Kazi na dawa

Acheni unafiki wenu hapa. Yohana na wafuasi wake walikuwa wanafunga waliambiwa wachoyo mwana adamu alikuwa anajua na kunywa Wakamwambi ni mlafi. Kumbe ubishani huu umeanza toka zama hizo. Leo watu wanakulana Kwa nyuma kwakuwa ni Siri wanaona si dhambi ila mtu akinywa bia mbili akalala ni dhambi Acheni unafiki watz. Anaglieni mioyo yenu si ya wengine unafiki chuki ungo ni dhambi mbaya zaidi kuliko chocht duniani.
Alikuwa anakunywa nini?

Au Biblia Wewe unaisoma Kama gazeti!

Neno LA Mungu sio lakutaniatania
Neno ni Neno
 
Swali.la.kizushi
Mbona hawanywi.mvinyo ambao ndion umejaa huko church wananunua kitu kigumu cha SAFARI.LAGER ???
 
Nilikuwa nafuatilia mada ila ukija kitu ambacho ni cha kizushi sitokaa kimya, huu ni uongo na ni upumbavu. Kama unatafuta njia ya kuweza kushawishi watu wajiunge na imani unayoifuata, jaribu kuhubiri na kuonesha umuhimu wa neno lako si kusambaza uzushi.



Kutumwa hiyo picha usikute kaweka mkristo mwenzenu, nani asiyejua kama RC na Sabato mna ugomvi. Usikimbilie kukashifu wasiyohusika.


Mbona waislamu wenye huwa hawatumii nguvu nyingi hivyo hadi kuunda picha za kizushi au kutia uongo kuhusu dini yenu. Heshimu imani ya mtu, hiyo picha usikute hajaweka mwislamu

Mbona ulikaa kimya uzushi wa hiyo Photoshop....
 
Usikurupuke kutoa lawama . Unauhakika kama kweli nao ni masister kweli? Tafakari kabla ya kutenda. Kwani yawezekana ni makusudi ya kulichafua KANISA katoliki kwani katoliki ndio lina waumini wengi na Shule nyingi kamaulivyo sema Na Sasa hivi Kumekuwa na Madhehebu Mengi sana hasa haya wanaita ya kiroho Yapo Kwa harakati kubwa ya kuvuna wanakondoo kutoka katoriki ili nao wajijenge .
Hata wale mapadri wanaofumaniwa kufanya ngono kwenye magar WANALICHAFUA RC kwakuwa lina waumini wengi
 
Dini huwa haipimwi kwa matendo ya waumini wake bali hupimwa kulingana na mafundisho yake, kwanza unaweza kunywa pombe na usifanye dhambi, ushawahi kujiuliza matendo ya kinyama na mauaji yanayofanywa na waislamu kwa mwamvuli wa uislamu?! Makundi ya kigaidi yanayojinasibisha na uislamu unayaona ni afadhali kuliko kunywa pombe ?
Kuua kupo ktk imani zote ajili ya Mungu, yaani ndani ya Biblia na hata Quran kwa maandiko mengi tuu, ila utaonekana waajabu kama huna Dola kufanya mambo hayo, tena kwa kukusaidia Vatican wanamiliki vyombo vya usalama ambavyo ni hatari zaidi duniani, 'kuhusu la pombe hilo ni lao' maana kwenye linaruhusiwa na pande nyingine halifai kabisa, ktk uislam hilo halifai kabisa lipo wazi. NB jamani someni ili msiwe warahisi kudanganywa elimu ya JF, FB na za udaku hazitoshi.
 
mnapaniki nini? ukatoliki haukatazi pombe unakataza kulewa
Atiiiiii
IMG_20170925_134501.jpg
 
Nyie wajinga kweli hamjui formula ya beer imegunduliwa na mafather huko Ujerumani Karne ya 15? Kwahiyo kukata beer kwa Roman katholik ni kitu ya kawaida huku ulaya sherehe za kanisa pombe kawaida kunyweka na heshima ipo pale pale.
 
Ni kweli wanakunywa ata marafiki zngu mapadre wa ruaha na mikumi wanatumia pombe kali ila awalewi wanajitambua nna ushaidi so sizn Kama ni tatz
Kila alaye anajua kuvimbiwa kukoje na kila anywaye anajua kulewa kukoje, tuache kudanganyana mnywaji yoyote ni mlevi aliyepita ama sasa au baadaye.
 
