Kauli ya Nape ni kauli ya kuiogopa CHADEMA

Kauli ya Nape ni kauli ya kuiogopa CHADEMA

blueray

JF-Expert Member
Joined
Sep 15, 2012
Posts
2,217
Reaction score
426
Angalia kauli kama hii iliyotolewa na Mheshimiwa Nape jana (22.08.2013):
"Taasisi zilitakiwa ziandae mabaraza ya katiba ambayo yatatumika kukusanya maoni. Hivyo sijui ni ushamba wa CHADEMA au kutokujua sheria wanafanya mikutano ya hadhara, maoni ya helikopta hayapokelewi kama alivyosema mzee warioba"

Hapa sijui ni nani mshamba kati ya Chadema Na yeye Nape. Kama viongozi wa CCM hawaendi kukusanya maoni-kwa wanachama wake kwa nini Nape atake Chadema nayo isikusanye maoni kwa wanachama?
Na kwa nini yeye Nape aisemee tume? Au yeye ndiye mwenyekiti mwenza wa tume ya kukusanya maoni ya rasimu ya katiba!

Mheshimiwa Nape anaogopa nini Chadema kufanya mikutano yake ya kukusanya maoni kutoka kwa wanachama na wapenzi wake?
Njia ya mikutano ya hadharani ya wanachama na wapenzi ni njia mojawapo tu ambayo chama kimeona inafaa ili kuwashirikisha wanachama na wananchi wengi na ni njia ya kidemokrasia iliyokomaa. Njia nyingine zinazotumika -ni kushirikisha wananchi katika mitandao na Simu kama matangazo mbalimbali yanavyosomeka. Njia hizi ni za uwazi na zinashirikisha watu wengi zaidi bila ubaguzi.

Inaelekea -nguvu ya Chadema ambayo ni nguvu ya wananchi imekuwa tishio kubwa sana kwa Nape na ndio maana uoga unampata anapoona wanachama wengi na wapenzi wanavyojitokeza mikutano ya maoni. Anapata kitu kinaitwa 'Chademaphobia'

Pia Nape anaeleza;
"... taasisi zilitakiwa ziandae mabaraza ya katiba ambayo yatatumika kukusanya maoni..."
Sasa sijui hapa haya mabaraza yatakutanaje bila kuhusisha wananchi!

Hapa swala la kujiuliza -hawa wanachama na wapenzi wa CCM wamekaa lini hadi kupata maoni ya kujadili vikao vya juu vya chama?

Mbona sisi huku mitaani hatujaona vikao! Na kama kulikuwa na vikao labda kwa viongozi wa chama na si kwa wanachama wote.

Hii inaonyesha uongozi wa CCM kutumia ubabe na kudharau wanachama wa ngazi za chini.

Bwana Nape anaendelea; "...Pia wiki hii CCM mbali na vikao vya sekretarieti ya chama,tutakuwa na kamati kuu ya chama itakayofanyika mwishoni mwa wiki hii baada ya mwenyekiti kurejea kutoka kwenye sherehe za kuapishwa kwa Rais Mugabe.
Baada ya Kamati kuu kutakuwa na vikao vya NEC"-
Hapa Inavyoelekea CCM taifa imekwishaandaa maoni yake bila kushirikisha wananchi.
Sasa kinachofanyika ni uchakachuaji na -kuhalalisha kwa vikao vya juu. Kitu ambacho ni ukiukwaji mkubwa wa demokrasia ndani ya chama cha mapinduzi.
 
Nape ni mwendawazimu...hayuko sawa upstairs. Sasa hivi amechanga nyikiwa pia anaweweseka mara kwa mara...mwigulu ndio karibu atavaa chupi kichwani...dawa yake ni jesca kishoa hahaha magamba ni majanga.
 
