Kazi ya kulea si mchezo, mbarikiwe wanawake

Kazi ya kulea si mchezo, mbarikiwe wanawake

Drone Camera

JF-Expert Member
Joined
Jul 25, 2017
Posts
14,121
Reaction score
14,032
Aisee hii kazi ya kulea kwa wanaume hapana, wacha niwapongeze tu wanawake.

Hii kazi ni ngumu. Mnaodai mnazalisha kisha mnalea naanza kuamini ni chai ya tangawizi kabisa! Labda kama unamchukua mtoto kwa mama yake ana miaka mitano kwenda juu. Tofauti na hapo utateseka na kukonda rafiki.

Juzi nimeachiwa watoto mapacha masaa matatu tu ila naona kama nimeachiwa mwaka mzima!

Ipo hivi: Majuzi mke wa kaka yangu, shem, kaugua kidogo. Hivyo wakampeleka hospitali. So mimi baadaye nikaenda kucheki hali ipoje pale home. Nikasalimia fresh. Sasa bro akaniambia dogo baki tu hapa utaondoka kesho shemeji yako akija. Nikakubali.

Sasa usiku sasa house girl na kaka wakatoka kufuata chakula sijui. Akaniambia ndugu tunakuja muda si mrefu, kuna watoto pia wamelala hapo (mapacha). Nikasema sawa. Dk 5 akaanza kulia mmoja.

Nikamchukua huyo anayelia. Akanyamaza sema aliponicheki usoni akaanza kulia zaidi (hanijui). Bembeleza wee wapi. Ni ka kike kana sauti kali kakamuamsha nduguye. Kazi ikawa ngumu zaidi.

Tumia mbinu zote zikafeli. Sipendagi ujinga wa hivi. Cha kufanya nikawabeba wote nikawapeleka chumbani kwenye kitanda kikubwa. Nikawaweka mwisho kabisa ili hata wakigaragara hapo kitandani wasianguke.Nikaendelea na mambo yangu.Wakalia hadi walipoona wametosheka.

Wale walivyorudi wakauliza vipi watoto hawajasumbua? Nikawahadithia wakafurahi wenyewe.

Mimi ukiniambia unazalisha tu halafu unalea nakusikitikia.

Ila kumbe mama zetu wanapotusikitikia huwa wanasikia uchungu sana.

Wakuu hii kazi ni ngumu. Mbarikiwe sana wanawake.
 
Drone Camera,

Kama kuna jambo tunapaswa tulifanye hapa dunian ambalo nilamsingi basi "Tuwatendee wema wazazi wetu"

Hebu jiulize kuna wakati mgumu kama kunyamanzisha mtoto ambae hujui analia kwa sababu gan? Maana yeye haongei hivyo sio rahis kujua kip kinamsumbua.

Lakin Mama husumbuka kuhakikisha mwanaye anakuwa katka har njema,Tuwape fadhira wazaz wetu.
 
Hakuna kama mama mkuu. Na hapo sasa bado hukubadilisha nepi na kuvilisha. Na bado havijaumwa usiku kucha vinalia homa imepanda. Unaweza kutamani ardhi ipasuke. Wanawake wamejaliwa moyo wa upendo na uvumilivu wa hali ya juu sana.

Mungu awabariki mama zetu na kuwapa maisha marefu; na waliotangulia kwake Awape pumziko jema. Nasi tukiwa na kauwezo japo kidogo tusiwasahau. Waliteseka na kutuhangaikia sana
 
Hakuna kama mama mkuu. Na hapo sasa bado hukubadilisha nepi na kuvilisha. Na bado havijaumwa usiku kucha vinalia homa imepanda. Unaweza kutamani ardhi ipasuke. Wanawake wamejaliwa moyo wa upendo na uvumilivu wa hali ya juu sana.

Mungu awabariki mama zetu na kuwapa maisha marefu; na waliotangulia kwake Awape pumziko jema. Nasi tukiwa na kauwezo japo kidogo tusiwasahau. Waliteseka na kutuhangaikia sana
Ujumbe safi mkuu. Ubarikiwe👏👏
 
Hapo tu !! Yaani Kaka yako na house girl wakatoka kwenda kutafuta chakula!! Wewe ukaambiwa dogo Baki na watoto!!!! Huyo house girl yaani amusindikize Kaka yako ikitokea wakakutana na watemi njiani house girl adhibiti we kidume umelala na watoto,,,ok sawa tumekuelewa
 
Hapo tu !! Yaani Kaka yako na house girl wakatoka kwenda kutafuta chakula!! Wewe ukaambiwa dogo Baki na watoto!!!! Huyo house girl yaani amusindikize Kaka yako ikitokea wakakutana na watemi njiani house girl adhibiti we kidume umelala na watoto,,,ok sawa tumekuelewa
Kiufupi mimi ndo nilichagua kubaki nyumbani. Hilo neno 'dogo' nimeliweka tu alishaacha kuniita hivyo miaka kumi iliyopita.
 
Aisee hii kazi ya kulea kwa wanaume hapana, wacha niwapongeze tu wanawake.

Hii kazi ni ngumu. Mnaodai mnazalisha kisha mnalea naanza kuamini ni chai ya tangawizi kabisa! Labda kama unamchukua mtoto kwa mama yake ana miaka mitano kwenda juu. Tofauti na hapo utateseka na kukonda rafiki.

Juzi nimeachiwa watoto mapacha masaa matatu tu ila naona kama nimeachiwa mwaka mzima!

Ipo hivi: Majuzi mke wa kaka yangu, shem, kaugua kidogo. Hivyo wakampeleka hospitali. So mimi baadaye nikaenda kucheki hali ipoje pale home. Nikasalimia fresh. Sasa bro akaniambia dogo baki tu hapa utaondoka kesho shemeji yako akija. Nikakubali.

Sasa usiku sasa house girl na kaka wakatoka kufuata chakula sijui. Akaniambia ndugu tunakuja muda si mrefu, kuna watoto pia wamelala hapo (mapacha). Nikasema sawa. Dk 5 akaanza kulia mmoja.

Nikamchukua huyo anayelia. Akanyamaza sema aliponicheki usoni akaanza kulia zaidi (hanijui). Bembeleza wee wapi. Ni ka kike kana sauti kali kakamuamsha nduguye. Kazi ikawa ngumu zaidi.

Tumia mbinu zote zikafeli. Sipendagi ujinga wa hivi. Cha kufanya nikawabeba wote nikawapeleka chumbani kwenye kitanda kikubwa. Nikawaweka mwisho kabisa ili hata wakigaragara hapo kitandani wasianguke.Nikaendelea na mambo yangu.Wakalia hadi walipoona wametosheka.

Wale walivyorudi wakauliza vipi watoto hawajasumbua? Nikawahadithia wakafurahi wenyewe.

Mimi ukiniambia unazalisha tu halafu unalea nakusikitikia.

Ila kumbe mama zetu wanapotusikitikia huwa wanasikia uchungu sana.

Wakuu hii kazi ni ngumu. Mbarikiwe sana wanawake.
Usisahau kuwapongeza ma house girl, hasa katika zama hizi
 
Back
Top Bottom