Akili Kichwani
JF-Expert Member
- Jan 7, 2010
- 1,508
- 216
Mkuu Akili,
Ni vizuri tunapotazama hili jambo tuamini kwamba utaratibu wa kikanuni na katiba ya chama katika uteuzi wa mgombea urais ulifuatwa.
Nataka nikuhakikishie kwamba hakuna mtu aliyenunuliwa kumpendekeza Dr. Slaa kuwa mgombea, utakumbuka kuwa hadi dakika za mwisho kabisa chadema haikuwa na mgombea uraisi na Dr. Slaa alikuwa amechukua fomu za kuwania ubunge Karatu, na ukumbuke kwamba kulikuwa na mazungumzo kati ya vyama vya upinzani kuona uwezekano wa kuungana na kuwa na mgombea mmoja, lakini hadi dakika za mwisho ikaonekana isingewezekana kuwa na mgombea mmoja kwakuwa vyama bado vilihitaji kukubaliana namna ya kugawana na majimbo zoezi ambalo lilishindikana, pia ilichangiwa na vyama kutoaminiana.
Kwa maoni yangu, labda kinachohitajika kwa sasa ni kuboresha utaratibu huu wa kamati kuu kufanya utafiti wa jina la mgombea anayefaa kukiwakilisha chama. Uwekwe utaratibu wa wazi na sifa za mgombea na mchakato wake uwe wazi kwa wanachama wote, ingawa bado kamati kuu itakuwa na jukjumu la kutafiti majina ya waliojitokeza ama hata nje ya hao waliojitokeza.
mkuu MM, shukrani sana kwa maelezo mazuri na ya kina..................... naona nikubaliane na wewe hapo kwenye bold kuwwa ni vyema huo utaratibu ukaboreshwa zaidi ili kuondoa kila aina ya swali ama utata juu ya namna ya kumpata flag bearer ndani ya chadema................. hilo litaimarisha imani ya wanachama na hata wasio wanachama juu ya demokrasia ndani ya chama................
uwe na siku njema mkuu.....................