Angalia kauli kama hii iliyotolewa na Mheshimiwa Nape jana (22.08.2013):
"Taasisi zilitakiwa ziandae mabaraza ya katiba ambayo yatatumika kukusanya maoni. Hivyo sijui ni ushamba wa CHADEMA au kutokujua sheria wanafanya mikutano ya hadhara, maoni ya helikopta hayapokelewi kama alivyosema mzee warioba"

Hapa sijui ni nani mshamba kati ya Chadema Na yeye Nape. Kama viongozi wa CCM hawaendi kukusanya maoni-kwa wanachama wake kwa nini Nape atake Chadema nayo isikusanye maoni kwa wanachama?
Na kwa nini yeye Nape aisemee tume? Au yeye ndiye mwenyekiti mwenza wa tume ya kukusanya maoni ya rasimu ya katiba!

Mheshimiwa Nape anaogopa nini Chadema kufanya mikutano yake ya kukusanya maoni kutoka kwa wanachama na wapenzi wake?
Njia ya mikutano ya hadharani ya wanachama na wapenzi ni njia mojawapo tu ambayo chama kimeona inafaa ili kuwashirikisha wanachama na wananchi wengi na ni njia ya kidemokrasia iliyokomaa. Njia nyingine zinazotumika -ni kushirikisha wananchi katika mitandao na Simu kama matangazo mbalimbali yanavyosomeka. Njia hizi ni za uwazi na zinashirikisha watu wengi zaidi bila ubaguzi.

Inaelekea -nguvu ya Chadema ambayo ni nguvu ya wananchi imekuwa tishio kubwa sana kwa Nape na ndio maana uoga unampata anapoona wanachama wengi na wapenzi wanavyojitokeza mikutano ya maoni. Anapata kitu kinaitwa 'Chademaphobia'

Pia Nape anaeleza;
"... taasisi zilitakiwa ziandae mabaraza ya katiba ambayo yatatumika kukusanya maoni..."
Sasa sijui hapa haya mabaraza yatakutanaje bila kuhusisha wananchi!

Hapa swala la kujiuliza -hawa wanachama na wapenzi wa CCM wamekaa lini hadi kupata maoni ya kujadili vikao vya juu vya chama?

Mbona sisi huku mitaani hatujaona vikao! Na kama kulikuwa na vikao labda kwa viongozi wa chama na si kwa wanachama wote.

Hii inaonyesha uongozi wa CCM kutumia ubabe na kudharau wanachama wa ngazi za chini.

Bwana Nape anaendelea; "...Pia wiki hii CCM mbali na vikao vya sekretarieti ya chama,tutakuwa na kamati kuu ya chama itakayofanyika mwishoni mwa wiki hii baada ya mwenyekiti kurejea kutoka kwenye sherehe za kuapishwa kwa Rais Mugabe.
Baada ya Kamati kuu kutakuwa na vikao vya NEC"-
Hapa Inavyoelekea CCM taifa imekwishaandaa maoni yake bila kushirikisha wananchi.
Sasa kinachofanyika ni uchakachuaji na -kuhalalisha kwa vikao vya juu. Kitu ambacho ni ukiukwaji mkubwa wa demokrasia ndani ya chama cha mapinduzi.

Ukisha kuwa kiongozi CCM, lazima upate maambukizi ya ugonjwa unaoitwa UKOSEFU WA KUFIKIRI. Hivi Nape ameshindwa kujua kwamba wananchi pia ni Taasisi!!?? Au anajiwa na fikra kwamba Taasisi ni zile zenye hati ya kuandikishwa tu kama ilivyo CCM? Na kama ndivyo anashindwa je kufahamu kwamba Hati ya kuandikishwa wananchi kuwa Taasisi ipo kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania!?

Kama ndivyo alivyo karirishwa na Mwenyekiti wa Tuma ya Rasimu ya Katiba mpya basi nao ni upofu pia.

Yeye andelee na MAGAMBA yao, ukizingatia kwamba siku hizi hata majukwaa wanayaogopa na ndio maana wameamua kuja na fasion mpya ya kujifungia kwenye maghala ya CCM na kuhalallisha eti ni vikao vya ndani.

