litre inaweza kuingia kwenye barabara kwamaana ya Tarura na Ruwasa.

Unaposema kuwa TBS hawana staff hilo nakataa kwa asilimia mia moja.wataalamu wapo wa kufanya hiyo kazi. Kikichokuwa kinafanyika ni mwendelezo wa wizi tuu hiyo kampuni ya vinasaba wanawajuwa walokuwa wanakula nao.
 
DISCLAIMER: Huu ni mtazamo wangu tu kuhusu hili suala kwa jinsi nilivyoliona na kulishuhudia. Sina maslahi yoyote na suala hili.

=========

Ni maajabu juu ya maajabu. Nchi ina maajabu sana hii.

Iko hivi:

Hivi karibuni bungeni, Mb. Shabiby na Tabasamu waliibua hoja kwamba serikali imepigwa sana pesa (Tsh 3B kila mwezi) na kampuni iliyokuwa inatumika kuweka vinasaba (marking) kwenye mafuta. Ifahamike kuwa hili siyo suala la kuweka kama walivyojaribu kupotosha wabunge pamoja na Speaker Ndugai, bali huhuhisha vipimo na utaalamu.

1- Kumbuka Uwekaji wa vinasaba (marking) hurahisisha ufuatiliaji wa mafuta yanayouzwa kwa siku ili kuweka kumbukumbu sawa za ulipaji kodi.

Na ili kurahisisha hili ndio maana serikali kupitia EWURA ikatangaza tender ya kuipata kampuni husika kwaajili ya kazi hiyo. Malipo ya kampuni hiyo yalitokana na tozo ya Tsh 17 kwa kila litre moja ya mafuta na ilipaswa kulipwa na wamiliki wa depots.

Mkanganyiko,

1: Mhe. Shabiby, Speaker Ndugai na Waziri Kalemani wanasemaje eti pesa ya serikali ilikuwa inapigwa wakati pesa inalipwa na wamiliki wa depots?

2: Hivi inakuwaje bunge lenye kamati ya kudumu ya nishati inashindwa kutembelea kampuni husika pamoja na depots na badala yake wanafanya maamuzi kwa kujishuku shuku tu?

3: Ieleweke kuwa kampuni husika iliyokuwa inafanya kazi ya vinasaba imekuwa ikipewa tender kila baada ya miaka 3. Na baada ya mkataba wao kyisha, EWURA walitangaza tender, ambayo inavyoonekana ilishinda kampuni ya Intertek.

Sasa ilikuwaje badala ya kupewa wao kazi, imepigwa U-turn wanapewa TBS?

Haya mambo ya serikali kufanya biashara yenyewe kwa yenyewe yataisha lini?

4: Unaposema ile pesa waliokuwa wanalipwa waweka vinasaba ipelekwe RUWASA na TARURA inakuwa vipi tena kuchota pesa kwa kumiliki wa mafuta na kuzipelekwa kwenye Maji na Barabara?

Je, wamiliki wa depots wakianza kuikataa hiyo tozo ya Tsh 17 itakuwaje?
Na, Je kama TBS wakiwa ndio wanafanya kazi maana watahitaji kuwa na staff wa kufanya kazi hiyo
Je, watawalipaje ikiwa pesa mnataka kupeleka RUWASA na TARURA?

5: Inakuwaje Waziri Kalemani anaongea tu kwente vyombo vya habari kwamba mafuta yote yawekewe vinasaba wakati TBS wenyewe hawana ujuzi wala hawajui kazi inafanyikaje mpaka sasa wala hawana staff wa kufanya kazi hiyo?

6: Hii kampuni iliyokuwa inafanya kazi mbona mpaka sasa bado inaendekea kufanya kazi Zanzibar kama ni ya kifisadi kama mlivyosema?
Kazi hiyo kupelekwa TBS ni kama vile ilivyopewa TASAC kufanya shughuli za mawakala wa forodha...
Ni mfumo flani wa kuua sekta binafsi na ajira huku "wafanyakazi/watendaji walio serikalini wakitumia ombwe hilo kunufaika"
 
Mkaruka,

Siyo kila kitu hufanyika kila mahali.
Uchaguzi wa kufanya hutegemea mambo mengi ikiwepo mazingira, faida, thamani inayoongezeka, mbadala wa gharama ndogo n.k.
Sasa kwa hilo la vinasaba, mafuta yanaweza kuuzwa bila hivyo na kusiwe na badiliko lolote.
Pili, utajiri unatoka nchini kuelekea nje (Israel kama ulivyoandika mwenyewe).
Tatu, kufanyika sehemu nyingine hakuhalalishi ufanisi au uhitaji wake.
Wengine wakifanya upuuzi, wewe utaiga tu.
Hizi ni mbinu za kuwachukulia pesa wananchi kiujanja ujania kwa kuwa mlipaji ni mlaji wa mwisho.
Read the masterpiece above. I can't keep curating the same thing over and over again.
 
Back
Top Bottom