Tatizo nililoona hapa watu wengi hawazijui hata dini zao na hata maandiko hawayajui, pia hawajui nini maana ya haramu na halali.
 
Wakristo hawana sheria ila huwa wana utaratibu, na yapo mambo mengi sana nikisema utahisi nabomoa acha nichangie hili moja tu la pombe maana mimi si mtoa thread hii.' 1Petro 4:3, 1Timotheo 5:23, Mithali 20:31, Warumi 13:13, Wimbo 31:4-5, Wimbo 104:14-15, Wakorintho 10:23-24, Isaya 62:8-9, Wagalatia 5:19-21, Wakorintho 9:19-23, Yohana 2:3-11. Hapo kuna uhalali na uharamu wa pombe uchaguzi unabaki wako na hili lipo ktk majambo mengi ya kikristo.
 
Mbona ulikaa kimya uzushi wa hiyo Photoshop....
Kuhusu dini yako sijawahi kupitia kila sehemu ya andiko lenu kuhusu pombe, vipi nikemee nisichokuwa na ushahidi nacho. Sijakaa kimya kufurahia kilichowekwa hapo, ndiyo maana sijakashifu niwaache wenye kuijua musafishe hiyo kashfa anayowapa.



Halafu hiyo picha image processing ya Photoshop imefanyika wapi mimi ni mtaalamu wa hizo kazi hebu zungusha duara nipaone.
 
Swali.la kizushi no.2
KWAHIYO HATA POPE ANAKATA BAPA KAMA MZEE WA UPAKO au kuna aina ya kilevi kacjoruhusiwa huko KATOLIKI na mimi niingie
 
..."Padri akilala na sister, haibadilishi ukatoliki"
"Imamu akizini nje ya ndoa, hatuukimbii msikiti"

Viva Roma viva.
 
