Troublemaker
JF-Expert Member
- Jun 8, 2015
- 20,814
- 40,572
Kwa hili nawapa heshima kwa kweli hiyo kazi si mchezo.
Uzoefu ninao ila sio sana maana nilishirikiana na partner wangu kipindi mwanangu yupo mdogo.Ni ngumu kweli lakini wewe umeiyongezea ugumu mara 3 yake.
Kwanza wewe sio mzoefu, pili ugeni wa watoto hawakukuzoea ndio maana ulipata changamoto kubwa. Hongera akina mama wote.
Hii ni kweli mkuu usumbufu wanaokutana nao ni mkubwa.Usisahau kuwapongeza ma house girl, hasa katika zama hizi
Alafu sijui kwanini mapacha wasumbufu mambo yao yanaendanaUzoefu ninao ila sio sana maana nilishirikiana na partner wangu kipindi mwanangu yupo mdogo.
Ila hata baba yao anakiri huwa wanamsumbua mno,mama yao ndo anawawezea.
hapo sasa changamoto kubwa huwa ni nini?Mungu atubariki na kazi huwa ngumu zaidi pale unapokuwa mwenyewe unatafuta ugali na kulea kwa pamoja.
Kwan kaka yako haez kufuata chakula adi aende na house girl? Kuna jambo hapo[emoji19]Aisee hii kazi ya kulea kwa wanaume hapana, wacha niwapongeze tu wanawake.
Hii kazi ni ngumu. Mnaodai mnazalisha kisha mnalea naanza kuamini ni chai ya tangawizi kabisa! Labda kama unamchukua mtoto kwa mama yake ana miaka mitano kwenda juu. Tofauti na hapo utateseka na kukonda rafiki.
Juzi nimeachiwa watoto mapacha masaa matatu tu ila naona kama nimeachiwa mwaka mzima!
Ipo hivi: Majuzi mke wa kaka yangu, shem, kaugua kidogo. Hivyo wakampeleka hospitali. So mimi baadaye nikaenda kucheki hali ipoje pale home. Nikasalimia fresh. Sasa bro akaniambia dogo baki tu hapa utaondoka kesho shemeji yako akija. Nikakubali.
Sasa usiku sasa house girl na kaka wakatoka kufuata chakula sijui. Akaniambia ndugu tunakuja muda si mrefu, kuna watoto pia wamelala hapo (mapacha). Nikasema sawa. Dk 5 akaanza kulia mmoja.
Nikamchukua huyo anayelia. Akanyamaza sema aliponicheki usoni akaanza kulia zaidi (hanijui). Bembeleza wee wapi. Ni ka kike kana sauti kali kakamuamsha nduguye. Kazi ikawa ngumu zaidi.
Tumia mbinu zote zikafeli. Sipendagi ujinga wa hivi. Cha kufanya nikawabeba wote nikawapeleka chumbani kwenye kitanda kikubwa. Nikawaweka mwisho kabisa ili hata wakigaragara hapo kitandani wasianguke.Nikaendelea na mambo yangu.Wakalia hadi walipoona wametosheka.
Wale walivyorudi wakauliza vipi watoto hawajasumbua? Nikawahadithia wakafurahi wenyewe.
Mimi ukiniambia unazalisha tu halafu unalea nakusikitikia.
Ila kumbe mama zetu wanapotusikitikia huwa wanasikia uchungu sana.
Wakuu hii kazi ni ngumu. Mbarikiwe sana wanawake.
Mnapitia mengi mkuu.Mungu awatie nguvu.Mungu atubariki na kazi huwa ngumu zaidi pale unapokuwa mwenyewe unatafuta ugali na kulea kwa pamoja.
😍😍Hakuna kama mama mkuu. Na hapo sasa bado hukubadilisha nepi na kuvilisha. Na bado havijaumwa usiku kucha vinalia homa imepanda. Unaweza kutamani ardhi ipasuke. Wanawake wamejaliwa moyo wa upendo na uvumilivu wa hali ya juu sana.
Mungu awabariki mama zetu na kuwapa maisha marefu; na waliotangulia kwake Awape pumziko jema. Nasi tukiwa na kauwezo japo kidogo tusiwasahau. Waliteseka na kutuhangaikia sana [emoji1545][emoji1545][emoji1545]
Ila nawatamani hatariWatoto mapacha wasumbufu sana.
Inawezekana hakuna changamoto.hapo sasa changamoto kubwa huwa ni nini?
Yani housegirl na kaka wakatafute chakula masaa 3? Badala akae kupika msosi.House girl na kaka wakatoka kuenda kutafuta chakula for three hours. Hapo inaonesha kwamba kwamba Kuna utamu wa chini ya kitovu kaka alienda kuupata kwa house girl .
Hizo kazi ndio sipendi, mtoto atakuwa wangu akishashiba na kuogeshwa ili nipate kumlaza tu kifuani.😍😍
Ameen
Unasemaaa!!!...muone unavyopenda Raha..malezi kusaidiana mtoto kanya mnawishe..akilia mbembeleze ili utengeneze chemistry nzuri na mtoto..we m'baba wewe..Hizo kazi ndio sipendi, mtoto atakuwa wangu akishashiba na kuogeshwa ili nipate kumlaza tu kifuani.
Akinya nakupa wewe, akilia nakupa wewe 🤣🤣🤣🤣🤣🤣
Sema mtoto wangu atakuwa sio kilizi sana 🤣🤣🤣🤣🤣!!!Unasemaaa!!!...muone unavyopenda Raha..malezi kusaidiana mtoto kanya mnawishe..akilia mbembeleze ili utengeneze chemistry nzuri na mtoto..we m'baba wewe..