"Serikali haina hela" huu ndio wimbo ambao nimeusikia sana katika awamu hii. Unajua kuna watu ambao wana external locus of control, yaani wao kila kitu wanasukumizia upande mwingine, they can't accept their mistakes. Wewe unakimbilia kusingizia mapato ya TRA, gharama za serikali (ambazo for sure ni fuel costs za ma-V8 ambayo sijaona sababu mpaka kesho ya kuwa nayo mengi kiasi hiki), wakati hali ya hospitali zetu ni chovu namna hiyo. Then leo tunakuja danganywa na Rais kuwa by 2015 kila mwalimu atakuwa ana computer wakati ameshindwa kutimiza simple tasks kama elimu, huduma safi za afya na kuishia kushangilia wimbo wenye kibwagizo cha "kwa hisani ya watu wa Marekani, China, n.k."
Mkuu hapo haujaweka Mishahara na posho za Mawaziri 60 ambao si watendaji bali wanasiasa. Miradi ya kipuuzi kama vitambulisho, yaani unatumia mabilioni kwenye issue kipuuzi tu.
Kama tungeamua hasa kwa dhati kuwa makini na matumizi basi nchi kama TZ ilitakiwa kuwa na mawaziri wasiozidi 15 tu. wengine wote ni redundant!