POMBE NI HARAMU,JE KWANINI WAKATOLIKI HURUHUSU KUNYWA POMBE,SIO DHAMBI?
Kati ya maswali yanayoulizwa na watu wengi sana,hasa ndugu zetu wa imani ya kiislamu na wakristo baadhi ni kuhusu suala la kunywa pombe kwa wakristo hasa wakatoliki.
hutuuliza, ninyi wakristo wakatoliki kwanini mnakunywa pombe na ni haramu hamjui mnatenda dhambi?
katika kutafuta kufahamu ukweli wa majibu ya jambo hili kwanini wakristo wakatoliki tunakunywa pombe na hatuoni kuwa ni dhambi nikaona nijaribu kukushirikisha kwa uchache kuhusu ukweli huu,si kwa kuwa ni mjuzi sana Hapana. Bali ni kwa sababu kristo ndiye mjuzi zaidi aliyeanzisha kanisa moja takatifu katoliki la mitume juu ya mwamba mathayo 16:18 na kutupa elimu kupitia nguvu ya mapaji saba ya Roho Mtakatifu Katika Kujua Kweli yake Yote.
Kwa Kuanza kujifunza swala hili,inatupasa kufahamu jambo moja kwamba Yesu Kristo mwenyewe alikunywa pombe,hili inaonesha ni jambo jipya kwako, lakini kuthibitisha hili ukiwa unapenda kusomasoma Biblia Fungua na urejee luka 7:33-34 inasema
33 Kwa kuwa Yohana Mbatizaji alikuja, hali mkate wala hanywi divai, nanyi mwasema, Ana pepo.
34 Mwana wa Adamu amekuja, anakula na kunywa; nanyi mwasema, Tazama, mlafi huyu, na mnywaji wa divai, rafiki wao watoza ushuru na wenye dhambi.
Hapo tunagundua kuwa YESU alilalamika kuwa walimwita mlafi na mnywaji wa divai kwa kuwa alikunywa, tofauti na mtangulizi wake Yohana Mbatizaji. Ambaye Hakula wala kunywa divai.
Pia Yesu aligeuza maji kuwa divai kule kana kwenye harusi rejea Yohana 2:1-12
anzia aya ya 6-11
inasema 6″Hapo palikuwa na mitungi sita ya mawe, ambayo kila mmoja uliweza kuchukua kiasi cha madebe mawili au matatu. Ilikuwa imewekwa hapo kufuatana na desturi ya Kiyahudi ya kutawadha. 7Yesu akawaambia, “Ijazeni mitungi hiyo maji.” Nao wakaijaza mpaka juu.
8Kisha akawaambia, “Sasa choteni mkampelekee mkuu wa karamu.”
9Mkuu wa karamu alipoonja hayo maji, kumbe yalikuwa yamegeuka kuwa divai. Yeye hakujua ilikotoka, (lakini wale watumishi waliochota maji walijua). Mkuu wa karamu akamwita bwana arusi, 10akamwambia, “Kila mtu huandaa DIVAI NZURI kwanza hata wakisha tosheka huandaa ile hafifu. Lakini wewe umeiweka DIVAI NZURI mpaka sasa!”.
Katika andiko hilo kuna wale wanaodai kuwa YESU Alitengeneza divai tamu/juisi na sio divai pombe kwa kuwa ilikuwa nzuri/mpya hivyo ni juisi wala sio pombe na ndiyo aliyokunywa Yesu.
Kwanza tukirejea katika luka 7:33-34 katika Biblia ya lugha ya kigiriki utagundua kuwa Yesu alitumia neno
Oinopotes.Neno hili Oinopotes linatokana na neno ‘oinos’ yaani(DIVAI/WINE/POMBE),Kumbe yesu mwanzo walimwita mlevi wa divai pombe,Kama Yesu angetaka kusema ile ilikuwa ni“Divai tamu/juisi” lingekuwepo neno“Glukohos”linalomaanisha Divai “tamu”lakini Yesu ametumia neno OINOS lenye maana Divai pombe.
lakini wale wanaodai divai Aliyotengeneza Yesu kwenye harusi ni mpya haikuchachushwa hivyo hailevi, Biblia Takatifu inawajibu hivi rejea kitabu cha HOSEA 4:11
inasema“Divai mpya na ya zamani
huondoa maarifa.
Kumbe Divai Mpya na ya zamani huondoa maarifa/hulevya sasa kama divai hii huondoa maarifa/hulevya utasemaje ni juisi tu wala sio pombe? mimi sitakuelewa.
Tena tunaambiwa hivi katika luka 5:37 divai mpya watu hawaweki katika viriba vichakavu kwani vitapasuka kwa wingi wa gesi ya divai rejea luka
5:37-38
inasema”Wala watu hawatii divai mpya katika viriba vikuukuu; kwani hiyo divai mpya itavipasua hivyo viriba, divai itamwagika, na viriba vitaharibika”.
ongezea na marko 2:22,mathayo 9:17
divai ya kana ilikuwa mpya kumbe iliweza kuondoa maarifa na hivyo ilikuwa pombe/divai iliyochachwa, Yesu alitengeneza pombe hawezi kukakataa kuitumia hivyo na kamwe hakujipinga mwenyewe.
Kitendo cha kunywa tu hakina tafsiri ya kutenda dhambi na kama ni dhambi basi hata hata kula kutakuwa ni dhambi, ULEVI ni kitendo cha kula au kunywa kupita kiasi/kuvimbiwa, kunywa mipombe kupita kiasi huko ndiko hakutakiwi kwani hupingana na fadhila ya KIASI,
