This is...
JF-Expert Member
- Dec 28, 2014
- 4,903
- 4,979
Waziri Mkuu ametilia shaka barakoa kutoka nje kuwa tujishonee wenyewe. Kuna watu wanabeza hii kauli, Kuna wanaodhihaki hata kutoa kauli chafu, kuna wanaotetea hii kauli kwasababu tu imetolewa na mwenzetu ktk serikali au chama. Kuna wanaoongea kwa hofu kwanini PM atoe kauli hii.
Kuna wanaofikiri nje box ambao Ni wachache na mimi ni mmoja wao.
Mosi, Watu wanahoji TBS kazi yao Ni nini km Waziri Mkuu anatoa kauli ya mashaka kama hii. Waziri mkuu anajua uwezo wa TBS katika kupima na kujiridhisha ubora wa bidhaa km hii. Hapa kuna mambo mawili ambayo mashaka ya Waziri Mkuu hayajagusia:
a. Je, Ni barakoa SALAMA lakini tatizo tu hazina ubora kwa maana hazina uwezo wa kuzuia kirusi kupenya.
b. Ni barakoa zenye UBORA lakini tayari zina maambukizi na si salama kwa matumizi.
Haya ndiyo ambayo unaweza kuyafikiria na kujiuliza Je, TBS wana uwezo wa kudhibiti yote mawili? Ubora na Usalama.
Pili, simsemei Waziri Mkuu, lakini fikra zangu zinanielekeza kuona kwamba hii ni kauli ya tahadhari kwasababu msimamo wa serikali yetu kimataifa unaeleweka juu ya suala la korona. Ni msimamo ambao si kuwafurahisha. Korona ni suala lenye malengo ya kiuchumi ndani yake, lengo ambalo Tanzania tunalikwamisha. Kwahiyo wanaweza kutumia njia ya kuingiza barakoa zisizo salama ili maambukizo yawe juu, vifo viwe vingi ili kuonyesha dunia kuwa tumefeli, na hivyo kwenda kusujudu kwao na kupokea chanjo ambayo pengine nayo si Salama.
Wametengeneza tatizo na wao ndiyo wanaokuja na suluhisho. Suluhisho Ni chanjo ambayo itawaingizia matrilioni ya shilingi, na pengine chanjo yenyewe si salama., Tukajikuta tunanunua mauti yetu kwa pesa zetu.
Tatu, Waziri Mkuu Ni mtu nwenye access ya habari nyeti za ndani na nje ya nchi, hivyo yuko informed vya kutosha kuhusu kinachoendelea hata kwa nchi majirani. Si nchi zote jirani zinakubaliana na msimamo wa serikali yetu. Wanaweza kutumika pia.
Chakula ulichopika mwenyewe nyumbani Ni salama kuliko cha hotelini au mghahawani.
Wakati mwingine kuna kauli zinatolewa na serikali Ni kwasababu ya tahadhari na nia njema. Kwa hali km hii Ni vyema tukadoubt kila kitu juu ya korona na tukachukua tahadhari.
Ushauri: Serikali inapaswa kutoka hadharani na kutangaza hadharani korona ipo na inauwa.Inatamkwa tu kuchukua tahadhari bila kukiri uwepo wake.
Kuna mwananchi kila kitu lazima asikie serikali inasema ndiyo anaona ni jambo siriazi.
Serikali ina plani gani baada pengine hii ya kujifukiza na tiba asili kufeli. Imejipanga kiasi gani?
Watanzania tuchukue tahadhari, tuache mzaha, si lazima kila kitu uambiwe na serikali.
Kuna wanaofikiri nje box ambao Ni wachache na mimi ni mmoja wao.
Mosi, Watu wanahoji TBS kazi yao Ni nini km Waziri Mkuu anatoa kauli ya mashaka kama hii. Waziri mkuu anajua uwezo wa TBS katika kupima na kujiridhisha ubora wa bidhaa km hii. Hapa kuna mambo mawili ambayo mashaka ya Waziri Mkuu hayajagusia:
a. Je, Ni barakoa SALAMA lakini tatizo tu hazina ubora kwa maana hazina uwezo wa kuzuia kirusi kupenya.
b. Ni barakoa zenye UBORA lakini tayari zina maambukizi na si salama kwa matumizi.
Haya ndiyo ambayo unaweza kuyafikiria na kujiuliza Je, TBS wana uwezo wa kudhibiti yote mawili? Ubora na Usalama.
Pili, simsemei Waziri Mkuu, lakini fikra zangu zinanielekeza kuona kwamba hii ni kauli ya tahadhari kwasababu msimamo wa serikali yetu kimataifa unaeleweka juu ya suala la korona. Ni msimamo ambao si kuwafurahisha. Korona ni suala lenye malengo ya kiuchumi ndani yake, lengo ambalo Tanzania tunalikwamisha. Kwahiyo wanaweza kutumia njia ya kuingiza barakoa zisizo salama ili maambukizo yawe juu, vifo viwe vingi ili kuonyesha dunia kuwa tumefeli, na hivyo kwenda kusujudu kwao na kupokea chanjo ambayo pengine nayo si Salama.
Wametengeneza tatizo na wao ndiyo wanaokuja na suluhisho. Suluhisho Ni chanjo ambayo itawaingizia matrilioni ya shilingi, na pengine chanjo yenyewe si salama., Tukajikuta tunanunua mauti yetu kwa pesa zetu.
Tatu, Waziri Mkuu Ni mtu nwenye access ya habari nyeti za ndani na nje ya nchi, hivyo yuko informed vya kutosha kuhusu kinachoendelea hata kwa nchi majirani. Si nchi zote jirani zinakubaliana na msimamo wa serikali yetu. Wanaweza kutumika pia.
Chakula ulichopika mwenyewe nyumbani Ni salama kuliko cha hotelini au mghahawani.
Wakati mwingine kuna kauli zinatolewa na serikali Ni kwasababu ya tahadhari na nia njema. Kwa hali km hii Ni vyema tukadoubt kila kitu juu ya korona na tukachukua tahadhari.
Ushauri: Serikali inapaswa kutoka hadharani na kutangaza hadharani korona ipo na inauwa.Inatamkwa tu kuchukua tahadhari bila kukiri uwepo wake.
Kuna mwananchi kila kitu lazima asikie serikali inasema ndiyo anaona ni jambo siriazi.
Serikali ina plani gani baada pengine hii ya kujifukiza na tiba asili kufeli. Imejipanga kiasi gani?
Watanzania tuchukue tahadhari, tuache mzaha, si lazima kila kitu uambiwe na serikali.