Atapiga kelele sana lakini elimu ya uraia inayo tolewa kwa waTanganyika na ime wakamata CCM hadi basi. Si tumeona hata M/Kiti wake siku hizi hapandi majukwaani bila kuwa na mashahidi kama akina Dr. Mwakyembe? Huku wakiwa na ushahidi wa utekelezaji wa ahadi hewa!!!!

Sisi tunasubiria uboreshwaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na Tume huru ya Uchaguzi. hapo ndipo tunataka kuonyesha hasira zetu kwa CCM. Maana mateso haya lazima yalipizwe kwa kitu kama hii "T 2015 CDM".
 
Nape hana jipya.Hayo ndio mawazo ya chama kwa ujumla na mwenyekiti JK KAYAPITISHA KWA KUONA SAWA. Wameshafilisika kimawazo.
 
Mda mwingine hawa jamaa zetu wa ccm ni kuwaacha akili zao kashika mwigulu sasa hapo unategemea nn?
 
mchakato wa katiba umeingiliwa kwa kiasi kikubwa na vyama vya siasa#poor normal citizen they just watchdog
 
Hapa swala la kujiuliza -hawa wanachama na wapenzi wa CCM wamekaa lini hadi kupata maoni ya kujadili vikao vya juu vya chama?

Mbona sisi huku mitaani hatujaona vikao! Na kama kulikuwa na vikao labda kwa viongozi wa chama na si kwa wanachama wote.

Hii inaonyesha uongozi wa CCM kutumia ubabe na kudharau wanachama wa ngazi za chini

Hapo kwenye red, Kuna mdau aliwahi kudadavua humu JF kuhusu utendaji na chain of Command za vyama hasa ccm na CHADEMA. ccm wao vijana hawana nafasi na huamriwa kufuata yale ya NEC yao wakti CDM vijana wanafanya tafiti na kushauri halmashauri kuu nini cha kufanya.
Hakuna mahali wana ccm walitoa maoni huru kuhusu katiba mpya wala mchango wao katika masuala ya ujenzi wa taifa hautambuliki. Wao uvccm ni daraja la kuwavusha wanaowania uongozi kama urais, ubunge n.k kisha wao vijana hubaki wakingojea kwa hamu uteuzi kwa nafasi kama za u-DC, RC n.k kama zawadi kwa kuvusha mgombea aloshinda.hakuna maoni huru katika ccm.
Tazama kuhusu maoni ya katiba mpya, kwanza alianza nape kutoa msimamo wa chama chao hata kabla ya nec yao kukaa. Alijadili na wanachama wapi??? wakaenda dodoma wakaja na yale waliolazimisha kila mwanachama wao akubali na ndio iwe ajenda yao, wakasambaza kuanzia ngazi ya taifa hadi kijiji kuwa hayo ndio maoni ya chama. hapa ushirikishwaji wa wanachama uko wapi???

Tofauti kubwa ukilinganisha na CDM ni kuwa BAVICHA wanapewa nafasi na wanafanya tafiti kujiridhisha na kushauri halmashauri kuu kuhusu nini cha kufanya. ndio maana kila siku unaona CDM wanakuja na mbinu mbadala za kuimarisha Chama.
 
CCM(Chama cha Mafisadi) ni JANGA la Maendeleo Tanzania kama ilivyo UKIMWI kwa afya za walimwengu

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Hivi Napengwa Ana Mastaz Kweli?

Mbona Ana Mawazo Kama Mtoto Wa Darasa La Pili La Mchana?
 
Hapa swala la kujiuliza -hawa wanachama na wapenzi wa CCM wamekaa lini hadi kupata maoni ya kujadili vikao vya juu vya chama?

Mbona sisi huku mitaani hatujaona vikao! Na kama kulikuwa na vikao labda kwa viongozi wa chama na si kwa wanachama wote.