maandiko yanasifia Pombe rejea katika Yohana 2:7-12, mbali na hilo tunaona pombe/divai inaruhusiwa kama dawa kwa kiasi ukirejea 1Timoteo 5:23 sasa wale wanaodai kuwa Pombe ni haramu inakuwaje tena iruhusiwe itumike kama tiba n.k je Mungu hajipinga?,Mungu hawezi kuruhusu jambo haramu lifanyike,Pombe bado inaendelea kusifiwa katika Methali 31:6-7, Hata kuhani yule Mkuu alimletea Ibrahim mkate na Divai(Pombe) soma katika kitabu cha Mwanzo sura ya 14:18, Tunaona Yakobo anampa Baba yake divai rejea pia Mwanzo 27:25, Hesabu 28:29.
Bado Mungu anaagiza sadaka ya DIVAI, tena Katika biblia ya kiebrania Limetumika neno ‘Shekar’ Linalomaanisha ‘Divai kali’,Zaidi soma Zaburi 104:14-19, Kumbukumbu La Torati 14:26, Isaya 25:6, Mpaka hapo umeleewa kiasi kuwa Kinachokatazwa ni ULEVI(kunywa kupitiliza) na siyo KUNYWA WA DIVAI/POMBE.
SI KILA ANAYEKULA BASI NI MLAFI,VILEVILE SI KILA ANAYEKUNYWA NI MLEVI.
Biblia katika agano jipya inafundisha na kukataza ULEVI ni hatari na sio unywaji wa pombe maandiko mbalimbali yanathibitisha hilo rejea rumi 13:13
inasema “Mwenendo wetu uwe wa adabu kama inavyostahili wakati wa mchana; tusiwe na ulafi na ulevi, uchafu na uasherati, ugomvi na wivu”. pia
waefeso 5:18 inasema
18 “Pia msilewe divai, kwa sababu huo ni upotovu, bali mjazwe Roho,ongezea na 1kor 5:11, 6:9-10, Galatia 5:21,
1Tim 3:2-3,
Tito 1:7.
Katika agano la kale pia maandiko yanakataza ulevi na sio unywaji wa pombe rejea isaya 5:22,23:29-35 mithali 20:1,23:20
kumbe ulevi unakatazwa lakini Unywaji wa kawaida tu haukatazwi, na pamoja kwamba Mungu kuruhusu wanadamu tutumie Divai(Pombe) anatutaka tuwe na kiasi kuepuka kulewa na kutenda dhambi ya ulevi kwa kuwa walevi, Agano la kale linazungumza kiusahihi kabisa likisisitiza kwa kusema “Divai huleta dhihaka na kileo huleta ugomvi” inapotumika kupita kiasi,lakini Mungu anafurahi tunapotumia Divai n kwa kiasi ili “Kufurahi mbele za Bwana” soma Kumbukumbu 14:26, Katika 1Korintho 6:9-10.
Paulo anasema“…Walevi hawataurithi ufalme wa Mbingu…” pia katika Galatia 5:21 ametumia Maneno ya kigiriki “methai na komoi” kumaanisha Walevi na siyo wanywaji wa kawaida tu, Pia katika Efeso 5:18 Paulo ametumia neno methyskethe linalomaanisha ULEVI na siyo unywaji wa kawaida wa divai/pombe, katika aya hizo zote Paulo angetumia neno pino kama alitaka kumaanisha mnywaji wa kawaida hataenda mbinguni.
3:3-8 Paulo hakatazi kunywa Divai/bali anatoa ushauri wake kuwa Maaskofu na mashemasi wawe na Kiasi katika kutumia divai au waache ikiwezekana, sivyo angependekeza Shemasi Timotheo atumie Mvinyo(Divai) kidogo kama dawa ya Tumbo rejea 1Tim 5:23, Moja kwa moja MUNGU hajipingi, katika Neno ukichunguza utaona Mungu anatukataza ULEVI(unywaji kupita kiasi) lakini hajakataza unywaji wa Kiasi/kawaida.
KANISA
Kanisa pamoja na kusema Watu Tutumie Divai/pombe bado linatuasa tuitumie Fadhila ya kiasi ili tusizidishe, “Fadhila ya kiasi inatuandaa kuzuia kila aina ya kupita kiasi: wenye Matumizi mabaya ya chakula, kileo, tumbaku au dawa, wanafanya kosa kubwa wale ambao kwa ulevi au kupenda mwendo wa kasi, huhatarisha usalama wao na wa wengine…..” rejea Katekisimu ya Kanisa Katoliki(KKK) no.2290.
Paulo anatuambia ; “Mtu ambaye hula kila kitu asimdharau Yule ambaye hawezi kula kila kitu, naye ambaye hula tu mboga za majani asimhukumu anayekula kila kitu, maana Mungu amemkubali” rejea Warumi 14:3.

MWISHO
Pombe ni kinywaji cha furaha na ni zao la mimea mbalimbali mfano ndizi, zabibu, mahindi, ngano n.k tutumie kwa furaha na kiasi kama YESU alivyotumia kwa kiasi. Kama tukiwa hatuwezi basi tuache kabisa kwa busara,bila kutangaza kuwa unywaji wa kinywaji hicho ni haramu na dhambi.

Tutumie Kwa Kiasi Tukishindwa Ni Vyema kuwaachia wale wanywao kwa kiasi. Na matumizi ya pombe kali zisizo na vipimo maalumu ni hatari kwa afya zetu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom