Kiongozi naona unapiga hesabu za rent za kuishi kwenye apartments ila sehemu za kuishi au kulala hapa UAE zimegawanyika kama ifuatavyo,kuna Bed space ambayo kwa mwezi inaanzia 200aed hadi 1000aed,pia kuna partition hizi zinaanzia 1000aed hadi 2000aed pia kuna chumba kizima hapa unalipa kuanzia 1500 na kuendelea ni kutokana na sehemu chumba kilipo
Ila hapa dubai kuna Labour cities ambazo makampuni mengi yamejenga accommodation zao kwa staff wake ambao wanaishi bure ila chakula wanajitegemea na kwenye hizo accommodation wanapewa na majiko ya gesi kwa ajili ya kujipikia chakula chao,usafiri wa kwenda kazini na kurudi ni bure,pia Medical insurance
Pia Dubai mshahara wake hauna kodi hata moja,pesa yako utaipata kama ilivyo
Ukiwa Tanzania na una kipato cha kuanzia 1M kila mwezi nakushauri usiondoke ila kama umepata 2M kwa bahati mbaya na huwezi kuizalisha ni bora ukasafiri ukatengeneza kipato cha uhakika kila mwezi
Free accommodation maana yake ni kwamba utapewa bed space kama zilivyo hostel za chuo,chumba kimoja watu wanne
Kila mtu lazima aanze kwenye humble beginning,Dubai ni platform iliyowapa watu maisha,leo hii utakuja kwa kazi ya construction ila uzuri wake kuna growth of careers uankuja unapata kazi nzuri na yenye maslahi mazuri na kuweza kuishi kwenye chumba kizuri