Hii inaonyesha uongozi wa CCM kutumia ubabe na kudharau wanachama wa ngazi za chini

Hapo kwenye red, Kuna mdau aliwahi kudadavua humu JF kuhusu utendaji na chain of Command za vyama hasa ccm na CHADEMA. ccm wao vijana hawana nafasi na huamriwa kufuata yale ya NEC yao wakti CDM vijana wanafanya tafiti na kushauri halmashauri kuu nini cha kufanya.
Hakuna mahali wana ccm walitoa maoni huru kuhusu katiba mpya wala mchango wao katika masuala ya ujenzi wa taifa hautambuliki. Wao uvccm ni daraja la kuwavusha wanaowania uongozi kama urais, ubunge n.k kisha wao vijana hubaki wakingojea kwa hamu uteuzi kwa nafasi kama za u-DC, RC n.k kama zawadi kwa kuvusha mgombea aloshinda.hakuna maoni huru katika ccm.
Tazama kuhusu maoni ya katiba mpya, kwanza alianza nape kutoa msimamo wa chama chao hata kabla ya nec yao kukaa. Alijadili na wanachama wapi??? wakaenda dodoma wakaja na yale waliolazimisha kila mwanachama wao akubali na ndio iwe ajenda yao, wakasambaza kuanzia ngazi ya taifa hadi kijiji kuwa hayo ndio maoni ya chama. hapa ushirikishwaji wa wanachama uko wapi???

Tofauti kubwa ukilinganisha na CDM ni kuwa BAVICHA wanapewa nafasi na wanafanya tafiti kujiridhisha na kushauri halmashauri kuu kuhusu nini cha kufanya. ndio maana kila siku unaona CDM wanakuja na mbinu mbadala za kuimarisha Chama.


Kweli kabisa, hapa Mkuu nakubaliana nawe asilimia mia.

CCM maamuzi yao hayatoki Chini kwenda juu Bali juu kwenda Chini.
 
CCM(Chama cha Mafisadi) ni JANGA la Maendeleo Tanzania kama ilivyo UKIMWI kwa afya za walimwengu

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums


Kweli mku CCM ni janga kuu la taifa Na Ni balaa!

Maovu yote yanatekelezwa ndani ya CCM. Bora hata ya ukimwi mtu anaweza kunywa dawa akaendelea kuishi lakini hiki chama kinaangamiza taifa
 
Mda mwingine hawa jamaa zetu wa ccm ni kuwaacha akili zao kashika mwigulu sasa hapo unategemea nn?


Ha ha ha ha ha, inaashangaza CCM kuishiwa kabissa Na hoja Na sasa kuacha akili ya Nchemba ndio ifikirie badala ya chama!

Amefuta kabisa fikra Na mwenyekiti ambazo zilitakiwa zidumu
 
Yaelekea Computer Room pale Lumumba bado hapajafunguliwa kwani team ya Buku 7 bado kutinga jamvini. Wakifungua tu mtaona akina CHAMA, RITZ, CHAMVIGA, LIZIBON & Co. Watakuja na njaa criticism.
 
Kweli kabisa, hapa Mkuu nakubaliana nawe asilimia mia.

CCM maamuzi yao hayatoki Chini kwenda juu Bali juu kwenda Chini.
ndio maana mbinu za kuiua zimekwama alfu mbona wasira tena kimya?
 
Yaelekea
Computer Room pale Lumumba bado hapajafunguliwa kwani team ya Buku 7
bado kutinga jamvini. Wakifungua tu mtaona akina CHAMA, RITZ, CHAMVIGA,
LIZIBON & Co. Watakuja na njaa criticism.

Tumewaachia kanafasi kidogo mpumue maana uwepo wetu hapa JF umekiwa kero kwa wengine. by the way Nape kaongea vizuri na yupo sahihi. tatizo ni uelewa mdogo wa viongozi wa CHADEMA
 
Back
Top Bottom